Nchi yetu inaitwa Tanganyika

Kumekuwepo na mjadala mkubwa sana wa kuendelea au kutokuendelea kwa Muungano baina ya Zanzibar na Tanzania bara. Lakini katikati ya mjadala huo kumezuka hoja ya kurudisha matumizi ya jina Tanganyika kama muungano utavunjika. Kwa maoni yangu nadhani hata bila ya kuuvunja Muungano baina ya nchi hizi mbili sisi ni watanganyika na wala si Watanzania Bara.

Hapo mwanzo wakati wa Muungano wa nchi hizi mbili ilifikiriwa kwamba nchi zote mbili zitakubali kuuacha (surender) utambulisho wa nchi zao na hatimaye zitambulike kwa majina ya Tanzania Bara na Tanzania Visiwani. Lakini kwa bahati mbaya Wazanzibar wakabakia na Jina lao la Zanzibar na Watanganyika wakakubali kuitwa Tanzania Bara bila ya kuwepo kwa Tanzania Visiwani.

Kosa kubwa walilolifanya Watanganyika ni kukubali kwao kujizoeza kujiita Watanzania Bara bila watu wa upande wa pili kukubali kuitwa Watanzania Visiwani. Wakati watanganyika waliamini wao ni nchi moja na Zanzibar, Wazanzibari waliamini kwamba wao na Watanganyika ni nchi mbili tofauti wenye haki zisizofanana.

Wazanzibari waliamini kwamba Watanganyika ni wakaliaji kimabavu nchi yao lakini wao Wazanzibari wana haki ya kuishi, kushika madaraka na kumiliki mali Tanganyika. Mzanzibari aliamini ana haki ya kuwa Diwani wa Buguruni lakini si ruhusa kwa Mtanganyika kuwa Sheha kwenye mitaa ya Mji Mkongwe Zanzibar.

Watanganyika walitoa haki zao kwa Tanzania lakini Wazanzibar wakachukua haki za Tanzania wakakataa kuzitoa haki zao za Zanzibar. Kwenye makubaliano ya uundaji wa Tanzania hakuna mahali kunapotajwa kwamba ili Tanzania iwepo kunamaanisha kuua Tanganyika na Zanzibar. Kinachotajwa ni kuvunjwa kwa nguvu za kidola za nchi hizi mbili na wala si majina ya nchi mbili hizi.

Mfano rahisi ni United States of America ambako nchi zilizoingia kwenye shirikisho hilo hazikubadili majina yao na kuwa labda Amerika ya Pwani, Amerika ya Nyanda za Juu bali kila nchi ilibakia na jina lake ila kilichobadilika ni kutoa baadhi ya mamlaka yake kwa Serikali Kuu ya shirikisho na dola ikawa ni moja USA. Kwa hiyo kwa maoni yangu si lazima tuuvunje Muungano ndiyo tuwe na haki ya kuitwa Tanganyika, hata sasa tunaweza kujiita Tanganyika kama tunaona inafaa.
 
Unfortunately Tanganyika is the country I did not see!!

The good thing is that 'she's forever young'. And her spirit will abide with me forever!

I Love you Mama Tanganyika! Let your name be exalted until we get you back home.
:Cry:
 
zanzibar imo kwenye ramani ya dunia na inajulikana hata katika google earth ukiiangalia itakuja bt tanganyika haipo ktk ramani ya dunia.

tanganyika haipo!
 
FREEDOM DREAMI ONCE SAID. "LET US ALL (THE WATANGANYIKA), WAKE UP AND FIGHT. WE CERTAINLY WILL BE KILLED (AFTER ALL BEING A SLAVE IS NOT REAL HUMAN), BUT OUR DESCENDANTS WILL PRAISE US AND PRAY FOR US.. FOR WE PLAYED OUR PART". INDIANS, SOUTH AFRICANS, AND MANY OTHERS WERE TORTURED AND KILLED; NOW THEY HAVE THEIR LAND AND FREEDOM. LET US ALL FROM, KIGOMA, BUKOBA, MARA MWANZA, S/WANGA, MBEYA, ARUSHA, TANGA , SONGEA, LINDI AND ALL REGIONS AND DISTRICTS…… MEET IN CHALINZE…… AND ADVANCE TO THE STATE HOUSE. OUR TARGET IS "TO GET JK OUT AND DECLARE OUR COUNTRY FREE". THE ARMIES AND THE POLICE WILL KILL US, BUT THEY WILL NOT FINISH ALL OF US." THOSE AT THE BACK WILL KEEP ON MATCHING TOWARDS THE LIVING ROOM OF JK. ALL BULLETS WILL BE FINISHED, ALL POLICEMEN, SOLDIERS AND GUARDS PERPLEXED, ALL MINISTERS DISAPPEARED, AND JK WILL BE ALONE....AND WE TAKE HIM TO SEGEREA... AND WE WILL FORM OUR GOVERNMENT..... THE DEMOCRATIC GOVERNMENT OF TANGANYIKA... DGT..... OH MY GOD.... YES DGT… THEN ALL OUR LAND, WITH ALL STOLEN FIXED PROPERTIES... AND ALL LAUNDERED FINANCES WILL BE REDISTRIBUTED.... AND OUR NATIONAL DEBT (14t) WILL BE PAID ..... AND WE WILL HAVE "PEOPLES GOVERNMENT" ….. AND NO CCM, NO JK, NO JK DESCENDANTS,…….. AND NO TO THIS POVERTY….. AS OUR MOTHER LAND IS RICH, FULL OF MINERALS (NOW STOLEN), FULL OF WILD ANIMALS (NOW POACHED AND SOLD), FULL OF FERTILE BASINS AND ARABLE LAND (NOW OWNED UNETHICALLY)….. FULL OF 40M CITIZENS (NOW SLAVES)….. OH NO….. TOO MUCH… TUANZE LEO/SASA WANDUGU, TWENDENI…. TWENDENI….. UKIKAA MBELE WEWE NDIO KIONGOZI…. UKIMKAMATA JK ….WEWE NDIO RAIS WA KWANZA WA DGT.
 
Znz ikiwa mbioni ktk harakati zake za kulibakisha Jina la ZANZIBAR ktk ramani ya dunia na kujivunia Jina lao, Je! kwa upande wa pili wa Muungano ni Lipi jina linalostahikki kati ya TANGANYIKA NA TANZANIA BARA? Na kwanini Tanganyika wanakataa jina lao?

NAKUKUMBUSHA TU, leo znz kama siku moja kubwa ktk harakati,nipo ktk viwanja vya maisara kwa kweli watu ni wengi mno sijawahi kuona,kama sikukuu vile au hata haijafikia... Ni kwa ajili ya dua kubwa ikitanguliwa na sala ya ijumaa,kwa ajili ya kudai ZANZIBAR NA KUIRUDISHA KTK RAMANI, ndio lengo la leo hapa.

Karibuni,kama nitapata nafasi nitakupeni dondoo za hapa.

SIKU YA UKOMBOZI IMEWAJIA
 
M/MUNGU ajaalie duaa iwe Maqbul. Kuhusu jina, kwa mtazamo wangu mimi kama mimi Globu. Ningependelea lirudi jina la TANGANYIKA.
 
historia, nimesoma japo si sana inaonekana hukunielewa vizuri kwa vile post imekaakaa kaa shairi fulani hivi, laki my point is:

1. Tanganyika ni nchi iliyobuniwa na kubatizwa jina hilo na wakoloni

2. Tanzania ni nchi iliyobuniwa na kubatizwa jina hilo na wazalendo

3. mimi na wingine wenye umri usiofikia miaka 47, tumezaliwa Tanzania na sio Tanganyika

4. muungano ni kielelezo cha umoja wetu na licha ya mapungufu yake, ni bora kuliko kutengana

5. changamoto tuliyonayo ni kuondoa mapungufu yake, iwe ni kwa kuunda serikali moja, tatu au kubaki na mbili za sasa, vyovyote vile, muhimu tuondoe kero zinazohusiana na muungano

kilichotufanya tusindwe kuijenga Tanzania si muungano uliopo, bali masuala mengi tu tunayojadili hapa kila siku kama ufisadi nk. kwa hiyo hata tukiuvunja muungano, tutashindwa kuijenga Tanganyika pia kama hatutapambana na matatizo haya (ufisadi nk)
nyerere aliwahi sema,,,hajui jina,,,,,tanganyika,,,,,lilianzia wapi,,,,,,chanzo chake ni wapi,,,,.niliwahi sikia ni wajeruman walilianzisha kutokana na jina tanga,,,,walipokuwa kule juu lushoto;;;walionyeshwa tambarare ile;;;kwa lugha za kipare na kisambaa,,,hata kizigua,,,tambarare kubwa chini ya milima,,,uwanda,,huitwa nyika,,hivyo jina leyewe sio tanga bali ndanga,,then,huo uwanda,,uliitwa ndanga nyika ,,,mjerumani akaandika tanganyika,,na ikulu ikajengwa lushoto,,,,,nawaomba na wengine wenye taarfa waweke humu tujue tanganyika ni nini na maana yake nini na asili yake wapi,,,,tutakua na hoja kuipnga au kuikubali,,,,,,,la tutapotosha kabisaa ,,,,,karibuni,,
 
ukosefu wa akili ndi unaotufanya tuone sisi ni watanzania na sio watanganyika. TANZANIA Ni muunganiko wa tanganyika na zanzibar wenzetu wanaendelea na zanzibar sisi tunang'an'ania utanzania ambao haupo. kama tunaona shida kuitwa watanganyika tutunge jina lingine lakini siyo tanzania ambayo ndani yake kuna zanzibar ambayo tayari imeshajitenga. wamevunja katiba ya JMT -URT,hakuna anawapeleka mahakamani MWANASHRIA MKUU ANAWAOGOPA WAZANZIBAR KULIKO HATA KATIBA YA TANZANIA, NDIO MAANA NASEMA SISI NI KAMA HATUNA AKILI SAWASAWA.
 
Wadau, naona Muungano huu haupo. Tujiandae kisaikolojia. Nashauri ukishavunjika taifa letu liendelee kuitwa Tanzania, maana wengi hatuijui Tanganyika. Mnasemaje?
 
Haliwezi kuendelea kuitwa Tanzania kama muungano ukivunjika, jina Tanzania ni result ya muungano so no muungano no Tanzania! Halfu umesema haujui Tanganyika sasa how did u come to write about it, au ulikua unarefer to a certain group of people?
 
Mi naona chochote kinafaa..........jina halina maana yoyote kwangu iwapo hakuna uhusiano wa jina na maendeleo....hata tukiitwa crazy country provided tuna maendeleo mi poa tu.
 
Km Czeck na Slovakia zilirudia majina yao baada ya Muungano kuvunjika, pia jamhuri za kisoviet i.e Ukraine, Lithuania, pia Senegal na Ghambia, why sisi tusirejeshe Tanganyika yetu?
 
Daressalaam iondolewe ni jina la enzi za Utumwa, Sultani wa Zanzibar iliita baada ya urahisi wa kupata watumwa
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom