Nataka nitoke na wewe leo

Equation x

JF-Expert Member
Sep 3, 2017
29,421
40,410

Ukitembea na pisi kali warembo wengine watakuwa wanajitongozesha wao wenyewe.

Jumamosi iliyopita, nilipata mwaliko kutoka kwa mpenzi wangu (mchepuko) tukutane katika kiwanja fulani, angalau tuweze kubadilishana mawazo.

Ilipofika saa nne usiku, ikabidi nifike eneo husika na bahati nzuri nayeye alikuwa ameshafika.

Mnavyojua tena wadada wa mjini; alikuwa amevaa mavazi ya ushawishi sana, gauni fupi sana, ukichangia na unene wake, urefu pamoja na rangi; lazima jogoo awe anasumbua sumbua kutaka kutoka nje.

Tumepiga vyombo vyetu (tungi) pale na nyama choma kidogo, huku tukiendelea kuburudika na mziki, mara napokea ujumbe kwenye simu kwa namba mpya ''njoo kaunta basi baby''. Nikamuuliza kwa ujumbe, ''wewe ni nani'', hakujibu swali zaidi ya kusisitiza niende kaunta tu.

Ikabidi ninyanyuke na kujifanya naenda 'toilet', lakini lengo ni kwenda kaunta. Ile nafika kaunta tu, nakutana na pisi kali iliyojiremba hatari, kwa bahati nzuri sura yake ilikuwa sio ngeni sana machoni mwangu.

Kutokana na ulevi, nikamwambia, ''baby nimeitikia wito wako niambie'', akaniambia, ''mume wangu, nataka nitoke na wewe leo, hapa nimechoka tuondoke wote''.

Nikahisi kuchanganikiwa, nikiangalia kule mezani, mrembo ananisubiri, na huyu mwingine anataka atoke na mimi, hapa nafanyaje.

Ikabidi nimpe jibu la kumridhisha, ''subiri nimalizane na mpenzi wangu pale tutaondoka wote''. Akaitikia kwa furaha, ''sawa, muhudumu atawalete vinywaji kwa bili yangu''.

Nimerudi pale mezani, tukawa tunaendelea na mazungumzo yetu; mara vinywaji vinakuja, mrembo wangu akamuuliza muhudumu, vimetoka wapi? Akajibiwa, ''kuna dada amependa 'vibe' letu akaamua kutupa ofa''.

Ile nimetulia, mara ujumbe ukaingia kwenye simu, ''baby twende mimi nina hamu kwa sasa''. Nikajikuta mawazo yangu yanahama, na kumuwaza yule mrembo pale kaunta namna nitakavyokwenda kumgaragaza.

Ikabidi nimwambie mchepuko wangu,''mimi sijisikii vizuri, naona kwa leo vinywaji vimenichosha, tutaendeleza kesho, nomba niende home nikapumzike kwanza.'' Akajibu, ''sawa haina shida, tumalizie hivi vinywaji tuondoke''.

Nikajitahidi ili niwe wa kwanza kumaliza; baada ya kumaliza nikamuomba mimi nitangulie, bahati nzuri akaniruhusu.

Nikajipitisha pale kaunta, na kumpa ishara yule mrembo tuondoke, naye akanipa ishara nitangulie nimsubiri kwa nje, kwa sababu tungetoka wote picha ingeharibika.

Nimefika kwa nje, kama baada ya dakika 3 hivi; mrembo huyu hapa. Ikabidi niondoke naye.

Kufika eneo la tukio, ikawa ni kazi ya kuchochea kuni tu; ila makelele yalikuwa mengi sana nikahisi labda anaigiza tu.

Mara ananiambia ''baby usiniache nataka uwe mpenzi wangu wa kudumu''. Nikamuuluiza, ''na yule uliyeniona naye nimuachie nani?''

Akanijibu, ''sisi wanawake tuko wengi na wanaume rijali wamepungua naomba tuwe wote, ata ukitupa zamu haina shida''

Nikamjibu, ''haina shida, maisha ni haya haya, kutesana kihisia haina maana najali hisia zako''. Mara akanikumbatia kwa nguvu akaja juu, kwa mhemko hatari.

Kwa ujumla nilifaidi sana, kweli alikuwa anataka atoke na mimi.​
 
Ila kuna watu mna uthubutu. Mtu hujawahi kuwasiliana naye, sawa hata kama sura si ngeni. Humjui, anakuambia twende nawe ka zuzu umo. Ukaletewa na kinywaji, nawe umo tu.
Hujiulizi pale kakujaje?

Mnaenda kunyanduana, wala hata huogopi. Hushtuki. Huna kinyaa Mkuu? Na pombe hizo, nadhani hata kondom hukukumbuka.

Aisee!.
 
Ila kuna watu mna uthubutu. Mtu hujawahi kuwasiliana naye, sawa hata kama sura si ngeni. Humjui, anakuambia twende nawe ka zuzu umo. Ukaletewa na kinywaji, nawe umo tu.
Hujiulizi pale kakujaje?

Mnaenda kunyanduana, wala hata huogopi. Hushtuki. Huna kinyaa Mkuu? Na pombe hizo, nadhani hata kondom hukukumbuka.

Aisee!.
Zana ni muhimu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom