Bujibuji Simba Nyamaume
JF-Expert Member
- Feb 4, 2009
- 74,986
- 156,264
Nilikuwa najua baba na mama ni ndugu. Kamwe sikujua kuwa ni watu kutoka koo mbili tofauti.
Mama yangu mdogo alipo olewa, alivaa nguo nzuri sana. Mimi na wadogo zangu tukaletewa nguo nzuri sana kutoka ng'ambo.
Hamu na kiu yangu sasa ikawa ni kuona mama naye akiolewa, ili apendeze na sisi tupate tena nguo toka ng'ambo.
Nilipo ona mama anakawia kuolewa, nikamuuliza baba, mama ataolewa lini kama anti Tutti ili tuletewe nguo toka ng'ambo?
Baba akafunguka, akasema yeye ndio mchumba wa mama, na tayari amesha muoa.
Akaingia chumbani na kutoka na kitabu kikubwa. Akaanza kunionyesha picha zao za harusi. Nichukia sana.
Hapo nilikuwa na miaka mitano tu.
Je wewe unakumbuka ni kisanga gani ulichokifanya ulipokuwa mtoto?
Mama yangu mdogo alipo olewa, alivaa nguo nzuri sana. Mimi na wadogo zangu tukaletewa nguo nzuri sana kutoka ng'ambo.
Hamu na kiu yangu sasa ikawa ni kuona mama naye akiolewa, ili apendeze na sisi tupate tena nguo toka ng'ambo.
Nilipo ona mama anakawia kuolewa, nikamuuliza baba, mama ataolewa lini kama anti Tutti ili tuletewe nguo toka ng'ambo?
Baba akafunguka, akasema yeye ndio mchumba wa mama, na tayari amesha muoa.
Akaingia chumbani na kutoka na kitabu kikubwa. Akaanza kunionyesha picha zao za harusi. Nichukia sana.
Hapo nilikuwa na miaka mitano tu.
Je wewe unakumbuka ni kisanga gani ulichokifanya ulipokuwa mtoto?