Feedback
JF-Expert Member
- Mar 14, 2011
- 7,988
- 4,507
MAMIA ya wakazi wa mji wa Moshi wamejitokeza kwenye ofisi ya Mbunge wa jimbo hilo, Philemon Ndesamburo (CHADEMA) kujiorodhesha majina kwa ajili ya safari ya kuelekea kwa Mchungaji Ambilikile Mwasapile, katika Kijiji cha Samunge, Loliondo anayetoa dawa ya kutibu magonjwa sugu.
Wananchi hao wamejitokeza baada ya mbunge huyo kuamua kutoa usafiri wa bure wa kuwapeleka na kuwarudisha wale wote wenye kusumbuliwa na magonjwa sugu ambayo tiba yake hutolewa na ‘Babu' baada ya kuona wananchi wengi wanahitaji kwenda ila wanakwamishwa na fedha za nauli ambazo zimefikia kiasi cha shilingi 150,000.
Akiongea na waandishi wa habari ofisini kwake jana huku nje kukiwa na misururu mirefu ya wananchi wanaojiorodhesha, Ndesamburo alisema kuwa watawapeleka wananchi hao kwa awamu ambapo kwa kuanzia leo (Jumanne) jumla ya watu 73 wataondoka majira ya saa kumi jioni kuelekea Loliondo na wakirudi wataondoka wengine.
Wananchi hao wamejitokeza baada ya mbunge huyo kuamua kutoa usafiri wa bure wa kuwapeleka na kuwarudisha wale wote wenye kusumbuliwa na magonjwa sugu ambayo tiba yake hutolewa na ‘Babu' baada ya kuona wananchi wengi wanahitaji kwenda ila wanakwamishwa na fedha za nauli ambazo zimefikia kiasi cha shilingi 150,000.
Akiongea na waandishi wa habari ofisini kwake jana huku nje kukiwa na misururu mirefu ya wananchi wanaojiorodhesha, Ndesamburo alisema kuwa watawapeleka wananchi hao kwa awamu ambapo kwa kuanzia leo (Jumanne) jumla ya watu 73 wataondoka majira ya saa kumi jioni kuelekea Loliondo na wakirudi wataondoka wengine.