Nani mwenye kosa

Oct 9, 2017
23
48


House girl alitandika kitanda cha bosi wake Kama Sehemu ya jukumu lake la kila siku. alipomaliza akakitazama sana kile kitanda cha bosi wake akasema naweza kufa bure bila ya kulalia kitanda
kama hiki akasema ngoja nijaribu kulala lau kidogo, akavua nguo zote akaziweka chini akabaki na gagulo tu akawasha AC akajifunika brangeti gubigubi akalala. kwa bahati mbaya usingizi
ukampitia kweli akalala fofofo.
Ghafla Mume wa bosi akarudi na haikuwa kawaida yake kurudi Muda huo. alipoingia chumbani akajua hakika huyu ni mke wangu na kwakuwa jana tulikwaruzana atakuwa amekasirika tu. Akaogopa
kumwamsha. mwanamme akasaula akabaki na msuli nae akajifunika hilohilo branget kwa taratibu sana kwa hofu ya kumwamsha mke wake. kwa bahati mbaya naye usingizi ukampitia akalala fofofo . bosi (mke )aliporudi akaingia chumbani akakuta watu wawili wamelala fofofo akafunua brangeti kwa nguvu akawakuta wote wawili yaani yule mfanya kazi na mume wake wamelala pamoja walipoulizwa kila mtu akaeleza ukweli wake.
Chemsha bongo.
1.Je, kama wewe ungekuwa ndiyo yule Mke wa
bosi ungewaelewa?
2.Je Kama Wewe ungekuwa ndiyo yule mfanyakazi
ungejitetea vipi?
3. Je, Wewe ungekuwa ndiyo yule bosi ungejitetea
Vipi???
4.Je hapo Ugomvi itakuwa umesababishwa nanani?
Mke,mume au mfanyakazi??
 
mwenye kosa bosi.... ni mzembe kupitiliza... huwezi kupitiwa usingizi wakati umegeuziwa tako
 
mwenye kosa ni boss(mume) alieshindwa kutumia fursa na kuhukumiwa kwa kosa asilotenda
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom