unjuthetallest
Member
- Mar 17, 2024
- 5
- 14
Habarini ndugu, kuna mwamba namdai pesa about 100m.. jamaa nilimkopesha na tuliandikishana mkataba. Ni muda mrefu miaka 5 sasa. Nilimpeleka police, lakini haikuzaa matunda kwa kuwa jamaa alikuwa na wadhifa fulani ndani ya chama na kaka yake ni mteule wa raisi hivyo nikagonga mwamba.. nikaenda mahakamani lakini pia ilionekana ni kama walimnunua mheshimiwa shauri likafutwa katika mazingira ambayo sikuyaelewa.. yaani tulipangiwa tarehe ya kusikiliza kesi, tulivyokwenda tukaambiwa kesi ilikua ni jana yake, kwamba hatukuwepo na mheshimiwa akafuta shauri. Kitu ambacho sio kweli, tarehe tuliyoambiwa ndio hiyo siku tuliyoenda. So kesi ikawa imefutwa.
Nafanyaje kupata pesa zangu?.. mahakama siiamini tena na ninaona ni kama naenda kupoteza muda na pesa huko. Nafanyaje kupata haki yangu?.
Nafanyaje kupata pesa zangu?.. mahakama siiamini tena na ninaona ni kama naenda kupoteza muda na pesa huko. Nafanyaje kupata haki yangu?.