Nilivyomchangia pesa ya harusi mpenzi wangu bila kujua

ankol

JF-Expert Member
Aug 21, 2012
2,113
3,484
Daah ama kweli ule usemi wa fear woman una ukweli.

Nilikua na mpenzi wangu mashallaah navimba naye kitaa. Mtoto kachanganyia mama mmoroni baba mbongo mweupeee. Full kuvimba naye mtaani kama hamo vile.

Siku zinakatika kila siku ananihimiza nimwoe wakati mi mpango sina, (nakula kisela).

Si nilikua bado najitafuta?

Basi bwana kumbe wakati mimi naremba kuna watu wakaenda mazima kwa mzee wake wakamsomesha mzee akaelewa.

Binti akashinikizwa na mzee wake aolewe na mrangirangi mwenzake mi mbara sitakiwi.

Daah dame akawa yuko na wakati mgumu akaaga anaenda kutembelea ndugu kumbe kaja kwangu magetoni full na kibegi.

Hakunichana wala nini yeye aliuliza tu ankoli utanioa lini? Mi nachulia poa tu swali lake la siku zote.

'Ankoli niko siriaz twende nyumbani at least wakuone'.

Basi buana sikutilia maanani.

Akaona hapa hamna muoaji hapa. Alivyosepa akapiga kimya kama wiki hivi kumbe alimkubali yule ami wa kipemba. Vikao vikaendelea.

Ikakata mwezi mara simu yake ikaita kupokea akaniambia Ana shida kubwa anahitaji kiasi cha pesa urgent. Mzee baba nikatuma 2laki.

Kumbe kesho yake ndio anaolewa nahisi budget iliyumba ndio akaamua anichangishe.

Kesho yake navigation simu anapokea mtu mwingine. Kwa ubabe nangaka' namtaka mwenye simu' . Yule mmama akajibu mmoroni leo anaolewa hakukwambia kwani?

Daah nilihisi kukata moto vile. Nikajikaza 'mwambie ndoa njema'.

Niliumia sana nikakumbuka ni jana tu nilimtumia pesa daah Wanamake nyie!
 
Pole sana... Hua nikiwaona wazee wanasema Wana experience na mapenzi nakaa tuu pembeni nawaangalia.. ila vijana sahivi tunakutana na mambo ambayo hata wao sidhani kama wanaweza kuyavumilia.. ila na ww ukizingua.. una laki ya haraka haraka hivyo na unasita kuoa..
Unahisi hili lililomkuta ni jipya sana? Swali tu la utanioa lini kwa wazoefu ni red alert kubwa mno iwapo ana malengo na binti na anajiandaa kisaikolojia kwa lolote iwapo hatapeleka posa.

Vijana wa leo wanachowazidi wazee ni kuishi kinyumba na mwanamke kabla ya ndoa. Unaishi na binti kama mkeo hata miaka m4 unajipakulia tu bila shida.
 
I mean no malice to nobody,
FB_IMG_17074712528157192.jpg
 
Back
Top Bottom