Mwambie gf wako ajifunze kukabiliana na mitongozo. Huko chuo anapoenda atakuwa anakushtakia kila anapotongozwa?
Namsikitikia Manyanza mpaka huyo binti anamaliza chuo anaweza kupata ugonjwa wa moyo,vitu vingine amalize mwenyewe bana-huo muda wa kurekodi mpaka maongezi duh!
Kaka binam yako hawezi kukurupuka "from no where" akaongea topic za ajabu kama hizo, huyo GF wako ndiyo alientertain mazungumzo mpaka jamaa kafika huko, kingine jifunze kuwa na MOYO WA CHUJIO vinginevyo akienda chuo utalia, hakuna sehemu rahisi kuwanasa mabinti kama huku chuo, sijui huwa wanakumbwa na shetani gani, so jifunze kuvumilia, kama GF wako ni kisu(mzuri) tegemea mitihani mingi zaidi, leo kaanzia audio kesho itakuletea video kabisa.. Halafu kuhusu binam unatakiwa ujue kuwa mtoto siyo pete ya ndoa so huyo nduguyo yupo huru kufanya lolote... Mwisho kabisa USIMWAMINI MWANAMKE hata siku1.
Ndugu ni ndugu huwezi gombana nae. Lakini kumbuka kuwa hata mwanamke ukishamuoa anakuwa na thamani kama ndugu au zaidi ya ndugu.
Ushauri wangu ni kuwa wala usimface huyo ndugu yako ila cha msingi kuwa nae makini saaana. Nasema hivyo kwa kuwa huyu mdada amemtolea nje na yawezekana mdada asiwe girlfriend wako wa mwisho; ila kukupa taharifa imekusaidia kujua what your cousin is capable of. Kuna ma player wana ethics na wanajua limits. Kuna wasio na limits. Jamaa atakuwa na katabia ka kuwinda wasichana wa wenzie ndio hao wanaozaa na wake za ndugu zao.
Keep a big distance from your so called cousin other wise akikwaa maugonjwa yake mnaondoka familia nzima. Who knows kama atakuwa anatolewa nje na wasichana wako wote? Who knows kama hajawahi kukumegea wasichana wako walopita??? Shukuru kwa taharifa kwani imekupa tahadhari no matter whether alichofanya mdada ni right au ange keep it as secret. Kwangu mimi si kila kitu ni worth to be called siri. Ikifichuka usingeamini kuwa alimtolea nje jamaa.
<br />Mh Manyanza pole sana. Hivi ni vitu ambavyo mimi huwa ninasema vya kutulia kwanza kabla ya kufanya lolote. Hebu jiulize siku ikitokea huyo huyo galfriend wako akakusaliti kwa mwingine, afu we umeshamtapikia huyo ndugu yako huyo vipepeo!! utauweka wapi uso wako?? Naungana na nyumba kubwa kuwa mpotezee but kaa nae chonjo!