Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,474
- 39,987
Kujaribu kuvunja Jamhuri ya Muungano kwa kisingizio chochote kile cha kisiasa ni uhaini. Mnaweza kutafuta kura na support ya wapiga kura lakini ukweli ni kuwa kuna nchi moja ambayo ni Jamhuri ya Muungano ambayo imetokana na kuungana kwa nchi mbili huru za Tanganyika na Zanzibar.
Jaribio la upande mmoja kuirejesha kinyemela nchi iliyokwisha ungana na nyingine ni kutangaza secession kutoka kwa Muungano na viongozi wote wanaopanga kufanya hivyo ni wa kutiwa pingu.
Sijawahi kufikiria kusema JWTZ liangalia ulinzi wa Katiba lakini wakati huu endapo mabadiliko yanayopendekezwa Zanzibar yatafanyika ni wakati wa kuwaangalia hawa "maadui wa ndani".
Ati wenyewe wamekaa kupitisha mabadiliko ya Katiba ya Zanzibar ili kipengele kimojawapo kisomeke hivi:
Kama a. Eneo la Jamhuri ya Muungano ni eneo "LOTE" la Tanzania bara na eneo "LOTE" la TAnzania Zanzibar, sasa Zanzibar ina ENEO GANI ambalo si sehemuya Eneo la Jamhuri ya Muungano? Kama seti moja inahusisha wanyama wote wa mwituni na seti nyingine inauhusisha simba na chui ambao nao ni wanyama wa mwituni, inakuwaje mtu anaanzisha seti nyingine inayosema "wanyama wa mwituni"?
Wanachezea maneno lakini maneno yana maana. Na miye natumia nasema kinachofanyika ni uhaini... (mnaweza kutafuta namna nyingine ya kulikwepa neno hilo). Lakini wataalamu wetu hawa hawa wanasahau Ibara ya 28:3 ya Katiba (waliyoapa kuilinda) inasema nini:
(
Halafu kama watu wasiojua Katiba wanasahau Katika ya Muungano inasemaje kuhusu wakuu wa mikoa. Katiba inasema hivi:
sasa magenius wetu wa Zanzibar wameamua kumnyang'anya madaraka Rais wa Muungano ya kushiriki uteuzi wa wakuu wa mikoa ya Zanzibar kama Katiba ya Muungano inavyotaka na kina Werema wamekaa na tai zao wanachekelea!
Sasa hawa wahuni wa Zanzibar wamepata wapi ujasiri wa kuridhia kuligawa taifa na kutengeneza nchi nyingine nje ya hii NCHI moja? Kuna njia moja tu ya kuunda Nchi ya Zanzibar- KUJITOA kwenye MUUNGANO. Nje ya hapo ni UHAINI!!!
I couldn't be more blunt than that.
Labda nikumbushie sehemu kidogo tu ya hotuba ya Baba wa Taifa kwenye Bunge lililoridhia Muungano Aprili 25, 1964 (msisitizo wangu):
I'm standing on guard, by CHOICE!
Jaribio la upande mmoja kuirejesha kinyemela nchi iliyokwisha ungana na nyingine ni kutangaza secession kutoka kwa Muungano na viongozi wote wanaopanga kufanya hivyo ni wa kutiwa pingu.
Sijawahi kufikiria kusema JWTZ liangalia ulinzi wa Katiba lakini wakati huu endapo mabadiliko yanayopendekezwa Zanzibar yatafanyika ni wakati wa kuwaangalia hawa "maadui wa ndani".
Ati wenyewe wamekaa kupitisha mabadiliko ya Katiba ya Zanzibar ili kipengele kimojawapo kisomeke hivi:
Wenyewe wanashangilia!! Lakini wanasahau kabisa waliapa kulinda Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayosema (msisitizo wangu):Zanzibar ni nchi ambayo eneo lake la mipaka ni eneo lote la visiwa vya unguja na pemba ambayo kabla ya muungano wa Tanganyika na Zanzibar ikiitwa jamhuri ya watu wa Zanzibar ….Zanzibar ni miongoni mwa nchi mbili zinazounda jamhuri ya muungano wa Tanzania
na Magenius wetu hawaoni tatizo hapo: Je hii ni chemsha Bongo? Hivi ukisoma katiba hizo mbili utaelewa kuna nchi "ngapi"? Hivi hata hesabu za seti hawazielewi masikini wa Mungu au somo la mantiki linahitaji kufundishwa kuanzia darasa la kwanza?1. Tanzania ni nchi moja na ni Jamhuri ya Muungano.
2.-(1) Eneo la Jamhuri ya Muungano ni eneo lote la
Tanzania Bara na eneo lote la Tanzania Zanzibar, na ni
pamoja na sehemu yake ya bahari ambayo Tanzania
inapakana nayo.
Kama a. Eneo la Jamhuri ya Muungano ni eneo "LOTE" la Tanzania bara na eneo "LOTE" la TAnzania Zanzibar, sasa Zanzibar ina ENEO GANI ambalo si sehemuya Eneo la Jamhuri ya Muungano? Kama seti moja inahusisha wanyama wote wa mwituni na seti nyingine inauhusisha simba na chui ambao nao ni wanyama wa mwituni, inakuwaje mtu anaanzisha seti nyingine inayosema "wanyama wa mwituni"?
Wanachezea maneno lakini maneno yana maana. Na miye natumia nasema kinachofanyika ni uhaini... (mnaweza kutafuta namna nyingine ya kulikwepa neno hilo). Lakini wataalamu wetu hawa hawa wanasahau Ibara ya 28:3 ya Katiba (waliyoapa kuilinda) inasema nini:
(
3) Mtu yeyote hatakuwa na haki ya kutia sahihi kwenye
mkataba wa kukubali kushindwa vita na kulitoa taifa kwa mshindi,
wala kuridhia au kutambua kitendo cha uvamizi au mgawanyiko
wa Jamhuri ya Muungano au wa sehemu yoyote ya ardhi ya
eneo la taifa na, bila ya kuathiri Katiba hii na sheria zilizowekwa,
hakuna mtu atakayekuwa na haki ya kuwazuia raia wa Jamhuri
ya Muungano kupigana vita dhidi ya adui yeyote anayeshambulia
nchi.
Halafu kama watu wasiojua Katiba wanasahau Katika ya Muungano inasemaje kuhusu wakuu wa mikoa. Katiba inasema hivi:
(3) Wakuu wa Mikoa katika Tanzania Zanzibar watateuliwa na
Rais wa Zanzibar baada ya kushauriana na Rais..
sasa magenius wetu wa Zanzibar wameamua kumnyang'anya madaraka Rais wa Muungano ya kushiriki uteuzi wa wakuu wa mikoa ya Zanzibar kama Katiba ya Muungano inavyotaka na kina Werema wamekaa na tai zao wanachekelea!
Sasa hawa wahuni wa Zanzibar wamepata wapi ujasiri wa kuridhia kuligawa taifa na kutengeneza nchi nyingine nje ya hii NCHI moja? Kuna njia moja tu ya kuunda Nchi ya Zanzibar- KUJITOA kwenye MUUNGANO. Nje ya hapo ni UHAINI!!!
I couldn't be more blunt than that.
Labda nikumbushie sehemu kidogo tu ya hotuba ya Baba wa Taifa kwenye Bunge lililoridhia Muungano Aprili 25, 1964 (msisitizo wangu):
Ooh how prophetic!!!Mr. Speaker and Honourable Members, The Union which I am recommending to this House today is a serious matter, deserving your most deep consideration. It will not be without difficulties. There will be plenty who will see in this development an indication that Africa WILL unite, and they will the exert all their efforts to frustrate our union, sow doubts, and cause disaffection. Against this we have to be on our guard. For once this Union comes into existence it become our duty to protect it and maintain it.
May God help us and our brothers in Zanzibar and Pemba to fulfill this responsibilities.
I'm standing on guard, by CHOICE!