Regia Mtema
R I P
- Nov 21, 2009
- 2,970
- 864
Wakuu leo tulikuwa tunafanya Mkutano Mkuu maalumu wa kumpitisha mgombea Urais na mgombea mwenza wa CHADEMA na kupitisha Ilani ya Uchaguzi 2010. Dr Slaa na Saidi Mzee Said wamepitishwa rasmi kupeperusha bendera ya CHADEMA.
Dr Slaa amehudhuria mkutano huu akitokea Hospitali alipokuwa amelazwa baada ya kufanyiwa upasuaji wa mkono wake. Baadaye alirejea tena hospitali kwa matibabu. It was so sad but it had to be that way..
Katika kikao hki tulialika wageni toka kada mbalimbali ikiwemo vyama vya siasa.
Kati ya Wageni waliohudhuria ni pamoja na kijana machachari aliyeangushwa kwenye kura za maoni za Ubungo Nape Nnauye. Wakati akitoa salamu toka chama chake amekiri kwamba CHADEMA ni chama kilichojijenga kitaasisi kuliko alivyokuwa akidhani. Nape alikuwa akimwakilisha Katibu wao Mkuu Yusuph Makamba. Amesema anaikubali CHADEMA sana.
Kwa upande mwingine Waziri wa Zamani Arcado Ntagazwa amepokelewa rasmi CHADEMA na kusema kuwa CCM sio mama yake mzazi hivyo amejiunga rasmi na CHADEMA na anatarajia kugombea Ubunge jimboni kwake.
Nape hajajiunga na CHADEMA kama inavyovumishwa
Dr Slaa amehudhuria mkutano huu akitokea Hospitali alipokuwa amelazwa baada ya kufanyiwa upasuaji wa mkono wake. Baadaye alirejea tena hospitali kwa matibabu. It was so sad but it had to be that way..
Katika kikao hki tulialika wageni toka kada mbalimbali ikiwemo vyama vya siasa.
Kati ya Wageni waliohudhuria ni pamoja na kijana machachari aliyeangushwa kwenye kura za maoni za Ubungo Nape Nnauye. Wakati akitoa salamu toka chama chake amekiri kwamba CHADEMA ni chama kilichojijenga kitaasisi kuliko alivyokuwa akidhani. Nape alikuwa akimwakilisha Katibu wao Mkuu Yusuph Makamba. Amesema anaikubali CHADEMA sana.
Kwa upande mwingine Waziri wa Zamani Arcado Ntagazwa amepokelewa rasmi CHADEMA na kusema kuwa CCM sio mama yake mzazi hivyo amejiunga rasmi na CHADEMA na anatarajia kugombea Ubunge jimboni kwake.
Nape hajajiunga na CHADEMA kama inavyovumishwa