ephen_
JF-Expert Member
- Oct 28, 2022
- 3,625
- 14,797
Habari! Wakuu,
Ipo hivi, imetimia miaka 8 tangu ndugu yangu aolewe kama mnavyojua ndoa ni baraka lakini hii mmmh hapana...
Mwaka flani hio familia ilikuja nyumbani kuomba kijana wao amuoe ndugu yangu, hakuepo mama wala baba wa huyo kijana sababu wamefariki. Kipindi hicho ndugu yangu alikua amemaliza form 6 anasubiri kwenda chuo.
Akaambiwa kuhusu ndoa japokua hakuwahi kua na mahusiano na huyo kijana hapo kabla, ndo mara ya kwanza wanakuja nyumbani kuomba ndoa na yeye akakubali kuolewa.
Kijana alikua na miaka 36 ndugu yangu 19. Kwasababu ndugu yangu alikubali kuolewa kwa masharti ataendelea na chuo akiwa ndani ya ndoa.
Lakini kuna swali liliulizwa kwenda upande wa waoaji kwamba " mnataka vipi kumuoa ijapokua kijana wenu hana kazi, hana nyumba anaishi kwa kaka yake?"
Jibu walilotoa ni kwamba wameshajipanga kuhusu ajira na nyumba, baada ya kutoka honeymoon watafikia kwenye nyumba yao.
Upande wetu tuliridhika na ninahisi ndugu yangu alikubali kuolewa labda alikua anakimbia shida za kiuchumi kwetu, upande wa mwanaume wapo vizuri japo sio sana.
Ndoa ilipita vizuri lakini walivyotoka honeymoon walienda palepale kwa shemeji mtu ambaye ni kaka wa bwana harusi.
Tulioji hii imekaaje tukaambiwa wataenda kwao muda si mrefu, lakini ndugu zangu! sasa hivi imeshatimia miaka 8 ya ndoa bado wapo palepale, ndugu yangu hakupelekwa chuo.
Mbaya zaidi mume wake hataki kujiajiri kwa chochoteeee! Yeye anasema anatafuta kazi aajiriwe alisomea ualimu, kazi yenyewe hatafuti akiamka asubuhi ni kuoga ataanza kuzunguka facebook asubuhi mpaka muda wa kulala.
Ndugu zake wamejitahidi kumtafutia kazi lakini akienda kwenye interview anaharibu. Kuhusu chakula, mavazi mpaka nauli za hapa na pale kaka mtu ndo anawapa.
Ndugu yangu amechakaa sanaa wakati alikua pisi kalii mnoo. Mwanaume hataki kazi yoyote zaidi ya kwenye kiyoyozi anasema yeye ni msomi hawezi kufanya kazi ya uwakala wa fedha, kuna kipindi aliambiwa afunguliwe ofisi.
Ndugu yangu anapata manyanyaso kutoka kwa mke mwenzake (mke wa kaka wa bwanaharusi) ameshawachoka kabisa sababu hawachangii hata kitunguu.
Ndugu yangu alipewa mtaji na mama ake afungue restaurant ili apate hela ajikimu sababu gharama za kumrudisha chuo mke wa mtu mama huo uwezo hana lakini biashara ilifilisika mume wake anataka hela ya vocha kila siku. Miaka yote ya ndoa mke ajashika ujauzito.
Tulimpa ushauri arudi nyumbani asiendelee kubanana kwenye hiyo nyumba sababu hapo kwao wageni kila siku awakauki watu wanawashangaa, wanawadharau kukaa kwa watu lakini ndugu yangu alikataa kurudi akasema hawezi kumkimbia mume wake kwenye dhiki halafu akipata hela arudi tena.
Mna ushauri gani kwenye hili sekeseke?
Ipo hivi, imetimia miaka 8 tangu ndugu yangu aolewe kama mnavyojua ndoa ni baraka lakini hii mmmh hapana...
Mwaka flani hio familia ilikuja nyumbani kuomba kijana wao amuoe ndugu yangu, hakuepo mama wala baba wa huyo kijana sababu wamefariki. Kipindi hicho ndugu yangu alikua amemaliza form 6 anasubiri kwenda chuo.
Akaambiwa kuhusu ndoa japokua hakuwahi kua na mahusiano na huyo kijana hapo kabla, ndo mara ya kwanza wanakuja nyumbani kuomba ndoa na yeye akakubali kuolewa.
Kijana alikua na miaka 36 ndugu yangu 19. Kwasababu ndugu yangu alikubali kuolewa kwa masharti ataendelea na chuo akiwa ndani ya ndoa.
Lakini kuna swali liliulizwa kwenda upande wa waoaji kwamba " mnataka vipi kumuoa ijapokua kijana wenu hana kazi, hana nyumba anaishi kwa kaka yake?"
Jibu walilotoa ni kwamba wameshajipanga kuhusu ajira na nyumba, baada ya kutoka honeymoon watafikia kwenye nyumba yao.
Upande wetu tuliridhika na ninahisi ndugu yangu alikubali kuolewa labda alikua anakimbia shida za kiuchumi kwetu, upande wa mwanaume wapo vizuri japo sio sana.
Ndoa ilipita vizuri lakini walivyotoka honeymoon walienda palepale kwa shemeji mtu ambaye ni kaka wa bwana harusi.
Tulioji hii imekaaje tukaambiwa wataenda kwao muda si mrefu, lakini ndugu zangu! sasa hivi imeshatimia miaka 8 ya ndoa bado wapo palepale, ndugu yangu hakupelekwa chuo.
Mbaya zaidi mume wake hataki kujiajiri kwa chochoteeee! Yeye anasema anatafuta kazi aajiriwe alisomea ualimu, kazi yenyewe hatafuti akiamka asubuhi ni kuoga ataanza kuzunguka facebook asubuhi mpaka muda wa kulala.
Ndugu zake wamejitahidi kumtafutia kazi lakini akienda kwenye interview anaharibu. Kuhusu chakula, mavazi mpaka nauli za hapa na pale kaka mtu ndo anawapa.
Ndugu yangu amechakaa sanaa wakati alikua pisi kalii mnoo. Mwanaume hataki kazi yoyote zaidi ya kwenye kiyoyozi anasema yeye ni msomi hawezi kufanya kazi ya uwakala wa fedha, kuna kipindi aliambiwa afunguliwe ofisi.
Ndugu yangu anapata manyanyaso kutoka kwa mke mwenzake (mke wa kaka wa bwanaharusi) ameshawachoka kabisa sababu hawachangii hata kitunguu.
Ndugu yangu alipewa mtaji na mama ake afungue restaurant ili apate hela ajikimu sababu gharama za kumrudisha chuo mke wa mtu mama huo uwezo hana lakini biashara ilifilisika mume wake anataka hela ya vocha kila siku. Miaka yote ya ndoa mke ajashika ujauzito.
Tulimpa ushauri arudi nyumbani asiendelee kubanana kwenye hiyo nyumba sababu hapo kwao wageni kila siku awakauki watu wanawashangaa, wanawadharau kukaa kwa watu lakini ndugu yangu alikataa kurudi akasema hawezi kumkimbia mume wake kwenye dhiki halafu akipata hela arudi tena.
Mna ushauri gani kwenye hili sekeseke?