MamaSamia2025
JF-Expert Member
- Mar 29, 2012
- 10,224
- 22,306
Hapa nchini kumekuwa na fikra kwamba kaskazini kote ni ngome imara ya upinzani kwa majimbo karibu yote ila kwa tunaofahamu vizuri hiyo kanda tuko tofauti kidogo. Ni kweli wapinzani wamesimika mizizi kwenye baadhi ya majimbo ila mengi hayako imara kusimama na upinzani kwenye chaguzi zote.
Kwa mfano watu wengi wanaweza dhani kwamba jimbo la Arusha mjini ni ngome imara ya upinzani na labda huenda CCM ndo inaongoza kwa mara ya kwanza. Kihistoria Arusha mjini ni jimbo la CCM kwa muda mrefu sana hadi alipojitokeza Lema mwaka 2010. Mwaka 1995 lilishawahi kuwakilishwa na Mh Makongoro Nyerere. Na baada ya hapo akafuatia Felix Mrema hadi 2010. Jimbo la Hai pia limekuwa likipokezana CHADEMA na CCM tangu 1995. Angalau jimbo la Vunjo ndo limeonyesha kuwa kambi ya upinzani kwa muda mrefu chini ya Lyatonga na baadae Mbatia.
Kwa kaskazini ni jimbo la Karatu peke yake halijawahi kupokezana na CCM tangu 1995 hadi 2020. Watu wa hili jimbo ni wabishi na ni wapinzani kwelikweli wakishaamua. Walisimama na Dr Slaa tangu 1995 hadi 2010. Na 2010 -2020 bado wakachagua upinzani. Uchaguzi wa 2020 hauna haja ya kuuongelea kwasababu haukuwa huru wala wa haki kuanzia kwenye kura za maoni hadi kwenye uchaguzi wenyewe. Kihistoria wananchi wa Karatu kisiasa wako mbele sana ya muda. Mwaka 1961 wakati Karatu ikiwa kwenye jimbo la Mbulu walishiriki kikamilifu kumkataa mgombea wa TANU Chifu Dodo na kumchagua mgombea binafsi Chifu Sarwatt.. baada ya ule uchaguzi ndo mambo ya mgombea binafsi yakafutwa.
Pamoja na kuwa wapinzani ila wananchi wa Karatu mwanzoni hawakuwa na tatizo na CCM hadi pale jina la mgombea waliyemtaka (Dkt. Slaa) kukatwa Dodoma na kurudishiwa jina la mgombea wasiyemtaka. Kwa hasira wakamchagua Dr Slaa aliyeamua kuhamia CHADEMA huku akimsapoti mgombea urais kwa tiketi ya NCCR Mageuzi hayati Mrema mwaka 1995.
Nimeandika huu uzi kukikumbusha chama kuwa makini sana kwenye kuteua mgombea wa CCM anayekubalika Karatu ili kuepusha jimbo kuangukia mikononi mwa wapinzani. Nashauri CCM wamsimamishe Dkt. Slaa kwasababu yule mzee ni kipenzi cha wanaKaratu. Hakuna mwenye ubavu wa kisiasa kumzidi Dr Slaa pale Karatu.
Kwa mfano watu wengi wanaweza dhani kwamba jimbo la Arusha mjini ni ngome imara ya upinzani na labda huenda CCM ndo inaongoza kwa mara ya kwanza. Kihistoria Arusha mjini ni jimbo la CCM kwa muda mrefu sana hadi alipojitokeza Lema mwaka 2010. Mwaka 1995 lilishawahi kuwakilishwa na Mh Makongoro Nyerere. Na baada ya hapo akafuatia Felix Mrema hadi 2010. Jimbo la Hai pia limekuwa likipokezana CHADEMA na CCM tangu 1995. Angalau jimbo la Vunjo ndo limeonyesha kuwa kambi ya upinzani kwa muda mrefu chini ya Lyatonga na baadae Mbatia.
Kwa kaskazini ni jimbo la Karatu peke yake halijawahi kupokezana na CCM tangu 1995 hadi 2020. Watu wa hili jimbo ni wabishi na ni wapinzani kwelikweli wakishaamua. Walisimama na Dr Slaa tangu 1995 hadi 2010. Na 2010 -2020 bado wakachagua upinzani. Uchaguzi wa 2020 hauna haja ya kuuongelea kwasababu haukuwa huru wala wa haki kuanzia kwenye kura za maoni hadi kwenye uchaguzi wenyewe. Kihistoria wananchi wa Karatu kisiasa wako mbele sana ya muda. Mwaka 1961 wakati Karatu ikiwa kwenye jimbo la Mbulu walishiriki kikamilifu kumkataa mgombea wa TANU Chifu Dodo na kumchagua mgombea binafsi Chifu Sarwatt.. baada ya ule uchaguzi ndo mambo ya mgombea binafsi yakafutwa.
Pamoja na kuwa wapinzani ila wananchi wa Karatu mwanzoni hawakuwa na tatizo na CCM hadi pale jina la mgombea waliyemtaka (Dkt. Slaa) kukatwa Dodoma na kurudishiwa jina la mgombea wasiyemtaka. Kwa hasira wakamchagua Dr Slaa aliyeamua kuhamia CHADEMA huku akimsapoti mgombea urais kwa tiketi ya NCCR Mageuzi hayati Mrema mwaka 1995.
Nimeandika huu uzi kukikumbusha chama kuwa makini sana kwenye kuteua mgombea wa CCM anayekubalika Karatu ili kuepusha jimbo kuangukia mikononi mwa wapinzani. Nashauri CCM wamsimamishe Dkt. Slaa kwasababu yule mzee ni kipenzi cha wanaKaratu. Hakuna mwenye ubavu wa kisiasa kumzidi Dr Slaa pale Karatu.