Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,476
- 39,995
Gloria Tesha
Daily News; Saturday,October 25, 2008 @00:02
Chama Cha Mapinduzi (CCM), kimesema nchi haijachafuka wala kuyumba kama wanavyosema baadhi ya viongozi wa vyama vya siasa na kuwataka Watanzania wapuuze kauli hizo zenye kila dalili ya uchochezi.
Aidha, CCM imemtaka Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe, kuacha mara moja tabia ya kumsema vibaya Rais Jakaya Kikwete kwa kile kilichodai kuwa ni udhalilishaji wa kiongozi huyo wa nchi na kamwe CCM haitavumilia jambo hilo.
Hayo yalisemwa jana na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa chama hicho, John Chiligati, alipokuwa akitoa tamko la CCM kuhusu hali ya kisiasa na kiusalama nchini kwa waandishi wa habari Dar es Salaam.
Chiligati alisema taarifa hizo za baadhi ya wanasiasa zinasambaza hofu, woga na wasiwasi mkubwa si kwa wananchi tu, bali hata kwa wawekezaji wenye nia njema ya kuwekeza na ambao tayari wapo nchini.
CCM inasema nchi ipo salama na haijayumba kama wasemavyo hao wapinzani na mali za wananchi na wawekezaji zipo salama hivyo kauli hizo ni za watu walioishiwa sera, alisema Chiligati.
Alisema viongozi hao wamekuwa wakitumia matukio na matatizo yanayolikabili taifa hivi sasa kama vile mgomo wa walimu, wastaafu wa iliyokuwa Jumuiya ya Afrika Mashariki, mafisadi wa EPA na Mwafaka wa CUF na CCM kwamba ndiyo ajenda kila wanapopanda majukwaani au kuzungumza katika mikutano na kusahau kwamba serikali imekwishasema inayafanyia kazi.
Alisema CCM inatambua kuwa changamoto hizo zipo, lakini masuala yote yanashughulikiwa kwa wazi na kila mtu anafahamu hilo na kusema kwa mfano suala la EPA mbona hata Novemba mosi haijafika watu wanaanza kusema, wasubiri waone ndipo waseme, maana Rais alishasema yote wanayoyasema bungeni Agosti mwaka huu.
Kuhusu madai ya walimu, aliiomba kamati ya pamoja ya kushughulikia madai hayo iliyoundwa kufanya kazi kwa haraka usiku na mchana ili uhakiki ukamilike na walimu walipwe mapema kwani ni haki yao.
Kuhusu mwafaka kati yao na CUF, Chiligati aliwataka CUF kurudi katika meza ya mazungumzo na kukanusha taarifa za chama hicho kwamba mwafaka tayari, akisema kilichokuwa tayari ni mapendekezo ambayo yamerekebishwa na vyama husika ili yajadiliwe tena na Kamati ya Mwafaka.
Kuhusu habari zilizoandikwa na gazeti moja la kila siku juzi zikimnukuu Mbowe kuhusu kumdhalilisha Rais Kikwete kwamba Watanzania walikosema kumchagua kuwa Rais kwa kuwa hana uwezo na ameshindwa kuongoza nchi, Chiligati alisema kauli hiyo ni ya uchochezi na anapaswa kuomba radhi.
Alisema maneno hayo hayana heshima hasa ikizingatiwa kuwa Kikwete ni Rais wa nchi aliyeshinda kwa kura asilimia 80 mwaka 2005, jambo lililoonyesha kuwa Watanzania wanamfahamu na wana imani naye ndiyo sababu wakamchagua.
Mbowe ni nani kwanza mpaka amchafue Rais kiasi hiki, amepata wapi ujasiri wa kusema haya? Hana sifa yoyote hapa nchini. Historia na sifa zinaonyesha kwamba ni mchezeshaji disko na kamari katika majumba ya starehe anayomiliki na si chochote wala lolote, alidai Chiligati.
Alisema kila raia kwa mujibu wa Katiba ya nchi, ana haki ya kuzungumza na kumkosoa Rais, lakini si katika hali ya udhalilishaji, kejeli au dharau na kwamba CCM inatoa onyo kali ikimtaka Mbowe achunge mdomo wake kwa kauli zake na heshima yake. Alisema demokrasia ya kweli inahitaji heshima na uungwana na endapo ataendeleza kashfa dhidi ya Rais, hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yake na kwa mwanasiasa ye yote atakayefanya hivyo.
My Take:
Hivi demokrasia lazima iwe na heshima na uungwana?
Daily News; Saturday,October 25, 2008 @00:02
Chama Cha Mapinduzi (CCM), kimesema nchi haijachafuka wala kuyumba kama wanavyosema baadhi ya viongozi wa vyama vya siasa na kuwataka Watanzania wapuuze kauli hizo zenye kila dalili ya uchochezi.
Aidha, CCM imemtaka Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe, kuacha mara moja tabia ya kumsema vibaya Rais Jakaya Kikwete kwa kile kilichodai kuwa ni udhalilishaji wa kiongozi huyo wa nchi na kamwe CCM haitavumilia jambo hilo.
Hayo yalisemwa jana na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa chama hicho, John Chiligati, alipokuwa akitoa tamko la CCM kuhusu hali ya kisiasa na kiusalama nchini kwa waandishi wa habari Dar es Salaam.
Chiligati alisema taarifa hizo za baadhi ya wanasiasa zinasambaza hofu, woga na wasiwasi mkubwa si kwa wananchi tu, bali hata kwa wawekezaji wenye nia njema ya kuwekeza na ambao tayari wapo nchini.
CCM inasema nchi ipo salama na haijayumba kama wasemavyo hao wapinzani na mali za wananchi na wawekezaji zipo salama hivyo kauli hizo ni za watu walioishiwa sera, alisema Chiligati.
Alisema viongozi hao wamekuwa wakitumia matukio na matatizo yanayolikabili taifa hivi sasa kama vile mgomo wa walimu, wastaafu wa iliyokuwa Jumuiya ya Afrika Mashariki, mafisadi wa EPA na Mwafaka wa CUF na CCM kwamba ndiyo ajenda kila wanapopanda majukwaani au kuzungumza katika mikutano na kusahau kwamba serikali imekwishasema inayafanyia kazi.
Alisema CCM inatambua kuwa changamoto hizo zipo, lakini masuala yote yanashughulikiwa kwa wazi na kila mtu anafahamu hilo na kusema kwa mfano suala la EPA mbona hata Novemba mosi haijafika watu wanaanza kusema, wasubiri waone ndipo waseme, maana Rais alishasema yote wanayoyasema bungeni Agosti mwaka huu.
Kuhusu madai ya walimu, aliiomba kamati ya pamoja ya kushughulikia madai hayo iliyoundwa kufanya kazi kwa haraka usiku na mchana ili uhakiki ukamilike na walimu walipwe mapema kwani ni haki yao.
Kuhusu mwafaka kati yao na CUF, Chiligati aliwataka CUF kurudi katika meza ya mazungumzo na kukanusha taarifa za chama hicho kwamba mwafaka tayari, akisema kilichokuwa tayari ni mapendekezo ambayo yamerekebishwa na vyama husika ili yajadiliwe tena na Kamati ya Mwafaka.
Kuhusu habari zilizoandikwa na gazeti moja la kila siku juzi zikimnukuu Mbowe kuhusu kumdhalilisha Rais Kikwete kwamba Watanzania walikosema kumchagua kuwa Rais kwa kuwa hana uwezo na ameshindwa kuongoza nchi, Chiligati alisema kauli hiyo ni ya uchochezi na anapaswa kuomba radhi.
Alisema maneno hayo hayana heshima hasa ikizingatiwa kuwa Kikwete ni Rais wa nchi aliyeshinda kwa kura asilimia 80 mwaka 2005, jambo lililoonyesha kuwa Watanzania wanamfahamu na wana imani naye ndiyo sababu wakamchagua.
Mbowe ni nani kwanza mpaka amchafue Rais kiasi hiki, amepata wapi ujasiri wa kusema haya? Hana sifa yoyote hapa nchini. Historia na sifa zinaonyesha kwamba ni mchezeshaji disko na kamari katika majumba ya starehe anayomiliki na si chochote wala lolote, alidai Chiligati.
Alisema kila raia kwa mujibu wa Katiba ya nchi, ana haki ya kuzungumza na kumkosoa Rais, lakini si katika hali ya udhalilishaji, kejeli au dharau na kwamba CCM inatoa onyo kali ikimtaka Mbowe achunge mdomo wake kwa kauli zake na heshima yake. Alisema demokrasia ya kweli inahitaji heshima na uungwana na endapo ataendeleza kashfa dhidi ya Rais, hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yake na kwa mwanasiasa ye yote atakayefanya hivyo.
My Take:
Hivi demokrasia lazima iwe na heshima na uungwana?