Naombeni ushauri wenu kwenye hili tafadhali.....

Usiache kabisa unaharibu mila kwetu wachaga ....jitahidi uicontrol pombe isikucontrol nashukuru hujataja uraibu wa uterezi hii ndio case study ya dunia
 
Mimi ni kijana mdogo wa miaka 19. Hivi karibuni nimekua nikipatwa na msukumo mkubwa wa kunywa pombe na kuvuta bangi. Kusema kweli najaribu sana kujizuia, lakini naona kama hizi jitihada zangu hazitozaa matunda.....

Kwa muda mrefu sasa, marafiki zangu nawaona wanachukulia hii ishu kawaida sana..... Tukiwa kwenye mitoko, hawawezi acha kulewa ovyo, kuvuta bangi na shisha, na ku-vape. Kwa mtazamo wao, ni kitu cha kawaida sana, na wanaona kama hakuna madhara yoyote yanaweza kutokea. Wanasema 'wanakula ujana', 'wanamwagilia moyo'.....
Miaka mingi sasa tumekua tukiishi haya maisha.... kwenda maclub weekend na 'kula bata'. Mimi nimekua nikijizuia mno...... nazugazuga chupa moja nainya hata masaa 2-3.....

Unaweza sema niko kwenye makundi mabaya, lakini mimi sioni hivyo.... hawa ni marafiki zangu wa muda mrefu, tumekua tukisaidiana sana, sema hapo kwenye mambo ya starehe ndo tunatofautiana.....

Pia ndugu, ukizingatia kwamba mimi ni mchaga(kote upande wa baba na mama), wanatumia sana haya mazaga na wamekua wakinishawishi sana, na hata wengine kuonyesha dharau.... Nakumbuka kuna siku nilitoka na bamkubwa nikakataa kunywa pombe.... alicheka sana na kunishangaa.....

Najua wengine mnaweza sema hakuna shida yeyote kwenye kutumia kidogo, lakini kama nilivosema..... mimi ni kijana mdogo, bado maisha yangu ni marahisi, nategemea wazazi, hivyo bado nina ndoto za kufanya vitu vikubwa na maisha yangu, hivyo naogopa sana pombe na bangi vitanirudisha nyuma. Nimeona watu wengi wakiharibikiwa kwasababu ya pombe na bangi....

Najua humu JF watu wazima mko wengi, naomba mnishauri..... Kuna namna ya kubalance maisha ya kawaida na hizi starehe?? Au niendelee kukaa navyo mbali.... na ikiwa hivyo, nitumie mbinu gani??
19 yrs old bado kijana mdogo??
 
Halafu mnanyegeshana na kuambiana upuuzi. Wazee tujitafakari.. Ngoja nihamie majukwaa ya maana labda nitakutana na Wazee wenzangu
Hahahaha!. Nimecheka sana.

Baadae unapanga kukutana naye, unamuona yule pale. Aibu na masikitiko kwa pamoja zinakuganda.

Hahahaha! Bora sisi wanaume, angalau!.
 
Kuna kila dalili hii ni chai lakini kama NI kweli basi tatizo kubwa ni hapa.
"Kwa muda mrefu sasa, marafiki zangu nawaona wanachukulia hii ishu kawaida sana..... Tukiwa kwenye mitoko, hawawezi acha kulewa ovyo, kuvuta bangi na shisha, na ku-vape. Kwa mtazamo wao, ni kitu cha kawaida sana, na wanaona kama hakuna madhara yoyote yanaweza kutokea. Wanasema 'wanakula ujana', 'wanamwagilia moyo'..."
Badilisha marafik ulionao kwano peer pressure Kwa makundi ya vijana ni Jambo ambalo ni vigumu kuliepuka.
Fata haki haijalishi Nani atakuonaje kwani kipindi unaangamia utakuwa mwenyw na wao watabaki wakikucheka .
Mwisho kabisa wewe ndiye utakae chagua destiny yako na wala si mzazi wako wala Nani yako kikubwa ni kutengeneza kesho yako iliyobora Kwa kupambana Leo.
Na hauwezi kuipambania kesho yako kama Leo yako ni
  • Kunywa pombe
  • Kuvuta bangi
  • Shisha
  • Kula mirungi
  • Uzinzi
  • Kuvuta shisha
  • Na starehe nyingine zinazofanania na hizo.
 
1. Simamia unacho amini.

2. Marafiki, ndugu wanaweza wakawa na msukumo mkubwa sana kwako (peer pressure) lakini tambua it is not worth it in the long run

3. Jivunie kutokunywa pombe sio kwa sababu inamadhara ila sababu ni misingi ya maisha yako unayojiwekea. Kumbuka you have freedom to choose

4. Ukiulizwa kwanini haunywi, jibu lako lisiwe kwa sababu ina madhara ila liwe kwa sababu sioni umuhimu wa kutumia.

5. Neno "nakula ujana" halina uhalisia kumbuka wewe ni kijana na una kesho nyingi. Na katika ujana wako 15-30 ndio umri wa kujiwekea misingi sahihi ya maisha.

Mdogo wangu: Kumbuka STAREHE haziwahi kuisha wa kupitwa na wakati ILA WATU NDIO WANAISHA.

CLUB ZILIKUWEPO TOKEA ENZI KABLA HATA YA TAIFA HILI KUPATA UHURU NA MPAKA LEO ZIPO ILA WATU (VIJANA WA MIAKA HIYO) SASA NI WAZEE WENGINE WAMEPOTEZA RAMANI YA MAISHA
 
Miaka mingi umekuwa ukienda klabu, ndiyo kwanza una miaka 19.


Hiyo miaka mingi ya kwenda klabu ni ipi? Ulianza kwenda klabu na miaka mingapi?

Turudi, unaweza kuwa na urafiki na hao wenzako lakini hulazimiki kwenda kwenye maeneo ya Starehe au wanapovuta bangi. Ambatana nao kwenye mambo mengine, ukishaona sada ni muda wa kwenda Club, wewe nenda nyumbani kalale. Nina hakika hawakulazimishi.

Kila kitu ni maamuzi. Ukishaamua hakuna kinachoshindikana. Ila mwenyewe huna imani tena juu yako. Weka imani yako thabiti.

Jiwekee sababu za kujizuia kunywa pombe au kuvuta bangi. Iwe kiafya na kiuchumi na hata kijamii. Sababu hizo ziwe kichocheo cha wewe kutotaka kujaribu kutumia vilevi.

Kuwa karibu na Mungu. Omba akuongoze. Mshinde shetani. Marafiki zako kuwa wavuta bangi isikufanye nawe uvute. Kama unalazimika basi badili aina ya marafiki.
miaka 14..... haikuwa club kipindi hicho.... tulikua tukifunga shule tunajichanga tunakodisha sehemu, tunafanya bash... ila pombe,bangi zilikuwepo
 
Usiache kabisa unaharibu mila kwetu wachaga ....jitahidi uicontrol pombe isikucontrol nashukuru hujataja uraibu wa uterezi hii ndio case study ya dunia
-Mnajivunia upumbavu sana.

-Mila kunywa na kulewa?? Nyie ndio pekee duniani mnakunywa?? Hahahaha

- Muone aibu kusambaza ujinga na mambo yasiyo na msingi
 
Back
Top Bottom