NDOA: Zamani vs Siku hizi

...asante mwj1....

...unapozungumzia changes una maanisha nini? kwa muono wako, wadhani mabadiliko haya yameanza lini kiasi cha kulinganisha uzamani wa wazazi wetu na huu usasa wa kikwetu?

...mtazamo wangu wa ndoa za kisasa nalinganisha waliooana 1980's kuja mpaka leo hii 2011....kasi ya watu kuoana na kuachana imekuwa kubwa kulikoni wazee wetu waliokuwa wameoana miaka ya 60's na kurudi nyuma...au?



Mbu kwanza kabisa naunga mkono hoja zote za waliochangia tayari. Nakubaliana na maelezo sawia aloyatoa AshaDii na wengineo ila naomba nitoe ufafanuzi kidooogo.
Kuhusu women's rights au kujitambua kwa wanawake kama ilivyosemwa na wengi waliotangulia. Kwa mtazamo wangu hiki si kitu kibaya hata kidogo. Sidhani kama ni vibaya kuwa au kuzitambua haki za kila mmoja wetu. Tatizo nilionalo hapa ni namna tulivyoyapokea haya "Mahubiri" ya Women's Rights. Wanawake wengi tumejikuta tukishabikia haki hizi kama wafungwa washabikiavyo msamaha wa rahic bila kufikiria ukitoka jela humu utaishije ili usiharibu tena. Wanawake wengi wamepotea mahubiri haya kwa ushindani ule wa ...haya sasa nasie tuna haki. Ushindani ambao umepelekea wengi wetu kujikuza na kujikweza huku tukizisahau staha zetu, heshima zetu na ustaarabu wetu.

Laiti tungeyapokea 'mahubiri' haya na kuyajazia kwenye kikapu chetu chenye staha, heshma na ustaarabu apaswao mwanamke badala ya kuzitoa staha, heshima na staarabu zetu na kuzitupa nje ili Women's rights zipate nafasi. (hapa ninayo mengi kuongea utafikiri nimelipwa na TAMWA)

Kuhusu Upendo:
Kwa mtazamo wangu mie haya mapenzi ya "Egoli" tuliyoyaiga toka kwa wazungu yamechangia kwa kiasi kikubwa udhaifu katika ndoa nyingi za siku hizi. Hii kujidai unataka kufall in love ndo uoe/olewe imetupelekea kuiumbia na kuikubali counterprt ya falling in love ambayo ni falling out of love. Siku hizi si jambo la kushangaza kujikuta unaitwa kwenye kusuluhoisha ndoa ambayo mmoja wa wanandoa hao alilala tu usiku na kuamka asubuhi akiwa ameshafall out of love na sasa anadai talaka au anataka kuvunja ndoa. Na ajabu sana kuna kila aina ya justification ya hii falling out of love ambayo mwisho wa siku tunalazimika kukubaliana na muota ndoto huyo.
Wazee wetu wa zamani hawakuwaga na falling in love bali walikuwa na Growing in love...it just keep on growing hakuna kufall out na ndio maana walikuwa wavumilivu. Kwa kuwa unaishi kwenye ndoa ambayo kadri siku ziendavyo love inajijenga, kukua na kukomaa hata ukifanyiwa kosa gani wewe unajihisi kumpenda zaidi ingawa kwa manung'uniko kwa ndani! Ndoa za siku hizi kwa kadri unavyokosea mwenzio ndivyo anavyoendelea kuizungusha door knob ya love na mwisho anaufunguua na baaam amefall out.

Samahani imekuwa ndefu.
 
Ahsante sana Kaka Mbu kwa huu uzi wa kufungia mwaka...naamini utasaidia kuwaelimisha wale waliokuwa wanalalamika kwamba MMU is not all about ngono!!

Hapa tulipo, tuko kwenye kipindi cha mpito...ni kama u-teenager! Kwa hiyo hii transition imezua mkanganyiko na mitafaruku ambayo imegusa maeneo mengi ya maisha ikiwemo taasisi ya ndoa!

Ngoja kwanza nipumue kidogo,

Babu DC!!
 
  • Thanks
Reactions: Mbu
Mbu tatizo ni kwamba watu tu hodari waku-exaggerate mambo. Haki za wanawake hazisimami kupingana na majadiliano ndani ya ndoa. Huo ukandamizaji unaoongelea unatokana na mwanaume kutaka kuwa mwamuzi juu ya maisha ya mwanamke badala ya kumfanya rafiki/partner wake, mtu wa kushauriana na kujadiliana mpaka kufikia muafaka kwenye kila jambo.

Hata kumtaka mtu abadili alichovaa kunaweza kuwa ukandamizaji iwapo unamuORDER kama mtoto, badala ya kumshawishi kwa kumueleza na kumuelewesha sababu ya wewe kutaka afanye hivyo. Ndoa/mahusiano yoyote ambayo mmoja (mke au mume) anataka awe mtu wa kusema tu "FANYA HIVI, FANYA VILE" na kutegemea "NDIO MZEE" toka kwa mwenzake lazima yawe na matatizo.Na hapa ndipo nnapokubaliana na FF kwamba haitakiwi mmoja amuoe mwenzake bali inatakiwa muoane. Muwe marafiki na wapenzi, sio mmoja awe boss wa mwenzake.
 
Kuhusu Upendo:
Kwa mtazamo wangu mie haya mapenzi ya "Egoli" tuliyoyaiga toka kwa wazungu yamechangia kwa kiasi kikubwa udhaifu katika ndoa nyingi za siku hizi. Hii kujidai unataka kufall in love ndo uoe/olewe imetupelekea kuiumbia na kuikubali counterprt ya falling in love ambayo ni falling out of love. Siku hizi si jambo la kushangaza kujikuta unaitwa kwenye kusuluhoisha ndoa ambayo mmoja wa wanandoa hao alilala tu usiku na kuamka asubuhi akiwa ameshafall out of love na sasa anadai talaka au anataka kuvunja ndoa. Na ajabu sana kuna kila aina ya justification ya hii falling out of love ambayo mwisho wa siku tunalazimika kukubaliana na muota ndoto huyo.
Wazee wetu wa zamani hawakuwaga na falling in love bali walikuwa na Growing in love...it just keep on growing hakuna kufall out na ndio maana walikuwa wavumilivu. Kwa kuwa unaishi kwenye ndoa ambayo kadri siku ziendavyo love inajijenga, kukua na kukomaa hata ukifanyiwa kosa gani wewe unajihisi kumpenda zaidi ingawa kwa manung'uniko kwa ndani! Ndoa za siku hizi kwa kadri unavyokosea mwenzio ndivyo anavyoendelea kuizungusha door knob ya love na mwisho anaufunguua na baaam amefall out.

Samahani imekuwa ndefu.

Hapa sasa umeanza kunigusa dada yangu,

Kuna kitu nimekiongea mara nyingi hapa ndani na kila huwa nahisi watu hawanielewi.....Suala la mapenzi limechukuliwa juu juu zaidi na watu wanadanganyika kwa vitu vya hovyo zaidi.....Romantic comedians wanatumia njia hizi kuwanasa wenzi wao!!

Growing in love is the perfect thing...na ndio maana watu ambao hawakufahamiana hapo awali waliweza kuishi pamoja na kuwa na familia imara!
 
ndoa za zamani walikuwa hawafahamiani wala kujuana lakini walijifunza kupendana na waliweza kuhimili lolote katika ndoa kwa uvumilivu na upendo wa dhati....za sasa imekuwa kama fasheni mtu anaolewa kuondoa aibu kwenye familia...unaweza kuta msichana anampenda mvulana lakini mvulana sio sana inabidi kuoa kwa huruma fulani vivyo hivyo kwa mvulana anapenda sana bi dada anakubali kwa vile asionekana mbaya au baada kukosa wa kumwoa.... pia wengine wanaoana umri unakwenda bora lolote au jamaa maisha yanalipa. kwa jumla maisha ya ndoa za sasa yanaangalia vitu na sio upendo wa dhati
 
Mbu tatizo ni kwamba watu tu hodari waku-exaggerate mambo. Haki za wanawake hazisimami kupingana na majadiliano ndani ya ndoa. Huo ukandamizaji unaoongelea unatokana na mwanaume kutaka kuwa mwamuzi juu ya maisha ya mwanamke badala ya kumfanya rafiki/partner wake, mtu wa kushauriana na kujadiliana mpaka kufikia muafaka kwenye kila jambo.

Hata kumtaka mtu abadili alichovaa kunaweza kuwa ukandamizaji iwapo unamuORDER kama mtoto, badala ya kumshawishi kwa kumueleza na kumuelewesha sababu ya wewe kutaka afanye hivyo. Ndoa/mahusiano yoyote ambayo mmoja (mke au mume) anataka awe mtu wa kusema tu "FANYA HIVI, FANYA VILE" na kutegemea "NDIO MZEE" toka kwa mwenzake lazima yawe na matatizo.Na hapa ndipo nnapokubaliana na FF kwamba haitakiwi mmoja amuoe mwenzake bali inatakiwa muoane. Muwe marafiki na wapenzi, sio mmoja awe boss wa mwenzake.

Samahani Lizzy,

Ndoa ni ya watu wawili kwa hiyo hatuwezi kusema kuwa matatizo ya ndoa yanasababishwa na wanaume peke yao.

Labda kama nimekuelewa vibaya!!
 
  • Thanks
Reactions: Mbu
ndoa za zamani walikuwa hawafahamiani wala kujuana lakini walijifunza kupendana na waliweza kuhimili lolote katika ndoa kwa uvumilivu na upendo wa dhati....za sasa imekuwa kama fasheni mtu anaolewa kuondoa aibu kwenye familia...unaweza kuta msichana anampenda mvulana lakini mvulana sio sana inabidi kuoa kwa huruma fulani vivyo hivyo kwa mvulana anapenda sana bi dada anakubali kwa vile asionekana mbaya au baada kukosa wa kumwoa.... pia wengine wanaoana umri unakwenda bora lolote au jamaa maisha yanalipa. kwa jumla maisha ya ndoa za sasa yanaangalia vitu na sio upendo wa dhati
Sasa mkwe kama zamani kupendana kulikua kunakuja baadae huo upendo wa dhati walikua wanaangalia vipi kabla ya kukubali/amua kuoana?
 
Pamoja na kukosa hofu ya Mungu, bado kuna sababu nyingine.

Nikupe mfano, huko nitokako mwanamke alikuwa anatafutiwa mume wala asiye mjua. Kunq upendo hapo? Utampendaje mtu usiyemjua unamwona siku ya ndoa?

Tena kuna wakati unaletewa kibabu, unalazimisha kuolewa kwa kupigwa lakini bado ndoa zilikuwa zinadumu.

Ukisema hofu ya Mungu, sidhani maana hizi dini ni tamaduni mpya. Lakini bado babu zetu wamekaana wake zao hadi vifo vilipowatenganisha wakati hawakuwa wanajua kanisa lolote zaidi ya matambiko ya jadi.

Mi naona ni mwingiliano wa tamaduni zaidi katika nyanja zote.

Ndoa za kisasa hazidumu kwa sababu watu wanaoana kwasababu zingine ukiacha sababu za kidini na upendo baina yao. Wanandoa wengi wa sasa hawana hofu ya mungu wala hawafati mila na desturi zao ambazo kwa namna moja au nyingine zingewasaidia kuwaweka pamoja.
 
ndoa za zamani walikuwa hawafahamiani wala kujuana lakini walijifunza kupendana na waliweza kuhimili lolote katika ndoa kwa uvumilivu na upendo wa dhati....za sasa imekuwa kama fasheni mtu anaolewa kuondoa aibu kwenye familia...unaweza kuta msichana anampenda mvulana lakini mvulana sio sana inabidi kuoa kwa huruma fulani vivyo hivyo kwa mvulana anapenda sana bi dada anakubali kwa vile asionekana mbaya au baada kukosa wa kumwoa.... pia wengine wanaoana umri unakwenda bora lolote au jamaa maisha yanalipa. kwa jumla maisha ya ndoa za sasa yanaangalia vitu na sio upendo wa dhati

BW,

Unayosema ni ya kweli. Kuna kitu kilisaidia sana kuziba hayo mapengo ya one sided love. Taasisi ya ndoa ililindwa na jamii yote kwa nguvu nyingi kiasi kwamba watu walijikuta wanawajibika kuilinda na kuenzi.

Hii tunu imepotea siku hizi kwa sababu ndoa imebinafsishwa...Ukizingatia kuwa bado tuko kwenye kipindi cha mpito ambapo hatuna system mbadala, ndiyo maana tunayumba na mawimbi yanaonekana kuwa makubwa sana kama tsunami!!
 
Samahani Lizzy,

Ndoa ni ya watu wawili kwa hiyo hatuwezi kusema kuwa matatizo ya ndoa yanasababishwa na wanaume peke yao.

Labda kama nimekuelewa vibaya!!

Babu hamna niliposema mwanaume ndie wakulaumiwa, ila katika harakati za kumjibu Mbu kuhusu mume kutaka mkewe avae kiheshima ili kulinda ndoa nimegusia kwamba inatakiwa wawili hao (wenye ndoa) wawe wanajadiliana badala ya mmoja kumuendesha mwenzake (iwe mke au mume).
 
Nionavyo mimi.......Haki za wanawake ni tatizo,ni tatizo coz wanawake wanachohitaji ni kuwa SAWA na wanaume.Mwanaume anaweza kuwa ana makosa lakini haya makosa yaangaliwe kimtazamo wa kimaandiko zaidi,na hayo makosa ya mwanaume yatazamwe kimaandiko!Mfano maandiko yamekataza mwanamke KUMTAWALA mwanaume,pia yamekataza KUMFUMDISHA mwanaume na hizi ni moja ya "haki" anazozipigania mwanamke,kwenye ndoa haiwezekani kila kitu kikafanywa na kila mwanandoa,yapo ya mwanamke yapo ya mwanaume,vurugu za usawa ndo chanzo cha talaka nyingi,matokeo yake watoto wanakosa malezi tunapata matokeo ya tabia nyingine za kijinga na za ajabu!
 
  • Thanks
Reactions: Mbu
Nionavyo mimi.......Haki za wanawake ni tatizo,ni tatizo coz wanawake wanachohitaji ni kuwa SAWA na wanaume.Mwanaume anaweza kuwa ana makosa lakini haya makosa yaangaliwe kimtazamo wa kimaandiko zaidi,na hayo makosa ya mwanaume yatazamwe kimaandiko!Mfano maandiko yamekataza mwanamke KUMTAWALA mwanaume,pia yamekataza KUMFUMDISHA mwanaume na hizi ni moja ya "haki" anazozipigania mwanamke,kwenye ndoa haiwezekani kila kitu kikafanywa na kila mwanandoa,yapo ya mwanamke yapo ya mwanaume,vurugu za usawa ndo chanzo cha talaka nyingi,matokeo yake watoto wanakosa malezi tunapata matokeo ya tabia nyingine za kijinga na za ajabu!
Inabidi na walimu wote wa kike mashuleni WAFUKUZWE.
 
  • Thanks
Reactions: Mbu
Sasa mkwe kama zamani kupendana kulikua kunakuja baadae huo upendo wa dhati walikua wanaangalia vipi kabla ya kukubali/amua kuoana?

Niliwahi kuelezea kitabu kimoja ambacho kinajadili haya mambo ya muhimu kwenye ndoa (marriage triangle...love, sex and living together) wapi pa kuanzia...Which to me, nakubaliana na mwandishi kwamba unaweza kuanza na lolote. Kama unajitambua, hakuna shaka kwamba ndoa yako itakuwa imara!!

Hebu chungulia hapa,

http://www.amazon.com/I-Married-You-Walter-Trobisch/dp/0966396669
 
Sasa mkwe kama zamani kupendana kulikua kunakuja baadae huo upendo wa dhati walikua wanaangalia vipi kabla ya kukubali/amua kuoana?

Upendo unafundishwa kwenye familia,ndoa ni uamuzi sio upendo,ukijua kupenda haitakua kazi kuanzisha familia na YOYOTE kwani unakua umempenda tayari!Umempenda coz kigezo cha kupenda ni huyo awe binadam na sio awe na hela au mrefu au miguu ya bia au mtanashati!
 
Nani kasema ndo za kisasa hazidumu? Mbona vijana wengi tu wanaowa na wanaishi na wake zao vizuri tena wanapendana kuliko wale wa zamani.

Inategemea kama umelelewa vizuri nyumbani kwenu lazima utaheshimu tu ndoa yako....Kama umetoka sehemu baba ana mnyanyasa mama na wewe utaiga mila za baba yako....

Mimi naona ndo za siku hizi kama hazidumu sababu ni ndogo sana,,,Wengi wamerukia kuowa kabla ya kujua ndoa ni kitu gani.

Na wengi wanarukia kuwashakia wake zao kwa sababu wao wenyewe wahuni ndo mana wanashakia na wake zao wahuni.

Mwanaume anaye thamini mke wake hawezi kumshakia shakia mke wake na mwanamke anaye mthamini mme wake hawezi kuwa na wasi wasi naye,

Mara nyingi ukiona kwenye ndoa kuna kasora basi kuna wivu...ulio pita kiasi....Mwanaume hajiamini na hamuamini mke wake...sasa kama hamuamini mke wake ya nini kaowa....na Mwanamke kama hamuamini mme wake ya nini kaolewa...
 
  • Thanks
Reactions: Mbu
Inabidi na walimu wote wa kike mashuleni WAFUKUZWE.

From the begining mwanamke hakutakiwa kutoka kwenda kuzurula kutafuta kazi,hiyo ilikua kazi ya mwanaume,Yes WAFUKUZWE!Kwani nini!
 
Niliwahi kuelezea kitabu kimoja ambacho kinajadili haya mambo ya muhimu kwenye ndoa (marriage triangle...love, sex and living together) wapi pa kuanzia...Which to me, nakubaliana na mwandishi kwamba unaweza kuanza na lolote. Kama unajitambua, hakuna shaka kwamba ndoa yako itakuwa imara!!

Hebu chungulia hapa,

http://www.amazon.com/I-Married-You-Walter-Trobisch/dp/0966396669
Sasa kama inaweza kuanzia popote kwanini unaona kwamba wanaoanza kwa kupendana wanakosea/ndio sababu ya ndoa kutokudumu?

Mara nyingi kinachofanya mtu afanikiwe sio anapo/anavyoanza bali ni malengo yake na namna anavyojituma kufikia matarajio yake. Zaidi ya hapo hata kama leo hii nikiamua kumchagua mtu randomly na kuoana nae huku nikiwa na malengo yasiyoendana nae au hata hiyo ndoa hatutofika popote. Mbaya zaidi ikitokea nikawa na matarajio ambayo sipo tayari kufanya kazi ili niyafikie, sitofikia na hivyo kunifanya mimi nione nilikosea step katika kumchagua mhusika even though tatizo lipo kwangu na sio kwake.
 
  • Thanks
Reactions: Mbu
Upendo unafundishwa kwenye familia,ndoa ni uamuzi sio upendo,ukijua kupenda haitakua kazi kuanzisha familia na YOYOTE kwani unakua umempenda tayari!Umempenda coz kigezo cha kupenda ni huyo awe binadam na sio awe na hela au mrefu au miguu ya bia au mtanashati!

Kupenda ni rahisi, kuishi na mtu ambae sio compatible na wewe ni habari nyingine kabisa.
 
  • Thanks
Reactions: Mbu
Matazamo wa mwanamke KUONGOZWA na mwanaume kuwa ni kukandamizwa iko siku mtajasema hata kumnyonyesha mtoto ni matokeo ya mfumo dume!Mnaimbishwa wimbo msioujua na wala hamjui ulipotokea!
 
Back
Top Bottom