Feld Marshal Tantawi
JF-Expert Member
- Dec 24, 2014
- 609
- 1,009
Hili suala la Bandari naona baadhi yenu mmelibeba katika namna fulani ya UDINI, kila nikimuangalia kiongozi wangu wa KIISLAM akisimama mahali analizungumzia katika upande wa UDINI.
Sikilizeni, TEC imejaa watu wenye ELIMU kuanzia ya Elimu Dunia hadi elimu ya DINI (THEOLOJIA), ndo maana utasikia Askofu Dr, Eng, Prof fulani fulani wa Parokia fulani. Sisi ukishamqliza kusoma Quran umemaliza, mengineyo ni majungu. Yaani mtu kama Prof Lipumba alitakiwa awe Imamu wa Msikiti fulani mahali fulani na kiongozi fulani katika nafasi za Bakwata taifa, lakini matokeo yake kule tumewaweka wengine. Sisemi kwamba waislam hatujasoma, hapana, PhD zilizopo katika nafasi za uongozi misikitini ni chache mno kulinganisha na wenzetu.
Ndo maana linapofikia jambo la kuongea na kiongozi mkuu wa nchi, hawa TEC, KKKT na mengineyo utaona utofauti, sisi runaomba kupunguziwa ama kuondolewa kodi za TENDE na kuomba tupatiwe VIFAA vya kisasa vya KUUTAZAMA MWEZI mtukufu. Wenzetu wanaomba mismaha ya kodi ya makontena ya vifaa tiba, vifaa vya elimu na mengineyo. Sisi tukishakunywa juisi za tende Ikulu tunashukuru na kuondoka na kushika shikashika videvu kama SUNNAH, tunaondoka.
Leo tunawaona TEC wabaya katika msimamo, mali zetu wenyewe tunashindwa kuzisimamia wenyewe, hapa Kinondoni nadhani kidogo tupigwe na wachache kwenye eneo letu ambalo Bakwata ipo. Tumshukuru Hayati Magufuli (Mkristo) alitusaidia na kutuombea msaada wa kujengewa Msikiti.
Kuna namna nawatazama viongozi kama wanafki, na mnafki siku zote maendeleo kwake yanakawia. Najua huu ujumbe mchungu na mnaweza hata kuitisha kikao mkanisomea ALBADIRI. Ndio, TEC wametoa WARAKA wenye HOJA, mbona hamzikosoi HOJA zao mnajikita katika UDINI? Kwani huu mkataba unaopingwa nyinyi hamkwenda IKULU pamoja nao kabla ya huu waraka? Mlienda kufanya nini? Si mlipeleka mapendekezo ya marekebisho?
Mbona leo mnasita kusema kwamba mlikuwa pamoja? UNAFKI mtupu! Ndo maana katika viongozi wa kidini namkubali Sheikh Nurdin Kishki, Mziwanda, Mazinge na Dr Sulle. Hawa hawana manenomaneno, kazi yao ni kutoa DAGH'AWA tu. Huu unafki nafki umebaki kwa wasiotambua wajibu wao. Kuna shule nyingi za kiislam, matokeo yake ni mabovu. Hatuangalii kuboresha shule zetu, tumekazana kuvaa kanzu na misuli kuzodoana. Tuache Unaa. Astaghafirulah!
Mmenikwaza sana. Kuna huo Sheikh mmoja amesema yeye atasambaza waraka wa kuunga mkono nchi nzima kama tamko la msikiti, huyu hasababishi UDINI, hachochei Udini? Nani katika Uislamu amemuonya aache huo ujinga?
Mnahitaji semina! Mnahitaji kujitokeza na tamko lenye mashiko la aidha kwa nini mnaunga mkono ama mnapinga huu mkataba na muwe na sababu za kujitosheleza. Msijitokeze kwa sababu TEC wametoa WARAKA, mnatengeneza mashindano na mtachochea vurugu zisizo na msingi wowote.
Tuache UDINI, huu mkataba haupingwi kwa sababu ulisainiwa Msikitini au mbele ya imamu na wala huu mkataba hauhusiani na msikiti kwa maana DP World hawaji kujenga misikiti wala kueneza Quran. Wanakuja kuwekeza katika bandari zetu. Tukipinga tupinge kwa hoja na tukikubali tukubali kwa hoja. Tunahitaji kueleweshana, inawezekana mimi sijaelewa na pengine akijitokeza mtu akanielewesha nitamuelewa na nitaunga mkono lakini ukitumia UDINI sintokuelewa. Maana naona kila anaesimama anasema "NYUMA YA PAZIA"; hiyo nyuma ya pazia kwenye ule waraka hiyo "NYUMA YA PAZIA " iko wapi?
Asalaam alaykum!
Sikilizeni, TEC imejaa watu wenye ELIMU kuanzia ya Elimu Dunia hadi elimu ya DINI (THEOLOJIA), ndo maana utasikia Askofu Dr, Eng, Prof fulani fulani wa Parokia fulani. Sisi ukishamqliza kusoma Quran umemaliza, mengineyo ni majungu. Yaani mtu kama Prof Lipumba alitakiwa awe Imamu wa Msikiti fulani mahali fulani na kiongozi fulani katika nafasi za Bakwata taifa, lakini matokeo yake kule tumewaweka wengine. Sisemi kwamba waislam hatujasoma, hapana, PhD zilizopo katika nafasi za uongozi misikitini ni chache mno kulinganisha na wenzetu.
Ndo maana linapofikia jambo la kuongea na kiongozi mkuu wa nchi, hawa TEC, KKKT na mengineyo utaona utofauti, sisi runaomba kupunguziwa ama kuondolewa kodi za TENDE na kuomba tupatiwe VIFAA vya kisasa vya KUUTAZAMA MWEZI mtukufu. Wenzetu wanaomba mismaha ya kodi ya makontena ya vifaa tiba, vifaa vya elimu na mengineyo. Sisi tukishakunywa juisi za tende Ikulu tunashukuru na kuondoka na kushika shikashika videvu kama SUNNAH, tunaondoka.
Leo tunawaona TEC wabaya katika msimamo, mali zetu wenyewe tunashindwa kuzisimamia wenyewe, hapa Kinondoni nadhani kidogo tupigwe na wachache kwenye eneo letu ambalo Bakwata ipo. Tumshukuru Hayati Magufuli (Mkristo) alitusaidia na kutuombea msaada wa kujengewa Msikiti.
Kuna namna nawatazama viongozi kama wanafki, na mnafki siku zote maendeleo kwake yanakawia. Najua huu ujumbe mchungu na mnaweza hata kuitisha kikao mkanisomea ALBADIRI. Ndio, TEC wametoa WARAKA wenye HOJA, mbona hamzikosoi HOJA zao mnajikita katika UDINI? Kwani huu mkataba unaopingwa nyinyi hamkwenda IKULU pamoja nao kabla ya huu waraka? Mlienda kufanya nini? Si mlipeleka mapendekezo ya marekebisho?
Mbona leo mnasita kusema kwamba mlikuwa pamoja? UNAFKI mtupu! Ndo maana katika viongozi wa kidini namkubali Sheikh Nurdin Kishki, Mziwanda, Mazinge na Dr Sulle. Hawa hawana manenomaneno, kazi yao ni kutoa DAGH'AWA tu. Huu unafki nafki umebaki kwa wasiotambua wajibu wao. Kuna shule nyingi za kiislam, matokeo yake ni mabovu. Hatuangalii kuboresha shule zetu, tumekazana kuvaa kanzu na misuli kuzodoana. Tuache Unaa. Astaghafirulah!
Mmenikwaza sana. Kuna huo Sheikh mmoja amesema yeye atasambaza waraka wa kuunga mkono nchi nzima kama tamko la msikiti, huyu hasababishi UDINI, hachochei Udini? Nani katika Uislamu amemuonya aache huo ujinga?
Mnahitaji semina! Mnahitaji kujitokeza na tamko lenye mashiko la aidha kwa nini mnaunga mkono ama mnapinga huu mkataba na muwe na sababu za kujitosheleza. Msijitokeze kwa sababu TEC wametoa WARAKA, mnatengeneza mashindano na mtachochea vurugu zisizo na msingi wowote.
Tuache UDINI, huu mkataba haupingwi kwa sababu ulisainiwa Msikitini au mbele ya imamu na wala huu mkataba hauhusiani na msikiti kwa maana DP World hawaji kujenga misikiti wala kueneza Quran. Wanakuja kuwekeza katika bandari zetu. Tukipinga tupinge kwa hoja na tukikubali tukubali kwa hoja. Tunahitaji kueleweshana, inawezekana mimi sijaelewa na pengine akijitokeza mtu akanielewesha nitamuelewa na nitaunga mkono lakini ukitumia UDINI sintokuelewa. Maana naona kila anaesimama anasema "NYUMA YA PAZIA"; hiyo nyuma ya pazia kwenye ule waraka hiyo "NYUMA YA PAZIA " iko wapi?
Asalaam alaykum!