Ni marufuku kufungua mtandao wa JF ukiwa katika ofisi za Serikali

Wakuu mambo ya Tanzania, sio kama huko majuu sio lazima iwepo any standing policy ili kuwanyima wananchi kutosoma JF, binafsi ninajua for a fact kuwa hiyo kitu ipo, hairuhusiwi kusoma JF katika ofisi za serikali bongo hakuna mtu anahitaji a standing law on that,

Majuzi nilikuwa ninaongea na mbongo mmoja akaniambia kuwa nimewasikieni huko kwenye mtandao, nasikia mna maneno sana lakini hamuelewi vizuri matatizo yetu wananchi, njaa tuliyonayo akitokea mtu anagombea ubunge akanipa kilo tano za mchele nitampa kura yangu tena bila wasi wasi hata kama simjui, nasikia huko kwenu ni dhambi kubwa sana,

akasema bosi wangu akisema saini hii karatasi mimi ni kusaini tu bila kuuliza, lakini nasikia huko kwenu mnasema hamtasaini, akasema Mungu awajalie sana msije fanya kazi kwenye serikali maana hamtaamini yanayofanyika na sisi wananchi tumeridhika saafi! Maana nikisha sain karatasi ya bosi ambayo sijui ni ya nini the mext thing ninapewa trip ya kwenda Europe kuhudhuria mkutano, ninakula perdiem na kule pia ninamnunulia bosi wangu zawadi nzuri sana, na sometimes mimi mwenyewe kabla ya kuondoka ninamuuliza bosi wangu kama anahitaji spare ya gari lake, aksiema ndio mimi ni kumnunulia tu, akasema nyie endeleeni na maneno yenu huko mtandaoni!



Jamani tuweni wakweli hata kama tunataka kuelezea jambo muhimu.

Kama mtu atahongwa kilo 5 kwa ajili ya kura, sidhani kama atakuwa anahitajika kusaini makaratasi ya bosi na kupigwa kitripu chenye padiemu ulaya.

Kama ni stori basi iwe ni stori, kama ni fakti, jamani naomba zibaki kama faktis.
 
Kubwajinga,
Mkuu duh kumbe huna habari kabisa na Bongo....yaani huijui nchi yako kabisa...
Kichekesho ni kwamba wote tunaodai ushahidi tuko nje ya Tanzania na kila mara sisi hufananisha mazingira ya huku nje na Tanzania...Jamani mwee Tanzania bado jamani tanzania bado asilimi 80 ya nyumba zetu hazina choo cha kuvuta bado wananchi wanafanya ushujaa wa kuepa makombora yao wenyewe! Imekwisha kuwa fan mojawapo na wameridhika! pamoja na kwamba udongo wa kutengeneza vyoo hivyo upo, utaalam upo na uwezo upo...basi tu tumezoea kula kwa mkono hata kama mtasema sio ustaarabu.
Ili upate kuielewa Tanzania yako ni lazima ufikirie kama vile uko Tanzania laa sivyo mtapata taabu sana..Tanzania hadi leo hairuhusiwi kuvaa nguo zinazofanana na zile za jeshi iwe hata kofia kwa sababu jeshi la Ulinzi Tanzania ni askari ambaye anaweza kuingia bank na kudai amekuja kulinda fedha!...Just Imagine TPDF (Army) kuwepo bank ama kusimamisha magari Njia kuu (highway) sio jambo la ajabu na halihitaji ushahidi!
Ama kweli kazi sii ndogo...

Mwisho mkuu, jiulize hivi Chenge na Lowassa waliwapa kitu gani wananchi wa majimbo yao hadi waandamane kuwaunga mkono hata baada ya kukabiliwa na mashtaka!...hawa leo wanaitwa mashujaa! now imagine unamuuliza mwananchi huyo aliyekuwepo ktk maandamano hayo, utapata jibu gani!
 
Jamani tuweni wakweli hata kama tunataka kuelezea jambo muhimu.

Kama mtu atahongwa kilo 5 kwa ajili ya kura, sidhani kama atakuwa anahitajika kusaini makaratasi ya bosi na kupigwa kitripu chenye padiemu ulaya.

Kama ni stori basi iwe ni stori, kama ni fakti, jamani naomba zibaki kama faktis.

hizi ndizo facts na ukweli kuhusu Tanzania na kama wewe unazo tofauti unaweza kuziweka hapa Ki-JF way au vipi mkuu?!?!?!
 
Siyo nilikuwa sijui, simply sikubaliani na upuuzi huu.

Hakuna yeyote anayeweza kuwasaidia wananchi kama wananchi wenyewe hawataamua kuachana na hizi mentality.

Swali langu ambalo halijajibiwa ni kuwa, huyu jamaa anaonekana kuamini na kushawishi watu kwamba "Watanzania ndivyo tulivyo" kwa hiyo mimi nipe trips nitasign chochote bila kusoma (hata kama ni waraka wa kuniua, basically umalaya wa kisiasa) anaposema watanzania ndivyo tulivyo ana mamlaka gani? Mbona kuna majimbo wamewaweka wapinzani na kutotingishwa na machinery za ufisadi na hongo za CCM?

Aseme anaongelea mafisadi na malaya wa kisiasa walio katika CCM na serikali pamoja na Watanzania wenye tabia kama hizo, lakini ni matusi ku imply taifa zima la watu milioni 40 halina watu wenye integrity.

Pundit,

Only in Tanzania my friend where morals and ethics do not exist at work place.

Wakubwa wanatumia extortion, vitisho and sometmes watu na familia zao huwa hatarini kupoteza maisha ili matakwa ya Mkubwa yatimizwe.

Ukiwa sugu na mbishi, utapoteza kazi, watahakikisha unaangamia na kuwa lofa wa kutupa.

Kuna wazee wengi sana na hata vijana ambao wamepoteza kazi kutokana na kuwa na misimamo ya kwa wakweli na kufanya kazi kwa mujibu wa kanuni na sheria (najua hili unalifahamu first hand).

Je ni sahihi kuendelea kufanya mambo kwa woga kama Ballali na pesa za EPA? si sahihi, lakini sisi ni binaadamu, kila mtu si sugu na kuweza himili vishindo.

Muulize Rutabanzibwa alivyoshinikizwa kupitisha mkataba wa IPTL ingawa kuna ushahidi tosha aliupinga kwa nywele zake zote!

Tanzania wenye nia ya kudhulumu na kuhujumu wakitaka kufanya hivyo, hakuna wa kumsimamisha haswa kama kuna mkono wa Kiongozi!

Hili la kukataza JF, ni woga wa hao wanaodhulumu na kuhujumu kuwa tunawafundisha wafanyakazi wa ngazi za chini na kati ujasiri wa kupima mambo na kufuata kanuni. Hakuna kitu Fidasi na Mbabaishaji anakiogopa kama mtu aliye jasiri.

Kuletwa kwa mikataba mingi hapa na kuzungumziwa kunaonyesha kuwa sasa hivi, kuna transition ya kujenga watu jasiri, ambao siyo "yes sir" type of people.

JF imesaidia wengi kufikiria nje ya boksi na kuwa jasiri, kukataa kuburuzwa. Ndio maana ni marufuku kusoma JF kwenye ofisi za Serikali na Mashirika ya Umma!
 
Jamani tuweni wakweli hata kama tunataka kuelezea jambo muhimu.

Kama mtu atahongwa kilo 5 kwa ajili ya kura, sidhani kama atakuwa anahitajika kusaini makaratasi ya bosi na kupigwa kitripu chenye padiemu ulaya. Kama ni stori basi iwe ni stori, kama ni fakti, jamani naomba zibaki kama faktis.


Mkuu naona una kazi kubwa sana maana kama huwezi kuelewa kuwa huyo mkuu alikuwa pia anawakilisha mawazo ya wananchi wa kawaida, basi tuna kazi kubwa sana hapa JF kuelimisha wananchi kama wewe, kwa sababu inaonekana kuwa huelewi kitu kabisaa kuhusu bongo, kwa sababu ni mtu gani wa kijijini aneyeweza kujali mambo ya huku kwenye mtandao?

Mtu yoyote mwenye akili timamu akisoma hii message yangu anaelewa the point, mtu wa kijijini anayeweza kununuliwa ka kilo tano za mchele atazisikia wapi hizi habari za mtandao, mpaka kujua what is dhambi hapa JF au what is not?

Mkuu endelea kuhangaika tu, naona nimekushika pabaya kwenye kila ishu karibu sana mkuu! Hizi lugha zingine mkuu tunazitumia ku-cover the source na sidhani kama kuna mtu mwenye akili timamu hapa ameshindwa kuelewa my point, lakini tutaendelea kukuelimisha mkuu naona unahitaji elimu nzito sana kuhusu bongo!

Wananchi wenye njaa ni rahisi kununuliwa kwa kilo tano za Mchele na mtu anayetaka ubunge, sasa nilifikiri utalikataa hilo au kukubali, lakini badala yake unataka ushahidi what a low mind? Here you are unataka kuharibu tena mjadala kwa sababu umeshikwa pabaya!

Unaambiwa kuwa bongo sasa hivii ni marufuku kuingia JF kwa kutumia mtandao wa serikali, wewe unaleta hadithi za abunuwasi, na kuuliza maswali hata mtoto mdogo anyeijua bongo hawezi uliza hivi unaishi nchi gani mkuu?
 
Jamani tuweni wakweli hata kama tunataka kuelezea jambo muhimu.

Kama mtu atahongwa kilo 5 kwa ajili ya kura, sidhani kama atakuwa anahitajika kusaini makaratasi ya bosi na kupigwa kitripu chenye padiemu ulaya.

Kama ni stori basi iwe ni stori, kama ni fakti, jamani naomba zibaki kama faktis.

Nadhani alichoeleza ni majumuisho ya matukio. Kuna wengine wanapewa kilo ya mchele, wengine watapewa trip ya Uropu, wengine ni... hakusema lakini watapewa ngono. Si kuna watu tunaambiwa ni Mawaziri kwa ajili hiyo tu!

Ndiyo maana anatumia wingi. yaani sisi huku Bongo.
Right?
 
Mkuu hapo umesema kweli maanake nusu ya wabunge wanawake TZ wamefika hapo walipo sii kwa kazi ndogo... Bunge letu ni Hollywood ya Tanzania..ngono tu mtu anakwaa madaraka makubwa..yaani nchi yetu imekwenda na maji!
 
Mkuu naona una kazi kubwa sana maana kama huwezi kuelewa kuwa huyo mkuu alikuwa pia anawakilisha mawazo ya wananchi wa kawaida, basi tuna kazi kubwa sana hapa JF kuelimisha wananchi kama wewe, kwa sababu inaonekana kuwa huelewi kitu kabisaa kuhusu bongo, kwa sababu ni mtu gani wa kijijini aneyeweza kujali mambo ya huku kwenye mtandao?

Mtu yoyote mwenye akili timamu akisoma hii message yangu anaelewa the point, mtu wa kijijini anayeweza kununuliwa ka kilo tano za mchele atazisikia wapi hizi habari za mtandao, mpaka kujua what is dhambi hapa JF au what is not?

Mkuu endelea kuhangaika tu, naona nimekushika pabaya kwenye kila ishu karibu sana mkuu! Hizi lugha zingine mkuu tunazitumia ku-cover the source na sidhani kama kuna mtu mwenye akili timamu hapa ameshindwa kuelewa my point, lakini tutaendelea kukuelimisha mkuu naona unahitaji elimu nzito sana kuhusu bongo!

Wananchi wenye njaa ni rahisi kununuliwa kwa kilo tano za Mchele na mtu anayetaka ubunge, sasa nilifikiri utalikataa hilo au kukubali, lakini badala yake unataka ushahidi what a low mind? Here you are unataka kuharibu tena mjadala kwa sababu umeshikwa pabaya!

Unaambiwa kuwa bongo sasa hivii ni marufuku kuingia JF kwa kutumia mtandao wa serikali, wewe unaleta hadithi za abunuwasi, na kuuliza maswali hata mtoto mdogo anyeijua bongo hawezi uliza hivi unaishi nchi gani mkuu?




Mkuu heshima yako.

Nadhani we endelea kutoa shule usichoke, kuna watoto au vijana humu wamekulia majuu either wazee wao walikuwa madiplomat au namna gani..kwa hiyo mambo mengine wanaona kama hayawezekani. Kifupi ulimwengu wao ni tofauti kabisa...na wa realTanzania. Infact wengine hata mchele hawapewi maana hiyo ni anasa..guess what? wanapata pombe ya kienyeji kama Rubisi, Kimpumu, Mbege nk...

Lakini kwa tunaoelewa..yaani maelezo yako na Mkandara, Reverend, MWK nk....yana reflect true picture ya maisha yetu watanzania.

Huwezi kusolve tatizo kama hujalielewa na kuliappreciate. LAZIMA KWANZA WATANZANIA TUJITAMBUE KWAMBA KIUKWELI TUKO HALI MBAYA MNO. WE ARE POOR BEYOND MAELEZO! Ukienda Dar usifikiri Tanzania inaishia sleepway au Mayfair Plaza....toka nje kidogo..Tanzania ni kubwa mno. Usione watu wanapiga kelele humu..Hali ya wananchi wetu bongo ni ngumu mno! Na wengi tunashindwa kuelewa kwa nini tuwe hivi na raslimali tulizonazo..ni maswali magumu lakini ndo JF hapa tunawekana sawa!
 
Ukweli unasimama kwamba jamaa wanapiga marufuku kutumia internet ya ofisi kusoma JF .Ila ukisoma mambo mengine hata kuangalia ngono sawa ila dhabi kumbwa ni JF
 
ukweli Unasimama Kwamba Jamaa Wanapiga Marufuku Kutumia Internet Ya Ofisi Kusoma Jf .ila Ukisoma Mambo Mengine Hata Kuangalia Ngono Sawa Ila Dhabi Kumbwa Ni Jf
mkuu Lunyungu, Maana Halisi Ya Zuio Hilo Si Nyingine Ila Ni Kuwa Jf Ni Kitovu Cha Habari Na Uelewa Ambao Ni Tishio Kwa Maslahi Ya Hao Walioko Madarakani Kwa Maslahi Yao Tuu.
Hata Hivyo Tusihofu Maana Hiyo Itawapa Udadisi Hata Wale Wasiotembelea Hapa Kujiuliza Kunani Huko Jf? Unaelewa Kitakachofata? Kila Mtu Atatembelea Na Akionja Hataacha. Asante Sana Serikali Kwa Promotion Hii.
 
Nadhani aliyetoa directive hiyo ni bora aondoe internet kabisa maofisini la sivyo watu wata visit tu jf. Maana kwanza jf ni addiction moja wapo. Nadhani kuna ambao kuikosa wataji sacrifice kuangalia hata kama ni kufukuzwa kazi kuliko kuikosa
 
Nadhani aliyetoa directive hiyo ni bora aondoe internet kabisa maofisini la sivyo watu wata visit tu jf. Maana kwanza jf ni addiction moja wapo. Nadhani kuna ambao kuikosa wataji sacrifice kuangalia hata kama ni kufukuzwa kazi kuliko kuikosa

Matokeo ya kushiba na wala si kulewa madaraka na kujua Dunia iliko sasa kwa kiasi kidogo .
 
JF hoyeeeeeeeeee, naona JF inazidi kutangazika bila garama zozote... kweli JF kiboko.... walitengemea kula hela zetu mpaka lini
 
KAZI zenyewe za kufanya humo kwenye OFISI ZA SERIKALI na TAASISI ZA UMMA zipo basi? Unakuta mtu mmoja au wachache tu kwa UTASHI na MATAKWA ya mkuu wa IDARA au TAASISI YA UMMA ndio wamepewa kuzifanya. Wengine wote ni WATAZAMAJI tu!
Hivi kweli mtu akiwa na KAZI ya kufanya atapata muda wa kuingia MITANDAONI?
 
Kisheria sehemu nyingi za kazi huruhusiwi kutumia mali ya kampuni kwa faida binafsi. Unapokuwa kazini muda ni mali ya kampuni. Hivyo kuna mashirika ambayo 'huzuia' kufungua website zisizohusiana na kazi yako wakati wa kazi au kutumia tarakishi za kampuni kufanya hivyo. Kuzuia website fulani, huo ni uonevu na upungufu wa kufuata sheria bila kupindisha..
 


Lakini kwa tunaoelewa..yaani maelezo yako na Mkandara, Reverend, MWK nk....yana reflect true picture ya maisha yetu watanzania.


Mkuu Masanja,
Nafikiri ni zaidi ya hatari kufikiria kuwa kuna watu wanaohodhi facts. Opinions kila mtu anaweza kuwa na zake lakini facts hazibadiliki. Tusichukulie kuwa umaarufu wa humu JF ikawa ndio kipimo cha ubora wa michango au bongo za wahusika. Naomba tuwe macho na hili.

Hizi habari za waungwana bongo kukatazwa, specifically kufungua JF, kwangu bado haliingii akilini, unless kama ni ofisi mbili-tatu. Maana ni kweli hata hiyo control yake sijui inakuwaje? Wanaiblock JF au wanakagua kila baada ya mtu kutumia kompyu?? This is strange if it is true, tuangalie tusije tukajipaka mafuta na mgongo wa chupa wenyewe.
 
Mkuu hapo umesema kweli maanake nusu ya wabunge wanawake TZ wamefika hapo walipo sii kwa kazi ndogo... Bunge letu ni Hollywood ya Tanzania..ngono tu mtu anakwaa madaraka makubwa..yaani nchi yetu imekwenda na maji!

Mkuu Mkandara,
Ingawa sijui kama ni off topic au ni vipi, ni vema tusiwapake wabunge wetu wengi hivyo kwa brashi moja. Wengine humu wana mama zao waliopo bungeni. Tusije tukazua matatizo ya wao kuanza kuwasumbua wazazi wao kuhusu hayo uliyoainisha.
 
Mtandao wa JF hauruhusiwi period, kama unashukiwa baada ya kazi wanaohusika hunagalia kompyuta yako, kwa ni kazi kubwa kujua hili? Kuna watu tunaowajua ambao hawana mitandao nyumbani sasa inabidi tuwa-printie habari nzito hapa na kuwafaksia,

Mkuu Bongo sio majuu, mambo bado ni tofauti, ndio maana bado ni wananachi wachache sana ambao hutuona kuwa hapa JF tuna akili, wengi hutuopna ni malofa wa akili, yes nimeambiwa hilo usoni mwangu mara nmyingi sana na sababu, za njaaa nyumbani, lakini haina maana tutaacha kuwepo hapa,

Hapana mpaka kieleweke!
 

Unajua, bungeni kuna mama wa wananchi wote wa Tanzania, na kwenye siasa za Tanzania kuna wanaume ambao kwanza ni baba zetu sisi wa-Tanzania wote, halafu tunafanana nao,

Mimi humu ndani ya hii forum ninamjua mkulu mmoja ambaye ana nafasi ya kazi ambayo nilimuomba amsaidie msichana wangu wa kazi, yaani housegirl wangu, jaama bosi mzima wa kazi mwenye mke na watoto, na anyeheshimika sana na jamii akaanza kumlazimisha yule msichana ambaye ni nusu ya umri wake, kuwa anataka aende naye Cinema, na akaanza kumpa hela za kmurubuni, amkubali na ushahidi kibao ninao mpaka leo ninaweza kuutoa, sio kwamba huyu mkulu alimfanyia house girl wangu tu, aliwafanyia na wengine pia wengi waliokuja kushitaki, lakini nikamezea tu! Ila kwa sababu mimi ni politician huwa ninaweka all evidence maan hujui mbele ya siasa utakutana na maadui wapi, wanaweza kuwa wale wale waliowahi kuwa your friends!

My ponit ni kwamba kama maneno ya Mkandara yana apply kwa kila mbunge na viongozi wetu kwa ujumla, basi Tanzania tuna tatizo kubwa sana maana hata viongozi wetu wananume wana tabia kama hizi zetu wananchi!, yaani tunafanana nao!

Tuwe makini sometimes na maneno yetu na midomo yetu, maana mdomo ni kitu kidogo sana lakini huponza mwili mzima, maana ikibidi itabidi tuyapenyeze kwa wake zetu knowing kwamba wengine huwa wanakula vibao na wake zao, ili wajue ukweli wetu wanaume viongozi, kuwa sisi wananchi ndio chanzo cha huu ujinga, na sio lazima iwe kwenye uongozi tu!
 
Back
Top Bottom