Ni uhaini - as simple as that!

Mkuu Mwanakijiji

Hakuna atakayekusikiliza hapa tumeweka Jambazi sugu pale magogoni unategemea nini? Ameweka group la banyamelenge, Iranians, hata nyang'au naambiwa wameingia kwa mlango wa uani usitegemee kitu kwenye hiki Chama Cha Majambazi.
 
WaMzizima,
Mkuu nakupata vizuri sana unakotokea lakini unashindwa kuelewa kwamba Kuunda kwa nchi yoyote duniani kumepitia hatua ambazo wewe na mimi tumezipokea tu baada ya nchi hizo kuwepo ktk ramani. What they went through hatujui zaidi ya kusoma ktk vitabu hivyo tunapouliza au kudadisi swala kama hili ni vizuri sana kuwa na ushahidi dhidi ya ule unaousikia. Nikiwa na maana kwamba leo hii ukisikia kwamba Baba yako unayemujua sii baba yako mzazi unaweza kumdadisi mama ili upate ukweli kuhusiana na baba yako.

Kinachofanyika Zanzibar ni uhuni, uhuni wa baadhi viongozi ambao kwanza hawakuwepo wakati swala hili la Muungano likiwakilishwa ktk baraza la Mapinduzi. Wengi wao hawakushiriki hata kupitisha artical of Union naifahamike wazi kwamba sii kweli madai ya baadhi viongozi kwamba Muungano ulipangwa na Nyerere na Karume tu. Haya sii kweli kwani toka mwanzo mbali na Karume, Abdallah Kassim Hanga, Abdul-Aziz Ali Twala na Salim Rashidi walishiriki kikamilifu kama wawakilishi wa Visiwani ktk kuunda Muungano. Na hata report ya Nyalali commission ilieleza wazi kwamba Artical of Union ilikupitishwa na Baraza la Mapinduzi.

Kero ya wananchi sio Uhalali wa Muungano hata kidogo hizi ni politics za kina Seif isipokuwa ni nafasi ya Zanzibar ndani ya Muungano. Wananchi kama watotowa Muungano huu wanataka kujua urithi wao, haki yao na kwa nini wanakosa baadhi ya huduma ambazo watoto wengine (bara) wanazipata. Lakini haya ya kuulizia ndoa yetu hayana faida wala maslahi kwa Wazanzibar kwani wakisha kuwa NCHI watafaidika kipi zaidi ya leo hii walivyo?

Kwa hiyo, kinachofanyika leo hii ni kuhoji uhalali wa ndoa ambayo wewe na mimi ni watoto walozaliwa ndani ya ndoa hii. Where and how they hook up wazazi wetu iwe ni udadisi tu wa kutaka kuijua historia yetu na sio kutafuta mbinu ya kuvunja ndoa. Hao kina Shariff Hamad ni watu wa Hizbu hawakushiriki isipokuwa wamepewa undugu kuoa ndani ya familia hii. Seif know nothing about Union zaidi ya kupinga kwa sababu alikuwa nyuma ya Sultan hali huyo Karume bado anatumia mbinu za marehemu Baba yake kujilinda yeye na maslahi ya familia yake.

Na sina maana hawana haki ya kuuliza swali lolote liwe la legitimacy, au nafasi ya Zanzibar ndani ya Muungano (artical of Union) laa hasha wanayo haki hiyo na zaidi ya kuuliza ikiwa watafuata sheria na taratibu simamizi badala ya kuanza kujitangaza kwamba Zanzibar ni NCHI. Hata sisi wengine hapa bara tunaona mabadiliko mengi yakifanyika kinyume lakini hatuwezi kuchukua sheria mikononi kwani ikumbukwe tu kwamba Muungano wetu umetokana na WOGA (fear) wa matukio kama haya.

Wapo wanaosema ilitokana na siasa kali za kina Abrahman Babu (communist) na wengine wakidai hofu ya kurudi kwa Sultan kutokana na Mapinduzi yenyewe kutokuwa na nguvu ya kutawala..Hivyo tunaporudia kuweka FEAR ndani ya mioyo ya wananchi kugawanyika ili maslahi ya Zanzibar yawe mikononi mwa kundi fulani, inarudisha hofu ileile iliyosababisha Muungano huu hivyo badala ya kuuvunja huu Muungano ndio kwanza Hofu hii itaufanya Muungano kuwa imara zaidi.

Kama alivyosema Mzee Mwanakijiji, kama kweli Wazanzibar hawautaki huu Muungano basi ifanyike referendum (kura za maoni) hata iwe kwa Wazanzibar peke yake. Hao viongozi kina Seif Sharrif na Karume wawaeleze wananchi FAIDA na kujitenga na hasara za Muungano kwani ndiko kwenye kero. Na wawaeleze Wazanzibar wakisha jitenga wao kama viongozi wataweza kufanya nini tofauti ambacho wameshindwa kukitimiza wakiwa ndani ya serikali hii ya Muungano maanke hjawa wote walikuwa viongozi wa ngazi ya juu ktk serikali hii.

Na unapotaka kuvunja ndoa zipo sheria na taratibu zake, sio rahisi kama kuvua pete ya harusi na kuanza kutangaza Ukapera. Ndani ya refendum Wazanzibar wataamua wanataka nini na hakika challenge hii nimeitoa kwa huyu Seif, hao CUF na hata Baraza la Mapinduzi toka wakati Mkapa akiwa madarakani lakini walishindwa kufanya hivyo wakisingizia mambo kibao. Maajabu ya Mussa swala la serikali ya mseto, hizo kura za maoni zimepigwa haraka pasipo kufikiria kero za Muungano sio jinsi ya kugawana madaraka baina ya viongozi wa bara na visiwani.

Huu ni usaliti kwa wananchi wa Bara na Visiwani kwa sababu mfumo huu unazidi kututenganisha zaidi tukifuata asili ya mtu kushika madaraka badala ya uwezo wa mtu kushika madaraka na kibaya zaidi tunakimbia kero kubwa ya kiuchumi ambayo hadi kesho serikali zote mbili zimeshindwa kuwa wazi kwa wananchi kuhusiana na mgao wa pato la taifa. Badala ya hawa viongozi kuondoa kero za Muungano ndiokwanza wameunda kero nyingine, viongozi wa vyama viwili kukutana na kukubaliana ku share Madaraka ktk sehemu ya nchi ambayuo wao wenyewe wanatutangazia kwamba sio Nchi wala Taifa. Na hata kama Zanzibar ingekuwa Taifa ndani ya nchi bado hakuna nchi yoyote duniani inayotawaliwa kwa mfumo unaotazama zaidi tamaa ya madaraka kwa viongozi zaidi ya mustakabali wa nchi na raia wake.
 
Balaza la wawakilishi lipo kisheria kama ilivyo kwa bunge la jamuhuri. Labda cha kujiuliza hapa ni je, baraza la wawakilishi linayo mamlaka ya kufanya mabadiliko iliyoyafanya katika katiba ya Zanzibar? Kama jibu ni ndiyo, then sioni uhaini unatokea wapi. Ndani ya mipaka ya jamuhuri, zanzibar ni nchi (lakini kimataifa hakuna nchi inayoitwa Zanzibar!)
 
Jamani hhebu wataalamu wa masuala ya miundo ya serikali na nchi tueleimishane kwanza kabla ya kutangaza uhaini, naomba kujua, kwenye muungano wetu huu:-

1. Ni nchi gani na nchi gani ziliungana?
2. Zilipoungana je kulizaliwa nchi mpya am laa?
3. Kama kulizaliwa nchi mpya?
4. kama jibu la 3 ni NDIO, je zilizaliwa nchi ngapi moja, mbili au mia?
5. Je nchi hiyo/hizo inaitwaje/zinaitwaje?
6. Je nchi hizo zina mipaka au hazina?
7. Je nchi hiyo/hizo ni huru na zinajitawala au kuna moja inatawala nyingine?
6. Je kwenye nchi hiyo/hizo kuna serikali ngapi?
7. Kama jibu la 6 ni serikali zaidi ya moja, je inawezekana kuwa na nchi moja yenye serikali zaidi ya moja? Toa mfano
8. Mwisho je wewe ni Mtanzania, Mtanganyika, Mzanzibari, muunguja au mpemba?
9. Je unaridhika na muundo huu?
10. Kama hauridhiki, ungependa nini kifanyike?
11. Asanteni kwa kunisikiliza
 
wazanzibar wakitaka kwenda zao waachieni kama wameamua kwa utashi wao. muungano haulazimishwi. huenda sababu zilizopelekea muungano hazipo tena. sasa kuwalazimisha wazanzibar kama hawataki muungano ni kuwapa hisia kuwa bara ndo wanafaidika kuliko wao ndo maana wanaung'ang'ania.
 
Umenena vizuri sana, Mkuu Makandara. Unajua kwa wenzetu wengi imani yao ni kuwa Bara hawataruhusu Muungano kuvunjika kwa hiyo wanaweza kutingisha kiberiti saizi yao bila wasiwasi wowote. Ndio maana ni vizuri kuweka wazi kuwa tuko tayari kuvunja Muungano kama upande mmoja utataka iwe hivyo. Wananchi wa kawaida wa pande zote mbili waelezwe maana ya kuwa na nchi mbili zilizohuru. Wazanzibari waelezwe kuwa watakuwa kama wakenya Tanzania. Watahitaji kuwa na vibali vya kuishi kama wageni wengine wowote. Waambiwe kuwa hawatakuwa na urahisi walio nao sasa kutumia huduma kama shule, hospitali n.k. zilizo Tanzania Bara. Waelezwe kuwa umilikaji wao wa ardhi na biashara utakuwa na masharti kama ilivyo kwa raia wengine wa nchi geni. Waelezwe kuwa watalazimika kuunda jeshi lao, polisi wao n.k. Waelezwe kuwa watakuwa na balozi zao na kwa hali hiyo misaada yote itakayopatikana itakuwa yao. Na vile vile kama nchi huru, wataweza ku-utilise mali asili yao jinsi wanavyotaka bila kuingiliwa na mtu. Waambiwe vile vile kuwa watakuwa huru kununua nishati kutoka nchi yeyote ile kama vile Bara hawatakuwa wanawajibika kuwapatia nishati kwa bei ya upendeleo. Kwa vile watu wa Bara hata hivi sasa wanafanywa kama raia wageni ndani ya Zanzibar ( haki zao ni circumscribed), kuvunjika kwa Muungano hakutabadilisha sana status yao. Baada ya yote haya na mengine kuwekwa wazi, ndipo wananchi wa pande zote mbili waulizwe kama bado wanataka kuendelea na Muungano. Na chips ziachiw ziangukie zitakapoangukia.

Amandla........
 
Jamani hhebu wataalamu wa masuala ya miundo ya serikali na nchi tueleimishane kwanza kabla ya kutangaza uhaini, naomba kujua, kwenye muungano wetu huu:-

1. Ni nchi gani na nchi gani ziliungana?
2. Zilipoungana je kulizaliwa nchi mpya am laa?
3. Kama kulizaliwa nchi mpya?
4. kama jibu la 3 ni NDIO, je zilizaliwa nchi ngapi moja, mbili au mia?
5. Je nchi hiyo/hizo inaitwaje/zinaitwaje?
6. Je nchi hizo zina mipaka au hazina?
7. Je nchi hiyo/hizo ni huru na zinajitawala au kuna moja inatawala nyingine?
6. Je kwenye nchi hiyo/hizo kuna serikali ngapi?
7. Kama jibu la 6 ni serikali zaidi ya moja, je inawezekana kuwa na nchi moja yenye serikali zaidi ya moja? Toa mfano
8. Mwisho je wewe ni Mtanzania, Mtanganyika, Mzanzibari, muunguja au mpemba?
9. Je unaridhika na muundo huu?
10. Kama hauridhiki, ungependa nini kifanyike?
11. Asanteni kwa kunisikiliza

Mkuu majibu ya maswali haya sio kero za Wananchi isipokuwa ni upotoshi wa makusudi. Tunashindwa kujibu maswali magumu zaidi kwa kutafuta urahisi kwani Muungano wetu ulilazimika kuwepo kutokana na hali ya kisiasa. Na ndivyo Muungano wa nchi nyingine ulipatikana na sio kwa kufikiria zaidi mipaka ya nchi isipokuwa WATU wake na MAZINGIRA yaliyokuwepo.

Hivyo sababu ambazo pekee zinaweza kuuvunja Muungano huu ni tofauti za WATU na MAZINGIRA tulokuwepo leo jambo ambalo litaamuliwa na wananchi wenyewe na sio siasa za kigabuzi kwa kutazama mipaka ya nchi badala ya wahusika. Hata nchi zote za USSR na Yugoslavia zilivunjika kutokana na kero zinazowahusu wananchi wenyewe na siii mipaka ya nchi zao au kutambulika kwa Taifa ndani ya nchi isipokuwa kumetokana na swala kubwa la KIUCHUMI au KIITIKADI.

Sisi tunapoendelea kudai Utengano kutokana na Historia ya mkoloni inaonyesha wazi bado tumetawaliwa kiakili. Tunashindwa kuyatafutia ufumbuzi maswala nyeti yaliyopo mezani tunatafuta tofauti za Uasili ya watu hivyo hata kama tukija tengana basi Pemba na Unguja watakuja tumia vigezo hivyo hivyo kutengana. Na vizuri sana ikiwa Wazanzibar mtaweka wazi kero yenu ndani ya Muungano kwani kudai kuitwa nchi au Taifa hali viongozi wenu wana mamlaka makubwa zaidi ya Muungano wowote naoujua mimi ni kufanya kufur.

Sijawahi kuona nchi moja ina Marais wawili, sasa nasikia kutakuwa na makamu wa rais na waziri mkuu (waziri Kiongozi) ktk serikali zote za Muungano na Visiwani, hii pekee inawafanya kuwa na madaraka makubwa kuliko nchi zozote ndani ya Muungano wowote ule. Na pengine haya ndio makosa makubwa yaliyowahi kufanyika kwani muungano wa nchi huondoa kabisa tabaka za kiramani ktk uongozi wa nchi. Lau kama Tanzania ingeungana pasipo kujali utaifa wa kila mmoja wetu tusingekuwa na matatizo kama haya isipokuwa lingezuka labda tatizo la Zanzibar kumezwa na Bara.

Binafsi naamini kabisa ikiwa kuna mpango madhubuti wa mgao wa urithi na mali ya Taifa zima, hii akikli ya Kitumwa ya kutazama mipaka ya mkoloni isingekuwa tatizo na hakika ni kwa jicho kama hili ndio maana Afrika tumeshindwa kudumisha Pan Africanism. Na hakika hizi ndizo athari za kutawaliwa kiasi kwamba Wazanzibar wanajisikia tofauti na karibu sana na Mwarabu (Oman) na Wabara kujisikia Uzungu huku tukitumia dini kama ndio sababu ya tofauti zetu.
Til then.. we still serving the Masters!
 
Mkuu majibu ya maswali haya sio kero za Wananchi isipokuwa ni upotoshi wa makusudi. Tunashindwa kujibu maswali magumu zaidi kwa kutafuta urahisi kwani Muungano wetu ulilazimika kuwepo kutokana na hali ya kisiasa. Na ndivyo Muungano wa nchi nyingine ulipatikana na sio kwa kufikiria zaidi mipaka ya nchi isipokuwa WATU wake na MAZINGIRA yaliyokuwepo.

Hivyo sababu ambazo pekee zinaweza kuuvunja Muungano huu ni tofauti za WATU na MAZINGIRA tulokuwepo leo jambo ambalo litaamuliwa na wananchi wenyewe na sio siasa za kigabuzi kwa kutazama mipaka ya nchi badala ya wahusika. Hata nchi zote za USSR na Yugoslavia zilivunjika kutokana na kero zinazowahusu wananchi wenyewe na siii mipaka ya nchi zao au kutambulika kwa Taifa ndani ya nchi isipokuwa kumetokana na swala kubwa la KIUCHUMI au KIITIKADI.

Sisi tunapoendelea kudai Utengano kutokana na Historia ya mkoloni inaonyesha wazi bado tumetawaliwa kiakili. Tunashindwa kuyatafutia ufumbuzi maswala nyeti yaliyopo mezani tunatafuta tofauti za Uasili ya watu hivyo hata kama tukija tengana basi Pemba na Unguja watakuja tumia vigezo hivyo hivyo kutengana. Na vizuri sana ikiwa Wazanzibar mtaweka wazi kero yenu ndani ya Muungano kwani kudai kuitwa nchi au Taifa hali viongozi wenu wana mamlaka makubwa zaidi ya Muungano wowote naoujua mimi ni kufanya kufur.

Sijawahi kuona nchi moja ina Marais wawili, sasa nasikia kutakuwa na makamu wa rais na waziri mkuu (waziri Kiongozi) ktk serikali zote za Muungano na Visiwani, hii pekee inawafanya kuwa na madaraka makubwa kuliko nchi zozote ndani ya Muungano wowote ule. Na pengine haya ndio makosa makubwa yaliyowahi kufanyika kwani muungano wa nchi huondoa kabisa tabaka za kiramani ktk uongozi wa nchi. Lau kama Tanzania ingeungana pasipo kujali utaifa wa kila mmoja wetu tusingekuwa na matatizo kama haya isipokuwa lingezuka labda tatizo la Zanzibar kumezwa na Bara.

Binafsi naamini kabisa ikiwa kuna mpango madhubuti wa mgao wa urithi na mali ya Taifa zima, hii akikli ya Kitumwa ya kutazama mipaka ya mkoloni isingekuwa tatizo na hakika ni kwa jicho kama hili ndio maana Afrika tumeshindwa kudumisha Pan Africanism. Na hakika hizi ndizo athari za kutawaliwa kiasi kwamba Wazanzibar wanajisikia tofauti na karibu sana na Mwarabu (Oman) na Wabara kujisikia Uzungu huku tukitumia dini kama ndio sababu ya tofauti zetu.
Til then.. we still serving the Masters!

Umenena vema...kitu kimoja ambacho sikipendi kuhusu huu muungano wetu ni kwamba umefanywa kuwa wa kiimani zaidi kwahiyo hautoi nafasi ya kujadiliwa.....ni kama masuala ya dini yalivo,,huruhusiwi kuyajadili jadili sana, kwanini?wanajua wao! kuna makosa yalifanywa wakati wa kuutengeneza, na kila watu wanapohoji makosa hayo, basi ile hali ya kiimani imani inarudishwa halafu mnaonekana kama wahaini...nadhani unanipata...ni sawa na mtu kuhoji ujio wa Muhamad au Yesu, ni kama unataka kuzua balaa ivi..

Nchi mbili zinaunganaje halafu bado zitoke nchi mbili tena zenye full kila feature ya nchi? katiba, bunge, serikali????????&&&kuna walakini hapa...watu wakitaka kurekebisha hizi kasoro basi inaonekana kama wanataka kuuvunja?tunaweza kuvunja ndio huu wa nchi mbili na serikali mbili halafu tukaunda wa nchi moja na serikali moja which is much better, na kwenye hilo mkuu Mkandara nakubishia kabisa kuwa eti Zanzibari itamezwa na Bara, imezwe vipi?ikiwa nchi moja both Tanganyika na Zanzibar zitamezwa na Tanzania, thats what I understand? si kila mmoja amekubali kuolewa, akubali kulala fululu!!!!

Huu muungano feki huu, utazamwe!!!!

Mimi ni Mmang'ati wa hanang so sina interest yeyote binafsi!
 
Haya mambo ni utata mtupu tuelimishane jamani.

Hivi hizi Articles of Union zipo ndani ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano Tanzania (KJMT) ? Ama pamoja na Katiba ya Zanzibar(KZ)?

Kama zipo sehemu zote mbili je mabadiliko ndani ya KZ inabidi yaridhiwe na upande wa Muungano? Au yanakuwa binding jumla jumla?

Kwa msingi huo nani mwenye mandate ya kutengua ama kubatilisha Articles of Union?

Mchakato wake upo vipi kisheria?

Hivi hili swala la Referendum linasemwa kwamba linawezekana upande wa pili yaani upande wa Bara. Lakini je Bara ni sovereign or semi-sovereign ndani ya KJMT? Si machozi ilishakwenda na maji?! Au ?

Na hili swala la Nje si Nchi ila ndani ni nchi na function of Nchi = {Rais,Bunge,Mahakama,Jeshi,Serikali, Mipaka etc}

Je Zanzibar kama Nchi ndani ya Bara La JMT inastahili kuwa na hizo instruments za Dola? Au Nchi < Dola ?

Tuelimisheni basi mabingwa wa elimu ya Katiba.
 
mi niseme yangu.
Znz wameanza harakati hizi kitambo tu, watu wote tukiwashuhudia hatua kwa hatua. walianza na wimbo wa wao wa taifa, nembo yao ya taifa, wakaja na madai ya utaifa wao, ikamletea waziri mkuu Pinda matatizo Bungeni, hawa ni watu waliojipanga kitambo, watu wanaojua nini wanataka.
Nyerere akiwa hai alikemea harakati zao za Mwanzo lilipoanza swala la OiC , akawaambia hawawezi kufanya hayo wakiwa ndani ya muungano , akawakumbusha katiba , kwasababu alikua akiogopewa wakanywea.
leo namuangalia Kikwete, nawaangalia washauri wake serikalini na wakwenye chama, namuona anapwaya, WaZnz hawamuogopi hasirani, wanampuuza, wanamuona aliepwaya, na wao wanatumia mwanya huo.
Kinachoendelea kule ni ukiukwaji mkubwa na katiba ya Jamuhuri, hawana haki yakufanya hayo bila ridhaa ya Umma, katika haipaswi kuchezewa na gunge fulani la wakora kwa faida zao za muda mrefu ama muda mfupi.
Katika ni kitu nyeti,, kama wataachwa hivihivi , ipo hatari siku moja tukaona vituko vya aina yake huko Visiwani.
 
Mzee Mwanakijiji,

BLW wamefanya mukutano wao wakati muafaka saana kwani walijua hili wakilishusha wakati kuna kikao cha bunge Dodoma, basi mjadala ungewaka moto hapo Dodoma. Lakini wanajua sasa hakuna kikao cha bunge na ni mpaka baada ya uchaguzi, ingawaje kwa marekebisho kama hayo, nafikiri ili hiyo rasimu iweze kuwa sheria ilitakiwa kiitishwe kikao cha dharura cha bunge. Swali kwangu yuko wapi AG? au waandishi wa habari kwa nini wasimuhoji AG atueleze kama katiba ya JMT haijavunywa?
 
Balaza la wawakilishi lipo kisheria kama ilivyo kwa bunge la jamuhuri. Labda cha kujiuliza hapa ni je, baraza la wawakilishi linayo mamlaka ya kufanya mabadiliko iliyoyafanya katika katiba ya Zanzibar? Kama jibu ni ndiyo, then sioni uhaini unatokea wapi. Ndani ya mipaka ya jamuhuri, zanzibar ni nchi (lakini kimataifa hakuna nchi inayoitwa Zanzibar!)

yaani hata hii kauli ya kipuuzi iliyotolewa na Kikwete mwanzoni (na niliipinga wakati ule vile vile) watu hawafikirii wanachosema: "NDANI YA TANZANIA ZANZIBAR NI NCHI". Really?
 
Mimi ni Mmang'ati wa hanang so sina interest yeyote binafsi!


thats exactly the point.. kila mtanzania au kundi la watanzania watakaoona kuwa Muungano hauwapi manufaa wanayotaka wajitenge. Hivi watu wa Kigoma (na wameshawahi kusema hili) wakisema Muungano hauwanufaishi au Tanzania Bara haiwanufaishi tutawabishia? Vipi kuhusu watu wa Mtwara na Lindi (nao wameshawahi kusema hili) wakisema kuwa Muungano hauwanufaishi na wangependa kuwa sehemu ya Msumbiji au kutangaja kijamhuri chao tutawaambia wanasema uongo au tutawakubalia ati kwa sababu muungano hauna manufaaa "kwa pande zote"? Hivi watu wa Chunya wananufaika vipi na Muungano? Watu wa Nansio, Mkongo na Duga wananufaika vipi na Muungano?

Hivi Wamarekani wote wananufaika na muungano wa US? Na wote wanafuraha?

Ndio maana nilisema wabongo tunapenda mambo mepesi mepesi!


@Mkandara, nimependa take yako.. thats whatsup!
 
Umenena vema...kitu kimoja ambacho sikipendi kuhusu huu muungano wetu ni kwamba umefanywa kuwa wa kiimani zaidi kwahiyo hautoi nafasi ya kujadiliwa.....ni kama masuala ya dini yalivo,,huruhusiwi kuyajadili jadili sana, kwanini?wanajua wao! kuna makosa yalifanywa wakati wa kuutengeneza, na kila watu wanapohoji makosa hayo, basi ile hali ya kiimani imani inarudishwa halafu mnaonekana kama wahaini...nadhani unanipata...ni sawa na mtu kuhoji ujio wa Muhamad au Yesu, ni kama unataka kuzua balaa ivi..

Nchi mbili zinaunganaje halafu bado zitoke nchi mbili tena zenye full kila feature ya nchi? katiba, bunge, serikali????????&&&kuna walakini hapa...watu wakitaka kurekebisha hizi kasoro basi inaonekana kama wanataka kuuvunja?tunaweza kuvunja ndio huu wa nchi mbili na serikali mbili halafu tukaunda wa nchi moja na serikali moja which is much better, na kwenye hilo mkuu Mkandara nakubishia kabisa kuwa eti Zanzibari itamezwa na Bara, imezwe vipi?ikiwa nchi moja both Tanganyika na Zanzibar zitamezwa na Tanzania, thats what I understand? si kila mmoja amekubali kuolewa, akubali kulala fululu!!!!

Huu muungano feki huu, utazamwe!!!!

Mimi ni Mmang'ati wa hanang so sina interest yeyote binafsi!
Mkuu nadhani nitatofautiana nawe ktk hili. Maudhui ya kuhoji Muungano ndiyo yanayokera watu kama mimi. Na siwezi kufananisha Muungano na dini kwa sababu dini ni Imani ya watu na Muungano unatokana na kutengeneza mazingira safi kwa jamii inayoungana. Hivyo tunaposhindwa kuelewa kwamba lengo kuu la Muungano ni kuunganisha WATU na swala la nchi ni kuyaweka Maingira yetu ktk hali ya kudumisha Umoja huo.

Sasa kama kuna mtu anahoji Muungano ambao ni wa WATu kwa kisingizio cha mipaka au nchi atueleze vizuri kumekosekana kitu gani kuufanya Muungano huu wa WATU usiwe imara..Nina hakika hakuna kati yao anayeweza kuzungumzia matatizo ya muungano kwa kigezo cha haki za wananchi wenyewe tofauti na Dini ambazo watu wanahoji haki na freedom ya waumini.

Ikumbukwe tu kuna thin line kati ya haki na freedom na abusive of the certain rights. Kila sheria inayohusiana na haki au freedoma za binadamu ni ktk kuleta USAWA baina ya wahusika wote na sio UTENGANO baina yao kuwa ndio right kama inavyoiombwa pasipo sababu zaidi ya kutumia mipaka ya ramani za mkoloni.


Mimi siepndi kabisa malumbano ya Muungano zaidi ya kuwatazama wananchi wenyewe na kero zao. Kero zote za Muungano zimetokana na Uongozi uliopo na wote hawa ni wanafiki wakubwa. Nakujmbuka Ni Karume aliyekubali Muungano, kisha alitaka kuuvunja baada ya kuondokana na kina Abrahman Babu. Muungano kwake ilikuwa kuhakikisha maradaka yake hayapati upinzani kama alivyofanya Nyerere kuua vyama vingi bara.

Kisha akaingia huyo Aboud Jumbe kuserve Muungano lakini ajabu ya Mussa naye akataka kugeuka na ya Firaun huyu Seif ndiye aliyepinga m,awazo ya Jumbe na kuwatonya kina Nyerere. Leo hii yeye ndiye mpiganaji maarufu hali hawa woote mwanzoni walipokuwa ndani ya serikali ya Muungano hawakutaka kabisa kusikia kuvunjika kwa Muungano lakini wanapokuwa nje ya madaraka ndio kelele zao zinaposikika.

Maadam wamelianzisha wao kuhusiana na Muungano nadhani sisi wananchi tunatakiwa kuwauliza wao maswali muhimu kwetu ktk kuvunjika kwa huu Muungano. Je, wataweza vipi kuunganisha jamii hizi mbili na kwa njia zipi za kudumu ambazo sisi wananchi tunazikubali kwani kesho kesho kutwa tunaweza kufukuzana mipakani tukitumia katiba hizi mpya wanazotunga wao leo hii.
 
wazanzibar wakitaka kwenda zao waachieni kama wameamua kwa utashi wao. muungano haulazimishwi. huenda sababu zilizopelekea muungano hazipo tena. sasa kuwalazimisha wazanzibar kama hawataki muungano ni kuwapa hisia kuwa bara ndo wanafaidika kuliko wao ndo maana wanaung'ang'ania.

Si waeleze kinagaubaga kuwa wanataka kutoka!?? Wafanye referundum na wanaotaka kuvunja Muungano wakishinda, tuanza process kwa uwazi bila kujificha. Personally nitapiga kura watuondokee, lakini sipendi waondoke kwa kumong'onyoa taifa letu kimya kimya kama wanavyofanya sasa!
 
Unajua kuna matatizo fulani ambayo wengi wa watu kutoka Tanganyika wanapungukiwa.Kila mtu anakuwa anajivunia utaifa wake na uzalendo wake, lakini kwa bahati mbaya nilisoma utafiti fulani unasema watanzania (watanganyika) ni watu wasio na tabia hii duniani.Sina uhakika ni kwanini, lakini huenda ikawa ni ile dhana ya kuwa Tanganyika ni taifa ambalo mipaka yake ya kuundwa na wakoloni.

Anyways, long story short naona wengi wenu muna mawazo ya kizamani ya miaka 64 tokea Nyerere alivyokuwa hai akitisha tisha wazanzibari na kuwaita wahaini.Mnasahau kama muda umeshapita na leo tuko karne nyengine kabisa, ambayo ukweli wa mambo wazanzibari wengi hawataki muungano

Personally, kama mzanzibari nimefurahi sana na momentum ya siasa za kwetu zinavyokwenda.Yaani ni juzi tuu saturday tumefanya re-union ndogo kufurahia GNU n.k.Hili la katiba kubadilishwa na kuwa nchi, ndio nimezidi kufurahi na naomba M.Mungu aniweke hai nishuhudie taifa langu likiweka tena bendera yake hapo U.N kama ilivyokuwa kabla ya Mhaini Nyerere kuja na wazimu wake.:mad2:

Sasa kusema M.Mwanakijiji unanisomea mie katiba ya Tanganyika, halafu ndio mjadala unaanzia na katiba hio naona kama unajisumbua.Maana hio katiba yenyewe ndio msingi wa matatizo haya :confused2: ..
 
thats exactly the point.. kila mtanzania au kundi la watanzania watakaoona kuwa Muungano hauwapi manufaa wanayotaka wajitenge. Hivi watu wa Kigoma (na wameshawahi kusema hili) wakisema Muungano hauwanufaishi au Tanzania Bara haiwanufaishi tutawabishia? Vipi kuhusu watu wa Mtwara na Lindi (nao wameshawahi kusema hili) wakisema kuwa Muungano hauwanufaishi na wangependa kuwa sehemu ya Msumbiji au kutangaja kijamhuri chao tutawaambia wanasema uongo au tutawakubalia ati kwa sababu muungano hauna manufaaa "kwa pande zote"? Hivi watu wa Chunya wananufaika vipi na Muungano? Watu wa Nansio, Mkongo na Duga wananufaika vipi na Muungano?

Hivi Wamarekani wote wananufaika na muungano wa US? Na wote wanafuraha?

Ndio maana nilisema wabongo tunapenda mambo mepesi mepesi!


@Mkandara, nimependa take yako.. thats whatsup!

Hapana Mkuu. Kigoma si sawa na Zanzibar. Mikoa yetu haifanani kabisa na State za Marekani. Mfano mzuri ungekuwa watu wa Yorkshire au Sussex n.k Uingereza wadai haki sawa na watu wa Scotland na Wales. Hii haiwezekani maana Yorkshire ilishamezwa zamani katika taifa la England. Kigoma, Mtwara hivyo hivyo. Hii ni mikoa ambayo hayajawahi kuwa taifa. Ni kama vile tuseme kuwa wakatoliki wadai nchi yao. Au ma-albino nao wadai. Tofauti iliyopo ni kuwa hiyo mikoa ni territorial. Teritory ambayo inaweza kuchezewa vyovyote vile ndani ya taifa la Tanzania. Mbona kila siku mikoa inagawanywa (Mtwara kuwa Mtwara na Lindi, Arusha kuzaa Manyara n.k.) bila matatizo yeyote? Hivi tunaweza kweli kuamua kugawa Zanzibar bila kupigiwa kelele. Mimi naamini kabisa kabisa kuwa kuufanya huu Muungano kuwa sacrosant, ndiyo kunachangia kwa kiasi kikubwa matatizo tuliyo nayo. Tungekubali kuwa unaweza kuvunjika, pengine watu wangekuwa waangalifu zaidi na wanachokisema!

Ingawa secession hairuhusiwi kwenye katiba ya Marekani lakini waliachia Phillipines wakitoe bila tatizo.

Amandla.....
 
yaani hata hii kauli ya kipuuzi iliyotolewa na Kikwete mwanzoni (na niliipinga wakati ule vile vile) watu hawafikirii wanachosema: "NDANI YA TANZANIA ZANZIBAR NI NCHI". Really?

Nadhani kuna ukweli wa kisheria juu ya kauli ya Kikwete. Ukisoma ile hukumu ya rufaa ya kina Machano, mahakama iligusia suala hili la kugawanyika kwa sovereignity (divisibility).
It is our considered opinion that on the basis of this principle of duality and the established fact of exclusive jurisdiction of the Revolutionary Government of Zanzibar over all non-Union Matters in Zanzibar, the only logical conclusion is that sovereignty is divisible within the United Republic.
 
Balaza la wawakilishi lipo kisheria kama ilivyo kwa bunge la jamuhuri. Labda cha kujiuliza hapa ni je, baraza la wawakilishi linayo mamlaka ya kufanya mabadiliko iliyoyafanya katika katiba ya Zanzibar? Kama jibu ni ndiyo, then sioni uhaini unatokea wapi. Ndani ya mipaka ya jamuhuri, zanzibar ni nchi (lakini kimataifa hakuna nchi inayoitwa Zanzibar!)

Kwanza nikiri sijaisoma Katiba ya sasa ya Zanzibar. Hivyo sasa nauliza wanaojua: Katiba hiyo imeweka provision kuhusu chombo chenye uwezo wa kuibadili na masharti ya kubadilishwa huko? Kama masharti yapo, je Baraza la Wawakilishi ndicho chombo halali cha mabadiliko hayo? Je yanayobadilishwa yamo miongoni mwa yanayoruhusiwa kubadilishwa kwa utaratibu waliotumia? Kama jibu la swali langu la mwisho hapo ni 'ndiyo' basi hakuna uhaini bali kuna mgogoro mkubwa wa kikatiba hapo.
 
Back
Top Bottom