Ndalichako kutemwa Baraza la Mitihani ili kumwokoa Shukuru Kawambwa

Nakubaliana na wewe 100%, inawezekana watu hawajui kazi na necta! kuna mchanganyiko wa mambo hapa! suala la sera ya elimu, liko wizara ya elimu, kusahihisha liko chini ya wizara ya eleimu pia, kufundisha liko kwa waziri ya tamisemi, maana wao ndio waajili wa waalimu..............ukisikia kachumba ndio hiiiiiii sasa

NECTA inatunga na kusahihisha mitihani na hatimaye kutangaza matokeo ya mitihani. Haihusiki na ufundishaji - sasa kitakuwa kihoja Mkurugenzi wa NECTA kuwajibishwa kutokana na maafa haya!!!! Waziri anaweza kuwajibishwa au kuwajibika (kisiasa) mwenyewe kwa vile yeye ndio kichwa cha sekta yote ya elimu nchini. Lakini hata hivyo lo lote linawezekana bongoland, itself another wonder of the world.
 
Mh. Mbatia alitaka education refoms wao (mawaziri na wabunge wa ccm ) wakang'ang'ania suala la mitaala tu. Hawa wanatupeleka pabaya.
 
Hiyo ni gia tu ya serikali kutimiza matakwa ya watu wanaowaogopa nchini(waislam).Ndalichako usikubali kuondoka we kataaa
 
NECTA inatunga na kusahihisha mitihani na hatimaye kutangaza matokeo ya mitihani. Haihusiki na ufundishaji - sasa kitakuwa kihoja Mkurugenzi wa NECTA kuwajibishwa kutokana na maafa haya!!!! Waziri anaweza kuwajibishwa au kuwajibika (kisiasa) mwenyewe kwa vile yeye ndio kichwa cha sekta yote ya elimu nchini. Lakini hata hivyo lo lote linawezekana bongoland, itself another wonder of the world.
Uko sahihi kimantiki, lakini kisiasa (kichama) sio.Nikiiamini taarifa ya mleta uzi kuwa Dr. Ndalichako aliombwa achakachue akakataa, kisha nikirejea alivyonukuliwa kwenye gazeti la Mwanachi la 19 Feb 13, baadhi ya wanafunzi waliandika namba zao tu kwenye karatasi za majibu akatolea mfano wa mtihani wa biolojia, na kuwa wao NECTA walifanya jitihada za kupiga simu kwa Walimu wa wanafunzi hao na kuambiwa kuwa wanafunzi walifanya hivyo kwa KUWA HAWANA WALIMU WA MASOMO HAYO! Kama nikweli, natarajia kabisa hiki kipengele kimtie matatizoni.
 
Nchi imelogwa hii! Madudu yanafanyika waziwazi hakuna anaechukua hatua,kuanzia rais mpaka wananchi wenyewe.
 
Mi nasubiri hayo matokeo kubadilika baada ya Ndalichako kuachishwa kazi
Hizo ziro zitakuwa One hahahhaha
 
Kama tuko kwenye vita ya udini kumuondoa Dr.Ndalichako kutaongeza tafrani ni bora kuliangalia tatizo liko wapi.Necta haina secondary bali Waziri ndiyo mwenye shule na walimu.
Hebu tuangalie kwa upande huu hivi Mwanafunzi wa uhasibu akifelie au wakifeli robo tatu ya watahiniwa tutaenda kuwaambia bodi ya wahasibu wajiuzulu sababu wanafunzi wa uhasibu wamefeli?Je ndio wanaofundisha wanafunzi wao?Tuache siasa,na kama ni kweli Dr.Ndalichako aliombwa achakachue matokeo then nadhani Chama Cha Mapinduzi hawana nia nzuri na watoto wetu.Rais aanzie tu na mawaziri kabla hajafika kwa Ndalichako.
Na ningemuomba Dr.Ndalichako wakimwajibisha akawashtaki.
 
Waziri mhusika awajibike. Necta hawana makosa kwani kazi yao ni kutunga kuhakiki na kusahihisha mitihani.[New jf member]
 
Kama siyo juhudi zako Nyerere X 3
Na Kikwete angesoma wapi

Kama siyo juhudi zako Nyerere X 3
Mama Salma angesoma wapi

Kama siyo juhudi zako Nyerere X 3
Na Wassira angesoma wapi

Kama siyo juhudi zako Nyerere X 3
Na Kawambwa angesoma wapi

Kama siyo juhudi zako Nyerere X 3
Na Makinda angesoma wapi

Kama siyo juhudi zako Nyerere X 3
Na Ndugai angesoma wapi
 
Habari zilizoenea miongoni mwa wafanyakazi wa NECTA na wizara ya Elimu tangu jana jumatano zinasema wakati wowote kuanzia sasa Katibu Mtendaji wa baraza la Mitihani - Dr. JOYCE NDALICHAKO atang'olewa katika nafasi yake!....
kumjenga
Anaondolewa ili kisiasa DR. Shukuru Kawambwa, kufuatia matokeo mabaya ya kidato cha nne!... Haya ni matokeo mabaya ya kihistoria katika nchi ya Tanzania... hayajawahi kutokea na pengine hayatatokea tena siku za usoni.Hizi ni TAKWIMU ZA UKWELI!.....

  • DIV ONE 1,641
  • TWO 6,453
  • THREE 15,421
  • FOUR 103,327
  • ZERO 240,903! SAFI SANA WALIMU!

Hofu kubwa imekuwa kelele nyingi za chini chini na wazi wazi Zinazomtaka Dr. Kawambwa ajiuzulu. Matukio ya uchomaji moto kanisa na mauaji ya padre Mushi yamepunguza kidogo presha na shutuma za matokeo.

Hofu pia inachangiwa na moto uliowashwa na Mbatia na kuungwa mkono na wapinzani wote kuhusu kuporomoka kwa ubora wa elimu na ukosefu wa mitaala. Kwa mujibu wa wafanyakazi hao hoja hii pia ilichangia ucheleweshaji wa kutangaza matokeo!...

Dr. Ndalichako pia analaumiwa kuwa aliwajibu vibaya wanasiasa walipomtaka ACHAKACHUE matokeo ILI KUFICHA aibu hii!.. Yeye aliwajibu kavukavu kuwa YEYE HAJUI NA TENA HAWEZI KUCHAKACHUA!.. Bifu hili liliendelea mpaka utangazaji wenyewe ukawa mikononi mwa waziri Kawambwa na msaidizi wake MULUGO!. KATIBU MTENDAJI - Ndalichako hakung'ara kama ilivyozoeleka wakati wa kutangaza matokeo.

MATOKEO HAYA Yamekuwa yakishambuliwa kupitia njia mbalimbali zikiwemo simu za mkononi na hii ni moja ya sms hizo:


ELIMU JUUUUUUUUUUUUUUUUUUUUU!!!! WALIMU SAFIIIIIIIIIII!!! WATANZANIA HASA WENYE TAALUMA YA UALIMU NA WENYE MAPENZI MEMA NA NCHII!

TUNATUMIA FULSA HII KUWAPONGEZA WALIMU WA SEKONDARI KWA MATOKEO MAZUR YA KIDATO CHA NNE AMBAYO HAYAJAWAH KUTOKEA TOKA BARAZA LA MITIHAN LIUNDWE NCHINI!

WALIMU WAMEONESHA FADHILA KWA SERIKAL YA CCM KWA MAMBO MEMA ILIYOWATENDEA! HII MTAALA WA WAZIR KAWAMBWA NA MULUGO UMETOA MATOKEO HAYA:

DIV ONE 1,641 TWO 6,453 THREE 15,421 FOUR 103,327 ZERO 240,903! SAFI SANA WALIMU!

MTAALA BORA ELIMU BORA YA CCM! UNALIPA UNAVYOLIPWA! HEKOHEKO WALIMU!
kwa aliyokuwa anaongea waziri wa elimu katika kipindi cha tuongee asubuhi siku ya jnne,anaetakiwa kujiuzulu ni waziri mwenyewe maana anaonyesha kwamba kufeli kwa watoto hilo sio jambo la kutisha
 
Yatakuwa maamuzi ya "Kimasaburi" kumpiga chini Dr Ndalichako!!!! Wanaotakiwa kupigwa chini ni Home Boy Shukuru kawambwa na kilaza philipo mulogoIla ikumbukwe Waislam kupitia sheikh ponda walitaka kumng'oa Dr ndalichako wakiadai eti kawafelisha waislam.Dhaifu awe makini na suala hili la kumtosa Dr Ndalichako.
 
Pamoja na reforms zoote tunazotaka kufanya, malezi na.makuzi yasisahaulike. Tunao ndugu, hata kama sio watoto wetu ambao wamefanya huu mtihani. Kuna aliepata division 3 na hakulala kwa kilio na masononeko. Kuna aliepata 4 na anakenua meno ukimuuliza matokeo. Lakini tofauti unaiona kwenye malezi ya wazazi wao.

Sichoki kuwaza wazazi wangu binafsi, ningewarudia na division 4 ama 0 (sheria ilikuwa hata 2 haikubaliki!), ingekuwaje. Watoto wakifeli na hata wasione soni juu ya hilo, kuna maswali zaidi ya kujiuliza!
kitu cha kwanza ili tufanikiwe na chochote katika nchi hii ni kuitoa ccm madarakani kwanza
 
Hakuna shule bila walimu, Serikali iondoe pamba masikioni na iwesikivu iache vitisho kwa walimu. hayo ni manyunyu Masika yanakuja mwakani labda kuficha aibu wafaulishwe hata waliofeli! nb. Kawabwa should go now not next year just to mantain his status.
 
Hivi hii badilishabadilisha silabasi kila kukichwa imefanywa na Ndalichako au Kawambwa??? Mbona hawaangalii walipojikwaa wanaangalia walipodondokea? Tutafika kweli jamani kwa mwendo huu?

si kwa sababu amekataa kuchakachua matokeo ili kuficha ukweli. hiyo ndio serikali ya ccm. mbovu kupita maelezo.
 
Ndugu hoja sijaielewa sana isipokuwa vyovyote iwavyo si sawa kumwajibisha Ndalichako kwa kuwa hahusiki na lolote lililotokea. Kawambwa awajibike kwa hiari tumuone ni shujaa. Hoja imekaa kimajungu fulani hivi!!!!!
 
Ndalichako anaingiaje tena? wasituongezee maudhi na kuwasha moto mwingine,
maana hapo tena litaibuka suala la udini kuwa walishapanga ila walikuwa wanamtafutia
sababu Ndalichako.

Hapa Kawambwa aachie ngazi" Hapa waache ujomba wao wakutane huko Bagamoyo"
 
Back
Top Bottom