Masikini_Jeuri
JF-Expert Member
- Jan 19, 2010
- 6,829
- 1,296
Wapendwa mabinamz na wapwaz!
Namshukuru Mungu kwa kuniokoa katika ajali iliyonipata juzi usiku nikielekea Iringa katika Hifadhi ya Taifa ya Mikumi umbali wa km 7 toka Mikumi mjini,
Kwenye gari tulikuwamo watu wa 5 na mmoja wetu hali yake si nzuri (tumuombee); alikimbizwa kwenye hospitali ya Kijeshi ya Lugalo baada ya kupitia Hospitali ya mt. kizito na baadaye hospitali ya serikali ya Morogoro..ni askari mwanafunzi wa kambi ya Mgambo Tanga.
Ukiachia kuchanika kidogo kidole cha mkono wa kushoto maumivu niliyo nayo ni ya msuli wa bega la kushoto na si makali sana. namshukuru Mungu.
Nilikuwa nikijitahidi kulipisha lori amablo lilionekana kujaa katikati ya barabara huku likwa limewasha taa zote; sikuwahi kusimama na kupunguza mwendo kiasi cha kutosha ndipo dereva wa lori alipotukwepa ghafla na kutuacha tukisemeza na body yake! impact ya kwanza ilikuwa ni kutoboka kwa tairi la mbele kulia upande wangu na gari kupinduka mara 3 kuelekea upande wa kulia na kutupwa porini mita 12 toka barabarani.
Namshukuru Mungu kwa kuniokoa katika ajali iliyonipata juzi usiku nikielekea Iringa katika Hifadhi ya Taifa ya Mikumi umbali wa km 7 toka Mikumi mjini,
Kwenye gari tulikuwamo watu wa 5 na mmoja wetu hali yake si nzuri (tumuombee); alikimbizwa kwenye hospitali ya Kijeshi ya Lugalo baada ya kupitia Hospitali ya mt. kizito na baadaye hospitali ya serikali ya Morogoro..ni askari mwanafunzi wa kambi ya Mgambo Tanga.
Ukiachia kuchanika kidogo kidole cha mkono wa kushoto maumivu niliyo nayo ni ya msuli wa bega la kushoto na si makali sana. namshukuru Mungu.
Nilikuwa nikijitahidi kulipisha lori amablo lilionekana kujaa katikati ya barabara huku likwa limewasha taa zote; sikuwahi kusimama na kupunguza mwendo kiasi cha kutosha ndipo dereva wa lori alipotukwepa ghafla na kutuacha tukisemeza na body yake! impact ya kwanza ilikuwa ni kutoboka kwa tairi la mbele kulia upande wangu na gari kupinduka mara 3 kuelekea upande wa kulia na kutupwa porini mita 12 toka barabarani.