Nataka biashara itakayonisomesha.

Black African

Member
Oct 17, 2011
24
3
Habari za leo imani yangu muwazima wa afya,nami namshukuru mungu naendelea vizuri.Naomba maoni yenu,me ni mwanafunzi kidato cha 5 ktk shule moja ya serekali hapa mjini znz,tangu nimefaulu nimekuwa nikajitegemea kwa gharama zote za kusoma pmj na matumizi madogomadogo,nimejipigapiga kutafuta kiasi cha pesa ili uwe ndio mtaji,hadi sasa nimefanikiwa kupata Tsh.100,000 nataka nifanye biashari ila sijuini biashara gani itaniendesha bila ya kuathiri masomo yangu.Ahsanteni
 
haipo biashara ya hivyo, sahau...


Acha kujibu majibu negative.., nyie ndo mnakatisha watu tamaa. Kwa nini umjibu mtu hivyo!! SIPENDI MIMI WATU KAMA NYIE! SIPENDI!!!

"...even a fool is considered wise when he keeps silence"
 
Jaribu kufanya utafiti wa matumizi ya mkaa mitaa unayoishi. Unaweza wakati wa weekend unaenda kununua gunia za mkaa sehemu unapouzwa kwa bei nafuu unakuja uza mtaani kwenu kwa jumla maana rejareja na wewe unasoma itakuwa shida labda uwe na msaidizi.
 
Tafuta eneo lenye mzunguko mkubwa wa watu mfano sokoni..vyuoni.. n.k.. tafitaia mahitaji yao ya vocha... jipenyeze hapo...zungusha mtaji wako..

Namfahamu jamaa alianza na kulisha ng'ombe wa mtu.... akaajiriwa katika kibda cha chipsi.. akajikusanya akachukua benchi akaliweka stendi ya daladala chuo kikuu UDSM akauza vocha kwa wanafunzi wa chuo(2000,1000,500,250..)... kafanikiwa akanunua pikipiki yake mwenyewe akamwachia mdogo wake kijiwe.. akashika hela akanza kula ngamia... sijui alipo hivi sasa lakini walau unapata picha watu walipoanzia...!Penye nia pana njia...

Ukikuza mtaji wako rudisha mrejesho humu upewe mawazo mapana zaidi..!
 
Nawashukuru wana JF ambao mmekuwa mstari wa mbele kumshauri huyu mdau. Ndg yangu Black African ushauri umepewa. Kimsingi mtaji ulionao unatosha kuanzisha biashara ya kiwango cha fedha hiyo 100,000/=. Pia soko kwa ajili ya biashara unayotakiwa kuanzisha liko ama katika eneo unaloishi au unakosomea kwani wadau wake ndo wanaotakiwa kuwa wateja wako. Mimi ninakupa ushauri huu:-
1. Nunua mifuko ya maji/barafu pakiti moja Sh. 1,000/= ambayo ina pcs 100 anafunga maji na kuyapoza kidogo kwenye fridge kisha kuyauza @ mfuko Sh. 50/=. Hapa una uhakika ya kupata gross income ya Sh. 5,000/= . Kazi ya kufunga maji ni nyepesi, haitumii muda mwingi na unaweza kuifanya kulingana na muda wako hata kama ni usiku, kama nyumbani kuna friji unaweka maji yako huko au ukatumia deli. Biashara hii unaweza kuwa unamwachia mtu ama mwenye duka au genge kwa makubaliano ua kumpa Commission. Itakulipa ndg yangu kwa ushauri zaidi tuwasiliane
2. Anzisha genge dogo kulingana na fedha uliyonayo. Biashara hii inahitaji uwe na msaidizi wakati unapokuwa shuleni au unapokuwa umetingwa na masomo. Pale unapokuwa na muda nawe simamia uongeze nguvu. Chagua vitu vidogo vidogo vinavyotumika sana kila siku majumbani mfano mkaa, vitunguu, mafuta ya kupima, pipi, n.k. Hapa unaweza kuuza vocha pia.
3. Fanye biashara ya kuuza vocha kwani zinabebeka na unaweza kuifanyia popote. Muhimu ni wateja wako kufahamu kwamba wewe ni muuza vocha.
Biashara hizi zote ukipata watu wa kushirikiana nao katika kununua mzigo itakupunguzia gharama mbalimbali na kuokoa muda wako. Pia kama unaweza kupata wateja maalum wa kuwauzia bidhaa hizi na nyinginezo kutaokoa muda wako na itakusaidia kukokotoa faida kwa wepesi ikiwa ni pamoja na kujifunza juu ya ukuaji wa biashara ya soko lako.
Mi niishie hapo. Ila nawaomba wana JF wengine muendelee kumpa ushauri huyu mwenzetu. Asante sana
 
I wish you all the best, kwani wadau wengi wamekupa mawazo mazuri mahali pa kuanzia biashara ni imani uliyonayo wewe moyoni kwako. Jitahidi penye nia pana njia
 
Tafuta eneo lenye mzunguko mkubwa wa watu mfano sokoni..vyuoni.. n.k.. tafitaia mahitaji yao ya vocha... jipenyeze hapo...zungusha mtaji wako..

Namfahamu jamaa alianza na kulisha ng'ombe wa mtu.... akaajiriwa katika kibda cha chipsi.. akajikusanya akachukua benchi akaliweka stendi ya daladala chuo kikuu UDSM akauza vocha kwa wanafunzi wa chuo(2000,1000,500,250..)... kafanikiwa akanunua pikipiki yake mwenyewe akamwachia mdogo wake kijiwe.. akashika hela akanza kula ngamia... sijui alipo hivi sasa lakini walau unapata picha watu walipoanzia...!Penye nia pana njia...

Ukikuza mtaji wako rudisha mrejesho humu upewe mawazo mapana zaidi..!



Nawashukuru wana JF ambao mmekuwa mstari wa mbele kumshauri huyu mdau. Ndg yangu Black African ushauri umepewa. Kimsingi mtaji ulionao unatosha kuanzisha biashara ya kiwango cha fedha hiyo 100,000/=. Pia soko kwa ajili ya biashara unayotakiwa kuanzisha liko ama katika eneo unaloishi au unakosomea kwani wadau wake ndo wanaotakiwa kuwa wateja wako. Mimi ninakupa ushauri huu:-
1. Nunua mifuko ya maji/barafu pakiti moja Sh. 1,000/= ambayo ina pcs 100 anafunga maji na kuyapoza kidogo kwenye fridge kisha kuyauza @ mfuko Sh. 50/=. Hapa una uhakika ya kupata gross income ya Sh. 5,000/= . Kazi ya kufunga maji ni nyepesi, haitumii muda mwingi na unaweza kuifanya kulingana na muda wako hata kama ni usiku, kama nyumbani kuna friji unaweka maji yako huko au ukatumia deli. Biashara hii unaweza kuwa unamwachia mtu ama mwenye duka au genge kwa makubaliano ua kumpa Commission. Itakulipa ndg yangu kwa ushauri zaidi tuwasiliane
2. Anzisha genge dogo kulingana na fedha uliyonayo. Biashara hii inahitaji uwe na msaidizi wakati unapokuwa shuleni au unapokuwa umetingwa na masomo. Pale unapokuwa na muda nawe simamia uongeze nguvu. Chagua vitu vidogo vidogo vinavyotumika sana kila siku majumbani mfano mkaa, vitunguu, mafuta ya kupima, pipi, n.k. Hapa unaweza kuuza vocha pia.
3. Fanye biashara ya kuuza vocha kwani zinabebeka na unaweza kuifanyia popote. Muhimu ni wateja wako kufahamu kwamba wewe ni muuza vocha.
Biashara hizi zote ukipata watu wa kushirikiana nao katika kununua mzigo itakupunguzia gharama mbalimbali na kuokoa muda wako. Pia kama unaweza kupata wateja maalum wa kuwauzia bidhaa hizi na nyinginezo kutaokoa muda wako na itakusaidia kukokotoa faida kwa wepesi ikiwa ni pamoja na kujifunza juu ya ukuaji wa biashara ya soko lako.
Mi niishie hapo. Ila nawaomba wana JF wengine muendelee kumpa ushauri huyu mwenzetu. Asante sana


Inawezekana mawazo yenu yakawa sahihi, ila muuliza swali anataka biashara ambayo haitaathiri masomo yake. Yaani ambayo you will earn higher for just few hours
 
Habari za leo imani yangu muwazima wa afya,nami namshukuru mungu naendelea vizuri.Naomba maoni yenu,me ni mwanafunzi kidato cha 5 ktk shule moja ya serekali hapa mjini znz,tangu nimefaulu nimekuwa nikajitegemea kwa gharama zote za kusoma pmj na matumizi madogomadogo,nimejipigapiga kutafuta kiasi cha pesa ili uwe ndio mtaji,hadi sasa nimefanikiwa kupata Tsh.100,000 nataka nifanye biashari ila sijuini biashara gani itaniendesha bila ya kuathiri masomo yangu.Ahsanteni

Habari nzuri.
Kama haya uliyoyasema yana ukweli 100% Nimejitolea kukugharamia kidato cha 6 au kukuongezea mtaji ufanye biashara itakayohusisha mtaji mkubwa zaidi , mara baada ya kuhakikisha mimi binafsi kwa kina hayo uliyoyasema ni ya kweli. Nitaamua moja ktk hayo niliyosema.

Kama huna kipingamizi tuwasiliane. Shule njema..Soma kwa bidii kama unasomea kijiji vile.
Arkad arkad690@yahoo.co.uk
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom