Mapenzi ya Michael na Shirley Garvin, yalivyogeuka tukio la mauaji

Intelligent businessman

JF-Expert Member
Sep 6, 2022
26,109
52,835
AMEPOTEA KISIWANI KEY WEST - 1 Umewahi kujua kwamba taa za barabarani huwekwa pia Kamera? Si kwa Tanzania, lakini katika miji mingine mikubwa taa za barabarani huwekwa Kamera ili ziweze kunakiri matukio mbalimbali na kusaidia vyombo vya ulinzi na usalama.

Fuatilia kisa hiki cha mwanaume mmoja aliyepotelewa na mke wake huko kisiwani Key West, nchini Marekani.

-------

Katika miji ambayo mitaa yake imefungwa kamera maalumu za kunasa matukio, karibu kila tendo linalofanyika mitaani hunaswa na kumbukumbu zake huhifadhiwa. Teknolojia ya leo inafanya matumizi ya simu hata kwa sekunde moja tu, kutosha kujua mahali mtumiaji wa simu alipo. Kila dakika, mfumo wa kutambua mahali alipo mtu au kilipo kitu, maarufu kama GPS (Global Position System) husaidia kuangalia mienendo ya vyombo vya usafiri vya ardhini na majini.

Kwa msaada wa teknolojia hiyo ya mawasiliano, katika miji miwili wapelelezi waligundua uhalifu uliotokana na usaliti, tamaa na uroho.

Ilikuwa siku ya mwezi wa Januari, 2003, Michael Garvin, wakala wa majengo na mmiliki wa kampuni ya Magnolia Properties aliondoka nyumani kwake mjini Jacksonville akiwa na mkewe Shirley kwenda kisiwa cha Key West kwa ajili ya mapumziko ya ‘weekend’. Asubuhi ya kwanza akiwa kisiwani huko, Michael alitembea hadi duka la dawa la karibu na kununua dawa kwa ajili ya mkewe. Aliporudi hotelini lisaa limoja baadaye, Shirley hakuwepo.

Michael alifikiri mkewe amekwenda mgahawani au pengine amekwenda kujinunulia mahitaji yake binafsi. Lakini alipogundua kuwa mkoba wa mkewe upo katika chumba kile cha hoteli, alianza kuhisi dalili ya jambo baya. Baada ya masaa mengi bila mkewe kurudi, Michael aliamua kupiga simu kituo cha polisi na kuripoti kuwa mkewe amepotea.

Maofisa wa polisi walipowahoji wahudumu wa hoteli, hakuna hata mmoja wao aliyekuwa amemuona Shirley asubuhi ile. Ndugu na jamaa walianza kupata mashaka, lakini habari za kustua ni kuwa Shirley si tu hakuwepo hotelini, bali hakuwepo katika kisiwa cha Key West. Tayari maofisa wa polisi kwa kushirikiana na vyombo vingine vilijiridhisha kuwa Shriley hayupo ndani ya kisiwa kile kidogo. Hakukuwa na mtu mwenye taarifa za mrembo huyo. Ndugu zake waliwaambia polisi kuwa wajaribu kufuatilia maduka ya vito vya thamani kwa sababu ndugu yao alipenda sana kuvaa pete na mikufu ya thamani kubwa. Lakini hata hilo halikusaidia.

Sasa maofisa wa polisi waliamua kuanza uchunguzi wa kimahakama mara moja kwa kutafuta alama za vidole za mtu tofauti na wawili wale yaani Michael na Shirley, ndani ya chumba chao cha hoteli. Hakukuwa na alama za vidole za mtu mgeni. Mbwa maalumu aliyefunzwa kunusa na kujua endapo kuna mgeni aliingia chumbani humo lakini hakupata taarifa yoyote.

Siku iliyofuata, habari ilitoka katika gazeti moja kisiwani humo ikiwa na kichwa cha habari kinachosema; ‘Nini kimetokea kwa Shirley Garvin’? Vyombo vya habari vilitangaza taarifa hiyo na kuwaomba wafuatiliaji kutoa taarifa zozote zitakazosaidia, lakini hakukuwa na taarifa.

Maofisa wa polisi na wapelelezi waliendelea kumtafuta Shirley katika maeneo yote ya kisiwa cha Key West ambacho kina ukubwa wa maili za mraba sita tu, bila mafanikio. Lakini walifanikiwa kupata jozi ya viatu vya wazi (sandals) vilivyofanana na viatu vya Shirley. Jambo hilo lilijenga hisia kuwa pengine Shirley alikuwa amezama baharini. Lakini pia kulikuwa na taarifa nyingine ya kutilia maanani.

download (15).jpeg
download (12).jpeg
 
AMEPOTEA KISIWANI KEY WEST - 2

Michael Garvin anatoa taarifa ya kupotelewa mkewe mara tu walipofika Kisiwani Key West kwa ajili ya mapumziko. Lakini maofisa wa upelelezi wana gundua taarifa tofauti na za kushtusha. Ni kisa cha mauaji yaliyo tokana na usaliti, tamaa na uroho.


Kabla ya Michael Garvin kukutana na kufunga ndoana Shirley, ali kwisha kuwa na mke mwingine hukonyuma ambaye alijiua kwa kujinyonga kwenye chumba cha chini ndani ya nyumba yao au maarufu kama
‘basement. Michael ndiye alikuwa mtu wa kwanza kukuta mwili wa marehemu, na ndiye aliyetoa taarifa polisi.

Na sasa mkewe mwingine mwenye umri wa miaka 55amepotea ndani ya kisiwa cha Key West na Michael Garvin ndiye mtu aliyeto taarifa polisi. Wakati wapelelezi wakiendelea kufanya
uchunguzi walitamani pia kujua historia na tabia ya mtu aliyepotea, yaani Shirley Garvin. Kwa hiyo walifanya mahojiano
na mumewe, Michael ili kupata taarifa nyingi za Shirley kadiri inavyowezekana. Maofisa wa polisi walimtaka Michael kuanza kueleza kila walichofanya tangu walipofika kisiwani humo. Michael alieleza kuwa walianza kuchukua chumba cha hoteli, kisha yeye alitoka kwenda kuchukua chakula cha jioni kwa ajili ya wote wawili. Michael anasema, alichukua kuku,(Chicken Sandwich) na vyakula vingine kwa ajili yakena mkewe. Wapelelezi wali nakili kila neno litokalo kwenye kinywa cha Michael na kuendelea na uchunguzi wao

Aliyefuatia kuhojiwa ni muhudumu wa mgawaha ambapo michael
alikwenda kununua chakula. Muhudumi alipo hojiwa alisema Michael alichukua chakula cha mtu mmoja tu, na sio watu wawili kama alivyodai. Hata nakala ya risiti ya manunuzi ilitoa uhakika kuwa Michael
aliagiza chakula cha mtu mmoja pale mgahawani. Umewahi kudhani kwamba risiti ya mgahawani yaweza kuwa kielezo muhimu katika upelelezi?

Taarifa hizo zilimfanya mpelelezi Bill Larkin kutilia mashaka maelezo ya Michael, na hata kupata hisia kwamba, pengine Shirley hakuwa na Michael katika safari hiyo ya mapumziko katika kisiwa cha Key West.

Polisi walichunguza pia kadi ya malipo (credit card) ya Michael na kugundua kuwa, akiwa safarini kuelekea kisiwa cha
Key West, Michael alisimama mjini Miami, akaingia dukani na kufanya manunuzi.

Mara moja, wapelelezi walisafiri hadi mjini Miami katika duka lile alipoingia Michael kufanya manunuzi. Uchunguzi ulifanyika kwenye Kamera za ulinzi maarufu kama CCTV, na kamera hizo za ulinzi zilimuonesha Michael akiwapeke yake ndani ya duka hilo. Pamoja na taarifa hiyo, Polisi hawa kuweza
kujua mara moja kama mkewe Michael alibaki kwenye gari, au hakuwepo kabisa katika safari hiyo.

Baadaye maofisa wa upelelezi waliamua kuchunguza kameraza ulinzi za barabarani zilizopo kwenye geti la kutoka mjini
Jacksonville kwenda Key West.

Walichambua maelfu ya magari yaliyopita eneo hilo, moja baada ya llingine,
hadi kufanikiwa kuliona gari la Michael aina ya Jaguar,lenye rangi nyeupe likipita eneo hilo majira ya saa9:10:31 mchana wa tarehe 27, Januari 2003. Baada yakukuza picha ya gari lile la Michael, wapelelezi
hawa kuona mtu kwenye kiti cha abiria cha mbele. Naam, Michael alikuwa peke yake mbele ya gari. Je! Shirley alikuwamo siti za nyuma?

Kabla ya kumuonesha Michael picha hizo
zilizo patikana kwenye kamera za
barabarani, wapelelezi walimuomba Michael aeleze namna yeye na mkewe walivyokaa ndani ya gari yao wakati wa safari.

Mke wako alikaa kwenye kiti kipi ndani ya gari? Wapelelezi waliuliza.
Naye bila kuchezwa na machale, Michael alijibu kuwa Shirley alikaa kwenye kiti cha
mbele cha abiria.

Alipoulizwa tena kama Shirley alihama
kiti wakati fulani wa safari na kuhamia siti ya nyuma,Michael alikataa.

Akaulizwa tena kama Shirley alishuka
kwenye gari wakati wowote, Michael akakataa.

Aliendelea kueleza kwamba mkewe alikaa kiti chambele cha abiria kutoka mwanzo wa safari hadi mwisho. Hapo ndipo wapelelezi walipomuonesha picha yagari zilizonaswa kwenye kamera za barabarani, huku
kiti cha mbele cha abiria kikiwa kitupu.

Michael Garvinakakosa maelezo ya ziada, akaanza kuwa mkali nakuweweseka.Maofisa wa upelelezi hawakuishia hapo, waliamuakuwahoji wafanyakazi wenza wa Michael katika ofisiya wakala wa majengo huko mjini Jacksonville. Lakinibaadhi ya wafanyakazi walishangaa kusikia kuwa
Michael alikuwa ameoa. Jambo hilo liliwashangazamaofisa wa upelelezi kwa sababu taarifa zilioneshakuwa Michael alifunga ndoa miaka 16 iliyopita lakini ya watu pale kazini hawakuwa wakijua. Jambolingine walilofanya wapelelezi ni kupekua nyumba yaMichael, lakini kwa macho ya kawaida kila kitukilikuwa sawa.

Mtaalamu wa uchunguzi wa eneo la
tukio la uhalifu (Crime Scene Technician) alitumia taamaalum kutafuta vielelezo vya ushahidi wowote ndani yanyumba huku akiwa amezima taa zote za kawaida na kumulika kwa taa maalum, lakini hakupata kitu.

Mtaalam wa Kompyuta wa timu ya upelelezi aliamua kuchunguza 'hard drive’ kwenye Kompyuta ya Michael na kugundua kuwa Michael alikuwa mtu wakujichanganya sana kinyume na tabia za watu walio
kwenye ndoa. Michael aliwasiliana na kukutana nawanawake wengi kupitia mitandao ya kijamii,alipanga kuonana nawo na kuwatumia zawadi namaua. Aliishi maisha ya mtu asiye na ndoa. Mtaalamu
wa Kompyuta alifanikiwa kuona tangazo la Michael kwenye tovuti ya 'Match’ ambayo hutumiwa nawatu kutafuta wapenzi.

Kwenye tangazo hilo taarifa za Michael zilionesha kuwa ni mtu aliyeachana na
mkewe, au ‘Divorced'. Lakini taarifa zote hizo hazikutoajibu kuhusu wapi alipo mwanamke aliyepotea, Shirley
Garvin.

Yupo wapi Shirley Fleming Garvin?
download (11).jpeg
 
AMEPOTEA KISIWANI KEY WEST - 3
Ni simulizi ya mauaji yaliyotokana na Tamaa na Visasi. Mwanaume Michael Garvin anasafiri hadi kisiwani Key West kwa ajili ya mapumziko, kisha anatoa taarifa za kupotelewa na mkewe aliyesafiri naye kisiwani hapo. Baada ya maofisa wa polisi kuanza uchunguzi wa kimahakama ili kupata jawabu la kupotea kwa mwanama huyo aloyeitwa Shirley Garvin, wanagundua simulizi tofauti kabisa.

Emma Willis, rafiki wa karibu wa Shirley Garvin alikuja na taarifa nyingine. Emma aliwaambia wapelelezi kuwa Shirley alikuwa na mpango wa kumuacha Michael na kutoroka. Emma aliongeza kuwa, Shirley
alikuwa akilalamika kuwa Michael hana nidhamu katika matumizi ya fedha na kwamba ana madeni mengi. Wapelelezi walipochunguza taarifa za kibenki za Michael na Shirley waligundua kuwa kadi ya malipo ya Michael ilikuwa ikidaiwa dola za kimarekani Elfu 86 huku mali nyingi za wawili hao zikiwa na jina la mwanaume Michael.

Kwa ajili ya uchunguzi zaidi, wapelelezi waliamua kuchunguza mienendo ya mawasiliano ya simu na safari za gari za Michael alizofanya wakati uchunguzi
ukiendelea. Wapelelezi walitumia mfumo wa satelaiti ili kupakua taarifa zilizopo kwenye kifaa cha GPS kilichokuwapo kwenye gari la Michael.

Siku hizi, wapelelezi hawana tena haja ya kuuliza kuhusu mahali gari ilipokuwa kwa wakati fulani, satelaiti
hufanya kazi hiyo. Mfumo wa GPS hufungwa kwenye gari na kurusha taarifa hadi kwenye satelaiti. Taarifa za picha za gari na mazingira ya jirani huweza kupakuliwa na kuchunguzwa.Teknolojia hiyo iliwasaidia wapelelezi kupata taarifa za gari la Michael na mazingira ya jirani ikiwa ni pamoja na matukio yaliotokea jirani na gari.

Uchunguzi uliendelea huku Michael akiwa huru akiendelea na shughuli zake. Maofisa walipotaka kumuhoji walimuita, huku wakifuatilia mienendo yake kimyakimya.

Wiki sita sasa tangu Shirley Garvin atoweke machoni pa ndugu jamaa na marafiki. Maofisa wa upelelezi wakifuatilia mienendo ya safari za Michael waliona kupitia GPS akiendesha gari yake hadi kwenye eneo lenye uwanja wa 'golf' na nyumba moja iliyotengwa, umbali wa maili 20 kutoka Nyumbani kwake. Uchunguzi ulibaini zaidi
jambo la kuvutia, kwamba siku ya asubuhi ya safari ya kuelekea kisiwani Key West, yaani wiki sita zilizopita, Michael alipokea simu kutoka eneo hilo aliposafiri sasa. Taarifa hizo zilizopatikana kwa msaada wa mfumo wa GPS, zilionesha kuwa siku hiyo Michael alitumia muda wa takribani dakika 20 katika eneo hilo kabla ya kusafiri
kwenda kisiwani Key West.

Eneo hilo lilikuwa na bwawa dogo la maji machafu. Maofisa wa upelelezi walifika na kukagua eneo hilo kwa kina. Baada ya kuhisi labda ndani ya bwawa lile kuna mwili wa Shirley Garvin, waliamua kuondoa maji yote kwa kuyavuta kwa mpira na mashine maalumu, zoezi lilochukua wiki moja.Hata hivyo hawakupata kitu chochote.

Siku 10 baadaye, mfumo wa GPS ulionesha
Michael akielekea eneo lilelile. Mtu aliyetumwa kumfuatilia Michael aliona msichana akishuka kwenye gari ile, msichana ambaye baadaye ilijulikana kumbe waliwasiliana mitandaoni na kuamua kukutana na Michael.

Michael na msichana yule walipoondoka, Polisi walifika katika eneo lile na kujaribu kuchunguza kama wanaweza kupata taarifa yoyote ya muhimu. Mpelelezi Michelle O’neil aligundua kitu tofauti. Aliona eneo ambalo halikuwa na majani tofauti na maeneo mengine yalivyokuwa, kana kwamba eneo hilo lilichimbuliwa siku kadhaa nyuma.

Wapelelezi waliamua kulifanya aneo hilo kuwa eneo la tukio la uhalifu (Crime scene) na kuanza kulichunguza. Walipogundua kuwa ardhi ya eneo lile inadidimia, wakapata uhakika kuwa eneo hilo
lilichimbwa na kufukiwa siku kadhaa zilizopita.Iliwachukua muda mchache kuchimbua na kukuta mwili wa binadamu, ukiwa ndani ya sandarusi iliyofungwa kwa utepe (Solar tape).


Ni mwili wa binadamu umekutwa ukiwa umefukiwa kwa siku kadhaa. Tayari umeharibika kiasi cha kutotambulika kirahisi. Je! Ni mwili wa nani? Ni Shirley Garvin au mtu mwingine? Sayansi ya mahakama inawezaje kutumika na kutambua taarifa za mwili ulioharibika!
Fuatilia.
download (12).jpeg
 
AMEPOTEA KISIWANI KEY WEST - 4
Maofisa wa upepelezi wamefanikiwa kufika eneo ambalo mwili wa Shirley ulifukiwa. Kwa msaada mkubwa wa teknolojia ya GPS, vyombo vya ulinzi vinaweza kufuatilia mienendo ya vyombo vya usafiri. Ndivyo walivyofanikiwa maofisa wa upelelezi waliofuatilia kesi ya kupotea mwanamama Shirley Garvin. Muuaji Michael Garvin, mume wa marehemu hakujua kama wapelelezi wamefunga kifaa cha GPS kwenye gari yake.

Endelea....

Michael na msichana yule walipoondoka, Polisiwalifika katika eneo lile na kujaribu kuchunguza kamawanaweza kupata taarifa yoyote ya muhimu.

Mpelelezi Michelle O’neil aligundua kitu tofauti.Aliona eneo ambalo halina majani tofauti na maeneomengine, kana kwamba eneo hilo lilichimbuliwa.Wapelelezi waliamua kulifanya aneo hilo kuwa eneo
la tukio la uhalifu (Crime scene) na kuanza
kulichunguza. Walipogundua kuwa ardhi ya eneo lileinadidimia, wakapata uhakika kuwa eneo hilolilichimbwa na kufukiwa siku kadhaa zilizopita.Iliwachukua muda mchache kuchimbua na kukuta
mwili wa mtu, ukiwa ndani ya sandarusi iliyofungwakwa utepe (Solar tape).

Ulikuwa mwili wa Shirley
Garvin, na kwenye mkono wake wa kushoto alivaa saa aina yaRolex, ikionesha tarehe 26, siku ya kifo chake. Hiyo ndio tareheambayo Michael aliondoka mjini Jacksonville kuelekeakisiwani Key West kwa ajili ya 'kupumzika na mkewe'

Uchunguzi wa mwili wa Shirley Garvin ulitoa majibu ya sababu ya kifo chake, alama za risasi mbili kichwani zilionekana. Risasi hizo zilitoka kwenye bastola yenye kipimo cha kaliba22. Wapelelezi hawa kuweza kupata ushahidi wowote kama Michael alimiliki bastola yenye upana wa
kipimo hicho. Hata hivyo kwenye chumba cha kuhifadhia vitu mbalimbali (store) katika nyumba ya Michael,wapelelezi walipata utepe, (sola tape) uliofanana na utepe ule uliofungwa kwenye mwili wa Shirley. Wapelelezi waliupeleka kwa mtaalamu wa uchunguzi DonnaWallace anayehusika na utambuzi wanyuzi ndogondogo au
(fibers) ili kubaini endapo utepe uliotumika kwenyekufunga mwili wa Shirley ni sawa na ule uliokutwakwenye stoo ya Michael.

Mtaalamu Donna Wallace aliona kwamba rangi yautepe uliotumika kwenye kuufunga mwili wa Shirley nitofauti kidogo na rangi ya utepe uliokutwa kwenyestoo ya Michael. Hata hivyo hakujipa uhakikakwasababu utepe uliofungwa kwenye mwili wa Shirley ulikuwaumekaa chini ya ardhi kwa wiki kadhaa, kwa hivyoinaweza kuwa sababu ya tofauti hiyo ndogo ya rangi.

Donna Wallace aliamua kutumia hadubini maalumu(Microscope) ili kuchunguza miisho ya kila kipandecha utepe, kati ya vile vilivyotumika kuufunga mwili wa Shiley na vilevilivyotoka stoo kwa Michael. Alipojaribu kuunganishamwisho wa kipande cha utepe uliofunga mwili waShirley na mwisho wa kipande cha utepe uliokutwakwa Michael, miisho hiyo ilionekana kufaana vema na
kuunda utepe mmoja mrefu.

Kwahiyo, uchunguzi huo wakutumia hadumini ulibaini kuwa vipande vya utepevilivyotumika kufunga sandarusi vilikuwa vimekatwakutoka kwenye utepe mrefu zaidi uliokuwa ndani yastoo ya Michael.

Wapelelezi walikaa na kuunganisha ushahidi na kisha kutengeneza taarifa ya upelelezi.

Kwanza, maelezo ya awali ya Michael yalikuwa ya uongo, kwani picha za kamera za barabarani ziliobeshahakuwa na Shirley kwenye gari, hakusafiri nayekwenda Key West, lakini pia eneo alilotembelea mara
kadhaa, ndilo eneo ambalo mwili wa Shirley ulifukiwa.

Pili, lengo la Michael lilikuwa kuhamisha uchunguzi wakupotea kwa Shirley usifanyike mjini Jacksonville, bali
ufanyike kisiwani Key West. Alikuwa mjanja, aliondoka na viatu vyaShirley na kuviacha ufukweni ili wapelelezi wahisikuwa Shirley amezama baharini. Pia kuna ushahidi
wa Michael kutumia utepe wake kufunga mwili wa Shirley.

Taarifahizo za ushahidiziliwaridhishawapelelezina kuamua kumshitaki Michael kwa kosa la kuua kwa kukusudia.
WapeleleziwaliaminikuwaShirleyalipanga
kumuacha Michael, lakini Michael aligundua kabla hawajaachana na hivyoaliamua kumuua. Ikiwa wangechana, basi Michael na Shirkey wangegawana mali, lakini Michael alikuwa na madeni mengi kutokana na maisha ya kifahari aliyopenda kuishi.

Alipo fikishwa mahakamani Michael hakusita kukiri kosa, lakini hakuwahi kuitaja silaha aliyotumia ali itoa wapi. Wapelelezi waliamini kuwa hata kifo cha mkewa kwanza wa Michael, pengine hakikuwa cha
kujinyonga bali aliuawa na Mwanaume huyo. Lakini hakukuwa na nguvu ya kutosha kuchunguza tukio hilo la zamani.

Mahakama ili jiridhisha na kumtia hatiani Michael Garvin kwa kuua kwa kukusudia.Michael alihukumiwa kifungo cha maisha bila uwezekano wamsamaha. (Life sentence without Parole)

FB_IMG_17072358494142900.jpg
 
Back
Top Bottom