salma juma
Member
- Oct 28, 2010
- 38
- 3
H abari wapendwa,si mgeni sana humu ila huwa nasoma zaidi kuliko kuchangia mada mbalimbali za jf na naridhika na michango ya wachangiaji karibia wote wa forum hii.Leo nna tatizo langu si kubwa wala dogo kivile,mimi ni mama wa mtoto mmoja wa kiume mwenye umri wa miaka 14 sasa na nna ndoa ya kanisani usitishike na jina tafadhali,tuliishi kwa maelewano sana na mme wangu japo kulikuwa na vimatatizo vya hapa na pale ila tulivimaliza na maisha yaliendelea kama kawaida,tatizo lilianza pale ambapo mwenzangu aliposhindwa kuelewa familia ni nini na inahitaji nini,mume wangu hana muda na familia wala kiajana wetu,anachojua nikutoa pesa tu,nimejitahidi kuongea nae sana juu ya hili kwa muda mrefu sana mwisho nami nimechoka nikajikuta natengeneza chuki za ajabu dhidi yake mpaka heshima yangu kwake imekwisha kabisa,hata nikijaribu kumuheshimu najikuta siwezi sio kwa kuwa najifanyisha imetokea tu mpaka chumba nimehama nadhani huu ni mwaka wa nne sasa,tunaishi kwa ajioli ya mtoto tu si yeye wala mimi aliewahi kumueleza mtu yoyote juu ya hili watu wakituona kwa nje wanaona ni mke na mume kumbe ndani hamna kitu,sina wivu nae hata kidogo,tunasalimia kama watu tusojuana na hata kama tuko pamoja kama kuna jambo tunatumia message kuelezana ila kuongea naona kichefuchefu maana akijaribu kuongea nnaona kama ananipotezea muda sielewi nini kimenikuta naomba msaada wenu jamani....wale waropokaji naona si mahala pake hapa huwezi changia soma kimyakimya.