Ni ufisadi wa Spika Samwel Sitta

Mzeepunch umetumwa hapa na spika sitta nini?
Mimi binafsi nimemsikia alivyosema. Ilikuwa ni baada ya kutambulisha utitiri wa wageni wa bunge.
Kwanza nashangaa mzeepunch ulivyohusisha thread hii na Tanzania Daima wakati ameitaja ikiwa ya pili baada ya gazeti la Tazama. Sasa mbona Tazama haimo kwenye heading yako? inaonekana amekutuma uiseme TD.
Kwa mujibu wa maelezo yake nimeona ni kama anavyofanya siku zote anapotuhumiwa. Huwa ana kawaida ya kusukumia zigo kwa wabaya wake kisiasa bila ya kuwataja ni wapi hao na siku zote amekuwa akiwa link na magazeti lakini hajawahi kukana tuhuma nzito zinazomkabili, ikimaanisha ni kweli yale anayotuhumiwa ila tu sasa wabaya wake wame capitalize kwa hayo ili kumbomoa. Hii haiwezi kumuepusha na tuhuma na lazima awajibike kuliko kulialia.
Yeye amekuwa akijifanya msafi kumbe si msafi kiasi hicho hicho kidogo kama wengine.
Kisha angalia alivyojichanganya. Yeye anasema kuwa wabaya wake wanakaa na magazeti na kufanya mikakati kutengeneza tuhuma kuanzia kwenye mitandao na kisha magazeti yanajifanya ku refer habari hizo kwenye mtandao. Bila shaka hapa inahusishwa JF. Lakini anasahau kuwa kashfa nyingi sana zimeanzia hapa JF na hata kuleta mabadiliko yasiyo ya kawaida.
Na kwa sababu hiyo si ajabu mzeepunch katumwa kuja kufanya matengenezo kwa kuleta haya anayoleta. Ningeamini anayosema kama angesema yote aliyosema mzee Sitta.
Mwisho siwezi kuamini yote anayotuhumiwa Sitta lakini kuna moja ninalojua kwa hakika huyu mzee ni mgonjwa kwalo nalo ni kufungua zip. Hapo kwa namna yoyote kuna kaukweli maana huu huwa ni ugonjwa wake.
Na sisi yeye pekee bali waheshimiwa wetu wengi wana kaugonjwa haka.
Anaweza kujitetea anavyoweza lakini ukweli utabaki rohoni mwake.

Mkuu MF, Mh S. Sitta alitakiwa kutueleza ukweli kama yeye anaamini kuwa wabaya wake wanasambaza uongo. Anapotumia mtindo kama wa mafisadi ambao tumekuwa tukiwaona wanajitetea kwa midomo na bahasha kwa waandishi hawezi kufuta hilo doa. Wengi tutaendelea kuamini kinachosemwa hata kama siyo kweli. Atupe ukweli wenyewe tujiridhikie na roho zetu.

Mzee Punch amesema kuwa Wahariri wa TZ Daima wamenunuliwa na RA ili wamshughulikie Spika SS. Hizi ni tuhuma nzito sana. Ili tuweza kuwatendea haki watu hao ambao mimi nawaheshimu sana, basi atoe ushahidi au afute kauli yake na kuwaomba radhi wote ambao tumesubuliwa kwa namna moja au nyingine na matamshi hayo. Hili gazeti linaheshimika sana na haliwezi kutuhumiwa kulala kitanda kimoja na mafisadi tukakaa kimya. These are very serious allegations which need to be backed with strong proofs. Kama ni udaku basi hata thread nzima ipigwe chini.
 
Nyie mnadhani EL ana raha huko aliko???
kumbuka kuna watu wapo ktk payroll ya mafisadi na wanaweza kufanya chochote ilimradi kutimiza lengo.

Ninaililia TISS imara kwani hii iliyoko sasa inaonesha meno yake ni kwa wanaoipenda nchi huku ikiwalinda na kuwasafisha wanaoitafuna nchi kwa kasi.

Kuhusu hoja dhidi ya SITTA nasita kuamini au kukataa kwani ktk kuelekea 2010 tutasikia na kuona mengi. Msimu huu hata wenye magego watavunja mifupa.

Ila amini amini nakuambieni kuna usaliti. tena usaliti mbaya sana wa kidhamira na kiuhalisia ambapo kuna kundi la watanzania wasio wazalendo wameamua kufanya lolote ilimradi walinde maslahi yao au waliowatuma. Tunaishi nao, tunakula nao ila wana lao moyoni. hawatanyamaa mpaka watimie. Sijui kesho tukiamka tutasikia jipya gani.
 
punch babu kafulia, tunataka six ajbu kama ni kweli au laa! je ni sahihi au laa!! very simple, tatizo viongozi wetu wapo too proud kujieleza au kujishusha for the sake of peace their peoples minds and doughts! hapo ndo ubabe unainingia sasa! lakini akitetea hata hizo 10m u never know akatoa hoja wenyewe tukakubali, but anakataa km mtoto mdogo? mi staki why? ni sitaki tu!! alaaH!
 
nampenda sana sita, kwanza, ni lazima kama tunataka democrasia au kama tunataka uwajibikaji wa wabunge na mawaziri pale bungeni, rais mpya mwakani anatakiwa kumchukua sita aendelee kuwa spika. kama hatafanya hivyo, hakika uchafu tu utaingia kule. ni spika bora kuliko wote waliowahi kutokea. hafagilii mafisadi, akiona fisadi linashambuliwa anaacha likipate kwanza...hahaha. angekuwa pius msekwa kama tulivyomzoea, nakwambia pale angekuwa amekaa tu kwaajili ya ccm, na asingeacha maovu kunyumbuliwa kama ilivyo sasa. ila spika nafurahi sana kwasababu, ni mmoja wa wapiga vita mafisadi. utadhani ni wa chama cha upinzani vila. hakina nakwambia, kama tunataka bunge zuri, ni lazima aendelee. Mungu ambariki sana.
 
Kama hamjui ni kwamba kuna kampeni maalum ya akina EL na RA kummaliza Sitta. Mimi nachukia mafisadi, na hata ikithibitika kwamba Sitta ni fisadi nitamchukia, kama ninavyowachukia hao wengine. Lakini kilichoni-touch ni kuona kwamba tuhuma zinazoelekezwa kwa Sitta, kama ni za kweli au la, zinaandikwa kwenye hayo magazeti yaliyotajwa kwa ufadhili wa EL na RA. Ninao ushahidi! Anayetaka aniandikie PM.
 
Najua kuna watakaonichukia kwa ukweli huu kuhusu kutumiwa kwa haya magazeti na watasema lolote. Lakini Walatini walisema 'VERITAS ODIUM PARET' (Truth creates hatred). Mimi ni mtu ninayefanya uchunguzi wangu independently na ninapata facts zote muhimu. Siwajui hao wahariri wa Tanzania Daima na wala sifahamiani na Sitta zaidi ya kumuona kwenye runinga, lakini ninazo facts za kutosha kuhusu kinachoendelea.
 
nawewe Punch sijui pancha huelewi nini hapo? hata kama ni mbinu za kumchafua six si atoe maelezo ya anayochafuliwa nayo? ili tujue wazi kuwa ni mbinu chafu! then watashindwa kuendelea, wewe basi mzee wa mtandao tuambie hizo tuhuma uzineutralize kwa kuzijazia uhalisia wake! rent! furniture, m-benz for 300+M! si we unabisha as if unajua ukweli? mwaga data jamvini tuseme nazo watalam
 
afadhali leo kawatolea uvivu tanznia daima full aibu laziama tuseme ukweli spika sitta ameboresha Bunge kwa kiasi kikubwa kiasi cha mawaziri kuongeza uwajibikaji hata kama anakula pesa poaa tu ilimradi Bunge linakuwa imara . Msekwa amekula wee na Bunge likwa muhuri wa serikali tu so hawa nafisadi , kibanda absolom, charles mullinda ni sawa tu na wanyma wakufugwa wasiojitafutia namuomba mbowe awatimue mara moja huko kwani huko mbeleni watamwaribia hadi CHADEMA.

duh!...i hope u didn't mean that!(hiyo kwenye nyekundu)
Kama hiyo ripoti ya hao wafanyakazi wa bunge ni uongo, solution ni moja, waite kampuni ya auditing kuja kuchunguza hesabu. Kwani kuna taabu hapo? Sina imani na chombo kingine chochote isipokuwa cha nje ya nchi kisicho na affiliation yeyote.
 
Wote sasa mawazo yao ni jinsi gani watarudi Bungeni tena, hivyo tutasikia na kuona mengi. Na sasa ndio wakatitutaanza kuwaona katika majimbo yetu wakija kutulaghai kwa mara nyingine, miaka yote walikuwa wakiishi Dar, kama sio Dar miji kama mijini (Arusha, Mwanza nk).


Si wanajua wadangamyika walivyo watakuja na hadithi hewa na ahadi kem kem na kwa matuamini makubwa wananchi walio wengi na waliopigika bado watawapa kura.Mimi kura yangu hawaipati ng'o na nafiki watu wengi wameanza kuwaelewa sasa kuwa hawa wabunge walio wengi ni wababaishaji tuu,hawatetei maslahi ya watanzania ila wanaangalia nasfi zao binafsi.Hawafai.
 
nawewe Punch sijui pancha huelewi nini hapo? hata kama ni mbinu za kumchafua six si atoe maelezo ya anayochafuliwa nayo? ili tujue wazi kuwa ni mbinu chafu! then watashindwa kuendelea, wewe basi mzee wa mtandao tuambie hizo tuhuma uzineutralize kwa kuzijazia uhalisia wake! rent! furniture, m-benz for 300+M! si we unabisha as if unajua ukweli? mwaga data jamvini tuseme nazo watalam

Jina liko very clear! PUNCH. Sasa hiyo Pancha imetoka wapi ndugu yangu. Au ni uchokozi tu. Anyway! Ila amini amini nakuambia ipo siku kila fisadi atawekwa hadharani kwa ushahidi usiopingikai. Nafanya kazi usiku na mchana ku-gather data na facts zote kuhusu viongozi wote mafisadi. Hili la Sitta tayari nalifanyia kazi. But it really gets on my nerves when people like RA or EL point an accusing fingure at SS. They don't have moral authority to do so! Nachukia zaidi wanahabari tunaowategemea wanapokubali kutumiwa na hawa mafisadi. Stop this prostitution!
 
Last edited:
yaaap kaka it seems upo ktk payroll,sasa kamba hukatika pabovu, labda nawewe punch utoe msimamo wako je hizo tuhuma ni sahihi kiongozi kuspend namna hiyo? achana na ni za uwongo/ukweli forgrt it, kwani hujazilaumu bali umengangania EL na RA tuuuu! just kuwa wazi, may be sisi tunachemka
 
We mzee Punch nafikiri umetumwakatika tasnia ya habari mtu aliyetajwa kwenye habari tena akihusishwa na tuhuma kama Spika wako 6 si lazima kile alichojitetea ukichukulie kama ndiyo ukweli wenyewe.we sema wazi kwamba umetumwa au una ugomvi na wahariri tajwa kwani kwa mtu anayefuatilia vyomvo vya habari atakubalina na minmi kuwa Tanzania daima ni moja ya magazeti yanayoandika mambo ya kusaidia nchi yetu.ugomvi wako na mulinda/kibanda peleka huko huko tujadili issue hapa kama wamekosea tupatie uweli wako siyo kuegemea kwenye utetezi wa spika(mtuhumiwa) sasa wew ulifikiri sita atakubalianana madai ya gazeti pole sana......chao
 
The speaker should stop beating around the bush, also he must refrain from attacking the messenger "Tanzania Daima." The allegations leveled against are serious ones,and more importantly have merits. It is imperative for the speaker to understand that by simply blaming the media and Mafisadi will not be enough to let him off the hook. The only way he can be vindicated from the aforementioned allegations will be by coming forward, and explain to Tanzanins in detail why he allowed his office to embark on a wasteful spending spree.
 
Last edited:
hii nchi itakuja kufilisika na ndio siku mwananchi anakwenda siku mbili bila ya kutia kitu tumboni ndio moto utakapoanza kuwaka sasa.
 
Nimesoma kote, sijaona ni wapi hasa kaliumbua gazeti, zaidi ya kukanusha tuhuma ambazo zipo wazi kabisa! Alaumu matendo yake mwenyewe, na sio gazeti. Pole wee!
 
nasema simwamini mzee mwanakijiji ni fisadi na anatumiwa ipo siku mtakubaliana na mimi nimemchunguza sana na hivi sasa nafanya security inteligence tracking juu yake ni mtu hatari sana.
 
nasema simwamini mzee mwanakijiji ni fisadi na anatumiwa ipo siku mtakubaliana na mimi nimemchunguza sana na hivi sasa nafanya security inteligence tracking juu yake ni mtu hatari sana.

si uweke mtutu wa bunduki kichwani mwangu halafu ufyatue ili uondokane na "hatari" hiyo?
 
Back
Top Bottom