Nape Nnauye afungia mtandao wa Clubhouse, haupatikani Tanzania bila VPN

Nape strikes again.

Ukishaonja kula nyama za watu, kamwe hutoacha.

Yuleyule aliyetuondolea bunge live wakati huo akiwa waziri wa habari kipindi cha utawala wa Magufuli, Leo tena akiwa na dhamana hiyohiyo ya Waziri wa habari ameufungia kimyakimya mtandao maarufu wa Clubhouse.

Mtandao wa Clubhouse, ni mtandao ambapo watu popote pale walipo duniani huingia kujadiliana vitu mbalimbali kwa Sauti. Kupitia mtandao huu watu hujadili mada mbalimbali za maisha yao, ikiwemo uchumi, mambo ya kijamii, siasa n.k Nape mwenyewe ashaalikwa katika mada mojawapo kujadili ishu za anwani makazi.

Kutokana na elimu ya kuwaamsha watu na maarifa makubwa ambayo watanzania wamekuwa wakipata kupitia mtandao huo, serikali ya CCM imeona ni tishio kwao. Sasa Nape kama kawaida yake kaufungia mtandao huu ili Watanzania waendelee kuwa gizani.

Nape alipofungia bunge live wananchi walimlaani sana, baadae alipowekwa nje ya madaraka na JPM alikiri kuwa anajuta kushiriki maamuzi yale ya kufungia bunge Live. Leo Nape karudi madarakani kafungia tena mtandao wa Clubhouse ili Watanzania wasiweze kucongregate na kujadili mambo muhimu ya nchi yao.

Tukumbuke Nape huyuhuyu ndo alikuwa kinara wa kutetea sheria kandamizi ya vyombo vya habari wakati alipokuwa waziri wa habari kipindi cha JPM.

Tunamtaka Nape na TCRA, wafungulie mara moja mtandao wa clubhouse. Haiwezekani Rais Samia anasema kuwa anataka kuifungua nchi, na uhuru wa maoni uwepo, na kukosoa utawala wake ruksa, halafu anakuja Waziri kimyakimya bila kuutarifu Umma anafungia mitandao.

Kwa hivi sasa bila kuwasha VPN huwezi kuupata mtandao huu kwa sababu Nape Nnauye kaufungia.

Huyu Nape anajisahau sana, hii mitandao anayoiona ni mibaya ndiyo hiyohiyo iliyokuwa sauti ya pekee kumtetea kipindi kile katolewa bunduki njenje. Hivi huwa hawajifunzi kitu hawa?
Si alikuwa anasifiwa juzi tu!
 
Nape strikes again.

Ukishaonja kula nyama za watu, kamwe hutoacha.

Yuleyule aliyetuondolea bunge live wakati huo akiwa waziri wa habari kipindi cha utawala wa Magufuli, Leo tena akiwa na dhamana hiyohiyo ya Waziri wa habari ameufungia kimyakimya mtandao maarufu wa Clubhouse.

Mtandao wa Clubhouse, ni mtandao ambapo watu popote pale walipo duniani huingia kujadiliana vitu mbalimbali kwa Sauti. Kupitia mtandao huu watu hujadili mada mbalimbali za maisha yao, ikiwemo uchumi, mambo ya kijamii, siasa n.k Nape mwenyewe ashaalikwa katika mada mojawapo kujadili ishu za anwani makazi.

Kutokana na elimu ya kuwaamsha watu na maarifa makubwa ambayo watanzania wamekuwa wakipata kupitia mtandao huo, serikali ya CCM imeona ni tishio kwao. Sasa Nape kama kawaida yake kaufungia mtandao huu ili Watanzania waendelee kuwa gizani.

Nape alipofungia bunge live wananchi walimlaani sana, baadae alipowekwa nje ya madaraka na JPM alikiri kuwa anajuta kushiriki maamuzi yale ya kufungia bunge Live. Leo Nape karudi madarakani kafungia tena mtandao wa Clubhouse ili Watanzania wasiweze kucongregate na kujadili mambo muhimu ya nchi yao.

Tukumbuke Nape huyuhuyu ndo alikuwa kinara wa kutetea sheria kandamizi ya vyombo vya habari wakati alipokuwa waziri wa habari kipindi cha JPM.

Tunamtaka Nape na TCRA, wafungulie mara moja mtandao wa clubhouse. Haiwezekani Rais Samia anasema kuwa anataka kuifungua nchi, na uhuru wa maoni uwepo, na kukosoa utawala wake ruksa, halafu anakuja Waziri kimyakimya bila kuutarifu Umma anafungia mitandao.

Kwa hivi sasa bila kuwasha VPN huwezi kuupata mtandao huu kwa sababu Nape Nnauye kaufungia.

Huyu Nape anajisahau sana, hii mitandao anayoiona ni mibaya ndiyo hiyohiyo iliyokuwa sauti ya pekee kumtetea kipindi kile katolewa bunduki njenje. Hivi huwa hawajifunzi kitu hawa?
Hahahah nakumbuka kitenge alimtetea akimwambia jamaa,ahh unaharibu😅😅
 
Kuna taarifa yoyote toka twitter inayozungumzia hili? kama unayo tuwekee hapa.

Isijekuwa kwasababu ulikuwa unakerwa na nondo za kule Space, umeona utafute sababu kutetea uamuzi wa kidikteta uliofanywa na serikali uipendayo.
Ntaiweka, subiri
 
Umeandika kama vile kuna tofauti kati ya Nape wa Magufuli, na Nape wa Samia.

Nape ni huyo huyo wa Magufuli, wakati ule Samia akiwa msaidizi wa Magufuli, hivyo sishangai tabia za Nape kuendelea kama sasa yule msaidizi wa Magufuli yupo ikulu.
Kwahiyo mkuu unaamini Samia anahusika au analijua hili jambo?
 
Napee huwa kichwan kajaza Uozo, ana siasa ya Akina kibajaji Domo!

Hata Elimu tuu, ana Elimu za wahindi zile ambazo, ukishindwa sana unabebwa bebwa.
Nape kama asingekuwa mtoto wa kiongozi, ungekuta leo hii ni dereva bodaboda huko Mtama!.
Sawa na yule mtoto wa Kawawa mbunge kule Namtumbo.
Yaani ukimcheki hata sura tu unauona ukilaza!!.
 
Tuna haki ya kujua sababu. So far kaufungia kimyakimya.

Na huo mtandao ni multipurpose, watu wanajifunza mengi, kila aina ya elimu.

“Tuna haki ya kujua” ni kweli lakin mbona hujauliza mamlaka husika?

Umeanza na assumptuion na malalamiko?

Huku jF hutopata direct answers why zaid ya speculation, how about umfuate muhusika?
 
Ni wenyewe wanaoumiliki ndio wameufunga, wanafunga kwa baadhi ya nchi, hasa za kiafrika, wameona hauna faida, na mwaka Jana wamepata hasara sana, nasikia Wana mpango wa kuuza, lakini hawajapata mteja.

Imekuwa ngumu kupata matangazo au faida, na kwamba muda mwingi watu wanapigizana kelele tu, na wengine wakiwa wamelewa

 
Ni wenyewe wanaoumiliki ndio wameufunga, wanafunga kwa baadhi ya nchi, hasa za kiafrika, wameona hauna faida, na mwaka Jana wamepata hasara sana, nasikia Wana mpango wa kuuza, lakini hawajapata mteja.

Imekuwa ngumu kupata matangazo au faida, na kwamba muda mwingi watu wanapigizana kelele tu, na wengine wakiwa wamelewa
Kumbe wanakuwa bwiii
 
Am sorry kukwambia yes he can. If he cant direct he can use his influence to do that. cheo alichonacho kinamoa hiyo power
Mamlaka nayo ninachosema ni kuwa kwa kipindi hiki Cha Samia Nape anakuwa lofa kufanya hivyo
 
Ni wenyewe wanaoumiliki ndio wameufunga, wanafunga kwa baadhi ya nchi, hasa za kiafrika, wameona hauna faida, na mwaka Jana wamepata hasara sana, nasikia Wana mpango wa kuuza, lakini hawajapata mteja.

Imekuwa ngumu kupata matangazo au faida, na kwamba muda mwingi watu wanapigizana kelele tu, na wengine wakiwa wamelewa
Hakuna kitu kama hicho.

Kampuni ya Clubhouse haijafunga mtandao wao, hii ni kazi ya mamlaka za humuhumu nchini.

Hakuna mtandao wa kijamii usiopenda wanachama wapya, maana members wengi ni potential money in the future.
 
Ni wenyewe wanaoumiliki ndio wameufunga, wanafunga kwa baadhi ya nchi, hasa za kiafrika, wameona hauna faida, na mwaka Jana wamepata hasara sana, nasikia Wana mpango wa kuuza, lakini hawajapata mteja.

Imekuwa ngumu kupata matangazo au faida, na kwamba muda mwingi watu wanapigizana kelele tu, na wengine wakiwa wamelewa
Hebu ficha upumbavu wako.
Wingi wa watu ndiyo mtaji kwa wamiliki wa hii mitandao, kamwe hawawezi kukubali kupoteza mtaji wao (watu) kizembe namna hiyo.
Kama wangeufungia wamiliki tusingeweza kuupata hata kwa vpn.
 
Hebu ficha upumbavu wako.
Wingi wa watu ndiyo mtaji kwa wamiliki wa hii mitandao, kamwe hawawezi kukubali kupoteza mtaji wao (watu) kizembe namna hiyo.
Kama wangeufungia wamiliki tusingeweza kuupata hata kwa vpn.
VPN mnaupata kwa kuzunguka sana, huo mtandao unakufa kama ilivyokufa yahoo
 
Back
Top Bottom