Nape Nnauye: Tukosoane kwa hoja na lugha za staha. Kutukanwa kwa mama mmoja ni kutukanwa kwa kina mama wote Tanzania

benzemah

JF-Expert Member
Nov 19, 2014
1,504
3,034
Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknoloji ya Habari, Mhe. Nape Nnauye (Mb) amewataka watanzania kutotumia lugha za matusi kukosoa jitihada mbalimbali zinazofanywa nchini na Rais wa Serikali ya Awamu ya Sita, Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Waziri Nape ameyasema hayo leo Julai 18 Mkoani Dar es Salaam alipokuwa akizungumza Katika Kongamano la Majadiliano ya Ripoti ya Tume ya Haki Jinai lililohudhuriwa na Wataalamu, Viongozi Wastaafu, Watumishi wa Serikali na Wanafunzi.

Nape amesema kuwa Rais Samia alipowaapisha Viongozi wa Wizara ya Mipango na Uwekezaji amewataka Viongozi hao wawasikilize wakosoaji wote na ikiwezekana wawajumuishe kwenye michakato mbalimbali ya kuboresha mambo mbalimbali katika nchi yetu na kusema kuwa kitendo cha baadhi ya wananchi wakiwemo wanasiasa kutumia lugha zisizofaa wanapotoa maoni yao sio sawa.

“Tukosoane, turekebishe, tutoe maoni bila ya kutukanana. Baba wa Taifa Mwalimu Nyerer alitufundisha tukosoane kwa hoja bila ya kutukanana. Kosoeni, toeni maoni, msidhalilishane na wala msitukanane na hasa inapokuwa ni Rais wa Nchi yetu mana yeye ni sura yetu sote”. Amesema Nape

“Kutukanwa kwa Mama ni kosa na hata kama hajakuzaa moja kwa moja unapomtukana basi ni sawa na kutukanwa kwa wazaza wote, tunao wajibu wa kuwaadhibu wote wanaotukana wazazi wa Nchi hii, kwani wazazi hawa wametulea, wametutunza, wametufikisha hapa tulipo salama na tusisahau kuwa utamaduni wa nchi yetu ni kuheshimiana” Ameongeza Waziri Nape.

Waziri Nape pia amempongeza Rais Samia kwa nia yake ya dhati kutaka kuona haki ikitendeka nchini na kusema kuwa mageuzi anayofanya katika kuboresha na kukusanya maoni ya watanzania kuhusu maboresho ya taasisi zinatoa haki nchini.

“Tunaposhuhulika na Haki Jinai, moyo wa Rais unataka haki. Haki italiinua Taifa letu,” amesema Nape.

 
TUSHINDANE KWA HOJA BILA KUPIGANA

Waziri wa Habari Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Nape Nnauye amewasihi Wananchi kutumia maneno ya staha pale wanapowasilisha hoja zao au kukosoa.

Waziri Nape ameyasema hayo mkoani Dar es Salaam alipokuwa akizungumza katika Kongamano la majadiliano ya Ripoti ya Tume ya Haki Jinai lililohudhuriwa na Wataalamu, Viongozi Wastaafu, Watumishi wa Serikali na Wanafunzi.

Amesisitiza utamaduni wa Taifa la Tanzania ni kuheshimiana huku akitaka kukosoa kufanyike na maoni yatolewe bila ya kutoa lugha za matusi.

Waziri Nape amekumbusha maneno ya Baba wa Taifa Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere
kuwa watu washindane kwa hoja bila ya kupigana.

Pia amekumbusha kuwa mijadala ya Haki Jinai inapoendelea Watanzania wakumbuke kuwa Moyo wa Rais Samia Suluhu Hassan unataka Haki hivyo msingi wa yote ni watu watendewe haki.

Aidha, Waziri huyo wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari amesema tayari amezielekeza taasisi zilizo chini ya wizara yake kuandaa majukwaa mbalimbali kwa ajili ya kujadili na kuchambua mapendekezo hayo ya Tume ya Hali Jinai kwa lengo la kupata maoni ya Wananchi ili ubora upatikane.

 
Kauli ya Nape iliyosukumwa na usisiemu wake pamoja na cheo alicho nacho iko too general it seems like huyo mama anashabikiwa na kila mtu wakati si kweli na mama Samia anajua kwa nchi yetu inayofuata mfumo wa hawezi pendwa na kila mtu.

Acheni kumpa mh Rais kiwewe kwa kukuza mambo kwa sababu ya vikali vya kisiasa vya wapinzani wake ambao kumkosoa ndio wajibu wao wa msingi .
 
Sawa....

Hoja kuu zinazohitaji majibu ni hizi hapa

1.) Tofauti ya ‘Makubaliano’ na ‘Mkataba’ ni ipi hasa kiasi mseme ule sio mkataba, kwamba ni makubaliano tu ya awali, na je Mkataba huo (makubaliano hayo) ni wa miaka mingapi? (UKOMO)

2.) Ni kwa faida ya nani kwamba DPW anapewa haki ya bandari zote za Tanganyika, kwamba hakuna mwekezaji mwingine yeyote anaweza kuja kufanya uwekezaji kwenye bandari za Tanganyika bila udalali wa DPW, je, ukiritimba huu ni kwa faida ya nani?

3.) Ni kwa faida ya nani, DPW apewe haki ya kudai kipande chochote cha ardhi yenye ukubwa wowote anaoutaka yeye ndani ya ‘Territory’ ya Tanganyika na sisi tumpe ardhi hiyo kwa kuondoa watu na miradi yote ndani ya eneo alilolitaka, na tumpatie bire kabisa kwa gharama zetu sisi, hata fidia tulipe sisi ili kuondoa watu kumpisha, huu uwendawazimu ni kwa faida ya nani?

4.) Ni kwa faida ya nani, kwamba sisi tuliowekeza matrillion ya mikopo kuendeleza bandari na tukiwa kama wamiliki wa rasimali ya bandari, tupate 0% ya faida itakayotokana na uendeshaji wa huduma za kibandari, yaani ni kana kwamba yeye kawekeza 100% na hivyo achukue 100%? Uwendawazimu huu ni kwa faida ya nani?

5.) Ni kwa faida ya nani, kwamba mkataba unahusisha bandari za Tanganyika tu na sio za Zanzibar, ilihali bandari ni suala la Muungano? Je, Zanzibar haitaki kunufaika au yenyewe haitaki matunda ya mkataba huu? Ukizingatia walioongia huu mkataba wote ni waZanzibari, kuanzia Samiah Suluhu Hassan, Makame Mbarawah, Hamza Johari na wenzao, kwamba hawataki Zanzibar yao ipate matunda mazuri ya mkataba huu?!

6.) Ni kwa faida ya nani kusema kwamba, hata DPW akavunja mkataba na kukiuka kanuni na taratibu zote zinazotambulika kimataifa, bado hatutaweza kuvunja , kuusema vibaya au kujitoa kwenye mkataba, milele! Uwendawazimu huu ni kwa faida ya nani?

7.) Ni kwa faida ya nani kwamba pamoja na kuwa DPW watachukua 100% ya faida, bado tena faida hiyo watapewa Msamaha wa kodi kwa 100%, yaani hata hicho wanachovuna nacho hatuchukui kodi, na wakti huo huo tunakamuliwa kodi za miamala, uwendawazimu huu ni kwa faida ya nani?
 
Kauli ya Nape iliyosukumwa na usisiemu wake pamoja na cheo alicho nacho iko too general it seems like huyo mama anashabikiwa na kila mtu wakati si kweli na mama Samia anajua kwa nchi yetu inayofuata mfumo wa hawezi pendwa na kila mtu .Acheni kumpa mh Rais kiwewe kwa kukuza mambo kwa sababu ya vikali vya kisiasa vya wapinzani wake ambao kumkosoa ndio wajibu wao wa msingi .
Hakuna tatizo lolote kumkosoa Mama, ila lugha iwe ya staha Heshima kitu cha bure! Kwanini Rais Samia, japo sio lazima apendwe na wote lakini ni lazima aheshimiwe na wote? Akosolewe kwa staha na asitukanwe!
P
 
Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknoloji ya Habari, Mhe. Nape Nnauye (Mb) amewataka watanzania kutotumia lugha za matusi kukosoa jitihada mbalimbali zinazofanywa nchini na Rais wa Serikali ya Awamu ya Sita, Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Waziri Nape ameyasema hayo leo Julai 18 Mkoani Dar es Salaam alipokuwa akizungumza Katika Kongamano la Majadiliano ya Ripoti ya Tume ya Haki Jinai lililohudhuriwa na Wataalamu, Viongozi Wastaafu, Watumishi wa Serikali na
Mtaachaje kutukanwa kama nyie mna tumia polisi kutunyamazisha tusiseme? Hovyoo division four..
Ulipo mwita Magu mshamba halikuwa tusi kwa Rais wakati ule?
Nape huna hoja best.
 
Ni kweli Matusi yamekuwa mengi sana mitandaoni FB Twtt na kwingineko

Na hii imetokana na utamaduni mpya wa kutoa maoni nyuma ya Avatar, ufunguaji wa nchi na kupewa uhuru wa kutoa maoni bila shuruti.

Ilhali mheshimiwa Waziri Nape alipokuwa akizungumza hayo katika Kongamano la Majadiliano ya Ripoti ya Tume ya Haki Jinai lililohudhuriwa na Wataalamu, Viongozi Wastaafu, Watumishi wa Serikali na Wanafunzi naamini akiwa amesimama kwenye msingi wa mila na desturi za Mtanzania na haki- Mheshimiwa Raisi Samia Suluhu Hassan siku ya wanawake duniani mbele ya baraza la wanawake wa CHADEMA na Dunia aligusia Upayukaji mitandaoni na athari zake "Kutunishiana misuli" na Kadhalika alisema "huwa naingia Jamiiforums, nawasoma nacheka, lakini nasema huu ni Utamaduni mpya"

Msikikize hapa chini dakika ya 12+

Mheshimiwa Waziri Nape, akubali kuwa huu ni Utamaduni mpya, Raisi alishakubali haya na ni suala la Mda tu kwa Watanzania kukubali matusi kama sehemu ya Utamaduni wa kujibishiana hoja. Hakika haizoeleki lakini ndipo tulipofikia.
 
Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknoloji ya Habari, Mhe. Nape Nnauye (Mb) amewataka watanzania kutotumia lugha za matusi kukosoa jitihada mbalimbali zinazofanywa nchini na Rais wa Serikali ya Awamu ya Sita, Dkt. Samia Suluhu Hassan.
Hii tabia ya ccm kutuibia halafu wanataka wabembelezwe kuwa wameiba ifiki mahali ikome mtu akiiba aitwe kwa jina Lake mwizi
 
Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknoloji ya Habari, Mhe. Nape Nnauye (Mb) amewataka watanzania kutotumia lugha za matusi kukosoa jitihada mbalimbali zinazofanywa nchini na Rais wa Serikali ya Awamu ya Sita, Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Waziri Nape ameyasema hayo leo Julai 18 Mkoani Dar es Salaam alipokuwa akizungumza Katika Kongamano la Majadiliano ya Ripoti ya Tume ya Haki Jinai lililohudhuriwa na Wataalamu, Viongozi Wastaafu, Watumishi wa Serikali na Wanafunzi.

Nape amesema kuwa Rais Samia alipowaapisha Viongozi wa Wizara ya Mipango na Uwekezaji amewataka Viongozi hao wawasikilize wakosoaji wote na ikiwezekana wawajumuishe kwenye michakato mbalimbali ya kuboresha mambo mbalimbali katika nchi yetu na kusema kuwa kitendo cha baadhi ya wananchi wakiwemo wanasiasa kutumia lugha zisizofaa wanapotoa maoni yao sio sawa.

“Tukosoane, turekebishe, tutoe maoni bila ya kutukanana. Baba wa Taifa Mwalimu Nyerer alitufundisha tukosoane kwa hoja bila ya kutukanana. Kosoeni, toeni maoni, msidhalilishane na wala msitukanane na hasa inapokuwa ni Rais wa Nchi yetu mana yeye ni sura yetu sote”. Amesema Nape

“Kutukanwa kwa Mama ni kosa na hata kama hajakuzaa moja kwa moja unapomtukana basi ni sawa na kutukanwa kwa wazaza wote, tunao wajibu wa kuwaadhibu wote wanaotukana wazazi wa Nchi hii, kwani wazazi hawa wametulea, wametutunza, wametufikisha hapa tulipo salama na tusisahau kuwa utamaduni wa nchi yetu ni kuheshimiana” Ameongeza Waziri Nape.

Waziri Nape pia amempongeza Rais Samia kwa nia yake ya dhati kutaka kuona haki ikitendeka nchini na kusema kuwa mageuzi anayofanya katika kuboresha na kukusanya maoni ya watanzania kuhusu maboresho ya taasisi zinatoa haki nchini.

“Tunaposhuhulika na Haki Jinai, moyo wa Rais unataka haki. Haki italiinua Taifa letu,” amesema Nape.

Je Tabia mbaya ya Mama moja ni Tabia mbaya ya WA Mama wote
 
Back
Top Bottom