Ni kitu gani unatamani ungefanya tofauti ulipokua na umri wa chini ya miaka 25?

AY 5225

JF-Expert Member
Jul 16, 2023
484
1,135
Heshima yenu wakuu.

Kuteleza na kuanguka kisha kuinuka tena na kusonga mbele ni shule nzuri sana ya vitendo ambayo humfanya mwanadamu kuwa na mbinu thabiti za kutatua changamoto zake za hapa na pale katika maisha. Wazungu wanasema, "mistakes are the best lessons".

Nawakaribisha kwenye uzi huu mje mtiririshe vitu ambavyo ulifanya miaka kadhaa iliyopita na unatamani usingefanya ama ungevifanya tofauti ili vitumike kama somo kwa wengine.

Binafsi mwezi huu umetimiza mwaka mmoja toka nihitimu shahada yangu ya kwanza na kitu ninachotamani ningefanya tofauti ndani ya huo mwaka mmoja uliopita toka nihitimu chuo ni kutokua mtu anaejifungia ndani na kuangalia series siku nzima kila siku.

Kipindi hicho chote nilikua niki'apply nafasi za kazi mbalimbali bila mafanikio na ilikua kila nikihudhuria interviews narudi ghetto nikiwa nimekata tamaa sana kwani mategemeo yalipitiza uhalisia wa mambo.

Baada ya kujiunga na JF na kupata busara za waliotangulia, hivi sasa nimekua mtu wa kujichanganya kutafuta mishe za hapa na pale na tabia ya kushinda ndani bila mpango imekoma.

Hata hivyo sijilaumu sana kwani ni rahisi sana kubadili uelekeo ila ni ngumu sana kubadilisha imani. Mtu aliekaa darasani kwa miaka 16 kwa imani ya kwamba akimaliza atapata kazi fulani, sio rahisi kumbadilisha imani kwa muda wa miezi kadhaa kwamba ajiajiri na hata kupata huo mtaji wenye ni changamoto.

Ushauri wangu kwa waliyo chini yangu; USIKAE NDANI MKUU. USIKAE NDANI MKUU. USIKAE NDANI MKUU. TOKA NENDA POPOTE TU UNAPOWEZA KUANZIA.
 
kutosoma Degree

Nina imani bado una nafasi mkuu in the near future. Ila the irony is, hata sisi tulionazo hizo degree muda mwingine tunatamani huo muda tungeutumia kwenye kufanya mambo ya kutujenga kiuchumi. Ila probably zitakuwa na tija kwetu hapo mbeleni.
 
Kutoka ndani au kukaa ndani hakuna uhusiano na kupata michongo nowdays tena mimi naamini kwenye kushinda ndani angalia series nk ukitoka uwe ni route ambayo Ni TARGET...nakwambia hivyo ukitoka physical kwenda kusaka hio michongo kilasehemu ukienda utaambiwa "hatutaki wafanyakazi" "tumejaa" "wengine wamefukuzwa"

Kazi nyingi nimepata kwa Kutafuta connection online ila kazi nyingi nilizoenda physical iwe ofisini au kibaruani unapewa majibu ya hovyo niliwaigi kwenda Carwash kuomba kazi jamaa akaniambia manager yule nilivyoenda kwa huyo jamaa kajibu "Unaona naonekana Kama manager" sehemu nyengine utaambiwa "nani kakwambia hapa Kuna kazi"

Kaa ndani tafuta Connection kwa Wana, watu wa online, kazi za online, jiunge Group za kazi FB, WhatsApp Kuna Group za wasap wanafanya mpaka session za kupeleka CV maofisini so unajua umetoka unaenda sehemu kufanya kitu JF wanaandika vitu visivyo na uharisia.
 
Kutoka ndani au kukaa ndani hakuna uhusiano na kupata michongo nowdays tena mimi naamini kwenye kushinda ndani angalia series nk ukitoka uwe ni route ambayo Ni TARGET...nakwambia hivyo ukitoka physical kwenda kusaka hio michongo kilasehemu ukienda utaambiwa "hatutaki wafanyakazi" "tumejaa" "wengine wamefukuzwa"

Kazi nyingi nimepata kwa Kutafuta connection online ila kazi nyingi nilizoenda physical iwe ofisini au kibaruani unapewa majibu ya hovyo niliwaigi kwenda Carwash kuomba kazi jamaa akaniambia manager yule nilivyoenda kwa huyo jamaa kajibu "Unaona naonekana Kama manager" sehemu nyengine utaambiwa "nani kakwambia hapa Kuna kazi"

Kaa ndani tafuta Connection kwa Wana, watu wa online, kazi za online, jiunge Group za kazi FB, WhatsApp Kuna Group za wasap wanafanya mpaka session za kupeleka CV maofisini JF wanaandika vitu visivyo na uharisia.

Nimekupata mkuu ila nadhani hakuna a "one size fits all" solution kwenye tatizo hili maana mimi kipindi nashinda ndani tu ndo sikuwahi kupata deal hata moja ila toka nimeanza kutoka toka angalau napata pata. Kwahiyo kwangu kutoka nje ndo the best remedy.
 
Nimekupata mkuu ila nadhani hakuna a "one size fits all" solution kwenye tatizo hili maana mimi kipindi nashinda ndani tu ndo sikuwahi kupata deal hata moja ila toka nimeanza kutoka toka angalau napata pata. Kwahiyo kwangu kutoka nje ndo the best remedy.
Ukijua strategy za kuingiza pesa kwa kushinda ndani unafaidi sana nilivyokua na PC yangu na access y WiFi ya bure mimi nilikuwa ndani tu natangaza Movies watu wanakuja tuna Meet Cafe naingiza 10,000 Tzs, wengine nawafuata, sema Modes walifut Uzi wangu bilasababu bila ya Modes mpaka sasa nisingelilia michongo ya 200,000 nilishauliza mpaka gharama ya kufunga WiFi Geto nipakue kwa urahisi mizigo niwe Full Time😭😭 nilikua nafanya Designing ndani tu natangaza Online nimefaka wateja tuna meet kazi hadi ya 150K.

Nowdays Sina resources za kutosha nikijipata kutoka itakuwa kuonana na potential people nitakaa ndani tu kupush Traction na metric za Products zangu tu.
 
Ukijua strategy za kuingiza pesa kwa kushinda ndani unafaidi sana nilivyokua na PC yangu na access y WiFi ya bure mimi nilikuwa ndani tu natangaza Movies watu wanakuja tuna Meet Cafe naingiza 10,000 Tzs, wengine nawafuata, sema Modes walifut Uzi wangu bilasababu bila ya Modes mpaka sasa nisingelilia michongo ya 200,000 nilishauliza mpaka gharama ya kufunga WiFi Geto nipakue kwa urahisi mizigo niwe Full Time😭😭 nilikua nafanya Designing ndani tu natangaza Online nimefaka wateja tuna meet kazi hadi ya 150K.

Nowdays Sina resources za kutosha nikijipata kutoka itakuwa kuonana na potential people nitakaa ndani tu kupush Traction na metric za Products zangu tu.

Tuombe uzima tu mkuu.😂
 
Back
Top Bottom