Dark City
JF-Expert Member
- Oct 18, 2008
- 16,253
- 11,599
Mzeepunch umetumwa hapa na spika sitta nini?
Mimi binafsi nimemsikia alivyosema. Ilikuwa ni baada ya kutambulisha utitiri wa wageni wa bunge.
Kwanza nashangaa mzeepunch ulivyohusisha thread hii na Tanzania Daima wakati ameitaja ikiwa ya pili baada ya gazeti la Tazama. Sasa mbona Tazama haimo kwenye heading yako? inaonekana amekutuma uiseme TD.
Kwa mujibu wa maelezo yake nimeona ni kama anavyofanya siku zote anapotuhumiwa. Huwa ana kawaida ya kusukumia zigo kwa wabaya wake kisiasa bila ya kuwataja ni wapi hao na siku zote amekuwa akiwa link na magazeti lakini hajawahi kukana tuhuma nzito zinazomkabili, ikimaanisha ni kweli yale anayotuhumiwa ila tu sasa wabaya wake wame capitalize kwa hayo ili kumbomoa. Hii haiwezi kumuepusha na tuhuma na lazima awajibike kuliko kulialia.
Yeye amekuwa akijifanya msafi kumbe si msafi kiasi hicho hicho kidogo kama wengine.
Kisha angalia alivyojichanganya. Yeye anasema kuwa wabaya wake wanakaa na magazeti na kufanya mikakati kutengeneza tuhuma kuanzia kwenye mitandao na kisha magazeti yanajifanya ku refer habari hizo kwenye mtandao. Bila shaka hapa inahusishwa JF. Lakini anasahau kuwa kashfa nyingi sana zimeanzia hapa JF na hata kuleta mabadiliko yasiyo ya kawaida.
Na kwa sababu hiyo si ajabu mzeepunch katumwa kuja kufanya matengenezo kwa kuleta haya anayoleta. Ningeamini anayosema kama angesema yote aliyosema mzee Sitta.
Mwisho siwezi kuamini yote anayotuhumiwa Sitta lakini kuna moja ninalojua kwa hakika huyu mzee ni mgonjwa kwalo nalo ni kufungua zip. Hapo kwa namna yoyote kuna kaukweli maana huu huwa ni ugonjwa wake.
Na sisi yeye pekee bali waheshimiwa wetu wengi wana kaugonjwa haka.
Anaweza kujitetea anavyoweza lakini ukweli utabaki rohoni mwake.
Mkuu MF, Mh S. Sitta alitakiwa kutueleza ukweli kama yeye anaamini kuwa wabaya wake wanasambaza uongo. Anapotumia mtindo kama wa mafisadi ambao tumekuwa tukiwaona wanajitetea kwa midomo na bahasha kwa waandishi hawezi kufuta hilo doa. Wengi tutaendelea kuamini kinachosemwa hata kama siyo kweli. Atupe ukweli wenyewe tujiridhikie na roho zetu.
Mzee Punch amesema kuwa Wahariri wa TZ Daima wamenunuliwa na RA ili wamshughulikie Spika SS. Hizi ni tuhuma nzito sana. Ili tuweza kuwatendea haki watu hao ambao mimi nawaheshimu sana, basi atoe ushahidi au afute kauli yake na kuwaomba radhi wote ambao tumesubuliwa kwa namna moja au nyingine na matamshi hayo. Hili gazeti linaheshimika sana na haliwezi kutuhumiwa kulala kitanda kimoja na mafisadi tukakaa kimya. These are very serious allegations which need to be backed with strong proofs. Kama ni udaku basi hata thread nzima ipigwe chini.