Nape, Mwigulu, Juliana na Mwampamba ndio wanaokidhalilisha na kuitia aibu CCM!

Badala ya kueleza mikakati waliyonayo(CCM) kuondoa kero za huduma ya jamii,wao wananunua kura!Kuwashawishi wagombea vyama vingine kwa pesa na vyeo serikalini ili wajitoe kugombea,waende CCM.SHAME CCM,mmevuna aibu yenu. Na BADO 2015,CCM mtasoma namba.
Mimi nina uwezo wa kushawishi wapiga kura 100 kijijini kwangu wapigie kura mabadiliko 2015,Je wewe?
 
Nimekukubali kaka umewapa ukweli wao. Mwambie Nape awahi kwenda CCJ maana Mchemba na timu yake wanakata mit walioukalia. Wakati umefika kwa watanzania kutambua kuwa Arusha ndo Jiji lililozaa Azimia la Wanyonge AZIMIO LA ARUSHA lililo uawa kue Zanzibar. Inabidi wana Arusha watambue hilo.

Kampeni za Lowassa za kuleta ukabila eti Arusha ni kwa ajili ya wamasai zimepitwa na wakati. Mbona yeyey asili yake ni Meru na watu wamekaa kimya au anadhani ni siri kile ambacho kilifanya wakajikuta Monduli.

CHADEMA MWENDO MDUNDO!!!!!!!!
 
SHONZA, MWAMPAMBA, MWIGULU SI SULUHISHO LA KERO ZA WANA-ARUSHA.

Wana Ccm sasa wamehakikisha, wametambua, wameelewa kuwa siasa za kanda ya kaskazini ni siasa nyingine si linganifu na siasa za pahala pengine.

Ushindi wa viti vinne vya udiwani kwa Chadema si USHINDI mkubwa kwao kwani walijua UCHAGUZI ule ulikuwa mechi ya nyumbani, na kurudia UCHAGUZI ule ulitokana na maamuzi yao ya kuwafukuza madiwani wa chadema kwa kukaidi maagizo HALALI ya kamati kuu ya chadema. Na walifikia maamuzi hayo magumu wakijua kabisa hata uchaguzi ungerudiwa siku yeyote wangeshinda tu! Swali la kujiuliza ni kwanini chadema wanajeuri ya kisiasa Arusha? Majibu yanaweza kuwa mengi kila mtu na lake lakini jibu la msingi ni kuwa wana Arusha wanauelewa mpana, wameelimishwa na wakaelimika, wmefundishika kuwa serikali tulivu ya CCM iliyokaa madarakani kwa miaka 50 ndiyo chanzo kikubwa cha UMASKINI wao.

Wao kukosa Huduma ya afya bora, elimu bora, miundombinu ya barabara bora, kupanda kwa gharama za maisha zinatokana serikali ya Ccm. Na wakaelezwa kuwa fedha zao zinazoibwa kupitia miradi mbalimbali Kama EPA, DEEP GREEN, KAGODA, DOWANS, MEREMETA n.k zinatumiwa na viongozi wa serikali ya Ccm na familia zao huku wakiacha maelfu ya Watanzania wakifa kwa kwashakoo, utapyamlo, wakifa kwenye foleni ya matibabu kwa kukosa elfu mbili ya kununua dawa ya kuharisha! Huku viongozi wao wakipigana vikumbo uwanja wa ndege wa Mwalimu Nyerere wakielekea hospitali yao ya rufaa Apollo nchini India kutibiwa malaria huku wakiambatana na mashosti, ndugu jamaa na marafiki.

Wana Arusha wanajua kuwa mashangingi ya viongozi wao yanauzwa milioni 80 lakini viongozi wa Ccm wameengeza mpaka yamefikia milioni Mia tatu, Pesa ya mlipa kodi! Wameelezwa na viongozi wengine( HOSSEA) kuwa serikali haitaki kuwafikisha mahakamani viongozi wala Rushwa, Mafisadi. Wanajua Tz ndio nchi pekee ambayo mwizi anapewa mda wa kutafakari, kujitathimini ili arudishe fedha alizoiba!

Cha kushangaza Ccm wanamtuma MWIGULU NCHEMBA, SHONZA, MWAMPAMBA, kwenda kuwaeleza wakazi wa Arusha kuwa chanzo cha matatizo yao, umaskini wao ni kwa sababu ya MAANDAMANO, LEMA na CHADEMA!!. Wakasahau kuwa wapiga kura wa Arusha wanaojitambua, wanajiielwa na kuwa adui wao namba moja ni CCM na serikali yake!

Mbaya zaidi vikafanyika vikao vya hadharani na faragha vya kueneza uwongo kuwa Arusha haitaendelea kwani chadema wapo nyuma ya mabomu, mauaji, ukatili, umwagaji wa Tindikali. Wakaendelea kuwachonganisha na Wamasai mpaka ikafika hatua kikao cha ma-LAIGWANANI kikaitishwa chini ya ufadhili wa Ccm wakatangaza kuwa watawafukuza WACHAGGA Arusha kwa sababu wanaleta fujo, maandamano pasipo kujua mbinu ile ilikuwa chafu kwani hata WACHAGGA ambao ni Ccm hawakupigia CCM kura kwa hasira.

Wana Arusha wanajua kuwa CHADEMA ni Chama kilichowakomboa kifikra, ni chama pekee kinachoifanya serikali kuwajibika kwa wananchi, ni chama kinachotetea maslahi mapana ya taifa, ni chama kinachojitanabaisha na wananchi. Ccm hata waende taifa gani kumpata mshauri mwenye shahada za uzamivu Mia Tisa, vyeti vya propaganda tani nne.

Kamwe hawataweza kuwashawishi wana Arusha kuwa CHADEMA ni chama hatari, Chama cha matukio, chama cha maandamano, chama cha kidini, chama cha WACHAGGA na kadhalika. CCM wao waharakishe maendeleo kwa wana Arusha wajenge miundombinu bora, watoe huduma ya afya bora, elimu bora hakuna mtu atatafuta mbadala wa CCM. SHONZA, MWAMPAMBA, MWIGULU hawawezi kubadilisha watu wanaojitambua kwa Kutoa matusi, kejeli na kutoa kauli tata kuwa msipoichagua Ccm watakiona cha MOTO,


NI CHUNGU LAKINI DAWA


(Kidumu Chama tawala CCM)

Hatujawahi kusema hao wote watatu ni suluhisho la kero zetu hapa Arusha. Ninachojua mimi wote hao ukijumuisha na kiongozi wao dhaifu na serikali yake, wote ni moja ya kero yetu hapa Arusha. Ukishakuwa ndani ya chama cha mafisadi, wewe ni kero popote utakapokuwa.
 
Ndo kwanza wanaendelea kujipa moyo kuwa CCM itatawala milele, hapo kwa A town mmefika na moto huo unaenda kusambaa mikoa mingine kwa kasi ya ajabu! mtakuja kustuka 2015 mpira uko golini huku Chama pinzani kikiendeleza ushindi wake wa 4-0!
Tuwakumbushe CDM ni mpango wa mungu baadhi ya makada wenu wameanza kukiri kuwa CDM kufa ni ngumu. Nyie endeleeni kuwatumia akina Mwigulu. Mmesahau kuwa Mbunge 1 wa CDM ni sawa na wabunge 10 wa CCM.
 
Naona kama vile ccm wote hawana akili kabisa kuanzia w/mkuu kwa kauli zake za kipumbavu na wahuni wengine km vile nape, mwiguluneti, shonza na mwampamba.....................ila uzuri wao ni kwamba wanaangalia mkono umeingia kinywani basi....maslahi ya taifa wanajua wenye taifa ambao ni wana cdm wote
 
Pamoja na hayo matatizo na kero za Tz, Chadema sio mwarobaini wa haya matatizo hata kidogo.
 
Ngoja mwenyekiti wa chama akusikie, unataka kuwachafua washauri wake wakuu?

Ushauri wa bure kwa mwenyekiti. Hawa ni janga la Chama. Shonza na Mwampamba ni mfupa uliomshinda fisi. Mwanadamu atauweza? Savimbi yeye ni kinara wa gutter politics. Wote hawa wanatuharibia chama chetu tawala.
 
Ushauri wa bure kwa mwenyekiti. Hawa ni janga la Chama. Shonza na Mwampamba ni mfupa uliomshinda fisi. Mwanadamu atauweza? Savimbi yeye ni kinara wa gutter politics. Wote hawa wanatuharibia chama chetu tawala.

Watu hawapendi kuambiwa ukweli kiongozi. Ni vyema ukatambua pia kwamba; "MBWA MZEE HAFUNDISHWI SHERIA MPYA"
 
Ndugu zangu wanajamvi ninaomba niwashirikishe tafakuri yangu juu ya usaliti wa vijana. Mimi ni kijana ambaye kwa kweli huwa ninapenda kukisimamia kile ninachokiamni kuanzia mwanzo mpaka mwisho. Hapa ndio msingi wa tafsiri yangu ya usaliti. Kwa tafsiri yangu usaliti ni kitendo cha kwenda kinyume na makubaliano ya pamoja iwe ni katika mapambano, harakati au suala lolote la kimaisha. Usaliti hapa unaweza kuwa kati ya mtu mwenyewe na nafsi yake au mtu na mtu mwingine au mtu na kundi jingine.

Ninawatumia hawa ndugu wawili Mtela na Juliana kama tu kielelezo cha usaliti wa vijana. Ni imani yangu kuwa kwa mujibu wa tafsiri yangu ya usaliti, wenye macho na akili ya kuelewa wanastahili kukub aliana na mimi kuwa hawa ndugu ni mfano mzuri wa usaliti unaofanywa na vijana wengi katika siasa.

Usaliti wa vijana hawa unatokana na ukweli kwamba kwa utashi wao wakiwa na akili timamu walijiunga na WANACHADEMA na CHADEMA Kwa maneno na matendo mbalimbali kuonesha uchafu na uovu wa CCM (Walionesha kukerwa na kuichukia CCM). Huenda (Sina uhakika) wakati mwingine walifanikiwa hata kuongeza baadhi ya wanachama wapya. Wananchi wa Mbozi wenye hamu ya mabadiliko waliwaunga mkono vijana hawa kwa matumaini ya kupambana na hatimaye kuiondoa CCM kwa njia ya kidemokrasia. Wengi waliamini na walidhamiria kumuunga mkono kijana Mwampamba. Kijana huyu na ndugu yake Shonza walisema mengi kuhusu udhalimu wa CCM. Maneno yao yalionesha kweli vijana hawa wanaichukia CCM na upuuzi wake wote. Wakati mwingine waliongea mpaka kulia (yaani kutoa machozi). Hali hii ilijenga imani kwa wananchi ambao wanayatafuta mabadiliko ambayo hayawezi kuletwa na CCM.

Jambo hili liliwahi kusemwa na Mwalimu Nyerere wakati akiwahutubia wajumbe wa mkutano mkuu wa CCM Taifa mwaka 1995 Huko Dodoma. Mwalimu alisema "watu sasa hivi wanataka mabadiliko na kama hawatayaona ndani ya CCM potelea mbali wataamua kuchagua hata upinzani"

Kutokana na jinsi watu walivyokuwa wakiitikia katika mikutano ya vijana hawa walijisahau wakajenga kiburi na kuona kwamba wao wanakubalika zaidi kuliko taasisi yao yaani CHADEMA. Kosa walilolifanya ni kushindwa kuelewa kuwa kwa sasa watu wanachokitaka ni mabadiliko na mabadiliko hayo hayawezi kuletwa na CCM bali ni upinzani. Kosa hili kwangu ninaliona kama chimbuko halisi la usaliti wa vijana wenzetu hawa. Vijana waliota jeuri na kuamini wao ni CHADEMA NA CHADEMA ni wao na bila wao hakuna CHADEMA. Tatizo hili linawatafuna vijana wengi sana, hawa ni mfano tu.

Kama ambavyo inaeleweka kuwa dhambi moja (usaliti) huzaa dhambi nyingine, kiburi chao kilisababisha kukosa utii kwa kisingizio cha demokrasia ndani ya chama na hivyo waliamini kabisa kuwa wapo huru kusema lolote sehemu yeyote na wakati wowote. Dhambi hii nayo ilifanikiwa kuleta dhambi nyingine ambayo ni kuwa tayari kununuliwa ili watumike kama vipaza sauti vya waliowanunua. Jambo hili ni la kawaida katika maisha kwani hata wahenga walisema "Alimpaye mpiga zumari ndiye huchagua wimbo"

Kutokana na mabadiliko ya kiuongozi ndani ya CCM, Kiliingia kikundi kinachoamini katika fanya lolote maadamu ushindi upatikane (iwe ni kuua, kutesa, kuleta hofu, kuiba, kutumia pesa, kuchonganisha, kuchafua watu wengine n.k). Hii kwa sasa ni sawa na Kashifa ya "WATERGATE" ambayo ilisababisha raisi wa Marekani Nixon ajiuzuru kutokana na siasa za kimafia dhidi ya wapinzani wake wakuu kutoka katika chama cha "Democratic" (Jambo hili nitaliandika makala yake kuonesha namna CCM na Mwigulu walivyoingia katika siasa za namna hii).

Huu ni mfano tosha wa namna ambavyo CCM nao waliitumia nafasi ya uasi na kiburi cha hawa vijana kuwatumia ipasavyo. Kama ni pesa si tatizo kwa siasa iliyopo CCM. Vijana wakajikuta wapo tayari kufanya lolote kutokana na kuwa na bei. Vijana wakajikuta wakisaliti nafsi zao na kuamua kusema wasichokiamini maadamu wameagizwa. Ghafla, vijana walioaminiwa na wananchi wakaanza kuropoka (si kusema) mambo ambayo ni kinyume na walichokuwa wakikiamini.

Je kwa hali hiyo unaweza kusema ni nini? Je labda ni utashi wao tu kuwa kwa sababu mwanadamu anabadilika na wao labda waliamua tu kutoka ndani ya mioyo yao? Jibu hili mimi siwezi kuliafiki kutokana na mtiririko wa matukio na ushahidi wa kimuktadha. Niliamua kuhitimisha kabisa kuwa huu ni usaliti na si vinginevyo.

Hauwezi kutoka upinzani ukaenda CCM chama ambacho umekirushia matusi mengi katika muda mwingi wa siasa hususani ulipokuwa upinzani. Angalau wangeenda chama kingine cha upinzani na wakaendeleza ukali waliokuwa nao dhidi ya ccm na huku wakionesha yale ambayo wametofautina na CHADEMA walau wangeeleweka.

Ila kwa sasa ninasimamia kabisa kuwa huu ni usaliti. Wamesaliti nafsi zao, watu waliowaunga mkono, pamoja na chama chao kwa ajili tu ya kutaka mafanikio ya kimaisha ya haraka. Ninaomba niwaeleze vijana hawa na vijana wenzangu wote kuwa hakuna njia ya mkato katika maisha. Maisha ni subira na maisha ni kujituma kwa bidii zote katika kile unachokiamini.

ATHARI YA TABIA YA VIAJANA HAWA
Athari kubwa kabisa ambayo vijana hawa na vijana wengine wa aina hii wanayoileta kwa vijana wote ni vijana kuwekwa katika kundi la kutoaminika. Kutokana na tama za kijinga kabisa za vijana hawa huenda huko mbozi vijana wenye mapenzi ya dhati ya kuomba uongozi kutoka kwa wanachi msiaminiwe tena. Pia hali hii imesababisha vijana kuonekana kuwa ni watu wa bei rahisi na wenye maamuzi ya kukurupuka katika maisha yao. Hii ni kutokana na ukweli kwamba siku za mwampamba na shonza zinahesabika katika medani za kisiasa na kuna uwezekano mkubwa wakajutia jambo hili katika maisha yao yote ya siasa. Uwezekano wa vijana hawa kujutia ni kutokana na viashiria vifuatavyo:

Mosi ni suala la historia, miaka yote CCM huwa inaonesha kumthamini mtu pale inapoamini kuwa mtu huyo anauwezekano wa kuinasua pale inapoelekea kuzama. Hebu jitafakari na muone hadhi ya Tambwe Hiza CCM je inaendelea kupanda au kushuka? (amegombea cheo gani akashinda ndani ya CCM?) Jikumbusheni yule mwanamke aliyeitwa kama niunakumbuka vema Angelina.

Mwanamke huyu alitumika kudhalilisha utu wake kwa ajili ya kumchafua Mrema (akisema kuwa amezalishwa na Mrema na kutelekezwa). Baada ya kazi yake kuisha hivi mnajua ni mambo gani yalimkuta mwanamke huyu? Kwa mfano wa hivi karibuni kabisa yupo ndugu yetu Mahimbo ambaye aliamua kudhalilisha utu wake pamoja na watoto wake kabisa kwa jambo ambalo alikuwa analielewa vema kabisa. Baada ya kazi kuisha Mahimbo kaachwa jinsi alivyo. Orodha ni ndefu sana ya watu waliotumika na kutupwa baada ya kazi waliyotumwa kuisha au kutokamilika ilivyotarajiwa.

Pili ni suala la kushindwa kuonesha msaada wowote wa maana kwa CCM. Ninaomba mzidi kujitafakari wenyewe zaidi ya ndugu mmoja kutumika kama kiburudisho au wengene hapa katika jamvi wanavyosema uwanja wa mazoezi wa savimbi. Je kuna jambo lolote la maana mablo mmeisaidia CCM? Katika hoja hii hapa ndio kifo chenu cha kisiasa kilipo. Mwampamba binafsi nilimuambia jambo hili facebook badala ya kunijibu kwa hoja akaamua "kuniblock".

Chaguzi hizi za udiwani katika kata 26 zinawaweka katika mazingira mabaya sana ya kufanyiwa tathmini. Mmepoteza mpaka kata ya nyumbani kwenu Mbeya huu ni upuuzi wa hali ya juu. Hivi ni nani atakayeendelea kuwapa posho nono bila matokeo chanya? Labda kama mtaanza kazi nyingine kwa mwanvuli wa siasa ndio itawapatia posho!

Tatu ni kushindwa kuleta athari tarajiwa kwa chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA). Kumbukeni kuwa huu nao ulikuwa ni wajibu wenu mkubwa sana. Hebu jiulizeni ni athari ipi ambayo mnaweza kujivunia kuwa mmeisababishia CHADEMA? Hebu jiulizeni tu hata kupitia marafiki zenu mliokuwa nao FB wakati mkiwa CHADEMA je ni nani aliamua kuwaunga mkono? Kwa sababu kila "mnachoposti" katika facebook kinashambuliwa vikali na marafiki zenu mpaka mmeamua kublock watu wote mnaowaona hawaungi mkono ujinga wenu. Mbaya zaidi hakuna zaidi ya hoja ya kutukana viongozi wa CHADEMA. Pia ninyi mkitukanwa midomo inarefuka sana. Sasa jitafakarini na chukueni hatua kabla hamjatupwa katika chombo cha takataka.

NNe ni kukabiliwa mapambano kutoka kwa vijana maslahi na vijana wazalendo wa CCM. Wengi wanalalamika huko iweje watu ambao hawaijui hata CCM kuja tu na kuanza kufaidi matunda ya ufisadi wa muda mrefu wa chama cha mapinduzi. Vijana hawa hawapo tayari kuona mkiendelea kupata posho. Kwa bahati mbaya sana, sasa hivi wana hoja za kutumia kuwaengua. Hii kwa kweli inakatisha tama watu wajitoe kwa muda marefu wakiamini kuwa wao ndio vijana wa chama halafu mgeni tu aje na kuanza kufaidi huku wao wakiambiwa kuwa subirini hawa tunawatumia tu kukamilisha malengo maalumu. Tatizo ni kwamba malengo maalumu yanaonekana kuzaa matunda hasi.

Hii ni kutokana na ukweli kwamba toka mmejiunga na timu ya kampeni ya CCM mmesababisha sijui CCM kupoteza viti vingi zaidi pamoja na kura kuzidi kupungua. Hili ni tatizo kubwa.

Tano ni tuhuma zinazowakabili kuwa ninyi ni mapandikizi ya CHADEMA. Tuhuma hizi zinapewa nguvu kutokana na hoja dhaifu mnazozitoa iwe ni kwa kujua ama kwa kutokujua. Hali hii inawaletea chuki miongoni mwa baadhi ya wanaCCM ambao bado wanaamini chama chao kinaweza kubadilika na kurudi katika misingi ya kuanzishwa kwake. Hoja hii inapewa nguvu na tuhuma ya Shonza kushushwa jukwaani huko Arusha baada ya kusema kuwa CCM ni chama cha mafisadi. Lakini pia hata bandiko lake la leo la kuifananisha CCM na mchicha dhidi ya CHADEMA. Kauli hii imeongeza mashaka ya wanaccm walio wengi. Watu (ccm) wanaamini kuwa ni ngumu sana mtu kuacha asili yake. Kinachoaminika kwa ccm ni pale tu mtu anapoondoka ccm na kuanza kuishambulia ccm kwa udhati hapo ndio wanajua kuwa huyo mtu amebadilika na utaona wanavyomuandama kwa mbinu halali na haramu ili kumuangamiza. Tafakarini sana jambo hili kwa umakini sana.

USHAURI KWA VIJANA
Ninatoa ushauri ufuatao kwa vijana wenzangu:
Mosi lazima tuelewe kauli ya Mwalimu Nyerere kuwa sasa hivi Watanzania wanataka mabadiliko na kama hawatayaona CCM watakuwa tayari kuchagua upinzani. Hivyo basi, Umaarufu tunaoupata ni kwa sababu watu wanataka mabadiliko ambayo wameona kuwa hayawezi tena kupatikana ndani ya CCM. Halii hii tuione kuwa umaarufu au uungwaji mkono tunaoupata katika vyama vya upinzani tulivyopo si kwa sababu kuwa sisi tunamvuto zaidi ya vijana wote bali ni kwa sababu tupo upande ambao umeaminiwa kuleta mabadiliko. Kama unabisha jifunze kupitia Shonza na Mwampamba na ujiulize je uungwaji walioupata wakiwa CDM bado unaendelea? Unadhani ni kwa nini? Jibu ni kwamba wamepishana na imani ya wananchi kuhusu mabadiliko.

Pili vijana tushinde vishawishi vya kupata pesa rahisi(za chee). Pesa za namna hii zinaendana na sisi kuwa tayari kununulika na kutumiwa kwa urahisi sana.Tuna haja ya kulinda utu wetu na wa wale wengine wote walionyesha kutuamini. Mapambano ya kumuondoa mkoloni mweusi si rahisi na wala si ya siku moja. Kama umedhamiria kuwasaidia wananchi kuyapata mabadiliko wanayoyatarajia ambayo wameshindwa kuyapata kupitia CCM ni lazima uwe imara na uikane nafsi yako. Kuwa tayari kupitia shida na magumu mengi kutoka kwa mkoloni mweusi CCM.

Tofauti na hapo ni kweli utapata pesa ya haraka lakini ambayo itagharimu utu wako na maisha yako kwa jumla. Usaliti wa namna hii unaharibu mpaka kwa ukoo wako wote kwani unawajengea mazingira magumu hata watu waio na hatia ambao wapo katikia familia au ukoo wako. Tujichunguze zaidi kama vijana kupitia hawa Shonza na Mwampamba.

Tatu hususani vijana wa kike kuweni makini sana na kuingia katika siasa kwa kutumia mgongo wa sura au urembo. Historia inaonesha kuwa hakuna aliyewahi kudumu katika siasa kwa kutumia urembo wake. Sanasana utatumika tu kama uwanja wa mazoezi na wakati ukikutupa nawe ndio hivyo siasa basi tena!

Nne vijana tuepuka kuifanya siasa kama ajira. Msukumo wa kisiasa utokane na haja yako ya kukerwa na hali ya taifa kwa sasa. Kwa wale wa CCM wajikite kutetea mfumo uliopo (kama unaona unakunufaisha na kunufaisha wengine). Wale wanaotaka kwenda upinzani wajiulize kwanza kabla ya kuingia katika sisa jiulize je mfumo na hali iliyopo sasa kweli inakukera kabisa. Jibu likiwa ni ndio kutoka ndani kabisa ya moyo wako utakuwa umekaribia kuushinda usaliti unaotokana na vishawishi vya hapa na pale. Kama unakerwa kabisa haitakuwa rahisi ukijiunga na upinzani halafu baada ya mwaka unaenda CCM. Ukifanya hivyo tutakuita msaliti tu hatuna jina jingine.

Tano ni kuelewa kuwa CCM haijawahi kumtumia mtu muda wote. Utapewa pesa na CCM kwa muda mfupi na baada ya hapo utatelekezwa na hata ikibidi utauawa ili kulinda siri za maovu yote ambayo umetumikishwa kwa manufaa ya CCM. Kumbukeni kuwa CCM ina wenyewe!

USHAURI KWA SHONZA NA MWAMPAMBA
Sitonesha uzalendo na uungwana kama nitahitimisha bila kuwashauri nini mfanye. Kumbukeni huu ni ushauri mnaweza kuufanyia kazi au kuuacha. Fanyenni lolote kati ya haya:

Mosi Jiondoeni katika siasa walau kwa muda. Hii itasaidia kulinda tu heshima na utu wenu kabla CCM hawajawatupa. Huu ni ukweli mchungu lakini kama vijana wenzetu ni lazima muelewe huenda mkawa na maisha marefu. Katika maisha haya nafsi zenu zitawahukumu kwa usaliti lakini pia mtaumia kutokana na usaliti ambao CCM watawafanyia muda si mrefu. Msisubiri kufukuzwa someni majira ya wakati. Hata katika mahusiano ya vijana ukiona mwenzio haeleweki usisubiri mpaka akuambie kuwa mimi sikutaki tena. Hii kidogo italinda utu wenu badala ya kusubiri kutelekezwa na posho kuyeyuka. Hebu muulizeni Tambwe Hiza kwa mara ya mwisho ni lini amepata posho kama mliyopata katika uchaguzi wa huu udiwani wa hapa majuzi? Historia inatabia ya kujirudia!

Pili ni Kujiondoa CCM na kurudi CHADEMA mkatubu madhambi yote na kuomba msamaha na muombe kabisa kuwa ni watu wa kawaida kabisa. Mkifanya hivi ni kweli mtasamehewa lakini hakuna mtu atakayekuwa anawaamini kama mwanzo. Ila jambo la msingi mtalinda utu wenu kwa kiwango kikubwa. Hatari nyingine ya uamuzi huu unaweza kusababisha CCM kikawadhuru. Uzuri mmepata bahati kidogo ya kuona namna ambavyo CCM wanatumia njia halali na haramu kufanikisha malengo yao. Ila ninaamini kuna namna itakayowaepusha na hasira hizo za CCM

Tatu ni kuendelea kukaa CCM mpaka pale mtakapotelekezwa kabisa (hamtafukuzwa uanachama). Hali hii itawasaidia nanyi kuingia katika historia ya watu niliowataja na jamii haitawasahau kwa usaliti wenu. Pia mtafikia hatua ya kuanza kujutia yote ambayo mliyafanya lakini hamtakuwa na nafasi wala ujasiri wa kuomba kusamehewa.

HITIMISHO
Ndugu zangu hii ni tafakuri yangu kuhusu kuhusu usaliti wa vijana katika medani za siasa. Ni muhimu tukumbushane, tuonyane, na turekebishane ili kujenga taifa lenye nidhamu na lenye mshikmano katika mambo ambayo kama taifa tuna amini kwa pamoja. Usaliti unaotokana na kununuliwa ni hatari kwa maslahi ya taifa.
 
Siku zote tunajua kwamba kila lenye mwanzo na mwisho wake pia upo! Kwa mwanadamu ambae mwisho wake umefika huishia kuoza Kaburini,na kwa wale wengine (Mabaniani)huishia kuchomwa moto hapa hapa duniani na sijui inakuaje huko kwa Muumba!!

Chama cha Siasa ni kama kitu chenye uhai kwa maana huanzishwa na pia huisha au kufutika na kubaki kumbukumbu.
Baada ya mfumo wa vyama vingi kuanzishwa kwa hapa Tanzania miaka 20 sasa tumeshuhudia Vyama vingi vya siasa vikianzishwa na baadhi Vikidumaa huku vingine Vikichanua na kustawi japo ktk mazingira magumu na ya shida.

Chama Cha Mapinduzi ndicho chama kikongwe na cha siku nyingi ktk Medani za Siasa kwa hapa Tanzania ukilinganisha na vyama km CUF, TPL, NCCR, CHADEMA nk.lakini kutokana na kulewa madaraka na kujiona Miungu watu kwa Viongozi wa Chama hiki Kikongwe sasa hatari inainyemelea Chama hiki na kwamba Siku yeyote kama sio 2015 kinaenda kufutika ktk ramani ya Siasa hapa Tanzani na kufuata jirani yake KANU kule iliko.

Kumekua na Sintofahamu kwa baadhi ya Wanasiasa ambao wamewahi kukitumikia Chama hiki miaka ya nyuma kwa jinsi ambavyo sasa kinaendeshwa kwa njia isiyopendeza wala kushawishi watu haswa vijana ambao ndio nguvu kazi kujiunga na Chama hiki.

Wakati wenzao CHADEMA wakiendelea KUSTAWI kila siku ktk Medani za siasa na vijana wakiendelea kukiunga Mkono ktk harakati zake za kujiandaa kutwaa na hatimae kushika Dola! Wao (Ccm) wamebaki kutumia Jeshi la polisi na Viongozi wachanga kisiasa kuijengea Uadui na wananchi na kuendelea kusogelea Kaburini huku Taa nyekundu ikiwa tayari imewaka kuashiria hatari!!

Kuporomoka kwa kasi kwa CCM kabla na baada ya uchaguzi mkuu 2010 ni ishara tosha kwamba uchaguzi mkuu 2015 utakua mgumu sana kwa chama hiki Kikongwe na cha zamani. Hakuna ubishi kuwa kwa sasa kila siku watu wanaojiunga na CCM ni wachache ukilinganisha na wanao kihama!! Huku haya yakiendelea kwa CCM jirani zao CHADEMA kila siku wanaojiunga ni wengi ukilinganisha na wanaokihama. Hapa ndipo utagundua tofauti kubwa kati ya Ccm na CDM!!

Wengi wanadhani kuwa kuendelea kuchukiwa na hata kukimbiwa kwa CCM na wanachama na Wapenzi wake labda ni kwa sababu ya Ufisadi,kushindwa kutimiza ahadi zake ilizozitoa ktk ilani ya uchaguzi na ugumu wa maisha! Ni kweli haya yote yanaweza pia kuwa sababu lakini kwa mtazamo wangu mimi bado isingekua kwa kasi hii tunayoiona sasa.

Kuna sababu kuu mbili ambazo CCM isipojiangalia 2015 wanaweza hata wasipate majimbo 50 ya ubunge.
1> SIASA za maji taka zikiongozwa na Naibu katibu mkuu bara Mwigulu Mchemba, Nape Nauye,Steven Wassira na Job Lusinde. Ukijaribu kuangalia watu wamechoka na siasa za namna hii. Kila mara viongozi hawa wamekua wakishindwa kuwaeleza watanzania kuwa ni kwanini hadi leo miaka 50 tangia tupate uhuru hatuna huduma za afya zinazorizisha kwanini Wanafunzi wanakaa chini,kwanini huduma za maji safi kwa wengine ni km Anasa na ni kwanini baadhi ya watu hata mlo mmoja kwa siku ni wa kubahatisha nk.!? Badala yake tunaambiwa Dk Slaa ni Padri,Mbowe ni Mchagga,na mengine mengi yasiyo na maana!

2> Jeshi la polisi kua sehemu ya kitengo cha Propaganda ya CCM kwa kukubali kutumiwa na kufanya kazi za Siasa km chama cha siasa huku ikiwanyanyasa Wapinzani kwa kuwakamata viongozi wake Wakuu na kuwafungulia kesi za uwongo na kuwatishia kila mara. Jeshi la polisi inatumia nguvu nyingi sana pasipo sababu kupambana na kuzuia wafuasi wa Vyama vya upinzani wakati wakifanya maandamano ya kudai haki huku wakishindwa hata kuzuia Uingizaji wa Madawa ya kulevya nchini, wanashindwa kuzuia Wauaji wa Tembo na kuwangoa Meno,lakini sio hayo tu bali Wameshindwa hata kuzuia Twiga mnyama mrefu kuliko wote asipandishwe kwenye Ndege.

Ukichanganya sababu hizi na zingine nyingi utagundua kwamba Watu wengi kama sio wote hawafurahishwi na jinsi CCM inavyotumia viongozi hao niliowataja Pamoja na Jeshi la polisi ktk kuishuulikia CDM chama kikuu cha upinzani. Na badala yake wanajenga chuki dhidi ya CCM huku Mapenzi yakizidi kwa Cdm.kwa kuwa wanaona kama vile wanaonewa.

Chukulia mfano uchaguzi wa kata 4 Jijini Arusha ambapo CCM iliwatumia Mwigulu ,Juliana Shonza na Mpamba ambao ktk mikutano yao yote hawakuwahi kuwaambia wananchi kuwa wakuwachagua CCM watawafanyia nini! Walichokua wakifanya ni kuituhumu tu CDM na kumpandisha Kijana aliemwagiwa tindikali jukwaani wakidai kuwa waliomfanyia hivyo ni CDM. Upande wa Jeshi la polisi wao kama kwaida yao hawakuacha kuwakamata viongozi wa Cdm na kuwalaza mahabusu lakini sio hivyo tu siku ambapo bomu lilirushwa ktk mkutano wa CDM bado polisi waliwashambulia kwa risasi za moto wafuasi wa CDM waliokua wakikimbia kuokoa maisha.

Mwigulu Mchemba,Nape Nauye, na William Lukuvi kwa nyakati tofauti walidai kuwa Cdm ndio wakijilipua na kwamba wakati polisi wakitaka kumkamata mtu alie rusha Bomu ndipo wafuasi wa CDM wakamtorosha. Shame on them!! Pamoja na yote lakini bado wananchi waliwapuuza na kupiga kura za hasira kwa CDM.

Ktk vituo vingi vya kupigia kura Wagombea wa CCM waliishia kupata kura namba za viatu yaani kura 7 kura 9 kura 5 nk.!
2015 Mwigulu na Jeshi la polisi watakua ndio Sanda na Jeneza la kuizika marehemu CCM. R.I.P!!
 
Hili la kupata kura namba za viatu sio uwongo ni kweli kabisa wana A town waliwafundisha Magamba Adabu. Wakati wa kampeni kada wa CDM Kalist maarufu km BUSH,alkua akisema kuwa Wagombea wa CCM watapata namba za viatu. Yaani kura 7 kura 8 kura 9 kura 6 nk. Na kweli ndicho kilichotokea.
 
Hili la kupata kura namba za viatu sio uwongo ni kweli kabisa wana A town waliwafundisha Magamba Adabu. Wakati wa kampeni kada wa CDM Kalist maarufu km BUSH,alkua akisema kuwa Wagombea wa CCM watapata namba za viatu. Yaani kura 7 kura 8 kura 9 kura 6 nk. Na kweli ndicho kilichotokea.

Mkuu inaitwa twanga kote kote...hakuna kulala mpaka kieleweke!
 
Mkuu inaitwa twanga kote kote...hakuna kulala mpaka kieleweke!

Ni kweli Kamanda. Ila kwa mbinu hii waliyotumia Marehemu mtarajiwa Ccm ktk Siasa za kampeni Arusha ilichangia kwa kiasi kikubwa CDM kupigiwa kura za hasira. Kumbuka Mwigulu alikua akijiamini sana kwamba mbinu ya kuitumia kile KINYAGO cha Mpapure (MUSA TESHA) kuombea kura ingewapa ccm kura za huruma. Lakini kinyume na matarajio yake hayo watu ndio walichukizwa zaidi na kitendo hicho.
 
tunapoendelea kumzungumzia mwigulu ambae anaumwa upunguani basi na sisi hapa jamvini tunaonekana mapunguani tuachane nae.
 
Back
Top Bottom