Au alikuwa mvulana wa Dar.... Maana hao ndo zao.... Bt poleeeLeo nimepita maeneo ya Mbalamwezi beach nikakumbuka kisa fulani kilichotokea 2012.
Nilipokuwa chuo mwaka wa kwanza, nilikuwa na kibaby flani cha kichaga. Alikuwa handsome balaa, ana gari (japo la kupewa na mama lakini gari ni gari), ana swaga, mrefu, anajua kudance (hiki kigezo kwangu muhimu). Yani dream guy.
Basi ile tumemaliza zetu mwaka wa kwanza ile June ndo tunaenda field. Mimi nilipata position Dar yeye alipata mkoa. Basi ndo tukaamua kuandaa kidate cha kuagana. Tukameet mwenge, haoo tukaenda kwanza Ubungo kumpeleka ndugu yake flani. Baada ya hapo tukasema twende Mbalamwezi, mara tukaingia petrol station akasema "Baby nimesahau wallet aisee halafu gari haina wese". Mtoto hapo nimekolea kimapenzi halafu wallet yangu ina laki moja na ushee, so nikamuuliza tuweke mafuta ya kiasi gani?. Akasema ya 30,000 yatatosha, nikatoa.
Tukatoka hapo haoo tukaenda Mbalamwezi. Tukaingia akasema "Mi sina hela we ndo boss so nakusikiliza". Nikamwambia tule tuu...Akaja mhudumu tukaorder mishkaki na chips na bia mbili zake na soda yangu (bill ilikuwa kama Elfu 40 na ushee, nikalipa mtoto wa kike). Tukala palee, tukapiga story wee...tukaenda beach tukaagana pale na maneno ya mahaba kibaooo...
Mimi nyumbani ilikuwa Ilala na yeye Tegeta. Kuondoka tukapanda kwenye gari kufika nje si ndo heeee baby ananishusha kituoni. Sikuamini macho, masikio wala pua yangu. Tena haoneshi wasiwasi wowote wala sura ya huruma. Akanikiss shavuni na kusema "Bye baby, ntakumiss sana sana". Yani niliishiwa nguvu lakini nilijivuta zangu nikachukua kipochi changu nikashuka nikaenda zangu kituoni. Kulikuwa na foleni ya hatari pale kwa Warioba, magari hayasogei hata kidogo upande huu wa kwenda morocco. Baada ya kama nusu saa or less ananitext "Baby yani huwezi amini nishafika home. Hamna hata foleni yani."
Yani hata kuniuliza kama nimepata gari hakuuliza. Nilikabwa na donge moja shingoni. Nitoe hela ya mafuta, nitoe hela ya lunch, halafu sipati hata a ride home?? Sio kwamba nilihesabu zile pesa au ziliniuma lakini jamani kweli ur girl anasimama kituoni kusubiri basi wakati unaweza kumpeleka home?...Yani siku ile ile nilimtoa moyoni na haikupita wiki nikabreakup nae bila sababu. Ilimsumbua sana kwani i was very rude, sitaki discussion. Sijawahi kumwambia ni kwanini tuliachana na sidhani kama anajua kosa lake au alifeel hata vibaya ile siku. Leo nimekumbuka na hasira ikanishika upya.
Nadhani alinifanya hata nichukie wanaume wenye magari (labda baba V tu). Akinisimamisha mtu na kigari chake huwa namchukia ghafla bila sababu. Hivi kweli kile ni kitendo cha kumfanyia umpendaye?
Nakuelewa sana shoga anguKudance ni muhimu kwangu aisee maana mie mwenyewe napenda kudance balaa
Teh teh..Ndo mana nampenda mpenzi wangu..Ni mtata balaa..Sijui unaanzaje kumuacha kituoni..
Sasa bibie kama mwanaume alishindwa kujiongeza kwann na ww ukakaa kimya..ukabaki kulia na moyo tu..Si ungemchana pale pale
Fatma Hassan, Fatma Huyu Nnaemjua Mimi?Yaani huyo alikuonyeshea dharau ya ajabu sana ulifanya vzur sana kuachana nae cz next time angeweza kukuacha hata usiku wa manane akasepa zake
Fikiria pia bila mafuta angeendaje tegeta!!!!!utu kivipi sasa? wewe aendeshe mpaka ilala then arudi tegeta...plzzzzzzzz be serious u got to be some inconsiderate lady to demand such a favour from a man.
Fikiria pia bila mafuta angeendaje tegeta!!!!!
Nanunua langu soon mkuu
Hahahahaaa in normal assumptions to any human being when he/she give out his/her money is expecting something in return.......
If its church offering a giver is expecting a blessing in return (after paying money)
If its giveaways a giver is expecting thank you note in return (after paying money)
If its shopping one is expecting goods in return (after paying money)
If its restaurant one is expecting food in return (after paying money)
Ila kuna ilee..... unakuwa umejiandaa kuungua kama mshumaa yaani utatoa laki jamaa atamtumia mama yake, utapika, utafua, utafanya usafi, utatumika na bado jamaa anakusindikiza hadi getini kwake na anakwambia hapendi kusindikiza wageni na hajazoea kuonekana mtaani anasindikiza wageni na hapo gari ikondani imepaki full wese tena anakuaga na kukwambia yeye anarudi kulala maana amechoka sana hahahahahahahaa kama umejitolea wala haiumi.
Ila ukishajiwekea akilini hapa ndo ntaolewa... yeeuwiii lazima ulie kila siku.
Then I declare that men are always right to ask for papuchi after taking care of all the bills.
Kasie.
Hahahahaah mkuu angekuwa amenilamba siku hiyo si ningelia...
i can go to that level if and only if that lady has shown beyond reasonable doubt that she can be my future wife. sasa wewe mwanamke kasha-mind kutumia buku 70 unadhani huyo kweli kakupenda? the guy read the signs kaka...he a smart man hahah
Itabidi unipeleke kozi basiHahaha wakaka wanaojua kucheza, kwenye harusi zao Sasa, hatareeee
Teh ticha nipo kwa ajili yakoItabidi unipeleke kozi basi
Kudance ni muhimu kwangu aisee maana mie mwenyewe napenda kudance balaa
Me yamanikuta ya ucku ..alafu no usafiri..unaambiwa panda bodaboda...daaah..mahaba Niue!Yaani huyo alikuonyeshea dharau ya ajabu sana ulifanya vzur sana kuachana nae cz next time angeweza kukuacha hata usiku wa manane akasepa zake