Tuko
JF-Expert Member
- Jul 29, 2010
- 11,178
- 7,320
Niliwahi kuchangia thrad moja humu kuwa kama tunataka kuboresha shule za serikali, basi tufute shule za private.
Hata hivo ninapotafakari uwezekano wa kufuta shule hizi, nahisi sio jambo rahisi ingawa ni zuri.
Juzi nilimsikiliza Mh Hamad Rashid akichangia, na nikaona wazo lake juu ya kutatua ubovu wa viwango vya shule za serikali. Binafsi, namuunga mkono, kama nitakuwa nilimuelewa vizuri
Tatizo
Tatizo la uduni wa viwango vya shule za serikali pamoja na mambo mengine mengi, linachangiwa sana na uwepo wa shule za private, ambazo hazidhibitiwi. Kama nilivyoeleza awali kuwa hii inasababisha kuwapo kwa hali kuwa wadau karibia wote wa elimu, ukianza na wanasiasa, viongozi watendaji na walimu wanakuwa wakiwasomesha watoto wao katika Shule private. Ni wazi kuwa katika hali kama hii kunakuwa hakuna mwenye uchungu sana na shule za serikali, miongoni mwa hawa ambao, kwa kiasi kikubwa wanategemewa katika kuchangia kuboreshwa kwa shule za serikali.
Wazo la Hamad
Kwa jinsi nilivyomuelewa Hamad, ni kuwa shule za private ziendelee kuwepo lakini zichangie maendeleo ya shule za serikali. Kwa maana hiyo, kama mtu anaona kuwa ana uwezo wa kumpeleka mwanae private, then indirectly achangie mfuko wa kuendeleza gov. schools. Hii inawezekana kwa mfano ukiwekwa utaratibu kuwa asilimia hamsini ya malipo yeyote yanayolipwa na mwanafunzi katika shule ya private yanakwenda kwenye mfuko wa kuboresha shule za serikali.
Faida yake
- Shule za serikali zitaendeleza haraka zaidi kwani zitapata mchango wa nyongeza
- Baadhi ya wadau wa elimu (walimu, watendaji wa serikali, na wanachi wengine), ambao awali walikuwa wanapeleka watoto wao kwenye shule za private, watalazimika kuepuka gharama na kupeleka watoto wao kwenye shule za serikali. Kwa kufanya hivi, kwa uwezo wao wa 'hali' na 'mali' wadau hawa watachangia maendeleo za shule hizi zaidi kwani watakuwa na uchungu zazo
Hasara zake
- Gharama za shule za private zitakuwa juu
- Upo uwezekano wa hiyo michango kwenda shule za serikali kuishia mifukoni mwa mafisadi wachache
Pamoja na hasara nilizozitaja hapo juu, bado naamini itakuwa muafaka kwa kuanzia, uwepo udhibiti wa namna hiyo wakati tukielekea katika sera ya kukataza kabisa shule za private katika ngazi ya primary na sekondari. Nimewahi kutembelea nchi ambazo shule za private haziruhusiwa, na huko perfomance ya shule za serikali ni ya kuridhisha...
Hata hivo ninapotafakari uwezekano wa kufuta shule hizi, nahisi sio jambo rahisi ingawa ni zuri.
Juzi nilimsikiliza Mh Hamad Rashid akichangia, na nikaona wazo lake juu ya kutatua ubovu wa viwango vya shule za serikali. Binafsi, namuunga mkono, kama nitakuwa nilimuelewa vizuri
Tatizo
Tatizo la uduni wa viwango vya shule za serikali pamoja na mambo mengine mengi, linachangiwa sana na uwepo wa shule za private, ambazo hazidhibitiwi. Kama nilivyoeleza awali kuwa hii inasababisha kuwapo kwa hali kuwa wadau karibia wote wa elimu, ukianza na wanasiasa, viongozi watendaji na walimu wanakuwa wakiwasomesha watoto wao katika Shule private. Ni wazi kuwa katika hali kama hii kunakuwa hakuna mwenye uchungu sana na shule za serikali, miongoni mwa hawa ambao, kwa kiasi kikubwa wanategemewa katika kuchangia kuboreshwa kwa shule za serikali.
Wazo la Hamad
Kwa jinsi nilivyomuelewa Hamad, ni kuwa shule za private ziendelee kuwepo lakini zichangie maendeleo ya shule za serikali. Kwa maana hiyo, kama mtu anaona kuwa ana uwezo wa kumpeleka mwanae private, then indirectly achangie mfuko wa kuendeleza gov. schools. Hii inawezekana kwa mfano ukiwekwa utaratibu kuwa asilimia hamsini ya malipo yeyote yanayolipwa na mwanafunzi katika shule ya private yanakwenda kwenye mfuko wa kuboresha shule za serikali.
Faida yake
- Shule za serikali zitaendeleza haraka zaidi kwani zitapata mchango wa nyongeza
- Baadhi ya wadau wa elimu (walimu, watendaji wa serikali, na wanachi wengine), ambao awali walikuwa wanapeleka watoto wao kwenye shule za private, watalazimika kuepuka gharama na kupeleka watoto wao kwenye shule za serikali. Kwa kufanya hivi, kwa uwezo wao wa 'hali' na 'mali' wadau hawa watachangia maendeleo za shule hizi zaidi kwani watakuwa na uchungu zazo
Hasara zake
- Gharama za shule za private zitakuwa juu
- Upo uwezekano wa hiyo michango kwenda shule za serikali kuishia mifukoni mwa mafisadi wachache
Pamoja na hasara nilizozitaja hapo juu, bado naamini itakuwa muafaka kwa kuanzia, uwepo udhibiti wa namna hiyo wakati tukielekea katika sera ya kukataza kabisa shule za private katika ngazi ya primary na sekondari. Nimewahi kutembelea nchi ambazo shule za private haziruhusiwa, na huko perfomance ya shule za serikali ni ya kuridhisha...