Namshukuru Mungu!

Wakuu MJ kanitumia some of teh snapshots za ajali yenyewe...Ni Kumshukuru Mungu kwamba kweli kuna watu wamepona....some more to come
OMG!!

Kaizer thanks for sharing these photos... inatisha na kusikitisha sana.. Poleni wote kwani tatizo la mwanajF hasa kujwaa hili, ni letu sote
 
Wapendwa mabinamz na wapwaz!

Namshukuru Mungu kwa kuniokoa katika ajali iliyonipata juzi usiku nikielekea Iringa katika Hifadhi ya Taifa ya Mikumi umbali wa km 7 toka Mikumi mjini,

Kwenye gari tulikuwamo watu wa 5 na mmoja wetu hali yake si nzuri (tumuombee); alikimbizwa kwenye hospitali ya Kijeshi ya Lugalo baada ya kupitia Hospitali ya mt. kizito na baadaye hospitali ya serikali ya Morogoro..ni askari mwanafunzi wa kambi ya Mgambo Tanga.


Ukiachia kuchanika kidogo kidole cha mkono wa kushoto maumivu niliyo nayo ni ya msuli wa bega la kushoto na si makali sana. namshukuru Mungu.

Nilikuwa nikijitahidi kulipisha lori amablo lilionekana kujaa katikati ya barabara huku likwa limewasha taa zote; sikuwahi kusimama na kupunguza mwendo kiasi cha kutosha ndipo dereva wa lori alipotukwepa ghafla na kutuacha tukisemeza na body yake! impact ya kwanza ilikuwa ni kutoboka kwa tairi la mbele kulia upande wangu na gari kupinduka mara 3 kuelekea upande wa kulia na kutupwa porini mita 12 toka barabarani.
SHUPAVU MJ

Pole sana kwa ajali na hongera sana kwa kutoka salama... kwa kuangalia picha, you must be walking with a very strong guardian angel

Wanasema ajali haina kinga, lakini baadhi ya ajali zinaweza kuzuilika... nyingi ni uzembe na hasa kwa wanaoendesha magari makubwa, they are very abusive wakiwa barabarani hasa nyakati za usiku

I wish you a quick recovery,

Just welcome to teh club na tunaomba uwe balozi mzuri was usalama barabarani... usisite kuchukua hatua pale ambapo umeona uzembe barabarani kwani huwezi jua utakua umeokoa roho ya nani
 
:doh:poleni sana.Mungu awaponye mapema. Lakini pia mshukuruni Mungu kwa kila jambo. Naamini Mwenyezi Mungu alikuwa na makusudi yake kuruhusu jambo hili litokee. Aisee, inabidi kwa kweli msali sana kumshukuru Mungu. Fikiria kama kungekuwa na mnyama mkali hapo karibu beyond the Mikumi park limit?, ingekuwaje?. Kwa tukio hili ninaomba kuhimiza jambo moja kubwa sana ambalo ni la kweli. Binadamu tuna adui mmoja mkubwa ambaye ni shetani/ibilisi. Yeye kazi yake kuu ni kuangamiza roho za binadamu ili ziende motoni, anasema 'tukaungue sote'. Matukio ya Vita na hizi ajali mara nyingi anazisababisha shetani ili watu wafe kabla hawajatubu(wakristo kwa waisilamu) au hawajaungama (kwa wakatoliki ) ili wakifa waende motoni na anatamani ikiwezekana binadamu wote wamfuate motoni lakini Mungu kwa wema wake anatulinda sana.Watu wachache sana wameweza kuonyeshwa mambo yasiyoonekana kwa macho mfano mtu ameona mkono mkubwa wa shetani unakuja kusukuma gari ili lipinduke na anasali shetani linafukuzwa. wengine waliona waliposafiri usiku pale kitonga jitu la kutisha likikatiza wakawa kimyaaaa ndani ya gari nyele zimewasimama na wakakumbuka kusali . Ujumbe ninaotaka kuutoa kwa manufaa yetu binadamu ni kuwa tusali siku zote kabla ya kusafiri na hata tukiwa safarini ili Mungu atuepushe na njama za adui yetu ambaye hatumuoni lakini yeye anatuona. Shetani haui ila anasababisha kifo.mfano huyu dereva wa lori anaweza kuwa alitumiwa na shetani asababishe ajali iwatoe roho watu lakini Mungu kasema hapana.Tumshukuru Mungu.
 
Some more images from the scene!
 

Attachments

  • DSC00614.JPG
    DSC00614.JPG
    76.4 KB · Views: 34
  • DSC00655.JPG
    DSC00655.JPG
    69.8 KB · Views: 40
  • DSC00621.JPG
    DSC00621.JPG
    37.7 KB · Views: 34
:sorry: DUH POLENI SANA JAMANI:confused::confused::confused::A S-confused1::A S-confused1::A S-confused1:MUNGU MKUU ATA WA:help::angel:
 
Hizo picha ni za kweli wakuu!!

Mbona zimejaa vumbi na kutu kwenye eneo la ajali?

Anyws,, tunashukuru,,kwani kura yako ni ya muhimu sana.
 
Pole MJ get well soon dear it was a disaster poleni sana na wengine. Mungu ni mwema sana na anawapenda.
 
Duh pole sana kaka yangu na tunamshukuru MUNGU kwa pamoja kwa kukunusuru na ajali hii. Majeruhi MUNGU atamponya.
 
POLE SANA MKUU,KILA JAMBO LINA MAANA YAKE,PENYE HERI MUNGU HUWEKA HERI PIA.POLE SANA TUPO PAMOJA
PATENI HABARI ZA UCHAGUZI
WWW.BBCUSTREAM.COM, UKISHAPATA NENDA TAFUTA THEN BBC SWAHILI,NI LIVE SINCE ASUBUHI MPAKA JIONI
CHAGUZI NJEMA
MKUU NAJUA UTATUWAILISHA KTK UPIGAJI KURA
 
duh, pole sana mpendwa.....Mungu awajalie mpate kupona haraka na sisi wanajamii wenzio tutazidi kuwaombea
 
Wapendwa mabinamz na wapwaz!

Namshukuru Mungu kwa kuniokoa katika ajali iliyonipata juzi usiku nikielekea Iringa katika Hifadhi ya Taifa ya Mikumi umbali wa km 7 toka Mikumi mjini,

Kwenye gari tulikuwamo watu wa 5 na mmoja wetu hali yake si nzuri (tumuombee); alikimbizwa kwenye hospitali ya Kijeshi ya Lugalo baada ya kupitia Hospitali ya mt. kizito na baadaye hospitali ya serikali ya Morogoro..ni askari mwanafunzi wa kambi ya Mgambo Tanga.


Ukiachia kuchanika kidogo kidole cha mkono wa kushoto maumivu niliyo nayo ni ya msuli wa bega la kushoto na si makali sana. namshukuru Mungu.

Nilikuwa nikijitahidi kulipisha lori amablo lilionekana kujaa katikati ya barabara huku likwa limewasha taa zote; sikuwahi kusimama na kupunguza mwendo kiasi cha kutosha ndipo dereva wa lori alipotukwepa ghafla na kutuacha tukisemeza na body yake! impact ya kwanza ilikuwa ni kutoboka kwa tairi la mbele kulia upande wangu na gari kupinduka mara 3 kuelekea upande wa kulia na kutupwa porini mita 12 toka barabarani.
Pole sana mkuu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom