Napendekeza kazi za kuhesabu idadi ya watu (Sensa 2022) ifanywe na wajumbe wa nyumba 10 , pesa zitakazookolewa zikajenge flyover TAZARA

FRANCIS DA DON

JF-Expert Member
Sep 4, 2013
36,079
40,733
Kwa kupitia serikali za mitaa / vijiji (local government) , wajumbe wa nyumba 10 wapewe fomu za sensa na wapite kwenye nyumba zilizochini yao, wapewe wiki moja tu wawe wameshazitembelea nyumba zote zilizochini yao na kuzijaza fomu zote kwa kila nyumba, wakazikabidhi fomu hizo kwenye ofisi za serikali ya mtaa/kijiji, ofcourse wapewe na posho kidogo.

Afisa mtendaji akusanye zote na kuziwasilisha ofisi ya wilaya/mkoa ya sensa kwa ajili ya majumuisho na uchakataji wa taarifa.

Pesa zitakazookolewa ziende zikajenge flyover pale TAZARA, foleni ya malorry pale imesababisha hali kuwa mbaya sana.

=================================
By @ Maulaga59

Najaribu kuangalia changamoto wanazopata maafisa wa sensa wanaotumwa na serikali katika kukusanya taarifa muhimu za idadi ya watanzania.

Ukweli ni kwamba kwa sababu ya mazingira ya Tanzania yalivyo kijiografia ni vigumu sana hawa maafisa kuweza kupata takwimu sahihi za kusudio lao. Kuna sehemu ambazo huwa siyo rahisi kufika kwa gai au kwa mguu kwa sababu mbalimbali kama vile mapori, mabonde, milima, wanyama wakali na kadhalika.

Wenyeji wa maeneo hayo wao wanao uzoefu hata wa kufika makao makuu ya wilaya lakini si kwa wageni na muda mfupi wanaokuwa wamepewa kufanikisha zoezi.

Balozi wa nyumba kumi wangepewa semina za kufanya zoezi hilo wangeweza kuja na takwimu sahihi zaidi kuliko zile za maafisa waliotumwa.

Kila balozi angeweza kupeleka takwimu za watu wake kwenye ofisi ya kata na ofisi ya kata ingeratibu zoezi hilo katika eneo lake, kisha kupeleka ngazi za juu hadi ngazi ya taifa.

Zoezi hili siyo tu lingeleta takwimu sahihi zaidi bali pia lingepunguza gharama kubwa ambazo serikali hutumia katika kufanikisha zoezi zima.

Kwa huu utaratibu unaotumika kila baada ya miaka 10 watu wengi huwa wanaachwa bila kuhesabiwa hasa kwenye maeneo magumu kijiografia.

Nadhani miaka ijayo kazi hii ifanywe na mabalozi wa nyumba kumi.

Nawasilisha.
==================================
 
Ile mfugale pale sio kitu mkuu ?

Gharama ya ujenzi wa fly over unasimama bei gan mkuu ?
 
Akili mtu wangu akili
Lakini budaa Kuna mtaa flani niliishi, mjumbe wa nyumba 10 hajui kusoma wala kuandika ukienda kufuata barua muhusika ndo unajiandikia,sababu ya ukada wa ccm kindakindaki ndo akapewa huo ujumbe

Vinnie.jpg
 
Pesa ziokolewe kila wilaya, flyover ijengwe tazara? Ningekuunga mkono kama ungesema zisaidie kuboresha huduma za afya
Basi nisameheni nimeteleza, zikatumike kila wilaya kuboresha huduma ya afya 😂😂. Ila foleni za malorry yanayoenda mikoa mbali mbali ikipungua, hata gharama za usafirishaji kwenda mikoa na wilaya husika inapungua.
 
Kuna mtaa flani niliishi, mjumbe wa nyumba 10 hajui kusoma wala kuandika ukienda kufuata barua muhusika ndo unajiandikia,sababu ya ukada wa ccm kindakindaki ndo akapewa huo ujumbe

View attachment 2218857
Mtu asiyejua kusoma wala kuandika hawezi kupewa ujumbe, hii kali sasa. Kama hii ni kweli, afisa mtendaji na mwenyekiti watawajibika kumjazia fomu zake, maana wao ndio walifanya uhuni wa kumpa ujumbe.
 
Kwa kupitia serikali za mitaa / vijiji (local government) , wajumbe wa nyumba 10 wapewe fomu za sensa na wapite kwenye nyumba zilizochini yao, wapewe wiki moja tu wawe wameshazitembelea nyumba zote zilizochini yao na kuzijaza fomu zote kwa kila nyumba, wakazikabidhi fomu hizo kwenye ofisi za serikali ya mtaa/kijiji, ofcourse wapewe na posho kidogo.

Afisa mtendaji akusanye zote na kuziwasilisha ofisi ya wilaya/mkoa ya sensa kwa ajili ya majumuisho na uchakataji wa taarifa.

Pesa zitakazookolewa ziende zikajenge flyover pale TAZARA, foleni ya malorry pale imesababisha hali kuwa mbaya sana.
Wazo lako ni kwa nia njema lakini naamini rahisi ni ghali. Nnavyoelewa sensa hutakiwa kufanywa kwa siku moja tu. Hawa wajumbe zetu wa nyumba kumi (siku hizi, nasikia bwana yule,alizifanya za nyumba 50, siyo 10 tena) watayaweza hayo?


Halafu kwanini zikajenge flyover palepale ambapo lipo halijamaliza hata miaka 10? Au bwana yule aliona ile design iliyotolewa wakati wa Kikwete haifai na yake na engineer wake imebuma?

Rahisi ni ghali.
 
Ziletwe Morogoro wajenge njia nne za kuingia na kutoka morogoro,magari ni mengi haswa maloli yanayolipa kodi nyingi ya mizigo.
 
Kwa kupitia serikali za mitaa / vijiji (local government) , wajumbe wa nyumba 10 wapewe fomu za sensa na wapite kwenye nyumba zilizochini yao, wapewe wiki moja tu wawe wameshazitembelea nyumba zote zilizochini yao na kuzijaza fomu zote kwa kila nyumba, wakazikabidhi fomu hizo kwenye ofisi za serikali ya mtaa/kijiji, ofcourse wapewe na posho kidogo.

Afisa mtendaji akusanye zote na kuziwasilisha ofisi ya wilaya/mkoa ya sensa kwa ajili ya majumuisho na uchakataji wa taarifa.

Pesa zitakazookolewa ziende zikajenge flyover pale TAZARA, foleni ya malorry pale imesababisha hali kuwa mbaya sana.
Yaani hili ni lipwenti of the decade... This is the great thinking we need. Bigup FRANCIS DA DON
 
Gharama yake ikitajwa hapa si mtakimbiana ....maana wa Tz tunapenda kulalamika ila hatupendi kujitoa kafara kwa ajili ya maendeleo yetu.....

Itoshe kusema awali hatukuwa na maono ya mbali, tuliamini ile mfugale ndio siluhu ya foleni,

Wakati inajengwa ile tulipaswa tujitafakari, binafsi naona tuli puyanga


Interchange ya Ubungo iligharimu 200 B roughly, Exclude VAT
 
Wazo lako ni kwa nia njema lakini naamini rahisi ni ghali. Nnavyoelewa sensa hutakiwa kufanywa kwa siku moja tu. Hawa wajumbe zetu wa nyumba kumi (siku hizi, nasikia bwana yule,alizifanya za nyumba 50, siyo 10 tena) watayaweza hayo?


Halafu kwanini zikajenge flyover palepale ambapo lipo halijamaliza hata miaka 10? Au bwana yule aliona ile design iliyotolewa wakati wa Kikwete haifai na yake na engineer wake imebuma?

Rahisi ni ghali.
 
Back
Top Bottom