Jikite kwenye hoja, hata maji Marefu ni Profesa.
Ni mfamasia wa miti shamba nayo ni taaluma
Chama
Gongo la mboto DSM
Jikite kwenye hoja, hata maji Marefu ni Profesa.
Take a cup of coffee and relax, si kila hoja inahitaji propaganda uchwara, kaa pembeni angalia michango ya wenzako unaweza ukaja kuongea la maana.Mkuu betlehem
Kauli ya Nape Nnauye sielewi inakupa shida wapi kwenye uchaguzi wa Kenya 2007 waliaonzisha vurugu ni walioshinda uchaguzi au walioshindwa?
Chama
Gongo la mboto DSM
Nape ndio anawafundisha hao masalia kutukana. Wasidhani watanzania hawana akili!
Back to topic, soma upya thread ili uelewe topic, spin Doctors hawahitajiki hapa.Ni mfamasia wa miti shamba nayo ni taaluma
Chama
Gongo la mboto DSM
Baada ya Jk, wa pili kueneza udini kwa kasi ni Nape Nnauye! Mbaya zaidi yeye ameongezea na ukabila sijui anapata faida gani huyu kijana kuona watanzania wanagawanyika!
Kwa hoja hii, anamanisha hata wakishidwa watatumia jeshi ilikunusuru hali halisi.
Ni ujinga sana kufikiri namna hii.
Back to topic, soma upya thread ili uelewe topic, spin Doctors hawahitajiki hapa.
Take a cup of coffee and relax, si kila hoja inahitaji propaganda uchwara, kaa pembeni angalia michango ya wenzako unaweza ukaja kuongea la maana.
Unasemaje sasa kulingana na tuhuma za Nape, zinawaharibia au zinakijenga zaidi chama???
Kwahiyo hapa tukubaliane Nape si Mtoto wa Musa Nnauye na ndio maana hakuwemo kwenye orodha ya Wanafamilia. Musa Nnauye alikuwa Mwislamu.Vijana wa Chadema mbona mnajichanganya sana kwenye hili la udini? JK muislamu; Nape Nnauye mkristo hivi mnaelewa mnachokiongea au nyie ndio mnaotawaliwa na dhambi ya udini?
Chama
Gongo la mboto DSM
mawazo yakao yako sawa,lakini ccm wameshaamua tuingie kwanye vita kuliko wao kuwa tayari kuachia dola,hivyo maneno ya nape hakuna kiongozi hata mmoja ataona yana hatari,maana hivyo ndivyo wanavyotakaNape alifanya mkutano na wananchi wa Goba (Dar es salaam) tarehe 17/2/2013. Mimi sikuwepo katika mkutano huo lakini nimesikiliza sehemu ya hotuba yake kupitia kipindi cha Chombo Kazini cha Redio Uhuru cha jana saa 8;30 usiku. Katika mazungumzo yake alisema mambo mengi ila mimi nitazungumzia machache tu yaliyonifanya nipate shida kidogo usiku wa jana.
Miongoni mwa mambo aliyosema ; alisema CCM inalinda amani na CHADEMA inavuruga amani. Alipokuwa akifafanua hoja hii, alitoa mfano wa uchaguzi wa Kenya akasema hivi "Mnaona nchini Kenya kwenye uchaguzi wa 2007, Kibaki na Odinga walikuwa na misuguano, Kibaki akaamua kujiepusha Odinga akaingiza watu mitaani na kusababisha mauaji".
Kauli hii imenipa shida sana hata nikajiuliza kama ndugu Nape katumwa kusema haya!, Je! Ndo msimamo wa chama au kaongea tu pengine bila kukusudia!. Mkuu Nape Nnauye; Unatakakuwaambia watanzania vurugu baada ya uchaguzi nchini Kenya zilisababishwa na upinzani? Mheshimiwa Nape unataka utuambie kwamba uchaguzi wa 2015 CCM ina mpango wa kuchukua nafasi ya Kibaki 2007 na CHADEMA wachukue nafasi ya Odinga?
Nape; Unaongea nini! Suala la uchaguzi 2007 nchini Kenya inaonekana wazi kwamba chama tawala kiliwadhulumu wapinzani na hili lipo clear Dunia nzima; Nape, unatoa taswira gani ya chama kwa jamii? Mkuu kwa hili mim[/COLOR]i betlehem umenikatisha tamaa kweli!. Hivi unadhani ni nani atakae endelea kukutetea kwa utaratibu huu; Hakika hata mtu aliepata division four hawezi kusimama na kutetea jambo hili na sasa naanza kupata mashaka kwamba hizidivision "0" 60% zimetokea kwa kukusudiwa ili kupata waungaji mkono wa hoja kama hizi.[/FONT][/SIZE]
Mh.Nape ; wewe umendelea kusema "CHADEMA ni chama cha kibaguzi". Hivi hoja ya kwamba ukisema chadema ni chama cha kibaguzi kwa misingi ya dini na ukabila utawawekea mazingira ya wao nao kusema CCM ni cha kibaguzi hujaielewa tu bado?
Ndugu yangu Nape, huoni unaendelea kuigawanya jamii na kuchochea chuki za kidini na kikabila? Ina maana pamoja na Mzee Mwanakijiji kutukosoa kwa kejeli za wazi katika uzi wake wa PENDEKEZO LA WASTANI: Tusiishie kutengana kwenye kuchinja; tutengane kwa kila kitu... wewe umeamua uwe mtu wa kwanza kutomuelewa! Kweli mkuu!
Ndugu yangu Nape; wewe umewalaumuCHADEMA kwa kutoa namba ya simu ya Spika na hatimae Spika katukanwa: Kulaumu ni sawa maana hata mimi nililaumu, lakini kwa hoja ya kwamba " ijapokuwa kutoa namba ni sahihi lakini mazingira haya kuwa sahihi".Sasa wewe unasema "kwa nini watoe namba ya spika na wasitoe namba za wake zao "
Hivi ndugu yangu Nape; Uko serious kwenye siasa, au unafanya masihara!. Hivi unadhani huu ni mudawa kuendelea kufanya siasa za hila badala ya hoja? ndugu yangu Nape; elewa kwamba wenzetu wa CHADEMA wana vijanawenye akili ambazo ziko fasta zaidi ya google. Wanaweza kutafakari kitu na kukitolea maelezo ya kitaalam ndani ya sekunde. Unadhani kwa siasa za hila tutatoboa?
Mkuu Nape; wewe umekuwa ukitumia maneno yakejeli dhidi ya CHADEMA. Kwa mfano; tarehe16/2/2013 wewe na Lema mlikuwa mnahojiwa na Deustche Welle, wewe ulikuwa unatumia maneno ya kejeli mpaka mtangazaji akakuonya. Sitaki kuyataja maana unayafahamu vyema. Je! huoni kwamba kufanya hivyo unawasukuma hawa wenzetu wa CHADEMA kutukejeli? Ona sasa wanamuita Rais/mwenyekiti wetu eti ni dhaifu! (Tunajidhalilisha watanzania.)
Ndugu yangu Nape; elewa kuwa hakuna mtu yeyote amabaye walau anafikiri hata kidogo atakaye kutetea kwa hoja hizi. Kwa mtindo huu hatuwezi kutoboa 2015. Na sio tu kwamba tutaangushwa bali tutaangushwa kwa aibu kubwa. Hakuna mtu mwenye akili ambaye atakubali aibu hii imkumbe akiwa ndani ya CCM. Tuangalie chama kisije kikafika 2015 kikiwa kimebakina viongozi wa Lumumba pekee huku wafuasi hakuna. Mkuu dawa ya homa kali ni sindano japo inauma. Sasa inapotokea mwana familia anaumwa tumuache afe? hapana; mimi betlehem nita hakikisha anapata sindano za masaa ili aweze kupona japo akilia kwa uchungu mimi itakuwa inaniuma sana!. Pamoja na sindano; Ikitokea akifa kwa sababu ya ukali wa homa, mungu atakuwa kampenda zaidi.
Nape, ikiwa nimekusingizia au hoja zangu si sahihi? Karibu uchangie mada na unikosoe!.
Did he really say that???????!:nono::A S 39::lalala: