Nape, Mwigulu, Juliana na Mwampamba ndio wanaokidhalilisha na kuitia aibu CCM!

Tulimumu

JF-Expert Member
Mar 11, 2013
14,305
12,969
Vijana hawa, Nape, Mwigulu, Juliana na Mwampamba kwa sasa ndio vijana wanaoidhalilisha na kuitia aibu CCM. Vijana hawa wamepewa uhuru mkubwa wa kusema na kutenda lolote ndani ya CCM kana kwamba hakuna watu wa kuelekeza na kuwashauri mambo ya kusema na kutokusema au mambo ya kufanya au kutokufanya. Vijana hawa wakifungua midomo wanaongea mambo ya hatari sana kwa mustakabali wa chi yetu. Naweza kusema bila woga kuwa hawa ndio watakuwa chanzo cha kuvurugika kwa amani na usalama wa nchi hii. Wakati mwingine huwa napata shita kuamini kama chama hiki kina mwenyekiti anayeona hatari inayoletwa na vijana hawa au anaifurahia hali hiyo na hivyo naye ni sehemu ya uchafu huu unoenezwa na vijana hawa.

Vijana hawa kwa sasa ndio wanaoeneza chuki za ukabila, udini na ukanda.Wameacha kabisa kuhubiri sera za CCM wamegeukia mambo hayo hatari. Wao kwa akili zao finyu wanadhani wanaidhoofisha CHADEMA bila kujua kuwa wanaidhoofisha nchi kwa ujumla. Bahati mbaya sioni mtu mwenye busara ndani ya CCM akiibuka kukemea mambo hayo.

Wakati Fulani CCM ilipoona inazidiwa na CHADEMA ikawa inatumia polisi kusamabaratisha shughuli za CHADEMA. Waziri mkuu mstaafu Fredrick Sumaye akawaambia CCM kuwa CHADEMA inafanya siasa kwahiyo na CCM nayo inatakiwa kufanya siasa si kuwazuia CHADEMA kufanya siasa. Mwanzoni walimpinga wakisema alipaswa atoe ushauri wake ndani ya vikao na sio hadharani na wakamzodoa kuwa anatamaa ya uraisi. Maana ndio CCM ya sasa. Mstaafu yeyote akitoa mawazo tofauti anaambiwa anautaka uraisi. Wamekuwa wanajadili watu badala ya hoja. Lakini pole pole tukaona wakitekeleza ushauri wake. Tuliona CHADEMA wakifanya mkutano Jangwani na wao wanafanya, CHADEMA wakienda mikoani kufanya mikutano, na wao wanakwenda kufanya mikutano kujibu hoja za CHADEMA tena wakaongeza nguvu ya mawaziri Mwakyembe,Magufuli na Tibaijuka kwenye ziara zao. Hiyo naona wakaona imeshindwa kudhoofisha nguvu ya CHADEMA. Wakarudi tena kutumia polisi. Ndipo tukashuhudia mauaji ya mwananchi mmoja kule Morogoro na baadaye mwandishi wa habari kule Iringa.

Kana kwamba hiyo haitoshi wakaendeleza hoja za wanasiasa waliofilisika za ukabila,udini na ukanda. Hiyo haikutosha. Sasa hivi tunaambiwa naibu katibu mkuu Mwigulu amekiri kuhusika na video ya Lwakatare. Hii ni aibu kubwa kwa chama tawala kutumia mbinu za kigaidi ili kukubalika kwa wananchi. Haya yote yanafanyika huku mwenyekiti akiwa kimya kabisa kana kwamba yuko ziarani ng'ambo kuhemea vibaba. Kama chama kingekuwa na uongozi imara, sasa hivi Mwigulu angelazimishwa kujiuzulu au kufukuzwa ili kulinda heshima ya chama. Na kama tungekuwa na polisi huru na si polisiCCM wa sasa huyu naye angekuwa ndani kama mtuhumiwa mkuu wa mchezo huo mchafu. Akina nape na kundi lake wangeonywa ili waache siasa mufilisi za ukabila, udini na ukanda. Nimekuwa najiuliza hivi Nape anapohubiri kuwa CHADEMA ni chama cha wachaga, anakuwa anawapa ujumbe gani wachaga ambao ni wanaCCM? Kuwa waondoke CCM? Na hivi majuzi alikuwa Moshi. Je alikwenda kuongea na wanaCHADEMA au CCM? Anapodai kuwa CHADEMA ni chama cha kanda ya kaskazini, je wanaCCM wanaotoka kanda hiyo anawapa ujumbe gani? Au anapodai CHADEMA ni chama cha kidini yaani wakristo, je wakristo waliopo ndani ya CCM akiwepo yeye mwenyewe ndio kusema waondoke waende CHADEMA?

CHADEMA ni chama halali kilichosajiliwa baada ya kukidhi taratibu na sheria za nchi na ndio maana hata Jakaya Mrisho Kikwete alijiandaa kujiunga nacho kama angetoswa kupitishwa kugombea uraisi kupitia CCM. Vile vile Nape mwenyewe aliomba kujiunga nacho wakati wa matatizo yake na UVCCM wakati ule.
-------------------------------------------
Mwanzoni baadhi ya wanaCCM walidhani wamepata mwanasiasa hodari kijana wakuweza kukinusuru chama chao lakini kadri siku zilipozidi kwenda ndivyo matumaini yao yakazidi kupotea kwa mtu anayeitwa Mwigulu Nchemba.

Mwigulu kwa sasa ni naibu katibu mkuu wa CCM Tanzania bara, amekuwa akifanya siasa kwa mtindo wa UMAFIA, MATUSI, HONGO na PROPAGANDA CHAFU kwa nia ya kujaribu kupambana na CHADEMA chama ambacho kinajaribu kufanya siasa zake kwa mtindo wa kimageuzi(Tafiti, Hoja, Mijadala na Harakati).

Mpaka sasa hakuna dalili yoyote kwamba mtindo huo wa Mwigulu kama unaweza kuzaa matunda chanya kwa CCM.
Kwa sasa kuna baadhi ya makada wa CCM wameanza mkakati wa chini kwa chini mjini Dodoma kukishawishi chama kimweke Pembeni Mwigulu kwani amekuwa akifanya siasa zenye kukipa sura mbaya CCM mbele ya jamii.

Mara ya mwisho kwenye kikao cha ndani cha juu cha CCM inadaiwa Mwigulu alilalamika sana kwa kitendo cha viongozi wenzie wa CCM kumwacha bila msaada wakati akipambana na Sakata la Lwekatare kisheria.

Kwa sasa Mwigulu yupo ziarani katika mikoa mbalimbali akiambatana na vijana watatu('Wacheza shoo wa Mwigulu'), wawili walifukuzwa CHADEMA na kisha kuhamia CCM na mmoja ni kijana aliyemwagiwa tindikali kule Igunga.

Kumekuwepo na Sintofahamu ktk ulingo wa siasa baina ya CDM na CCM mara tu baada ya kuteuliwa hapo mwaka jana MWIGULU MCHEMBA kuwa Naibu katibu mkuu wa CCM. Hii ni kutokana na ndugu Mwigulu kuacha Siasa za Kistaarabu na badala yake kuamua kufanya siasa chafu na za kipumbavu dhidhi ya CDM na viongozi wake. Tumeshuhudia mwigulu akiwatumia baadhi ya watu ndani na nje ya CDM kuhakikisha kwamba anaichafua Chama cha Chadema na viongozi wa juu wa chama hicho ili tu kukifanya kichukiwe au kisusiwe na Watanzania.

Mara tu baada ya mbinu yake chafu ya kukihusisha chadema pamoja na Mwenyekiti wa ulinzi na usalama wa CDM ndugu LWAKATARE NA UGAIDI kufeli, Mwigulu alihakikisha kua bado atatumia mbinu mbadala kuihusisha CDM na Ugaidi,na ndipo alipo mchukua kijana musa na kumtembeza ktk mikutano ya siasa kama ile SANAMU maarufu miaka ya 90 kwa jina la JOYCE WOWOWO! kuvutia watu na kuwaeleza kuwa hali aliyonayo ni CDM ndio waliomfanyia hivyo.

Hiyo haikutosha tangia ujio wa huyu bwana mkubwa Mwigulu jijini Arusha,kumekuepo na fujo za hapa na pale dhidi ya Wafuasi na Wapenzi wa CDM ukifanywa na vijana wa CCM maarufu kama Green guard! Yote haya yanafanyika aidha kwa Maelekezo au kwa Amri ya Mwigulu. Leo ktk kuhitimisha Mkutano wa kampeni kwa CDM tumeendelea kushuhudia Umwagikaji wa Damu ktk mkutano huo kwa Watu watatu kupoteza maisha na wengine zaidi ya 60 Wakijeruhiwa.

Hadi sasa haijulikani ni nani karusha bomu hilo ktk mkutano huo wa CDM na katumwa na nani na kwa sababu zipi! Siku zote lengo la Mwigulu kwa CDM ni kuwahusisha na Mabaya lakini pia akihakikisha kwamba watanzania hawataiamini Cdm na kuwa kitakosa wafuasi.
Cdm kwa mkoa wa Arusha especialy Jimbo la Arusha mjini hawana upinzani kwa Ccm na kuwa mikutano yake yote huudhuriwa na Watu wengi ambao huja wenyewe ukilinganisha na CCM ambao hutumia Wanamuziki wa Bongo fleva na kuwalipa vijana wa Boda boda 20,000 kwa siku ili washiriki ktk mikutano yao.

Pamoja na haya yote lakini bado Mikutano ya Ccm haiudhuriwi na watu wengi kama mikutano ya CDM. MWIGULU alishuhudia haya yote kwa siku ambazo amekuepo jijini Arusha.mbinu aliyobaki nayo baada ya kushindwa ktk jukwaa la siasa ni kutumia UMAFIA kama ambavyo tumeshuhudia leo ktk viwanja vya SOWETO.

Najiuliza kuwa Mwigulu anafanya haya yote kwa manufaa ya nani? Ndio maana nathubutu kusema Tanzania kwa sasa akuwepo Mwigulu sio sehemu salama ya kuishi.

WARAKA WA WAZI KWA Mwigulu Nchemba Nape Moses Nnauye na Mtela Mwampamba

CCM 'INAANGUKA' KWA KUACHA MISINGI YAKE NA MALENGO YAKE YA KUANZISHWA.

Chama Cha Mapinduzi CCM kipo katika hata ya kuanguka kwa kuacha misingi yake ya kuanzshiswa na hasa suala la kutumia Rasilimali watu katika kujenga Nchi na Chama,

Kwa siku za karibuni nimekuwa nikishangazwa sana na VIONGOZI wa sekretarieti ya CCM kina Nape na Mwigulu Nchemba Kushindwa kuitumia vyema rasilimali watu ya Vijana wa CCM katika kukijenga Chama.

CCM kwa mda mrefu kina utaratibu wa kuandaa VIJANA WAKE Chipukizi Kijana na UVCCM, Na pia kuwaandaa makada wake kupitia mafunzo maalumu ya ITIKADI kama kwenda Ihemi, KIVUKONI, Na hata wengine walienda URUSI Kujifunza ukada.

Cha ajabu ni hii CCM ya leo inayoweza kumwokota mtu leo barabarani na kesho akawa ndio 'KADA NA KINARA WA KUINADI' Wakati hajui hata misingi ya Kuanzishwa CCM wala hajui hata nini majukumu ya CCM kama Chama tawala.

NAANDIKA WARAKA HUU KWA KUWALENGA MOJA KWA MOJA VIONGOZI WA CCM WA JUU,
KUANZIA KINANA-KATIBU MKUU, MWIGULU NA NAPE,

Hawa ndio wamekuwa Vinara wa kufanya mikitano ya Chama na kuwapandisha juu kina Mtela Mwampamba ambao kazi yao kubwa ni kueleza madhambi na mabaya ya Chadema na kuacha kukijenga chama na kukieneza.

Cha kusikitisha badala ya watu kupongeza utaratibu huo kuishia kuuponda kwa sababu hauwasaidii wananchi na wana CCM waliokipa kura Chama 2010.

Mfano jana Mtela Mwampamba kaweka post ya kizushi juu ya mgombea udiwani wa Chadema kuhamia CCM hata kama ni kweli lakini kwa jiansi alivyoliripoti ni wazi Mtela alilenga kuuvuruga ule mapango.

MAONI YANGU YA JUMLA KWA WOTE.

CCM itumie VIJANA wake na makada waliokulia ndani ya chama ili kukisaidia kuendelea kuwepo.

CCM Iachane na mpango wa kukutana na mtu barabara anapewa kadi leo kwa makosa aliyofanya kwingine na ahuku anakuwa ndio shujaa wetu na kuwa tegemeo letu.

CCM iendeleze utaratibu wa kuwaandaa MAKADA wake kupitia mafunzo wa kiitikadi kama ya IHEMI.

VIJANA wa CCM JITOKEZENI BILA WOGA KUKEMEA KINACHOFANYWA SASA KWANI HAKILENGI KUKISAIDIA CHAMA NA HASA UZUSHI NA MATUSI BINAFSI KWA VIONGOZI WA UPINZANI.

VIJANA WA CCM nyinyi ndio jukumu lenu kukisemeo chama na msiwaachie wapita njia na waliokutana na chama barabarani.

Na mwisho kwa Mtela Mwampamba kaka kaa tulia jifunze SIASA na ujiue nini kati ya CHAMA TAWALA NA CHAMA CHA UPINZANI CCM ni chama tawala kwa hiyo kazi yake ni kutekeleza ahadi. KAZI KWANZA NA SIO UZUSHI NA KUILAMU CUF NA CHADEMA.

Na mwisho niwaombe radhi kwa mliokerwa na kila aina ya Uzushi unaojitokeza kwenu.

ASANTENI SANA NAOMBA ALIYE KARIBU NA KINANA, NAPE NA MWIGULU WAWAPE HUU UJUMBE NIMEUANDIKA KWA MASLAHI YA CHAMA.

WATAFAKARI UPYA NAMNA YA KUTUMIA RASILIMALI WATU YAANI VIJANA WA CCM MAKADA WLIOKULIA NDANI YA CHAMA.

ASANTENI SANA.
- with Ally Salum Hapi and 31 others at Ccm Lumumba.

Ndugu zangu wanajamvi ninaomba niwashirikishe tafakuri yangu juu ya usaliti wa vijana. Mimi ni kijana ambaye kwa kweli huwa ninapenda kukisimamia kile ninachokiamni kuanzia mwanzo mpaka mwisho. Hapa ndio msingi wa tafsiri yangu ya usaliti. Kwa tafsiri yangu usaliti ni kitendo cha kwenda kinyume na makubaliano ya pamoja iwe ni katika mapambano, harakati au suala lolote la kimaisha. Usaliti hapa unaweza kuwa kati ya mtu mwenyewe na nafsi yake au mtu na mtu mwingine au mtu na kundi jingine.
Ninawatumia hawa ndugu wawili Mtela na Juliana kama tu kielelezo cha usaliti wa vijana. Ni imani yangu kuwa kwa mujibu wa tafsiri yangu ya usaliti, wenye macho na akili ya kuelewa wanastahili kukub aliana na mimi kuwa hawa ndugu ni mfano mzuri wa usaliti unaofanywa na vijana wengi katika siasa.
Usaliti wa vijana hawa unatokana na ukweli kwamba kwa utashi wao wakiwa na akili timamu walijiunga na WANACHADEMA na CHADEMA Kwa maneno na matendo mbalimbali kuonesha uchafu na uovu wa CCM (Walionesha kukerwa na kuichukia CCM). Huenda (Sina uhakika) wakati mwingine walifanikiwa hata kuongeza baadhi ya wanachama wapya. Wananchi wa Mbozi wenye hamu ya mabadiliko waliwaunga mkono vijana hawa kwa matumaini ya kupambana na hatimaye kuiondoa CCM kwa njia ya kidemokrasia. Wengi waliamini na walidhamiria kumuunga mkono kijana Mwampamba. Kijana huyu na ndugu yake Shonza walisema mengi kuhusu udhalimu wa CCM. Maneno yao yalionesha kweli vijana hawa wanaichukia CCM na upuuzi wake wote. Wakati mwingine waliongea mpaka kulia (yaani kutoa machozi). Hali hii ilijenga imani kwa wananchi ambao wanayatafuta mabadiliko ambayo hayawezi kuletwa na CCM. Jambo hili liliwahi kusemwa na Mwalimu Nyerere wakati akiwahutubia wajumbe wa mkutano mkuu wa CCM Taifa mwaka 1995 Huko Dodoma. Mwalimu alisema "watu sasa hivi wanataka mabadiliko na kama hawatayaona ndani ya CCM potelea mbali wataamua kuchagua hata upinzani"
Kutokana na jinsi watu walivyokuwa wakiitikia katika mikutano ya vijana hawa walijisahau wakajenga kiburi na kuona kwamba wao wanakubalika zaidi kuliko taasisi yao yaani CHADEMA. Kosa walilolifanya ni kushindwa kuelewa kuwa kwa sasa watu wanachokitaka ni mabadiliko na mabadiliko hayo hayawezi kuletwa na CCM bali ni upinzani. Kosa hili kwangu ninaliona kama chimbuko halisi la usaliti wa vijana wenzetu hawa. Vijana waliota jeuri na kuamini wao ni CHADEMA NA CHADEMA ni wao na bila wao hakuna CHADEMA. Tatizo hili linawatafuna vijana wengi sana, hawa ni mfano tu.
Kama ambavyo inaeleweka kuwa dhambi moja (usaliti) huzaa dhambi nyingine, kiburi chao kilisababisha kukosa utii kwa kisingizio cha demokrasia ndani ya chama na hivyo waliamini kabisa kuwa wapo huru kusema lolote sehemu yeyote na wakati wowote. Dhambi hii nayo ilifanikiwa kuleta dhambi nyingine ambayo ni kuwa tayari kununuliwa ili watumike kama vipaza sauti vya waliowanunua. Jambo hili ni la kawaida katika maisha kwani hata wahenga walisema "Alimpaye mpiga zumari ndiye huchagua wimbo"
Kutokana na mabadiliko ya kiuongozi ndani ya CCM, Kiliingia kikundi kinachoamini katika fanya lolote maadamu ushindi upatikane (iwe ni kuua, kutesa, kuleta hofu, kuiba, kutumia pesa, kuchonganisha, kuchafua watu wengine n.k). Hii kwa sasa ni sawa na Kashifa ya "WATERGATE" ambayo ilisababisha raisi wa Marekani Nixon ajiuzuru kutokana na siasa za kimafia dhidi ya wapinzani wake wakuu kutoka katika chama cha "Democratic" (Jambo hili nitaliandika makala yake kuonesha namna CCM na Mwigulu walivyoingia katika siasa za namna hii). Huu ni mfano tosha wa namna ambavyo CCM nao waliitumia nafasi ya uasi na kiburi cha hawa vijana kuwatumia ipasavyo. Kama ni pesa si tatizo kwa siasa iliyopo CCM. Vijana wakajikuta wapo tayari kufanya lolote kutokana na kuwa na bei. Vijana wakajikuta wakisaliti nafsi zao na kuamua kusema wasichokiamini maadamu wameagizwa. Ghafula, vijana walioaminiwa na wananchi wakaanza kuropoka (si kusema) mambo ambayo ni kinyume na walichokuwa wakikiamini. Je kwa hali hiyo unaweza kusema ni nini? Je labda ni utashi wao tu kuwa kwa sababu mwanadamu anabadilika na wao labda waliamua tu kutoka ndani ya mioyo yao? Jibu hili mimi siwezi kuliafiki kutokana na mtiririko wa matukio na ushahidi wa kimuktadha. Niliamua kuhitimisha kabisa kuwa huu ni usaliti na si vinginevyo. Hauwezi kutoka upinzani ukaenda CCM chama ambacho umekirushia matusi mengi katika muda mwingi wa siasa hususani ulipokuwa upinzani. Angalau wangeenda chama kingine cha upinzani na wakaendeleza ukali waliokuwa nao dhidi ya ccm na huku wakionesha yale ambayo wametofautina na CHADEMA walau wangeeleweka. Ila kwa sasa ninasimamia kabisa kuwa huu ni usaliti. Wamesaliti nafsi zao, watu waliowaunga mkono, pamoja na chama chao kwa ajili tu ya kutaka mafanikio ya kimaisha ya haraka. Ninaomba niwaeleze vijana hawa na vijana wenzangu wote kuwa hakuna njia ya mkato katika maisha. Maisha ni subira na maisha ni kujituma kwa bidii zote katika kile unachokiamini.
ATHARI YA TABIA YA VIAJANA HAWA
Athari kubwa kabisa ambayo vijana hawa na vijana wengine wa aina hii wanayoileta kwa vijana wote ni vijana kuwekwa katika kundi la kutoaminika. Kutokana na tama za kijinga kabisa za vijana hawa huenda huko mbozi vijana wenye mapenzi ya dhati ya kuomba uongozi kutoka kwa wanachi msiaminiwe tena. Pia hali hii imesababisha vijana kuonekana kuwa ni watu wa bei rahisi na wenye maamuzi ya kukurupuka katika maisha yao. Hii ni kutokana na ukweli kwamba siku za mwampamba na shonza zinahesabika katika medani za kisiasa na kuna uwezekano mkubwa wakajutia jambo hili katika maisha yao yote ya siasa. Uwezekano wa vijana hawa kujutia ni kutokana na viashiria vifuatavyo:
Mosi ni suala la historia, miaka yote CCM huwa inaonesha kumthamini mtu pale inapoamini kuwa mtu huyo anauwezekano wa kuinasua pale inapoelekea kuzama. Hebu jitafakari na muone hadhi ya Tambwe Hiza CCM je inaendelea kupanda au kushuka? (amegombea cheo gani akashinda ndani ya CCM?) Jikumbusheni yule mwanamke aliyeitwa kama niunakumbuka vema Angelina. Mwanamke huyu alitumika kudhalilisha utu wake kwa ajili ya kumchafua Mrema (akisema kuwa amezalishwa na Mrema na kutelekezwa). Baada ya kazi yake kuisha hivi mnajua ni mambo gani yalimkuta mwanamke huyu? Kwa mfano wa hivi karibuni kabisa yupo ndugu yetu Mahimbo ambaye aliamua kudhalilisha utu wake pamoja na watoto wake kabisa kwa jambo ambalo alikuwa analielewa vema kabisa. Baada ya kazi kuisha Mahimbo kaachwa jinsi alivyo. Orodha ni ndefu sana ya watu waliotumika na kutupwa baada ya kazi waliyotumwa kuisha au kutokamilika ilivyotarajiwa.
Pili ni suala la kushindwa kuonesha msaada wowote wa maana kwa CCM. Ninaomba mzidi kujitafakari wenyewe zaidi ya ndugu mmoja kutumika kama kiburudisho au wengene hapa katika jamvi wanavyosema uwanja wa mazoezi wa savimbi. Je kuna jambo lolote la maana mablo mmeisaidia CCM? Katika hoja hii hapa ndio kifo chenu cha kisiasa kilipo. Mwampamba binafsi nilimuambia jambo hili facebook badala ya kunijibu kwa hoja akaamua "kuniblock". Chaguzi hizi za udiwani katika kata 26 zinawaweka katika mazingira mabaya sana ya kufanyiwa tathmini. Mmepoteza mpaka kata ya nyumbani kwenu Mbeya huu ni upuuzi wa hali ya juu. Hivi ni nani atakayeendelea kuwapa posho nono bila matokeo chanya? Labda kama mtaanza kazi nyingine kwa mwanvuli wa siasa ndio itawapatia posho!
Tatu ni kushindwa kuleta athari tarajiwa kwa chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA). Kumbukeni kuwa huu nao ulikuwa ni wajibu wenu mkubwa sana. Hebu jiulizeni ni athari ipi ambayo mnaweza kujivunia kuwa mmeisababishia CHADEMA? Hebu jiulizeni tu hata kupitia marafiki zenu mliokuwa nao FB wakati mkiwa CHADEMA je ni nani aliamua kuwaunga mkono? Kwa sababu kila "mnachoposti" katika facebook kinashambuliwa vikali na marafiki zenu mpaka mmeamua kublock watu wote mnaowaona hawaungi mkono ujinga wenu. Mbaya zaidi hakuna zaidi ya hoja ya kutukana viongozi wa CHADEMA. Pia ninyi mkitukanwa midomo inarefuka sana. Sasa jitafakarini na chukueni hatua kabla hamjatupwa katika chombo cha takataka.
NNe ni kukabiliwa mapambano kutoka kwa vijana maslahi na vijana wazalendo wa CCM. Wengi wanalalamika huko iweje watu ambao hawaijui hata CCM kuja tu na kuanza kufaidi matunda ya ufisadi wa muda mrefu wa chama cha mapinduzi. Vijana hawa hawapo tayari kuona mkiendelea kupata posho. Kwa bahati mbaya sana, sasa hivi wana hoja za kutumia kuwaengua. Hii kwa kweli inakatisha tama watu wajitoe kwa muda marefu wakiamini kuwa wao ndio vijana wa chama halafu mgeni tu aje na kuanza kufaidi huku wao wakiambiwa kuwa subirini hawa tunawatumia tu kukamilisha malengo maalumu. Tatizo ni kwamba malengo maalumu yanaonekana kuzaa matunda hasi. Hii ni kutokana na ukweli kwamba toka mmejiunga na timu ya kampeni ya CCM mmesababisha sijui CCM kupoteza viti vingi zaidi pamoja na kura kuzidi kupungua. Hili ni tatizo kubwa.
Tano ni tuhuma zinazowakabili kuwa ninyi ni mapandikizi ya CHADEMA. Tuhuma hizi zinapewa nguvu kutokana na hoja dhaifu mnazozitoa iwe ni kwa kujua ama kwa kutokujua. Hali hii inawaletea chuki miongoni mwa baadhi ya wanaCCM ambao bado wanaamini chama chao kinaweza kubadilika na kurudi katika misingi ya kuanzishwa kwake. Hoja hii inapewa nguvu na tuhuma ya Shonza kushushwa jukwaani huko Arusha baada ya kusema kuwa CCM ni chama cha mafisadi. Lakini pia hata bandiko lake la leo la kuifananisha CCM na mchicha dhidi ya CHADEMA. Kauli hii imeongeza mashaka ya wanaccm walio wengi. Watu (ccm) wanaamini kuwa ni ngumu sana mtu kuacha asili yake. Kinachoaminika kwa ccm ni pale tu mtu anapoondoka ccm na kuanza kuishambulia ccm kwa udhati hapo ndio wanajua kuwa huyo mtu amebadilika na utaona wanavyomuandama kwa mbinu halali na haramu ili kumuangamiza. Tafakarini sana jambo hili kwa umakini sana.
USHAURI KWA VIJANA
Ninatoa ushauri ufuatao kwa vijana wenzangu:
Mosi lazima tuelewe kauli ya Mwalimu Nyerere kuwa sasa hivi Watanzania wanataka mabadiliko na kama hawatayaona CCM watakuwa tayari kuchagua upinzani. Hivyo basi, Umaarufu tunaoupata ni kwa sababu watu wanataka mabadiliko ambayo wameona kuwa hayawezi tena kupatikana ndani ya CCM. Halii hii tuione kuwa umaarufu au uungwaji mkono tunaoupata katika vyama vya upinzani tulivyopo si kwa sababu kuwa sisi tunamvuto zaidi ya vijana wote bali ni kwa sababu tupo upande ambao umeaminiwa kuleta mabadiliko. Kama unabisha jifunze kupitia Shonza na Mwampamba na ujiulize je uungwaji walioupata wakiwa CDM bado unaendelea? Unadhani ni kwa nini? Jibu ni kwamba wamepishana na imani ya wananchi kuhusu mabadiliko.
Pili vijana tushinde vishawishi vya kupata pesa rahisi(za chee). Pesa za namna hii zinaendana na sisi kuwa tayari kununulika na kutumiwa kwa urahisi sana.Tuna haja ya kulinda utu wetu na wa wale wengine wote walionyesha kutuamini. Mapambano ya kumuondoa mkoloni mweusi si rahisi na wala si ya siku moja. Kama umedhamiria kuwasaidia wananchi kuyapata mabadiliko wanayoyatarajia ambayo wameshindwa kuyapata kupitia CCM ni lazima uwe imara na uikane nafsi yako. Kuwa tayari kupitia shida na magumu mengi kutoka kwa mkoloni mweusi CCM. Tofauti na hapo ni kweli utapata pesa ya haraka lakini ambayo itagharimu utu wako na maisha yako kwa jumla. Usaliti wa namna hii unaharibu mpaka kwa ukoo wako wote kwani unawajengea mazingira magumu hata watu waio na hatia ambao wapo katikia familia au ukoo wako. Tujichunguze zaidi kama vijana kupitia hawa Shonza na Mwampamba.
Tatu hususani vijana wa kike kuweni makini sana na kuingia katika siasa kwa kutumia mgongo wa sura au urembo. Historia inaonesha kuwa hakuna aliyewahi kudumu katika siasa kwa kutumia urembo wake. Sanasana utatumika tu kama uwanja wa mazoezi na wakati ukikutupa nawe ndio hivyo siasa basi tena!
Nne vijana tuepuka kuifanya siasa kama ajira. Msukumo wa kisiasa utokane na haja yako ya kukerwa na hali ya taifa kwa sasa. Kwa wale wa CCM wajikite kutetea mfumo uliopo (kama unaona unakunufaisha na kunufaisha wengine). Wale wanaotaka kwenda upinzani wajiulize kwanza kabla ya kuingia katika sisa jiulize je mfumo na hali iliyopo sasa kweli inakukera kabisa. Jibu likiwa ni ndio kutoka ndani kabisa ya moyo wako utakuwa umekaribia kuushinda usaliti unaotokana na vishawishi vya hapa na pale. Kama unakerwa kabisa haitakuwa rahisi ukijiunga na upinzani halafu baada ya mwaka unaenda CCM. Ukifanya hivyo tutakuita msaliti tu hatuna jina jingine.
Tano ni kuelewa kuwa CCM haijawahi kumtumia mtu muda wote. Utapewa pesa na CCM kwa muda mfupi na baada ya hapo utatelekezwa na hata ikibidi utauawa ili kulinda siri za maovu yote ambayo umetumikishwa kwa manufaa ya CCM. Kumbukeni kuwa CCM ina wenyewe!
USHAURI KWA SHONZA NA MWAMPAMBA
Sitonesha uzalendo na uungwana kama nitahitimisha bila kuwashauri nini mfanye. Kumbukeni huu ni ushauri mnaweza kuufanyia kazi au kuuacha. Fanyenni lolote kati ya haya:
Mosi Jiondoeni katika siasa walau kwa muda. Hii itasaidia kulinda tu heshima na utu wenu kabla CCM hawajawatupa. Huu ni ukweli mchungu lakini kama vijana wenzetu ni lazima muelewe huenda mkawa na maisha marefu. Katika maisha haya nafsi zenu zitawahukumu kwa usaliti lakini pia mtaumia kutokana na usaliti ambao CCM watawafanyia muda si mrefu. Msisubiri kufukuzwa someni majira ya wakati. Hata katika mahusiano ya vijana ukiona mwenzio haeleweki usisubiri mpaka akuambie kuwa mimi sikutaki tena. Hii kidogo italinda utu wenu badala ya kusubiri kutelekezwa na posho kuyeyuka. Hebu muulizeni Tambwe Hiza kwa mara ya mwisho ni lini amepata posho kama mliyopata katika uchaguzi wa huu udiwani wa hapa majuzi? Historia inatabia ya kujirudia!
Pili ni Kujiondoa CCM na kurudi CHADEMA mkatubu madhambi yote na kuomba msamaha na muombe kabisa kuwa ni watu wa kawaida kabisa. Mkifanya hivi ni kweli mtasamehewa lakini hakuna mtu atakayekuwa anawaamini kama mwanzo. Ila jambo la msingi mtalinda utu wenu kwa kiwango kikubwa. Hatari nyingine ya uamuzi huu unaweza kusababisha CCM kikawadhuru. Uzuri mmepata bahati kidogo ya kuona namna ambavyo CCM wanatumia njia halali na haramu kufanikisha malengo yao. Ila ninaamini kuna namna itakayowaepusha na hasira hizo za CCM
Tatu ni kuendelea kukaa CCM mpaka pale mtakapotelekezwa kabisa (hamtafukuzwa uanachama). Hali hii itawasaidia nanyi kuingia katika historia ya watu niliowataja na jamii haitawasahau kwa usaliti wenu. Pia mtafikia hatua ya kuanza kujutia yote ambayo mliyafanya lakini hamtakuwa na nafasi wala ujasiri wa kuomba kusamehewa.
HITIMISHO
Ndugu zangu hii ni tafakuri yangu kuhusu kuhusu usaliti wa vijana katika medani za siasa. Ni muhimu tukumbushane, tuonyane, na turekebishane ili kujenga taifa lenye nidhamu na lenye mshikmano katika mambo ambayo kama taifa tuna amini kwa pamoja. Usaliti unaotokana na kununuliwa ni hatari kwa maslahi ya taifa.

MATUKIO ya kikatili yanayofanywa na vyombo vya ulinzi na usalama dhidi ya wananchi wasiokuwa na hatia kwa kisingizio kuwa ama wameamua kuandamana au wamekusanyika kwenye mikutano isiyokuwa na kibali hakutoi adhabu mbadala ya watu kupigwa risasi za moto.

Kushamiri kwa vitendo hivyo dhidi ya makundi ya raia kunaonyesha hofu na mashaka makubwa kwa jumuiya zote za wapenda haki na amani na ni nadra sana kukubali kuwa haki ya msingi waliyonayo walinzi wa amani ni kuona wananchi wakiumizwa.

Kadiri miaka inavyozidi kwenda kuna kila dalili za wazi kuwa matukio mengi yanayotokea yanasukumwa na utashi wa kisiasa. Mifumo ya kisiasa inayotumiwa na chama tawala kikiiongoza serikali yake kuadhibu wananchi kunaleta mtazamo mbaya.

Wananchi wanashuhudia matukio ya kutisha, wanaona jinsi wenzao wasiokuwa na hatia wakiuawa kwenye mikusanyiko ya amani na vyombo vya ulinzi na usalama vikihusishwa moja kwa moja na mashambulio hayo.
Kuwa matukio mengi ni ya kupangwa na yanayoshinikizwa kwa nguvu za kisiasa bila kujali ulinzi na usalama wa wananchi walioamua kukusanyika pamoja kufanya mikutano yao kwa amani na utulivu.
Risasi za kisiasa zinatumika hovyo ili kuwadhuru wananchi wanaoonekana kuwa na misimamo tofauti dhidi ya chama tawala na serikali yake, wanaoona kuwa hawatendewi haki wanapoamua kudai haki zao kwa njia ya majukwaa ya kisheria, wanapigwa na kujeruhiwa.

Inawezekana kwa kiasi kikubwa serikali inajitia doa kubwa kutoka kwa watendaji wa vyombo vya ulinzi na usalama ambao hawaipendi serikali iliyopo madarakani na kwa makusudi nao wanaona inafaa kuwadhuru watu ili kujenga chuki dhidi ya mamlaka.

Si jambo la kubeza au kutupiana mpira kwa mtindo ulioanza kuwadhuru viongozi wa dini, wanaharakati na wananchi wasiokuwa na hatia kwa sababu hawana mwelekeo wa kukubali uongozi na mfumo wa kiutawala uliopo.

Viongozi wa dini, wanaharakati, wanahabari na wengine waliouawa kwenye mikutano ya siasa bado haijulikani waliohusika walitumwa na nani na pia anayeratibu utitiri wa matukio ya kinyama dhidi ya wapigania haki.

Naita risasi za siasa kwa kuwa matukio mengi ya watu kuuawa yanajitokeza kwenye harakati za siasa na huko ndiko zana za kijeshi hutolewa kwa lengo la kulinda na kuzuia harakati hizo.
Kwa hali waliyonayo Watanzania, kwa jinsi wanavyopenda amani, wanaishi kama ndugu na marafiki. Watanzania sio watu wa kuuana wenyewe kwa wenyewe hasa ikizingatiwa kuwa idadi yao kubwa hawamiliki silaha.

Wananchi wanaokwenda kwenye mikutano ya vyama vyao vya kisiasa hawabebi mabomu na risasi za moto. Wanaowajibika kubeba zana hizo ni wana usalama.
Tumeshuhudia wenyewe nyumba za ibada zikichomwa moto na watu wasiojulikana, lakini wapo viongozi wa kisiasa wanaoingia kwenye nyumba hizo hizo kutaka kujijenga kwa waumini wa madhehebu hayo hayo kwa lengo la kuusaka urais.

Tumeshuhudia viongozi wa dini wakiuawa na kumwagiwa tindikali, wanaofanya vitendo hivyo wapo na vyombo vya ulinzi na usalama vipo, lakini watu hao hawashikiki na wanasiasa wanaoutaka urais nao wanapita humo humo kwenye nyumba za ibada ambako viongozi wao wa dini wameuawa na kumwagiwa tindikali.

Haifurahishi na ndiyo maana nasema wazi kuwa risasi za siasa zinawaua watu wasiokuwa na hatia na ili kuweza kuondoa hali hii bado hofu na mashaka kunaongezwa na viongozi wanaotoa kauli zenye utata zinazoshinikiza vyombo vya ulinzi vipambane na raia wanaopigania haki na maslahi yao kwa njia za amani.

Kauli hizo zinasababisha risasi za siasa zitumiwe vibaya dhidi ya wananchi badala ya kutumika kupambana na majambazi, wawindaji haramu wa wanyama wetu (majangili) na maharamia. Kinyume chake risasi hizo zinatumika mchana kweupe kuwadhuru wananchi wasiokuwa na hatia.
Kwa kuwa nchi yetu imejaliwa kuwa na viongozi wanaowapenda wananchi wao wakati wa kampeni za uchaguzi, basi ipo haja wakatambua kuwa kila mwananchi aliyethubutu kunyanyua mguu wake, kupanga foleni na kuamua kupiga kura thamani yake ni kubwa na zawadi waliyostahili kupewa si risasi na mabomu au kumwagiwa tindikali.

Kubariki matumizi ya risasi za moto kwenye mikutano ya hadhara na kwenye maandamano kunazidi kuitia doa serikali, hasa ikizingatiwa kuwa haijawahi kutokea wananchi wakafanya vurugu kwa kudhamiria ili wapigwe risasi za moto.

Ipo haja serikali ambayo ndiyo mmiliki vya vyombo vyote vya dola ijaribu kuangalia mifumo ya kiutendaji na mianya inayotumiwa na watendaji wake ili kuwadhoofisha wananchi. Hakuna sababu ya kuwafanya wananchi waanze kuishi kwa woga ndani ya nchi yao.

Hakuna sababu za msingi zinazowafanya wananchi wajenge uhasama mkubwa kati yao na vyombo vya ulinzi na usalama. Yaliyotokea Mtwara wananchi wanajua jinsi risasi za kisiasa zilivyotumika, waliouawa Arusha wananchi wameshuhudia jinsi risasi za moto na mabomu yalivyotumika hadi makanisani.
Waliouawa Morogoro wananchi walishuhudia jinsi risasi za kisiasa zilivyotumika na maajabu ya Nyololo yaliyosababisha mwandishi wa habari wa Channel Ten, Daudi Mwangosi auawe. Wananchi wanajua jinsi bomu la siasa lilivyotumika kumuua Mwangosi.

Sasa tutaendelea kuuana hadi lini? Ikumbukwe kuwa chama chochote cha siasa kinaweza kuondoka madarakani, lakini si rahisi kwa watumishi wote wa umma walioajiriwa wakafukuzwa kazi baada ya chama walichokuwa wakikitetea kwa risasi kitakapoondolewa.

Si rahisi wanachama wa chama kilichokuwa kikishika dola kinapoangushwa, wanachama hao wakafukuzwa nchini bali wataendelea kuwepo na watageuka kuwa wanachama wa chama cha upinzani dhidi ya chama kingine kitakachofanikiwa kushika dola.

Kwa maana hiyo na kwa mazingira ya demokrasia na utawala bora hakuna sababu wala tija yoyote ikiwa chuki za kisiasa zitapandikizwa kwa wananchi wanaoishi kwenye nchi moja.
Kitendo cha vyombo vya ulinzi na usalama kukikumbatia chama kimoja cha siasa kwa hofu ya kupoteza ajira zao, kunawapaka doa la damu watendaji hao ambao wametoka kwenye nyumba zenye heshima, wamezaliwa kwa ajili ya kumtumikia Mungu na wanadamu.

Hakuna kiongozi wa kisiasa wala serikali aliyezaliwa na shetani ili atende unyama dhidi ya wenzake, kuua raia wasiokuwa na hatia kwa ajili ya kutekeleza matakwa ya kisiasa, kwa vile hiyo ni dhambi kubwa mbele ya Mungu na mshahara wa dhambi ni mauti.
 
...mwigulu,nape,shonza,lukosi na mwampamba ni safu ya kampeni ya mgombea urais ajaye kupitia ccm chini ya uongozi wa kinana a.k.a mzee wa tembo na mangula a.k.a bwana harusi...
 
Pro CHADEMA mkiyasikia/kuyaona hayo majina mnahisi kushikwa na PepoPunda.

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Pro CHADEMA mkiyasikia/kuyaona hayo majina mnahisi kushikwa na PepoPunda.

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums

Wakati flani inafaa kuweka ushabiki na mahaba kando na kujipa nafasi ya kuchambua hoja zinazoletwa na wale tusiokubaliana nao kimtazamo labda katika yale wanayoyasema tutajifunza jambo kuliko kuweka mbele ushabiki ambao utatupoteza.
 
Pro CHADEMA mkiyasikia/kuyaona hayo majina mnahisi kushikwa na PepoPunda.

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums


Hii kitu ndio inaharakisha kifo na maziko ya CCM....Nyie hawa jamaa mnaona wanawasaidia sana?! mmefanya tathmini isiyo na makengeza?
 
CCM hakifi lakini cha moto itakiona itakapokuwa upande wa upinzani pamoja na makinda wao na naibu wake. Wewe subiri tu. SI unaona chama kilichokuwa tawala Zambia, Malawi na Kenya vinavyohaha hivi sasa? Siasa bwan, weacha tu.
 
Wakati flani inafaa kuweka ushabiki na mahaba kando na kujipa nafasi ya kuchambua hoja zinazoletwa na wale tusiokubaliana nao kimtazamo labda katika yale wanayoyasema tutajifunza jambo kuliko kuweka mbele ushabiki ambao utatupoteza.

Mkuu Baba V, heshima yako.

Hawa watu mimi wananishangaza sana. Watu wakiziweka kasoro/mapungufu ya Dr. Slaa wanachokimbilia kusema ni Dr. Slaa ni dawa ya CCM ndiyo maana hatuachi kumtaja.

Siku za hivi karibuni hayo majina yaliyotajwa na mwanzisha thread hayaachwi kutajwa humu kila siku which means ni dawa ya CHADEMA.

Au unataka kuniambia akishutumiwa/kutajwatajwa kiongozi wa CCM shutuma zinakuwa ni za kweli ila akishutumiwa/kutajwatajwa kiongozi wa CHADEMA yeye anakuwa ni dawa ya CCM?

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:
Msaliti ni Msaliti tu hata ukimvika ngozi ya kondoo. Hivi unategemea Shonza na Mwampamba wakikosa wanachokitafuta CCM wataendelea kuwa CCM. Mwampamba asau kupata ubunge Mbozi, labda arudi kwa mababu zake Umalila.
Njaa inawasumbua.
 
Hii kitu ndio inaharakisha kifo na maziko ya CCM....Nyie hawa jamaa mnaona wanawasaidia sana?! mmefanya tathmini isiyo na makengeza?

Wanatusaidia sana ndiyo maana mnalialia kila siku hapa Jukwaani kuhusu wao.

Ukisikia yalaaaaaah!...........

Mkipigwa kombora moja chama kinatetereka kuamka ni hadi ipite miezi mitatu, nyie mngekuwa ndiyo CCM hayo makombora inayorushiwa si mngekuwa mmeshagawana hela za ruzuku na furniture za pale makao makuu ili kila mtu afe na chake chama kifie mbali?

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Kwa kuwa ni wa CCM serikali haitawachukulia hatua mpaka wajitokeze wengine wa upinzani wafanye kama hawa vijana ndio serikali itaamka usingizini na kufanya kuchukua hatua. Refer Saga la uchochezi wa kidini na kufungiwa kwa Radio Imaan na Radio Neema.

Kwa nini tunasubiri matokeo badala ya kutibu mzizi ilhali dalili ziko wazi?!!! Nachoka kabisa
 
Inasikitisha sana majukwaa ya siasa yakitumiwa kugawa watu kisekta,kikanda,udini na ukabila hizo zilikuwa tunu za nchi kwamba tuliweza kuuwa kwa kiasi kikubwa tofauti za kidini,kikabila,kikanda ndio maana kwa kiasi kikubwa tumeishi kama familia moja.Kosa kubwa sana kwa mwenyekiti wa CCM kuendekeza hizi siasa ni mbaya nchi yetu kubwa sana ikitokea tukagawanyika kwa mtindo huo itakuwa ngumu kutawala na kujiletea maendeleo,Jakaya Kikwete aache kushadadia ugawaji wa waannchi kimafungu ili MACCM yaendelee kutawala ,ni mbaya ,tena mbaya,maumivu yake yatatuchukua miaka kuyamaliza
 
...mwigulu,nape,shonza,lukosi na mwampamba ni safu ya kampeni ya mgombea urais ajaye kupitia ccm chini ya uongozi wa kinana a.k.a mzee wa tembo na mangula a.k.a bwana harusi...

Wakitumika hawa kwenye kampeni CCM itaangukia pua vibaya mno kwenye uchaguzi. Ikifika saa nne asubuhi siku ya uchaguzi nchi itakuwa imerudi mikononi mwetu toka kwa hawa dhalimu wa CCM. Kampeni za uchaguzi ni kueleza utafanyia nini wananchi, CCM itamtumiaje mtu anayemta Dr Slaa mara mia tano kwa siku??
 
Wakitumika hawa kwenye kampeni CCM itaangukia pua vibaya mno kwenye uchaguzi. Ikifika saa nne asubuhi siku ya uchaguzi nchi itakuwa imerudi mikononi mwetu toka kwa hawa dhalimu wa CCM. Kampeni za uchaguzi ni kueleza utafanyia nini wananchi, CCM itamtumiaje mtu anayemta Dr Slaa mara mia tano kwa siku??
..hawajui kuishambulia chadema ni kuitangaza na kuisifia ni kuijenga..sijui watatokea wapi mafisadi..! mpaka kieleweke...
 
..hawajui kuishambulia chadema ni kuitangaza na kuisifia ni kuijenga..sijui watatokea wapi mafisadi..! mpaka kieleweke...

Sisi tuliosemea Marketing tunafurahishwa sana na tabia za hawa vijana wa CCM kuitangaza CHADEMA na Dr Slaa. Italipa sana kunako 2015 na kupunguza gharama za CDM kujitangaza.
 
Aliyeleta mada ameongea vizuri sana,ametoa makosa ya vijana wanaotumia vibaya majukwaa,ametoa angalizo kwa CCM na viongozi wake na kwao pia kwani AMANI na UMOJA wa Tanzania ni zaidi ya vyama.

Ninampongeza kwa mada nzuri na njema hakuzungumzia undani wa mtu amezungumzia matendo.Kabla ya kuwepo CHADEMA ilikuwepo CCM tu,yaani tulikuwa na siasa za chama kimoja.Na ni viongozi hawa hawa wa CCM waliona mbali kwa kukubali vyama vingi tujiulize leo kumetokea nini sarakasi hizi zinatokea?Kwa nini vyama hivi visipingane kwa hoja badala yake vinapingana kwa kutumia DINI,KABILA,UKANDA wa mtu anakotokea na baada ya kuona haya yote hayasaidii wameanza siasa chafu na mbaya za kubambikia watu kesi mbaya ambazo zinaondoa utu wa mtu.

Tujiulize kwa nini viongozi wetu wa serikali na chama tawala wamekuwa adui wa upinzani.Kumetokea nini?Tukipata majibu tutaweza kuepuka chuki miongoni mwetu.

Kitu kimoja kikubwa kilichotokea ni kwa viongozi kujilimbikizia mali kwa kupitiliza,kuuza ardhi ya wananchi wanyonge,kutumia jeshi (polisi) kwa manufaa ya uongozi na wala siyo watanzania.Tujiulize wanatuficha nini?Kwanini Watanzania tusiwe wamoja kupiga vita hali hii badala ya kutumia muda mrefu kupigana vijembe,matusi,kebehi na kudharauliana.Hivi Mkristu au Muislamu akifa ati sababu ya kuchinja tunapata faida gani?Kwa nini tugawanywe kama nyanya na vitunguu?Maana nafuu ya nyanya na vitunguu mwisho wa siku vinatengeneza mchuzi.

Rai yangu kwa watanzania na hasa Members humu tuwe Pro-Tanzanians na siyo Pro-CHADEMA au Pro-CCM jamani watu wa kawaida hatufaidiki na hali ya kisiasa iliyopo tunaumia na wenzetu wanachekelea wameshinda sana tu.

Ona watoto wa viongozi wapo nje kwenye shule na vyup vizuri,familia zao zinatibiwa hospitali zenye mazingira bora,masafi na yenye vitendea kazi vya kutosha.Mimi,wewe na familia zetu hatujui hata kula yetu kesho kama ipo.Hospitali kwa sasa tumeanza kwenda kwa waganga.

Tumpongeze mleta mada,tujadili hoja na si watu.Kama kuna mahali nimekosea naomba kusahihishwa na si kutukanwa.
 
Wanatusaidia sana ndiyo maana mnalialia kila siku hapa Jukwaani kuhusu wao.

Ukisikia yalaaaaaah!...........

Mkipigwa kombora moja chama kinatetereka kuamka ni hadi ipite miezi mitatu, nyie mngekuwa ndiyo CCM hayo makombora inayorushiwa si mngekuwa mmeshagawana hela za ruzuku na furniture za pale makao makuu ili kila mtu afe na chake chama kifie mbali?

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums

Ndivyo mnavyoitia upofu....CHADEMA inakua kwa spidi kubwa mno ukilinganisha ilhali CCM inazidi kuporomoka siku hadi siku. Wajinga ndio wali-wao!
 
Back
Top Bottom