ki ukweli hili la kunyima unyumba ni kitu ambacho hakiwezekani, labda niondoke nyumbani, kwa sasa hata yeye hana maambukizi tulipima naye, cha msingi mimi naona nijipange kujiondokea kabla hajaniletea huwezi jua ni lini, lakini huwezi kuishi na mwanaume ndani ya nyumba moja huku unamnyima unyumba ni hatari anaweza hata akakudhuru.
SALAAM wanaJMF!! mimi ni mgeni hapa, lakini kutokana na post nyingi nilizosoma humu moyo wangu umeridhia kwamba nitaweza kupata ushauri ambao unaweza kuniondoa kwenye msongo wa mawazo niliyonayo!!,. Mimi ni mama mwenye umri wa miaka 28 nimeolewa na nimebahatika kupata watoto wa 3, kinachonifanya niombe ushauri ni mume wangu kuwa na na wanawake wengi, kwa kifupi tumeishi kwa miaka 9 hadi sasa, yeye ana miaka 39. kwamuda wa miaka yote 9 mwenzangu amewabebesha wasichana wa kazi 2 mimba, anamtoto wa miaka 2 ambaye amezaa na mwanamke ambaye yeye hata haeleweki anafanya kazi gani, amezaa tena na muhudumu wa baa mtoto ambaye ana mwaka sasa halafu kwa sasa kuna muhudumu mwingine wa baa ana ujauzito wa miezi 6 na wote hao akisha wabebesha ujauzito anawageuzia kibao yaani hawataki wala watoto hawatunzi, hivi karibuni ameanzisha uhusiano na muhudumu mwingine wa baa, ( mwanaume huyu siyo mlevi ni msomi wa chuo kikuu anapesa za kutosha na ana kampuni kubwa tu ya uchimbaji madini ambayo pia mimi ninashare kwenye hiyo kampuni) niliwahi kumlalamikia kuhusu hii tabia yake, aliacha kujihusisha na wasichana wa kazi za ndani lakini kwa hao wa nje haonekani hata kujali malalamishi yangu zaidi aliwahi kuniambia niamue nitakavyo yeye anaweza kuishi bila mwanamke na nikitaka kuondoka niondoke na watoto wangu. mimi nimelelewa bila baba na isitoshe watoto wanampenda sana kwa ukweli huwa anamahusiano mazuri tu na watoto. yaani hii Ndoa mimi ndiyo niamue kuvumilia uchafu wake au niondoke yaani ki ukweli naumia na matendo yake lakini watoto wangu pia sitaki waishi kama mimi nifanyeje??? huwa hashauriwi na mtu niliwahi kumkuta na mwanamke tena nyumabani kwetu nikaenda kumweleza wazazi wake alimwambia baba yake naona umechoshwa na mkeo unataka kumwoa na mke wangu alinibeba juu juu mbele ya wazazi wake, huku baba yake akipelekwa Hospital kwa kupandwa na presha., ushauri pls!!!
Afu umesema umeshaongea na mwanasheria kuhusu divorce..afu haujamwambia ukweli sababu ya wewe kudai talaka. My dear siku zote ukweli utakuweka huru...Najua hapa JF imekuwa rahisi kwako kuandika ukweli kwa kuwa unaongea na computer lakini ikifikia unataka kuvunja ndoa hakuna siri tena... kuwa wazi kutakusaidia.
nashukuruni kwa ushauri sana jamani walau Moyo wangu unaanza kupata mwanga, na wogo wa kufanya mahamuzi unaanza kunitoka, nitaufanyia kazi na nitarudi tena kuwashukuru!! Asanteni