Ni tukio gani lilitokea ukiwa mbali na mazingira husika ukatamani ungekuwepo kwa muda huo?

Half american

JF-Expert Member
Sep 21, 2018
26,184
68,521
Habari wakuu, maisha yana mjumuiko wa matukio mengi sana.

Kuna matukio ambayo wengi wetu tunapenda kuyasikia sana na hayatupi shida yeyote, haya ni matukio mazuri au habari njema mfano, kupata mtoto, mavuno mazuri n.k
Kuna matukio tusiyopenda kuyasikia ni mwiba mkali maishani mwetu kwa wakati husika, haya ni matukio mabaya au habari mbaya. Kwa mfano fumanizi, ugomvi wa familia, ajali n.k

Haya matukio ni kawaida sana kutokea kwenye jamii na maisha yetu. Kuna muda upo mbali na linatokea tukio ambalo unahisi ungekuwepo karibu ungeweza kufanya kitu. Kwa wakati huo zinakujia hisia unatamani hata ungekuwa na mbawa upae ufike eneo la tukio ufanye chochote kizuri au kibaya(ukizingatia matukio yanatofautiana). Lakini kiuhalisia ni jambo lisilowezekana ni hisia tu kutokana na kinachoendelea mbali na ulipo.

Tukio la kwanza. Nakumbuka hali hii ilinitokea nilipopewa taarifa za kuumwa kwa bibi yangu na alikataa katu kwenda hospital, ni miongoni mwa watu niliokuwa nawapenda sana, nilitamani sana ningekuwepo alipo nimuone na niongee nae maana kipindi cha nyuma nilikuwa naongea nae mpaka anakubali kwenda, haikupita masaa mawili nikapokea taarifa za kifo chake. Huenda ningekuwa karibu ningekuwa msaada kwa namna moja. Niliumia sana may her soul R I P.

Tukio la pili. Long distance relationship, hakika fimbo ya mbali haiui nyoka. Mtu ananiambia yupo na wenzie hostel hajui kama mwanaume alienae kashaiba namba zangu kwenye simu yake na anawasiliana na mimi na picha kanitumia wakiwa wote. Nilitamani nipae nimuibukie alipo maana ile hasira na maumivu hayakuwa ya kawaida. Niliamua kumuacha kimya kimya ila nilikoma.

Habari nyingine nikizisikia natamani niwe eneo husika ni taarifa za kuuguliwa na wazazi wangu, huwa simu zinaita sana mpaka hali iwe shwari.

Matukio yapo mengi share lako zuri au baya.

Siku njema wadau.
 
Da, tukio ambalo nalikumbuka, mdogo wangu alichoma nyumba, vitu vyote vya ndani vikaungua... Safari ya maisha yakaaza upya tena.
Pole sana, hili limenikumbusha kuna watoto walikuwa peke yao nyumbani kwao mmoja akawa anachezea kiberiti na kuwasha makaratasi na mwisho moto kuwa mkubwa ambapo mdogo wake alifia ndani
Mpaka leo anajuta maana kesi iliandikwa ajali ya moto
 
Tukio la gari ya bank kupinduka halafu watu wameshuka na kuanza kuokota hela
Hata wewe ungeomba upae hapo
Screenshot_20231217_095058_Google~2.png
 
Habari wakuu, maisha yana mjumuiko wa matukio mengi sana.

Kuna matukio ambayo wengi wetu tunapenda kuyasikia sana na hayatupi shida yeyote, haya ni matukio mazuri au habari njema mfano, kupata mtoto, mavuno mazuri n.k
Kuna matukio tusiyopenda kuyasikia ni mwiba mkali maishani mwetu kwa wakati husika, haya ni matukio mabaya au habari mbaya. Kwa mfano fumanizi, ugomvi wa familia, ajali n.k

Haya matukio ni kawaida sana kutokea kwenye jamii na maisha yetu. Kuna muda upo mbali na linatokea tukio ambalo unahisi ungekuwepo karibu ungeweza kufanya kitu. Kwa wakati huo zinakujia hisia unatamani hata ungekuwa na mbawa upae ufike eneo la tukio ufanye chochote kizuri au kibaya(ukizingatia matukio yanatofautiana). Lakini kiuhalisia ni jambo lisilowezekana ni hisia tu kutokana na kinachoendelea mbali na ulipo.

Tukio la kwanza. Nakumbuka hali hii ilinitokea nilipopewa taarifa za kuumwa kwa bibi yangu na alikataa katu kwenda hospital, ni miongoni mwa watu niliokuwa nawapenda sana, nilitamani sana ningekuwepo alipo nimuone na niongee nae maana kipindi cha nyuma nilikuwa naongea nae mpaka anakubali kwenda, haikupita masaa mawili nikapokea taarifa za kifo chake. Huenda ningekuwa karibu ningekuwa msaada kwa namna moja. Niliumia sana may her soul R I P.

Tukio la pili. Long distance relationship, hakika fimbo ya mbali haiui nyoka. Mtu ananiambia yupo na wenzie hostel hajui kama mwanaume alienae kashaiba namba zangu kwenye simu yake na anawasiliana na mimi na picha kanitumia wakiwa wote. Nilitamani nipae nimuibukie alipo maana ile hasira na maumivu hayakuwa ya kawaida. Niliamua kumuacha kimya kimya ila nilikoma.

Habari nyingine nikizisikia natamani niwe eneo husika ni taarifa za kuuguliwa na wazazi wangu, huwa simu zinaita sana mpaka hali iwe shwari.

Matukio yapo mengi share lako zuri au baya.

Siku njema wadau.
Hilo namba 2 ndio maana vijana wanakataa ndoa🤣

Tukio langu 2 weeks ago liko kinyume,natamani nisingekuwepo.
 
Ni utundu tu, alipigisha short ya umeme, ilikua balaa sana 😟
Ila kesi nyingi za moto hasa maeneo ya nje ya miji chanzo ni watoto kuchezea moto. Kuna mtoto alikuwa anatafuta kiatu uvunguni aliingia na kisosi chenye mshumaa, alivyopata kiatu akaacha mshumaa ukawaka ukakamata godoro wanakuja kushtuka ilikuwa too late nyumba ikateketea yote.
 
Back
Top Bottom