Nimeamua Kustaafu Rasmi JF, Utangazaji na Uandishi wa Habari Baada ya Kuhudumu Miaka 30. Niko Free Kujiunga Siasa, Nimejiunga CCM na Nitagombea Ubunge

Poa
Wanabodi,
Mimi mwanabody mwenzenu, nilianza kazi ya media tarehe kama ya leo, miaka 30 iliyopita, hivyo ilipofika tarehe hii siku ya leo, ndio siku yangu rasmi ya kustaafu kazi hii ya media, hivyo sasa nimestaafu rasmi uandishi wa habari, utangazaji na pia nimestaafu rasmi jf.

Kustaafu uandishi wa habari na utangazaji ni kufuatia kuhudumu kwa muda mrefu wa kutosha katika tasnia ya habari, kuhudumu fani moja kwa miaka 30 sii haba.

Kufuatia media ethics za misingi mikuu ya fani ya uandishi wa habari, ni truthfulness, Objectivity, Impartiality na Balancing, mwandishi wa habari wa ukweli ili aweze ku practice objectivity na impartiality hapaswi kuwa mwanachama, mfuasi au mshabiki wa chama chochote cha siasa, huwezi kuwa mwanachama wa chama cha siasa halafu ukawa objective au impartial, hivyo mimi siku zote humu jf nilikuwa sina chama, lakini sasa kuanzia leo baada ya kustaafu rasmi, leo hii hii majira ya saa 10:00 asubuhi, nitaelekea pale ofisi ndogo ya CCM Lumumba kwa Polepole kujiunga rasmi CCM na kukabidhiwa kadi yangu ya uanachama wa Chama cha Mapinduzi CCM.

Sababu ya kuamua kujiunga na chama cha Mapinduzi ni sababu kuu 7.
  1. CCM ndicho chama kilicholeta uhuru na ukombozi Tanzania kutoka katika makucha ya wakoloni, wakati huo kikitwa TANU. Hivyo CCM ndicho chama pekee mkombozi wa Watanzania, na ni kufuatia sifa hii, CCM kimepewa hatimiliki ya kuitawala Tanzania milele.
  2. Kufuatia kukubalika sana na kuaminika sana na Watanzania, CCM ndicho chama pekee nchini Tanzania chenye long experience ya uzoefu wa muda mrefu wa uongozi na kuitawala Tanzania, hivyo unajiunga na most experienced party yenye long experience ya uzoefu wa muda mrefu.
  3. CCM kimefanya mengi makubwa, mazuri nchini mwetu tangu tumepata uhuru kwa kuongoza vita dhidi ya maadui umasikini, ujinga, maradhi, rushwa, uzembe, ufisadi, ukoloni mambo leo, unyonyaji, ukupe, ukabaila, ubepari, hadi vita hizi za kisiasa za ubeberu, utandawazi na kuongoza mapambano ya kiuchumi kuipeleka Tanzania kuwa nchi ya viwanda, nchi ya uchumi wa kati kuelekea Tanzania kuwa donor country.
  4. Japo Tanzania ni nchi ya vyama vingi vya siasa, lakini kiukweli kabisa, tunapozungumzia chama haswa cha siasa kwa maana halisi ya chama cha siasa, kwa Tanzania, kiukweli kabisa tuna chama kimoja tuu cha siasa ambacho ni CCM ambacho pia ni chama dola, vyama vingine vyote ni kama vyama vijivyama au vikundi tuu vya watu wanaofanya tuu siasa, vingine ni vyama watu, vingine ni saccos na vingine ni vyama vibaraka tuu na vingine ni vya jina tuu au vyama makaratasi tuu, kule ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa, hivyo in reality Tanzania hatuna any serious opposition party ya kushindana na CCM, hivyo kama kuna mtu yoyote anayeamua sasa kujiunga siasa, chama pekee cha kujiunga nacho ni CCM.
  5. Sababu ya 5 na ya mwisho ni lisemwalo, lipo kama halipo linakuja. Japo mimi ni Msukuma, na jina langu la ubini ni Mayalla, siku zote nimekuwa nikielezwa na Wasukuma wa Ukweli maana ya jina Mayalla kwa Kisukuma ni ukame, drought unaosababisha famine, baa la njaa, lakini siku hizi kuna Wasukuma wa aina nyingi nyingi wengine ni wakuja tuu hivyo hata maana ya jina la Mayalla linabadilika badilika kutegemeana na Msukuma wa wapi. Toka siku ile nilipouliza lile swali Ikulu nikajibiwa kuwa Mayalla kwa Kisukuma ni Njaa, kiukweli kauli nyingine huumba, tangu nilipoitwa Njaa, kauli ile ikaniumbia njaa ya ukweli, hadi jina langu humu na mitaani ninaitwa Pasco Manjaa!. Baada tuu ya swali lile, contracts zangu zote za kampuni yangu ya PPR za serikalini zilisitishwa hivyo njaa ikaanza kunitembelea, tenda za maonyesho ya Saba Saba zikafutwa, tenda za kuandaa kipindi vya elimu kwa umma zikafutwa, ile ofisi yangu jengo la NHC pale Mtaa Mkepu niliokuwa nalipia pango sawa mshahara wa DC nikafunga, nilikuwa na wafanyakazi 20, nikawapunguza 15, tukabaki 5 na kuhamia kwenye kaji chumba jengo la Posta House. Kwa kwa vile mimi ni mwandishi wa habari, baada ya kufungiwa huko kote nikaamua kurejea newsroom kuandika makala za magazeti nako ndio vile tena nikaitwa Dodoma kuhojiwa na Kamati ya Bunge. Kila ninachogusa hakiendi. Sasa limeingia hili janga la Corona, ndio kabisa, hakuna kazi kabisa, ofisi nimefunga niko home sina hili wala lile ndipo likanijia hili wazo la kujiunga CCM na kugombea ubunge ili sasa nikawatumikie watu. Mtaji wa ubunge nimeamua kuuza kila kitu changu, kuanzia nyumba, na kila kitu kilichomo, magari, na container lililosheni mali za thamani kubwa. Kwa kuanzia nahitaji just 15M za hizo items. Nikipitishwa naiuza hiyo nyumba Thamani yake TZS 900. Mila mimi nitauza kwa TZS 500.M. Hii ndio fedha ya kampeni, Msimamizi wa Uchanguzi nimemtengea, 100M kuwapiga pingamizi wagombea wengine wote, 100M ya michango mbalimbali, 100M nakichangia Chama, 100M ya logistics na 100M ya akiba. Politics is science, political science na politics is business, you invest na zinarudi na ku multiply three fold.
  6. Kwa vile aliyenisababishia njaa hii ni Rais Magufuli kuniita njaa, kauli yake imeumba njaa, hivyo sasa najiunga CCM na kugombea ubunge jimbo fulani lililokuwa linashikiliwa na upinzani, kwasababu madhila haya amenisababishia rais Magufuli ambaye sio tuu ni home boy wangu, bali ndiye Mwenyekiti wa CCM, japo kwenye kura za maoni CCM, mimi sitaongoza, lakini siamini kama ataweza kunipita hivi hivi homeboy wake aliyemuita Njaa na kumsababishia njaa, hivyo nitateuliwa kupeperusha bendera ya CCM uchaguzi wa 2020.
  7. Kufuatia Kukubalika sana kwa CCM nchi nzima kulikosababishwa na kasi ya Awamu ya 5, ukiishateuliwa kupeperusha bendera ya CCM, wewe unakuwa tayari ndio Mbunge mtarajiwa unaesubiri kuapishwa tuu na ili kuokoa gharama za kufanya kampeni, kama kawaida ya CCM, uchaguzi Mkuu tutautumia ule wembe wa uchaguzi wa serikali za mitaa. Hivyo nitamsaidia sana rais Magufuli katika eneo la sekta ya habari.
  8. Kufuatia CCM kuwa ni watu wasiopendwa sana humu jf, nimenote wana CCM ambao ni wana jf, akiwemo Paul Makonda, Nape Mnauye, Juliana Shonza, Kigwangala, Prof. Tibaijuka, Mwigulu na wengine, hawachangii tena mijadala humu jf, hivyo na mimi nikiishajiunga tuu na kupokekewa pale CCM Lumumba na Polepole from then nitakuwa sichangii tena mijadala yoyote humu jf kama makada wengine watangulizi wangu. Nitakuwa Facebook, Twitter, Instagram na Snapchat
  9. Hivyo kwa bandiko hili, kwanza nawashukuru sana wana jf kwa Ushirikiano wenu katika kipindi chote cha miaka zaidi ya 10 tuliokuwa wote humu jf, nawaaga kwaherini ya kuonana, japo nitakuwa sichangii ila jf nitaendelea kuitembelea na likes nitakuwa naendelea kuzimwaga ila kiukweli nitawa miss sana na kufuatia uraibu wangu na jf, pia mimi mwenyewe nitateseka sana.
  10. Uamuzi huu wa kujinga CCM, niliufikiria siku nyingi na pia niliwashirikisha wana jf kabla ya kuufikia na hapa walinipa mawazo yao
  11. Je, mtu kujiunga CCM ni ujinga? Je, wana CCM ni wajinga? Je, watanzania wanaoichagua CCM, kila uchao ni wajinga? Its not fair!. - JamiiForums
Nimalizie kwa kuwaomba Ushirikiano wenu, naombani support yenu kwa kuniunga mkono katika safari yangu hii ya kujiunga CCM, kugombea ubunge na kumsaidia rais Magufuli na kuisadia nchi yangu Tanzania.
Paskali
06:00 am

Update: 10:00 am
Saa 4:00 ndio hii, bado sijafanikiwa kumpata Polepole ili kujiunga CCM, hivyo mpaka sasa bado sijastaafu, na jf bado sija acha, naendelea kumfuatilia Polepole kujiunga CCM, siku nikifanikiwa ndipo nitastaafu na nitaaga rasmi kwa ku update uzi huu.

Kwa wale mlionitakia maisha mema ndani ya CCM, asanteni.
Wana CCM mlionikaribisha CCM, asanteni nitakaribia muda utakapowadia.
Kwa wale mliodhania hii ni sikukuu ya leo, poleni, this is for real.
Nawatakia siku njema.
Paskali

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tuacheni utani kabisa, hii habari usipoangalia jina la mleta mada unaweza ukahisi aliyeandika ni Kidukulilo,au Zero IQ.

Kwanza kabisa siamini kama alichoandika paskal anamaanisha, Pili kama anamaanisha basi jamaa yuko kwenye shinikizo sio akili zake kabisa.

Mwisho kabisa naomba nikuulize mkuu Paskal

1. Hoja yako mojawapo umesema ishu ya uandishi wa habari ni transparency etc... kwahiyo unaona uachane na uandishi wa habari na kuegemea CCM, Kwanini usingebaki na fani yako ukaandika habari zako za ukweli na uwazi.

2. Pia umesema Tanzania ni Donor country, Unaweza kututhibitishia hilo au ulikusudia Dona country kwa maana ya ugali?
jamani mnisaidie sasa wakuu, mbona mimi nimemuelewa tofauti kabisa bwana pascal tofauti na wenzangu!!?
pascal ameishia kuinanga ccm kisanii, tu na mwishoni amehitimisha alichomaanisha.
 
Wanabodi,
Mimi mwanabody mwenzenu, nilianza kazi ya media tarehe kama ya leo, miaka 30 iliyopita, hivyo ilipofika tarehe hii siku ya leo, ndio siku yangu rasmi ya kustaafu kazi hii ya media, hivyo sasa nimestaafu rasmi uandishi wa habari, utangazaji na pia nimestaafu rasmi jf.

Kustaafu uandishi wa habari na utangazaji ni kufuatia kuhudumu kwa muda mrefu wa kutosha katika tasnia ya habari, kuhudumu fani moja kwa miaka 30 sii haba.

Kufuatia media ethics za misingi mikuu ya fani ya uandishi wa habari, ni truthfulness, Objectivity, Impartiality na Balancing, mwandishi wa habari wa ukweli ili aweze ku practice objectivity na impartiality hapaswi kuwa mwanachama, mfuasi au mshabiki wa chama chochote cha siasa, huwezi kuwa mwanachama wa chama cha siasa halafu ukawa objective au impartial, hivyo mimi siku zote humu jf nilikuwa sina chama, lakini sasa kuanzia leo baada ya kustaafu rasmi, leo hii hii majira ya saa 10:00 asubuhi, nitaelekea pale ofisi ndogo ya CCM Lumumba kwa Polepole kujiunga rasmi CCM na kukabidhiwa kadi yangu ya uanachama wa Chama cha Mapinduzi CCM.

Sababu ya kuamua kujiunga na chama cha Mapinduzi ni sababu kuu 7.
  1. CCM ndicho chama kilicholeta uhuru na ukombozi Tanzania kutoka katika makucha ya wakoloni, wakati huo kikitwa TANU. Hivyo CCM ndicho chama pekee mkombozi wa Watanzania, na ni kufuatia sifa hii, CCM kimepewa hatimiliki ya kuitawala Tanzania milele.
  2. Kufuatia kukubalika sana na kuaminika sana na Watanzania, CCM ndicho chama pekee nchini Tanzania chenye long experience ya uzoefu wa muda mrefu wa uongozi na kuitawala Tanzania, hivyo unajiunga na most experienced party yenye long experience ya uzoefu wa muda mrefu.
  3. CCM kimefanya mengi makubwa, mazuri nchini mwetu tangu tumepata uhuru kwa kuongoza vita dhidi ya maadui umasikini, ujinga, maradhi, rushwa, uzembe, ufisadi, ukoloni mambo leo, unyonyaji, ukupe, ukabaila, ubepari, hadi vita hizi za kisiasa za ubeberu, utandawazi na kuongoza mapambano ya kiuchumi kuipeleka Tanzania kuwa nchi ya viwanda, nchi ya uchumi wa kati kuelekea Tanzania kuwa donor country.
  4. Japo Tanzania ni nchi ya vyama vingi vya siasa, lakini kiukweli kabisa, tunapozungumzia chama haswa cha siasa kwa maana halisi ya chama cha siasa, kwa Tanzania, kiukweli kabisa tuna chama kimoja tuu cha siasa ambacho ni CCM ambacho pia ni chama dola, vyama vingine vyote ni kama vyama vijivyama au vikundi tuu vya watu wanaofanya tuu siasa, vingine ni vyama watu, vingine ni saccos na vingine ni vyama vibaraka tuu na vingine ni vya jina tuu au vyama makaratasi tuu, kule ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa, hivyo in reality Tanzania hatuna any serious opposition party ya kushindana na CCM, hivyo kama kuna mtu yoyote anayeamua sasa kujiunga siasa, chama pekee cha kujiunga nacho ni CCM.
  5. Sababu ya 5 na ya mwisho ni lisemwalo, lipo kama halipo linakuja. Japo mimi ni Msukuma, na jina langu la ubini ni Mayalla, siku zote nimekuwa nikielezwa na Wasukuma wa Ukweli maana ya jina Mayalla kwa Kisukuma ni ukame, drought unaosababisha famine, baa la njaa, lakini siku hizi kuna Wasukuma wa aina nyingi nyingi wengine ni wakuja tuu hivyo hata maana ya jina la Mayalla linabadilika badilika kutegemeana na Msukuma wa wapi. Toka siku ile nilipouliza lile swali Ikulu nikajibiwa kuwa Mayalla kwa Kisukuma ni Njaa, kiukweli kauli nyingine huumba, tangu nilipoitwa Njaa, kauli ile ikaniumbia njaa ya ukweli, hadi jina langu humu na mitaani ninaitwa Pasco Manjaa!. Baada tuu ya swali lile, contracts zangu zote za kampuni yangu ya PPR za serikalini zilisitishwa hivyo njaa ikaanza kunitembelea, tenda za maonyesho ya Saba Saba zikafutwa, tenda za kuandaa kipindi vya elimu kwa umma zikafutwa, ile ofisi yangu jengo la NHC pale Mtaa Mkepu niliokuwa nalipia pango sawa mshahara wa DC nikafunga, nilikuwa na wafanyakazi 20, nikawapunguza 15, tukabaki 5 na kuhamia kwenye kaji chumba jengo la Posta House. Kwa kwa vile mimi ni mwandishi wa habari, baada ya kufungiwa huko kote nikaamua kurejea newsroom kuandika makala za magazeti nako ndio vile tena nikaitwa Dodoma kuhojiwa na Kamati ya Bunge. Kila ninachogusa hakiendi. Sasa limeingia hili janga la Corona, ndio kabisa, hakuna kazi kabisa, ofisi nimefunga niko home sina hili wala lile ndipo likanijia hili wazo la kujiunga CCM na kugombea ubunge ili sasa nikawatumikie watu. Mtaji wa ubunge nimeamua kuuza kila kitu changu, kuanzia nyumba, na kila kitu kilichomo, magari, na container lililosheni mali za thamani kubwa. Kwa kuanzia nahitaji just 15M za hizo items. Nikipitishwa naiuza hiyo nyumba Thamani yake TZS 900. Mila mimi nitauza kwa TZS 500.M. Hii ndio fedha ya kampeni, Msimamizi wa Uchanguzi nimemtengea, 100M kuwapiga pingamizi wagombea wengine wote, 100M ya michango mbalimbali, 100M nakichangia Chama, 100M ya logistics na 100M ya akiba. Politics is science, political science na politics is business, you invest na zinarudi na ku multiply three fold.
  6. Kwa vile aliyenisababishia njaa hii ni Rais Magufuli kuniita njaa, kauli yake imeumba njaa, hivyo sasa najiunga CCM na kugombea ubunge jimbo fulani lililokuwa linashikiliwa na upinzani, kwasababu madhila haya amenisababishia rais Magufuli ambaye sio tuu ni home boy wangu, bali ndiye Mwenyekiti wa CCM, japo kwenye kura za maoni CCM, mimi sitaongoza, lakini siamini kama ataweza kunipita hivi hivi homeboy wake aliyemuita Njaa na kumsababishia njaa, hivyo nitateuliwa kupeperusha bendera ya CCM uchaguzi wa 2020.
  7. Kufuatia Kukubalika sana kwa CCM nchi nzima kulikosababishwa na kasi ya Awamu ya 5, ukiishateuliwa kupeperusha bendera ya CCM, wewe unakuwa tayari ndio Mbunge mtarajiwa unaesubiri kuapishwa tuu na ili kuokoa gharama za kufanya kampeni, kama kawaida ya CCM, uchaguzi Mkuu tutautumia ule wembe wa uchaguzi wa serikali za mitaa. Hivyo nitamsaidia sana rais Magufuli katika eneo la sekta ya habari.
  8. Kufuatia CCM kuwa ni watu wasiopendwa sana humu jf, nimenote wana CCM ambao ni wana jf, akiwemo Paul Makonda, Nape Mnauye, Juliana Shonza, Kigwangala, Prof. Tibaijuka, Mwigulu na wengine, hawachangii tena mijadala humu jf, hivyo na mimi nikiishajiunga tuu na kupokekewa pale CCM Lumumba na Polepole from then nitakuwa sichangii tena mijadala yoyote humu jf kama makada wengine watangulizi wangu. Nitakuwa Facebook, Twitter, Instagram na Snapchat
  9. Hivyo kwa bandiko hili, kwanza nawashukuru sana wana jf kwa Ushirikiano wenu katika kipindi chote cha miaka zaidi ya 10 tuliokuwa wote humu jf, nawaaga kwaherini ya kuonana, japo nitakuwa sichangii ila jf nitaendelea kuitembelea na likes nitakuwa naendelea kuzimwaga ila kiukweli nitawa miss sana na kufuatia uraibu wangu na jf, pia mimi mwenyewe nitateseka sana.
  10. Uamuzi huu wa kujinga CCM, niliufikiria siku nyingi na pia niliwashirikisha wana jf kabla ya kuufikia na hapa walinipa mawazo yao
  11. Je, mtu kujiunga CCM ni ujinga? Je, wana CCM ni wajinga? Je, watanzania wanaoichagua CCM, kila uchao ni wajinga? Its not fair!. - JamiiForums
Nimalizie kwa kuwaomba Ushirikiano wenu, naombani support yenu kwa kuniunga mkono katika safari yangu hii ya kujiunga CCM, kugombea ubunge na kumsaidia rais Magufuli na kuisadia nchi yangu Tanzania.
Paskali
06:00 am

Update: 10:00 am
Saa 4:00 ndio hii, bado sijafanikiwa kumpata Polepole ili kujiunga CCM, hivyo mpaka sasa bado sijastaafu, na jf bado sija acha, naendelea kumfuatilia Polepole kujiunga CCM, siku nikifanikiwa ndipo nitastaafu na nitaaga rasmi kwa ku update uzi huu.

Kwa wale mlionitakia maisha mema ndani ya CCM, asanteni.
Wana CCM mlionikaribisha CCM, asanteni nitakaribia muda utakapowadia.
Kwa wale mliodhania hii ni sikukuu ya leo, poleni, this is for real.
Nawatakia siku njema.
Paskali
Wait! WooooWooooWhat?!
Kwani kuwa mbunge kunakuzuia nini kuendelea na Uandishi Uporojo na mengineyo!
All the Best Mkuu!
 
Hata hivyo Covid 19 ishapata dawa rasmi na magonjwa wote wameshaanza kutumia na nusu wameshapona kabisa.
Duh..!. Kumbe Corona imeishapata tiba rasmi na watu nusu wameisha pona!. Hii ni taarifa nzuri hivyo basi sasa naendelea kumtafuta Polepole taratibu huku humu jf nikiwa bado nipo nipo tuu.
P
 
Nahisi saikoloji yako ni ndogo sana ulichokiandika sawa na mtoto darasa LA nne LA zamani. Sasa sielewi kama umesomea vyuo vya kata kama vipo, au hujasoma kabisa.
Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu Magashashi, mimi sio nimesomea vyuo vya kata, bali sijasoma kabisa, niliishia darasa la 7 tuu la enzi za UPE, hivyo uko vey right, saikoloji yangu ni ndogo sana sawa na mtoto darasa LA nne LA zamani.

Watu humu tunatofautiana viwango na uwezo wa uelewa, kama mimi nimeishia la 7 tuu, halafu wewe kiwango chako cha uelewa ni kiwango cha darasa la 4 la zamani, ukisoma andiko hata la professor wa Ph.D, kite utakachoweza kukielewa ni kile tuu cha kiwango chako cha uelewa. Hivyo hata hii mada yangu ya darasa la 7, mtu wa kiwango cha uelewa cha darasa la nne, ataelewa kwa kiwango chake. Asante kwa kunielewa kwa kiwango hicho. Mambo ya viwango haya ni kila mtu na kiwango chake, cha muhimu ni uwezo wa kusoma na kuelewa, ukiwa ni mtu wa kiwango cha uelewa wa darasa la nne la zamani, ukakutana na mada ya kiwango cha uelewa cha darasa la saba kama hii, lazima utatoka kapa.
Pole.
P
 
Jana yote nilikuwa busy kiasi sijuweza kuingia JF na kuiona thread hii ya mzee mwenzangu Pascal Mayalla.
Hakika imeandikwa kwa ufundi mno na mjadala wake ulipaswa uishie Jana SAA 4 asubuhi au uchukue sura mpya sio hii ya sasa.
Hapa hakuna cha ubunge wala nini, hapa ni Polepole na ccm wamegongwa za USO mchana kweupe na huyu waliye msababishia "NJAA".
Na kwa wale wanao mhukumu Pasco kwa kuuliza swali mkidhani ni statement msije mkafanya hivyo kwenye hilo swali na 11, " jee kujiunga ccm ni ujinga?"
Ujumbe wa thread hii ni mkubwa sana kuliko wengi wafikiviavyo, nitarudi baadae kuujadili.
Muda huu naona mama Yeyoo kama vile kuna jambo anahitaji naweka simu pembeni kwanza. Naweza kuchelewa hapa hata mazoezi ya SAA 12!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Watu huwa wanapata shida sana kumuelewa huyu jamaa..nashkuru huwa namwelewa sana na kila mada anayoianzisha humu ukiisoma kwa kutafakari mstari kwa mstari unaweza ukajikuta unacheka maana huwa anafikisha ujumbe kwa style ambayo si rahisi akili ndogo kumwelewa!
Bandiko la Paskal hata kama ni la utani lakn ndani yake kuna kuwa na ujumbe mzito sana! Hata bible ukiisoma utaelewa maandishi yanasomekaje lakn ni ngumu kuelewa kilichokusudiwa! Hongera sana mkuu kwa hakika haya mabandiko yako yanadhihirisha ubobevu wako na unguli kwenye sanaa hii ya uandishi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
style ambayo si rahisi akili ndogo kumwelewa!
1585794468520.png
 
Mkuu Pascal Mayalla, nikuulize, Kwani kujiunga na chama cha siasa ni lazima uache taaluma yako uliyosomea? Maana umeunganisha mambo mawili kwa pamoja ni kama yana mahusiano.

2. Je umejihakikishia 100% kuwa utapata huo ubunge hata kutangaza kuacha mbachao wako wa miaka 30?

3. Kwani kuwa Mbunge, ni haramu kuwa member wa JF? Mbona wengine wapo humu?

4. Kwa hiyo huduma yako ya elimu kwa umma inakuwa haina tena maana kwa vile unautaka ubunge? Au baada ya ubunge?

5. Je huoni mchango wa JF ktk kukupa wewe jina? Au unaona kuendelea kuwa mdau wa JF itakukosesha ubunge?

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu Nzwangendaba
  1. Msingi wa uandishi wa habari ni truthfulness, objectivity, impartiality na balancing. Ili mwandishi kuyatimiza hayo hupaswi kuwa member, mfuasi au mshabiki wa chama chochote na hivyo ndivyo mimi nilivyokuwa kipindi chote cha miaka 30 niliyohudumu kwenye sekta ya habari. Ukiisha jiunga na chama chochote cha siasa, lazima sasa uta take sides, mfano hakuna mwana CCM CCM yoyote anaweza kukubali kusema ukweli kuwa CCM ndio chanzo cha umasikini wa taifa hili uliosababishwa na sera mbovu zilizochochea rushwa, uhujumu na ufisadi karibu wote. Lazima niitetee CCM kwa kutousema ukweli kama huo. Huwezi kuwa objective wakati wewe ni sehemu ya tatizo, huwezi kuwa impartial wakati tayari ume take side, huwezi ku balance haki bin haki, lazima utaegemea upande wako. Lakini kufuatia dalili za kauli na matendo ya CCM ya Magufuli na Dr. Bashiru Ally Kakurwa, wanaonyesha kuirudisha ile CCM ya Nyerere ya tujisahihishe hivyo hii CCM ninayo azimia kujiunga nayo ni CCM mpya.
  2. Sijajihakikishia 100% ndio maana ninafanya maandalizi kwa phrases. Phase 1 inahitaji just TZS 15M za maandalizi. Jimbo ninalolimendea ni jimbo very lucrative hivyo ushindani wa jimbo hilo ndani ya CCM ni mkubwa. Wataibuka vigogo wa CCM wenye vipochi vinene. Kwa vile mimi najijua uwezo wangu wa kujenga hoja ni mkubwa ila uwezo wangu wa kiuchumi ni limited, kupitishwa kutategemea tunashindana na wakina nani na wana uwezo gani kujenga hoja na nguvu gani ya Kiuchumi, hivyo hapa karata kubwa ni ya kumtumia home boy wangu aliyeniita njaa na kunisababishia njaa itambidi anibebe kunifidia njaa alionisababishia. Nikipitishwa ndio nakuja phase 2 ya kuuza nyumba to secure TZS 500m za kampeni. Kwa political dynamics za siasa za Tanzania kwa sasa, mgombea wa CCM ndiye mshindi kila kona isipokua jimbo moja huku bara, majimbo mawili Zanzibar na majimbo yote Pemba. Ndio maana niliwahi kueleza haya Trend Reading: Wanaohamia CCM wasibezwe! Wanaona mbali, 2020 Majimbo yote kurejeshwa. Je tunarejea nchi ya Chama kimoja? - JamiiForums
  3. Kuwa Mbunge sio haramu kuwa jf . Kwenye andishi langu nimesema kuwa Mbunge ni kuwatumikia wananchi, lakini kwa Profile yangu, nitamsaidia sana Magufuli, kiukweli kabisa katika sekta yangu timu ya Magufuli iliyopo wanajitahidi sana lakini bado. Ni katika muktadha huo ndio nitasita kuchangia jf kama watangulizi wangu. Nitolee mfano wana jf watatu hawa niliowazungumzia hapa Baraza Jipya: Pongezi kwa JamiiForums, WanaJF watatu(VERIFIED) waukwaa uwaziri - JamiiForums hawa jamaa walikuwa wachangia wazuri humu, baada ya kuukwaa uliwaona tena humu?. Juzi kati baada ya ndio nilimuona mmoja wao akirejea kujibu hoja ili tuu kujiokoa na kuti kavu kule jimboni kwake, na tulipombana kwa maswali magumu bila kuacha loose ends alikimbia jumla!. Hivyo na mimi nafauata tuu nyanyo. Angalia kina Juliana Shonza, walikuwa very active members baada tuu ya kuukwaa.. kimya. Mbunge pekee aliyesemama na jf ni Zitto, hivyo sijui kama hawa wa CCM wanakatazwa au laa, nikaamua niage mapema tuu.
  4. Utoaji elimu kwa umma utaendelea lakini sasa sio kupitia mitandao ya kijamii bali sasa ni kupitia mainstream media na vyombo rasmi kama mule Bungeni. Baada ya uelimishaji umma kwa miaka 30 kupitia media, sasa muelimishaji umma anakuwa ameingia jikoni kwenye vyombo vya maamuzi na utekelezaji, hivyo sasa nakuwa ni mpishi kabisa wa elimu kwa umma.
  5. Hili la jf kunipa jina ni kweli, kuna wengi wanaitumia jf kama ngazi tuu ya kuikanyaga na kupandia juu, wakishafika huko juu, hawana tena time na ngazi, kama lilivyo dekio, . Siku wakianguka ndipo huikumbuka ngazi, na siku kukitokea ajali ya kunwagika soda mbele ya wageni ndipo dekio hukumbukwa. Kwa upande wangu, kwa muda mrefu kwa muda mrefu nililazimika kuishi double life, kwa vile mimi huwa ninafanya Radio, TV Programs na public appearances, I had to live double life ya Pasco wa JF ambaye ni very critical na Pascal Mayalla ambaye ni verified member, bringing the two together into one was a challenge. Hivyo kwenye Programs zangu nikipata fursa huwa naichomekea jf, nikimpata Max namwalika, nikipata fursa ya kuipaisha jf, naipaisha. Kwa vile mimi siko ndani ya CCM kujua ni nini kinachowafanya members wana CCM kuitumia jf kama ngazi tuu ya kupandio kule juu lakini wakiisha fika, jf hugeuzwa dekio, sijui kama wana katazwa, hivyo naitumia formula ya "when in Rome, do as the Romans does", ndio maana bado naomba support ya wana jf kunisupport kujiunga CCM, kunipigania niingie Bungeni, you never know usikute hao waliopo ni uoga wao tuu kutoendelea kuitumia jf baada ya kuula, lakini mimi nitakapoingia, tukajikuta naibeba jf na kuiingiza kwenye hansard and you never know tukajikuta tunaipandisha jf to unimaginable heights kwa kuingiza jf hadi ndani kabisa kule kunako. Just pray for support me in joining CCM and persue ubunge
P
 
Haaa Mayalla bwana,umesema una sababu kuu 7 sasa umeweka zaidi ya 7 au zingine ni ni kuu saidizi?
Ila sababu yako ya tano imejitosheleza .bilashaka bado hujampata polepole hivyo bado hujastafu rasmiiiiiiiiii
 
jamani viongozi wa JF hakikisheni pascal anakaa mbali kabisa na JF servers, siku pascal akipata access ya server za JF wengi wetu tutakwisha, wasiojulikana watatumaliza…………………ukisikia mtu anatamani kuhamia CCM kaa ukijua huyo siyo mwezio tena, tena mtenge kabisaa
 
Wanabodi,
Mimi mwanabody mwenzenu, nilianza kazi ya media tarehe kama ya leo, miaka 30 iliyopita, hivyo ilipofika tarehe hii siku ya leo, ndio siku yangu rasmi ya kustaafu kazi hii ya media, hivyo sasa nikiisha jiunga rasmi CCM, automatically nitakuwa nimestaafu rasmi uandishi wa habari, utangazaji na pia nimestaafu rasmi jf.

Kustaafu uandishi wa habari na utangazaji ni kufuatia kuhudumu kwa muda mrefu wa kutosha katika tasnia ya habari, kuhudumu fani moja kwa miaka 30 sii haba.

Kufuatia media ethics za misingi mikuu ya fani ya uandishi wa habari, ni truthfulness, Objectivity, Impartiality na Balancing, mwandishi wa habari wa ukweli ili aweze ku practice objectivity na impartiality hapaswi kuwa mwanachama, mfuasi au mshabiki wa chama chochote cha siasa, huwezi kuwa mwanachama wa chama cha siasa halafu ukawa objective au impartial, hivyo mimi siku zote humu jf nilikuwa sina chama, lakini sasa kuanzia leo baada ya kustaafu rasmi, leo hii hii majira ya saa 10:00 asubuhi, nitaelekea pale ofisi ndogo ya CCM Lumumba kwa Polepole kujiunga rasmi CCM na kukabidhiwa kadi yangu ya uanachama wa Chama cha Mapinduzi CCM.

Sababu ya kuamua kujiunga na chama cha Mapinduzi ni sababu kuu 7.
  1. CCM ndicho chama kilicholeta uhuru na ukombozi Tanzania kutoka katika makucha ya wakoloni, wakati huo kikitwa TANU. Hivyo CCM ndicho chama pekee mkombozi wa Watanzania, na ni kufuatia sifa hii, CCM kimepewa hatimiliki ya kuitawala Tanzania milele.
  2. Kufuatia kukubalika sana na kuaminika sana na Watanzania, CCM ndicho chama pekee nchini Tanzania chenye long experience ya uzoefu wa muda mrefu wa uongozi na kuitawala Tanzania, hivyo unajiunga na most experienced party yenye long experience ya uzoefu wa muda mrefu.
  3. CCM kimefanya mengi makubwa, mazuri nchini mwetu tangu tumepata uhuru kwa kuongoza vita dhidi ya maadui umasikini, ujinga, maradhi, rushwa, uzembe, ufisadi, ukoloni mambo leo, unyonyaji, ukupe, ukabaila, ubepari, hadi vita hizi za kisiasa za ubeberu, utandawazi na kuongoza mapambano ya kiuchumi kuipeleka Tanzania kuwa nchi ya viwanda, nchi ya uchumi wa kati kuelekea Tanzania kuwa donor country.
  4. Japo Tanzania ni nchi ya vyama vingi vya siasa, lakini kiukweli kabisa, tunapozungumzia chama haswa cha siasa kwa maana halisi ya chama cha siasa, kwa Tanzania, kiukweli kabisa tuna chama kimoja tuu cha siasa ambacho ni CCM ambacho pia ni chama dola, vyama vingine vyote ni kama vyama vijivyama au vikundi tuu vya watu wanaofanya tuu siasa, vingine ni vyama watu, vingine ni saccos na vingine ni vyama vibaraka tuu na vingine ni vya jina tuu au vyama makaratasi tuu, kule ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa, hivyo in reality Tanzania hatuna any serious opposition party ya kushindana na CCM, hivyo kama kuna mtu yoyote anayeamua sasa kujiunga siasa, chama pekee cha kujiunga nacho ni CCM.
  5. Sababu ya 5 na ya mwisho ni lisemwalo, lipo kama halipo linakuja. Japo mimi ni Msukuma, na jina langu la ubini ni Mayalla, siku zote nimekuwa nikielezwa na Wasukuma wa Ukweli maana ya jina Mayalla kwa Kisukuma ni ukame, drought unaosababisha famine, baa la njaa, lakini siku hizi kuna Wasukuma wa aina nyingi nyingi wengine ni wakuja tuu hivyo hata maana ya jina la Mayalla linabadilika badilika kutegemeana na Msukuma wa wapi. Toka siku ile nilipouliza lile swali Ikulu nikajibiwa kuwa Mayalla kwa Kisukuma ni Njaa, kiukweli kauli nyingine huumba, tangu nilipoitwa Njaa, kauli ile ikaniumbia njaa ya ukweli, hadi jina langu humu na mitaani ninaitwa Pasco Manjaa!. Baada tuu ya swali lile, contracts zangu zote za kampuni yangu ya PPR za serikalini zilisitishwa hivyo njaa ikaanza kunitembelea, tenda za maonyesho ya Saba Saba zikafutwa, tenda za kuandaa kipindi vya elimu kwa umma zikafutwa, ile ofisi yangu jengo la NHC pale Mtaa Mkepu niliokuwa nalipia pango sawa mshahara wa DC nikafunga, nilikuwa na wafanyakazi 20, nikawapunguza 15, tukabaki 5 na kuhamia kwenye kaji chumba jengo la Posta House. Kwa kwa vile mimi ni mwandishi wa habari, baada ya kufungiwa huko kote nikaamua kurejea newsroom kuandika makala za magazeti nako ndio vile tena nikaitwa Dodoma kuhojiwa na Kamati ya Bunge. Kila ninachogusa hakiendi. Sasa limeingia hili janga la Corona, ndio kabisa, hakuna kazi kabisa, ofisi nimefunga niko home sina hili wala lile ndipo likanijia hili wazo la kujiunga CCM na kugombea ubunge ili sasa nikawatumikie watu. Kufuatia kuweko kwa CCM mbili, CCM ya Nyerere chini ya Magufuli na Dr. Bashiru Ally ambayo sifa ya kuteuliwa kugombea ni uwezo wako wa uongozi na utumishi wa umma, na CCM Mafisadi ambapo sifa ya kuteuliwa ni urefu wa mkono wako, una weza kumwaga fwedha kiasi gani kununua uongozi. Hivyo hata kwa CCM ya Nyerere, uteuzi wa ngazi ya chini lazima us spend kidogo japo maji ya kunywa tuu kwenye vikao vya chini vya uteuzi ngazi ya kata na tarafa. Hivyo mimi najiandaa for both, CCM safi ya Nyerere chini ya Magufuli na Bashiru, na CCM Mafisadi ya "mkono mtupu haulambwi" hivyo najiandaa kwa hali na mali. Mtaji wa ubunge nimeamua kuuza kila kitu changu, kuanzia nyumba, na kila kitu kilichomo, magari, na container lililosheni mali za thamani kubwa. Kwa kuanzia nahitaji just 15M za hizo items. Nikipitishwa ndipo nausoma upepo, kama mwelekeo ni CCM mafisadi, then naiuza hiyo nyumba Thamani yake TZS 900m ila mimi nitauza kwa TZS 500m only. Hii ndio fedha ya kampeni, Msimamizi wa Uchanguzi nimemtengea, 100M kuwapiga pingamizi wagombea wengine wote ili nipite bila kupigwa. 100M ya michango mbalimbali, 100M nakichangia Chama, 100M ya logistics na 100M ya akiba. Politics is science, political science na politics is business, you invest in politics na zinarudi na ku multiply three folds, hii ya zinarudije ni masuala ya ndani, not for public consumption.
  6. Kwa vile aliyenisababishia njaa hii ni Rais Magufuli kuniita njaa, kauli yake imeumba njaa, hivyo sasa najiunga CCM na kugombea ubunge jimbo fulani lililokuwa linashikiliwa na upinzani, kwasababu madhila haya amenisababishia rais Magufuli ambaye sio tuu ni home boy wangu, bali pia ndiye Mwenyekiti wa CCM, japo kwenye kura za maoni CCM, mimi sitaongoza, lakini siamini kama ataweza kunipita hivi hivi homeboy wake aliyemuita Njaa na kumsababishia njaa, hivyo itambidi tuu anibebe na nitateuliwa kwa kubebwa ili kupeperusha bendera ya CCM uchaguzi wa 2020. Ila ikitokea kuna mgombea more able kuliko mimi, akipitishwa nitakubali kushindwa na mimi ndio nitakuwa campaign manager wake tunalirejesha jimbo letu muhimu CCM.
  7. Kufuatia Kukubalika sana kwa CCM nchi nzima kulikosababishwa na kasi ya Awamu ya 5, ukiishateuliwa kupeperusha bendera ya CCM, wewe unakuwa tayari ndio Mbunge mtarajiwa unaesubiri tuu kuapishwa tuu na ili kuokoa gharama za kufanya kampeni, kama kawaida ya CCM, uchaguzi Mkuu tutautumia wembe ule ule wa uchaguzi wa serikali za mitaa. Hivyo nitamsaidia sana rais Magufuli katika eneo la sekta ya habari ambayo kiukweli... naomba hapa nisiseme, niishie hapa.
  8. Kufuatia CCM kuwa ni watu wasiopendwa sana humu jf, nimenote wana CCM ambao ni wana jf, akiwemo Paul Makonda, Nape Mnauye, Juliana Shonza, Kigwangala, Prof. Tibaijuka, Mwigulu na wengine, wakiisha ula tuu, huwa hawachangii tena mijadala humu jf, hivyo na mimi nikiishajiunga tuu na kupokekewa pale CCM Lumumba na Polepole from then nitakuwa sichangii tena mijadala yoyote humu jf kama makada wengine watangulizi wangu. Nitakuwa Facebook, Twitter, Instagram na Snapchat, ili nikiwa ndani ya CCM ndipo nitajua ni nini huwa kinatokea kwa watu kuitumia jf kama ngazi tuu ya kupandia, lakini wakiishafanikiwa na kufika juu, jf wai bull shit kama dekio.
  9. Hivyo kwa bandiko hili, kwanza nawashukuru sana wana jf kwa Ushirikiano wenu katika kipindi chote cha miaka zaidi ya 10 tuliokuwa wote humu jf, nikifanikiwa kujiunga CCM, nawaaga rasmi kwaherini ya kuonana, japo nitakuwa sichangii actively humu jf nitaendelea kuitembelea na likes nitakuwa naendelea kuzimwaga ila kiukweli nitawa miss sana na kufuatia uraibu wangu na jf, pia mimi mwenyewe nitateseka sana, lakini ikotokea kuwemo CCM haukatazwi kuchangia jf, then niombeeni na mnisupport kujiunga CCM ili tuwe na wana jf waandamizi ambao ni makada safi wa chama cha Mapinduzi hivyo kuipeleka JF Bungeni.
  10. Uamuzi huu wa kujiunga CCM, niliufikiria siku nyingi na pia niliwashirikisha wana jf kabla ya kuufikia na hapa walinipa mawazo yao Je, mtu kujiunga CCM ni ujinga? Je, wana CCM ni wajinga? Je, watanzania wanaoichagua CCM, kila uchao ni wajinga? Its not fair!. - JamiiForums
Nimalizie kwa kuwaomba ushirikiano wenu, wana jf wenzangu wote, naombani support yenu kwa kuniunga mkono mwana jf mwenze katika safari yangu hii mpya ya kujiunga CCM, kuwa kada wa Chama cha Mapinduzi kumuunga mkono rais Magufuli na kugombea ubunge kwa lengo sio tuu la kuwatumikia wananchi wa Tanzania kama Mbunge wao, bali pia kuonyesha uzalendo wangu kwa kumsaidia rais Magufuli na seikali yake na kuisadia nchi yangu na taifa langu Tanzania.
Mungu Nisaidie.
Paskali
06:00 am

Update: 10:00 am
Saa 4:00 ndio hii, bado sijafanikiwa kumpata Polepole ili kujiunga CCM, hivyo mpaka sasa bado sijastaafu, na humu jf bado nipo nipo, sijaacha, naendelea kumfuatilia Polepole ili kujiunga CCM, siku nikifanikiwa kujiunga CCM, nitawajulisha kupitia uzi huu, na baada ya kujiunga rasmi CCM, ndipo nitastaafu na nitaaga rasmi kwa ku update uzi huu.

Kwa wale mlionitakia maisha mema ndani ya CCM, asanteni.
Wana CCM mlionikaribisha CCM, asanteni nitakaribia muda utakapowadia.
Kwa wale mliodhania hii ni sikukuu ya leo, poleni, this is for real.
Nawatakia siku njema.
Paskali
Kaka unajua kuandika yaani makala zako huwa nazisoma sichoki,yaani navutiwa kusoma zaidi,unanikumbusha makala za miaka ya 2000 mwanzoni za Ndemacha na kaka yake kama sijakosea majina wakiandika tokea UK
 
Brother Pascal Mayalla nimesoma badiko, kuna wakati nikajikuta nacheka kwa nguvu, sijui kwa nini.Ila kwakweli wewe ni bonge la Bonge la muandishi, ninashukuru kubahatika kusoma maandiko yako.

Tatizo umeandika vitu vingi sana vya ukweli kutoka moyoni kwako, umesahau kuwa vitu vingine vya ukweli utakiwi kuvitoa moyoni inabidi wakati mwingine vibaki tu moyoni ikibidi tu ufe navyo.

Mchanganua wa ile M500 ya nyumba utakayo uza ndio umeniacha hoi kabisa.

umetumia falsafa ya juu sana kwenye huu uzi.
 
Back
Top Bottom