Mujumba
JF-Expert Member
- Jan 20, 2011
- 853
- 306
safari ya kwenda loliondo ilinipa nafasi ya kufika jimboni Karatu na kujionea mambo mengi yaliyonivunja moyo na kunikatisha tamaa kabisa juu ya uwezo wa Dr Slaa! nilikutana na msururu wa kinamama wakiwa na ndoo wakienda sehemu za mbali kutafuta maji,pia kwa macho yangu niliweza kuona foleni ndefu sana za maji hii ilithibitisha kuwa kuna shida kubwa ya maji,pia niliweza kuona watoto wengi wa shule wakiwa hawana viatu miguuni,pia wananchi kwa ujumla walionekana wamekata tamaa ya maisha na nyuso zao zilionyesha hivyo! nikajiuliza hili si ndio jimbo la bwana slaa ambalo aliltumikia kwa miaka mingi,sasa kwanini alishindwa kutatua hizi kero za wananchi?? miaka yote alikuwa anafanya nini kama mbunge? kama jimbo dogo hili limemshinda je nchi angeiweza? nilijiuliza maswali mengi sana ambayo nilishindwa kuyapatia majibu kabisa
(Hii ni email niliyofowadiwa na rafiki yangu Mussa Mosha anayemiliki kampuni ya utalii pale Arusha na mfuasi mzuri wa chadema)
(Hii ni email niliyofowadiwa na rafiki yangu Mussa Mosha anayemiliki kampuni ya utalii pale Arusha na mfuasi mzuri wa chadema)