Ni lazima kumchangia mtu send-off ama harusi?

Chakorii

JF-Expert Member
Jul 11, 2015
18,586
50,683
Habari jamani, mnaendeleaje? Hebu acha niende moja kwa moja kwenye hoja.

Iko hivi, miezi kama miwili au mitatu katika kupiga stori za hapa na pale one of my colleagues (KE) akaniambia unajua fulani anaolewa na fulani (wote wanafanya kazi pamoja)? Nilifurahi kwa mshangao maana sikuwahi kujua kama walikuwa wako na mahusian, so stori ikaishia hapo tukaendelea na habari za maisha mengine.

Sıjakaa sawa ilibaki kama wiki mbili au tatu akafunge ndoa ndio akaja kuniambia Chakorii nafunga ndoa na fulani, naomba support yako. Nikamjibu kwakuwa muda uliobaki ni mfupi na hili swala lako limekuja kwa haraka, sina uhakika asılımia mia kama nitaweza kuku support, akasema sawa.

Kiukweli majukumu yalinizidi nikamsahau kabisa! Yooo, nakuja kuonana nae tena ni baada ya likizo, sasa sijui ndio alitoka kufunga ndoa ama alikuwa likizo kawaida maana sikuona kiashiria chochote cha kuwa huyu mtu alikuwa kwenye hekaheka.

Kilichonifanya nikaleta uzi sasa, heee si kaninunia huyo mwanadada, hata nikimsaliamia haitiki! Nikasema labda pengine amevurugwa akili. Siku nyingine tena nikamsalimia kaitika kama kalazimishwa, mind u mimi ndie huwa namuanzaga.

Sasa juzi kaja sehemu ambapo mimi ndie muhusika, hakunisalimia tena nikamuuliza “My love mimi na wewe tuna matatizo?” Akanijibu hapana mambo ni mengi tu, nikajisemea ahhaa mambo mengi ee, nikamtukana kimoyo moyo, wewe siku ukiisikia salam yangu uniite dog ingawa mimi sio dog!

Sasa kila nikimuona yulee nainyanyua simu najifanya naongea na mtu kwa simu. Akili imemkaa sawa anataka kunisalimia lakini ninaongea na simu, nimeshamfungia vioo na si mfungulii tena.

Ni lazima kuchanga kwenye vitu vya umuhimu ambavyo vinakuja bila taarifa. Harusi ama send-off ni swala la kuvuta pumzi na kujipanga, sio lazima kusumbua watu wakuchangie.

Hallelujah 🤸‍♀️
 
Jitahidi sana mkuu, usiishi kwa vinyongo na watu, yeye hata kama akikuonyesha chuki, wewe jitahidi kuwa at peace with everything. Negative energy is contagious.

Tukirudi kwenye mada, si lazima kumpa mtu mchango wa harusi ama msaada wowote ule. Na si kosa kutompa mtu kitu alichokiomba, tatizo watanzania wengi bado tunakula kiporo cha Ujamaa. Hivyo huyo colleague wako anatakiwa kubadili mtazamo wake katika hili.
 
Haya mambo ya michango ya harusi sijui send off siyapendii, mama angu nilishamuambia kabisa ikitokea naolewa sitaki shereheee, wala sitaki kusumbua watu, hii kitu naonaga ni kusumbua tu watu, labda nina roho mbaya afu sijijui 😂, harusi yenu mnaenda kuishi nyie ila kuwasumbua watu wakuchangie eboo.
 
Unaungwa group...
SMS za kawaida unatumiwa..
Wakiona kimya ..kamati inakupigia wakiwa live kikaoni wanataka u pledge....
Sometimes kujuana na watu shida sana

Wakikomalia sana naahidi ila sitoi kwani lazima,na sijawahi ona sherehe iliyokuwa planed ikashidwa kufanikiwa eti kisa michango,hela huwa wanayo sema wanahitaji vya nyongeza tu.
 
Halafu wenyewe siku izi wanasema usipowachangia wanakusubri na wewe yako ifike.

sijui wanahisi watu wote tunategemea michango kufanya sherehe.

Huchangiwi na yangu ikifika nakupa kadi ya mualiko uamue uje au usije.
 
Unaungwa group...
SMS za kawaida unatumiwa..
Wakiona kimya ..kamati inakupigia wakiwa live kikaoni wanataka u pledge....
Sometimes kujuana na watu shida sana
Nilifanyiwa hivyo wakiwa kikaoni kwakua n watu wazima sana nikaona isiwe kesi nikaropoka "laki 3"

Sijaitoa ile hela hadi na kesho sherehe ishafanyika na yangu ikifika wanaalikwa na siwachangishi maana najua wanansubiri yangu ifike.
 
mimi sio harusi tu, hata waomba hela ovyoovyo ety msaada, nikikupa basi jua huyo ni roho wa bwana kasema mpe
mbali na hapo hata fifte hulambi 🤣🤣😁

Kuna bro mmoja ana kazi nzuri tu na mshahara lakini kwenye kuowa ni kanisani, baada ya hapo kwakeee hakuna kelele.
Lakini maskini sasa ndio utaona fujo zao, utafikiri washuhudiaji wakiwa wengi itasaidia muwe na ndoa nzuri 🤣🤣🤣
 
Kuchangia harusi au send off ni sehemu ya matumizi halali!! Si lazima lakini ni muhimu!! Hela kazi yake ni kutumikas!! Hela zako zitatumika tu kama siyo kwenye michango ya harusi na send off zitatumika kwenye mambo mengine ambayo pia hayana tija kwako ya moja kwa moja na hayaachi kumbukumbu yoyote yenye sifa njema!!. So at the end of the day it makes no difference!!

Ila kumnunia mtu kwa kuwa hajakuchangia hiyo hapana!! Ila kuna watu huwa hawana shukrani!! yeye ulimbeba kwenye jambo lake, inapofikia zamu yake kukubeba anajifanya ana mambo mengi!! Angekumbuka kuwa hata watu waliokubeba wewe kwenye jambo lako walikuwa pia na mambo mengi lakini mengine wakayaweka pembeni ili kufanikisha jambo lako kwanza!! Maisha ni mzunguko hilo lisisahaulike!!
 
Back
Top Bottom