Mkwawa
JF-Expert Member
- Jun 8, 2011
- 1,334
- 1,464
Baada ya kutafakari kwa kina, nimegundua kuwa kamati nyingi zinazoundwa ama na bunge au serikali aua na chombo chochote kile cha serikali ni kwa ajili ya kula fedha za wananchi tu bure. Hata kama za kudumu za bunge zote ni hadaa na zinakula fedha zetu bure kabisa bila kazi yeyote.
Kamati hizi za bunge zote zinatuhumiwa ama baadhi au kamati nzima kula rushwa kabla ya kutenda kazi, haiingii akili unayemchunguza anakupa usafiri, malazi, chakula na wakati mwingine posho. hizi kamati sio huru wala hazina tija kwa watanzania.
Ukijaribu kuangalia maddudu ya Tanesco ziko kamati nyingi sana zimeyafanya na zinaendelea kuyafanya ila wanatuona WaTZ wote vilaza ndio maanaa wanatuimbia ngonjera kila siku nasi tunakubali.
Tuanze na tuhuma hizi za wabunge wa hii kamati kula rushwa. Kwa sababu wana JF wako kila mahali na ndani ya wizara ya nishati na madini na wanaishi na hawa wabunge ama kufanya nao kazi au kufanya biashara zao. Naomba kwa mara ya kwanza wanaJF mfanye kazi kubwa sana ya uchunguzi bila kumpendelea mtu au chuki.
Rushwa ziko za mfumo na njia nyingi naomba tuchunguze rushwa za namna zote kwa wanakamati hawa.
1. Rushwa ya fedha
2.Rushwa ya kuapatiwa biashara na wizara ya nishati na madini moja kwa moja au kwa njia za panya
3. Rushwa ya kazi kwa ndugu , watoto na jamaa
4. Rushwa ya ngono
5. Rushwa ya kusaidia cheo au debe
6. Rushwa ya chakula malazi na usafiri
8. Rushwa ya ada au kozi mbali za shule.
9. Rushwa ya udhamini wa wizara au miradi ya maendeleo isiyokuwepo kwenye bajeti
10. Rushwa ya nguo kama suti, viatu, manukato, safari za nje na mikutano
11. Rushwa ya posho
Kila mbunge aliyekuwepo kwenye ile kamati iliyovunjwa tumchekeche mpaka tujue ukweli.
Pili Kamati ya Ngwilizi na yenyewe tuichunguze kama imekula rushwa ya kuchunguza kiini macho ili kuficha ukweli.
Chief Mkwawa wa kalenga
Polisi mzuri ni mwananchi mlinda nchi ni mwananchi msema kweli ni muathirika wa uchumi huu wa TZ . Huu ndio muda tuikomboe nchi yetu
Kamati hizi za bunge zote zinatuhumiwa ama baadhi au kamati nzima kula rushwa kabla ya kutenda kazi, haiingii akili unayemchunguza anakupa usafiri, malazi, chakula na wakati mwingine posho. hizi kamati sio huru wala hazina tija kwa watanzania.
Ukijaribu kuangalia maddudu ya Tanesco ziko kamati nyingi sana zimeyafanya na zinaendelea kuyafanya ila wanatuona WaTZ wote vilaza ndio maanaa wanatuimbia ngonjera kila siku nasi tunakubali.
Tuanze na tuhuma hizi za wabunge wa hii kamati kula rushwa. Kwa sababu wana JF wako kila mahali na ndani ya wizara ya nishati na madini na wanaishi na hawa wabunge ama kufanya nao kazi au kufanya biashara zao. Naomba kwa mara ya kwanza wanaJF mfanye kazi kubwa sana ya uchunguzi bila kumpendelea mtu au chuki.
Rushwa ziko za mfumo na njia nyingi naomba tuchunguze rushwa za namna zote kwa wanakamati hawa.
1. Rushwa ya fedha
2.Rushwa ya kuapatiwa biashara na wizara ya nishati na madini moja kwa moja au kwa njia za panya
3. Rushwa ya kazi kwa ndugu , watoto na jamaa
4. Rushwa ya ngono
5. Rushwa ya kusaidia cheo au debe
6. Rushwa ya chakula malazi na usafiri
8. Rushwa ya ada au kozi mbali za shule.
9. Rushwa ya udhamini wa wizara au miradi ya maendeleo isiyokuwepo kwenye bajeti
10. Rushwa ya nguo kama suti, viatu, manukato, safari za nje na mikutano
11. Rushwa ya posho
Kila mbunge aliyekuwepo kwenye ile kamati iliyovunjwa tumchekeche mpaka tujue ukweli.
Pili Kamati ya Ngwilizi na yenyewe tuichunguze kama imekula rushwa ya kuchunguza kiini macho ili kuficha ukweli.
Chief Mkwawa wa kalenga
Polisi mzuri ni mwananchi mlinda nchi ni mwananchi msema kweli ni muathirika wa uchumi huu wa TZ . Huu ndio muda tuikomboe nchi yetu