Ni kweli mabinti wa Tanzania ni omba omba sana katika mahusiano au wanaume ndio mabahili?

Nafikiri hakuna shida sana kwa walio katika ndoa mwanaume kuhudumia kila kitu kwa sababu huo ndio umekuwa utaratibu wa karibia binadamu wote kwa mke na mume. Tatizo ni kwa watu waliokutana tu hata hawajamaliza mwezi kuanza kubebeshwa majukumu ya mume au baba mzazi kwa mwendokasi.
Binafsi sipingi suala la baba kujitoa kuhudumia familia lakini napinga huu mtindo wa maisha wa vijana wa sasa tena hata kabla hawajaingia katika ndoa.

Ubinafsi wa jinsia ya kike kwa mwenza wake unakua kwa kasi sana hasa katika kipato na mali na tabia hii inaonekana ya kawaida tu wala haina tatizo hata kwa wanaume.

Binafsi sipendezwi na ubinafsi wa jinsia ya kike iwe katika uchumba hata katika ndoa tena hasara zaidi ubinafsi ukiwepo hata katika ndoa. Ndoa hiyo itakuwa imeshikiliwa na uzi mwembamba wa fedha za mwanaume siku account ya mwanaume ikikata au kipato kuyumba au ujira kupotea hakutakuwa na uhai wa hiyo ndoa tena.

Hizi tabia ulizo andika hapa ndizo hizo tabia zinazo zalisha ubinafsi wa kimali wa jinsia ya kike mpaka kukomaa ndani ya ndoa.

Leo hii vijana wanaona sio ajabu mwanamke mwenye kipato kikubwa kabisa cha kueleweka kushindwa kujihudumia mahitaji yake ya msingi na kutegemea fedha za mwanaume wake hata zile kidogo unabaki kujiuliza pesa yake mwanamke wa kileo inafanya kazi gani ?

Mama zetu walishindwa kuwa na mchango mkubwa wa kifedha katika familia kutokana na kuwa mama wa majumbani ila katika shughuli ndogo ndogo walizokuwa wakifanya hata za kuuza nyanya pesa ndogo walizopata wali wasaidia wazee wetu hata madaftari madogo wali tununulia na hakuna mahali walilalamika na kuona baba zetu hawatimizi wajibu wao ila kwa hawa wanawake wa kileo kama sio kutangazwa mtaa mzima basi hiyo ndoa inayumba.

Unajiuliza kwa nini wanaume wa kisiasa wanafagilia ubinafsi wa mwanamke ambao ni hatari kwao na kwa ndoa yao ? Unashindwa kuelewa akili zao.

Mwanamke ombaomba kiasili ni mbinafsi aliye pindukia ambae chake kibaki kuwa chake pasipo kufahamu kinafanya nini wala kinaenda wapi ila chako kiwe chake huu ni muungano wa Tanganyika na Zanzibar ni hatari kwa ustawi wa ndoa
 
Kuna mmoja nilimtongoza maeneo fulani hapa Dar Es Salaam ilikuwa Saa Tatu hivi asubuhi tukapeana Namba tukaachana, kufika jioni Saa kumi the same day ananiomba hela na hata kumlala sijamlala!

Nilim-block na sikuwahi kumtafuta tena

Elimu ya mapenzi na mahusiano wengi hawana, wanachojua ni kukupa utamu na kuomba hela

Sijawahi kudate Mtoto yoyote wa kishua kwahiyo sijuwi hao kutoka familia za kitajiri wana act vipi wakipata kichwa (mwanaume).
 

Ni sijui kwa nini waombaji huwa wanaanza mbali sana badala ya kwenda kwenye point ya msingi moja kwa moja!

Hapo unawekewa mitego, ukileta ubishi utaambiwa si ulikubali mwenyewe uambiwe kitu?

Kuna watu wanajua kuomba ni haki yao ya kikatiba, na kukataliwa ni makosa dhidi ya ubinadamu.

Lakini kiukweli hawa wanawake mnawasema sana labda wao wamezidi tu.

Kibongobongo utamaduni wa kupigana mizinga kirahisirahisi umekomaa sana.
Na mitandao inazidisha mizinga, maana zamani mtu kumpiga mzinga mpaka umuone mwenyewe, siku hizi mizinga inakuja kimtandao tu.

Kila mtu anataka maisha rahisi, bila mpango.

Kila January watu kibao wanapig mizinga ya kodi za nyumba na ada za kusomesha watoto.

Unaazaaje watoto kibao wakati huna uhakika wa kuwasomesha maisha haya?
 
rejea hapa

 
Mkuu ni sawa mwanaume kumplia ada ya chuo, kodi na mahitaji mengine mengi mpenzi tu ambaye wanaweza kuachana hata kwa meseji muda wowote??
Mwanamke hafanyiwi booking kama tiketi ya basi au ndege Kuwa nakulipia na ku book ili tuje tuoane ujinga mtupu

Ukifika wakati wa kuoa tafuta mwanamke aliye tayari kuolewa muda huyo sio huyo wa booking wa miaka ijayo.Ukiwa tayari kuoa tafuta aliye tayari kuolewa muda huo huo

Lakini kama ni booking isiwe na kuingia mfukoni sana kugharimia kiasi Kuwa akikubwaga unachinja mtu .Kama booking ni Bure au Kwa gharama zisizoumiza hata ukibwagwa Ruksa

Lakini kama unaiona hizo gharama ukibwagwa utapandisha mashetani ya kimasai na kutaka kuua mtu acha .Tafuta aliye tayari kuolewa oa huyo achana na huyo wa booking anayekugarimu mfukoni sana Hadi roho inakuuma Kwa gharama unazotumia
 
Mie kitu ambacho sipendi ni kununua au kutoa hela kwenye mambo yakipumbavu.

Niombe hela ktk vitu vya maana na sio unaniomba hela ukasuke sijui ununue wigi..

Niombe hela unataka Kula (sio chips na pizza) omba hela ya kununua kilo hata 20 za mchele uweke ndani.

Omba hela ya kodi.. sio unakaa unaniomba hela elf 5 ya umeme, mambo ya kipumbavu kabisa. Mwanamke mwenye mindset ya kimasikini anaekosa hata nauli au elf 5 ya umeme huyo mie simtak hata kumsikia. Ndio.

Sasa maisha ni kusaidiana, sasa mie nikikwama naangukia kwa nani sasa? Huyu huyu niliemzoesha kumpa vihela atanikimbia maana sina cha kumpa na yeye hana cha kunipa backup zaidi ya kunip K.
 
Tamaa zimezidi mno mabinti wa Sasa,kazi za kujitafutia hela kama za kuuza maandazi na matunda wanaona za kishamba!Matokeo yake ni mizinga kwenda mbele,ukimkuta ana boyfriend mmoja shukuru!mmoja wa voucher, mmoja wa saloon,mmoja wa luku,gesi,pango,msosi nk .
 
Binafsi sipingi suala la baba kujitoa kuhudumia familia lakini napinga huu mtindo wa maisha wa vijana wa sasa tena hata kabla hawajaingia katika ndoa.

Ubinafsi wa jinsia ya kike kwa mwenza wake unakua kwa kasi sana hasa katika kipato na mali na tabia hii inaonekana ya kawaida tu wala haina tatizo hata kwa wanaume.

Binafsi sipendezwi na ubinafsi wa jinsia ya kike iwe katika uchumba hata katika ndoa tena hasara zaidi ubinafsi ukiwepo hata katika ndoa. Ndoa hiyo itakuwa imeshikiliwa na uzi mwembamba wa fedha za mwanaume siku account ya mwanaume ikikata au kipato kuyumba au ujira kupotea hakutakuwa na uhai wa hiyo ndoa tena.

Hizi tabia ulizo andika hapa ndizo hizo tabia zinazo zalisha ubinafsi wa kimali wa jinsia ya kike mpaka kukomaa ndani ya ndoa.

Leo hii vijana wanaona sio ajabu mwanamke mwenye kipato kikubwa kabisa cha kueleweka kushindwa kujihudumia mahitaji yake ya msingi na kutegemea fedha za mwanaume wake hata zile kidogo unabaki kujiuliza pesa yake mwanamke wa kileo inafanya kazi gani ?

Mama zetu walishindwa kuwa na mchango mkubwa wa kifedha katika familia kutokana na kuwa mama wa majumbani ila katika shughuli ndogo ndogo walizokuwa wakifanya hata za kuuza nyanya pesa ndogo walizopata wali wasaidia wazee wetu hata madaftari madogo wali tununulia na hakuna mahali walilalamika na kuona baba zetu hawatimizi wajibu wao ila kwa hawa wanawake wa kileo kama sio kutangazwa mtaa mzima basi hiyo ndoa inayumba.

Unajiuliza kwa nini wanaume wa kisiasa wanafagilia ubinafsi wa mwanamke ambao ni hatari kwao na kwa ndoa yao ? Unashindwa kuelewa akili zao.

Mwanamke ombaomba kiasili ni mbinafsi aliye pindukia ambae chake kibaki kuwa chake pasipo kufahamu kinafanya nini wala kinaenda wapi ila chako kiwe chake huu ni muungano wa Tanganyika na Zanzibar ni hatari kwa ustawi wa ndoa
Umemaliza mkuu!
 
Back
Top Bottom