Mdau
JF-Expert Member
- Mar 29, 2008
- 1,789
- 470
Nimesikitishwa sana na wimbi la ubakaji wa demokrasia linaloendelea kuelekea uchaguzi mkuu 2010..kubwa katika yote,ni hili suala la 'kupita bila kupingwa" kwa baadhi ya wagombea katika majimbo mbalimbali..nimeguswa zaidi na jimbo la Sengerema, ambalo mbunge anayemaliza muda wake ni Waziri wa Madini;William Ngeleja,mtu muhimu sana katika mchakato mzima wa uwekezaji kati ya Tanzania na makampuni ya kigeni,katika sekta ya madini..katika jimbo hili, wagombea wawili wa upinzani, kutoka CHADEMA na CUF wametolewa katika mchakato eti 'kwa kushindwa kukamilisha taratibu za ujazaji fomu'...kama mfuatiliaji wa siasa za Tanzania, nina maswali yafuatayo kwa yeyote mwenye majibu ama mchago wa nyongeza:
1. Je, ni kweli makampuni makubwa ya nje huingilia siasa za nchi changa ili kuhakikisha viongozi wanaoyasaidia hayo makampuni waendelee kushikilia nafasi zao za kisiasa??
2. Je, ni kweli kwamba katika mchakato wa kura za maoni za CCM mojawapo ya mgombea ktk jimbo la Sengerema alipoteza kandarasi yake ktk mojawapo ya migodi ya dhahabu kwa vile tu alimpinga Ngeleja??
3. Je, ni kweli mgombea wa CHADEMA, ambaye ni katibu wa vijana wa mkoa wa Mwanza, mhitimu wa Sheria toka UDSM mwaka 2009 na mwenyeji wa Sengerema alishindwa kutimiza wadhamini 25 na pia kusahau kujaza fomu moja??
4. Je, ni kweli mgombea wa CUF alishindwa kabisa kujaza fomu zake??
Majibu ya maswali haya (kama yapo), na michango ya ziada itasaidia kupata ukweli wa mambo katika utaratibu huu wa "kupita bila kupingwa"..PCCB tayari wanazo taarifa za kutoa rushwa za Nimrod Mkono..nadhani ni vema wakitanua wavu wao ili waweze kutoa utata katika matukio mengine kama haya..
1. Je, ni kweli makampuni makubwa ya nje huingilia siasa za nchi changa ili kuhakikisha viongozi wanaoyasaidia hayo makampuni waendelee kushikilia nafasi zao za kisiasa??
2. Je, ni kweli kwamba katika mchakato wa kura za maoni za CCM mojawapo ya mgombea ktk jimbo la Sengerema alipoteza kandarasi yake ktk mojawapo ya migodi ya dhahabu kwa vile tu alimpinga Ngeleja??
3. Je, ni kweli mgombea wa CHADEMA, ambaye ni katibu wa vijana wa mkoa wa Mwanza, mhitimu wa Sheria toka UDSM mwaka 2009 na mwenyeji wa Sengerema alishindwa kutimiza wadhamini 25 na pia kusahau kujaza fomu moja??
4. Je, ni kweli mgombea wa CUF alishindwa kabisa kujaza fomu zake??
Majibu ya maswali haya (kama yapo), na michango ya ziada itasaidia kupata ukweli wa mambo katika utaratibu huu wa "kupita bila kupingwa"..PCCB tayari wanazo taarifa za kutoa rushwa za Nimrod Mkono..nadhani ni vema wakitanua wavu wao ili waweze kutoa utata katika matukio mengine kama haya..