Mwitikio wa serikali na wananchi kusaidia wahanga wa milipuko ya Mbagala

Belinda nimekupata tatizo hapa ni moja tu kuwapata mods imekuwa kazi wao wangeweza kukusanya michango na kuipeleka pale Ofisi ya mkuu wa mkoa misaada itafika tu kwa walengwa.
 
Belinda nimekupata tatizo hapa ni moja tu kuwapata mods imekuwa kazi wao wangeweza kukusanya michango na kuipeleka pale Ofisi ya mkuu wa mkoa misaada itafika tu kwa walengwa.

Kwa Lukuvi,???? He he he
Anyway, njia rahisi mtumie ujumbe wa faragha Robot usikie ana lipi na kusema juu ya hili, naamini ameiona hii thread labda anafiria kitu.
PAMOJA mkuu..
 
Kwa Lukuvi,???? He he he
Anyway, njia rahisi mtumie ujumbe wa faragha Robot usikie ana lipi na kusema juu ya hili, naamini ameiona hii thread labda anafiria kitu.
PAMOJA mkuu..

Lukuvi Mnyalukolo humwamini?
Hata mm naona jamaa kuna kitu wanafikiria na wanajaribu kuangalia pande zote mbili.
 
@ nguli, hiyo thread ilianzishwa na game theory inaitwa 'picha itakayomsuta jk na wabunge wake mamilionea'...nimeshindwa kuweka link ila ipo jukwaa la siasa..kuna picha inawaonyesha wanafunzi wamekaa chini na sare zao za shule ( yaani ndo darasani kwao hapo kwenye mchanga).

@ fidel - imani ya watu kuchangia wana mbagala ipo ila jinsi ya kufaniksha hili zoezi ni gumu maana watu tupo sehemu mbalimbali na pia hupati uhakika kama walengwa watafikiwa na msaada wetu. Nikijua utaratibu, nitakujulisha na mie..

Siku njema!!

belinda nakushukuru sana, nina search nikipata nitakufahamisha na mchango wetu tukitoa katika hio shule tutakutumia picha katika private msg/mail....
 
Karibu mkuu, uta-update imekuwaje na hizo pic!..

Tumepata ile picha aliyoitoaga GAME THEORY tunaitumia kama supporting evedence kupata hela za kununua madawati au hata mabati ya ku-create shed ya muda wakati mipango endelevu kutoka kwa wakuu au taasisi zitakazo jitokeza...
 
Tunashukuru mkuu Nguli na jitahidi sana.
Nakutakia kila kheri fanya hivyo mkuu.
 
Tumepata ile picha aliyoitoaga GAME THEORY tunaitumia kama supporting evedence kupata hela za kununua madawati au hata mabati ya ku-create shed ya muda wakati mipango endelevu kutoka kwa wakuu au taasisi zitakazo jitokeza...[/QUOTE]

Du umenimaliza nguvu kabisa, hadi msubiri hao wakuu wajitokeze watoto wataendelea kung'atwa na sungusungu kwenye makalio, serikali yao pia inasubiri wafadhiri. Hongera fidel kwa kuanzisha juhudi za kuchangia sisi wenyewe, binafsi sitoweza kuhangia hapa kwani nimekwisha fanya hivyo kwenye avenue nyingine.
 
wakuu JF! kama Mungu amekujalia kipato hata kidogo think of others who have nothing at all, unampomsaidia mtu kielimu utakuwa umemsaidia sana kwa sababu education is power, mimi mwenyewe ni kati ya wengi tuliosoma kwa shida -because we know where the shoes pinches lets wake up and provide little hope where seems to be lost.
 

Peter Masangwa na Salum Pazzy


SERIKALI imeahidi kuwalipa mafao kwa muda wa maisha yao yote, watu wote waliopata ulemavu wa aina mbalimbali kutokana na milipuko ya mabomu iliyotokea katika ghala la silaha la Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), Aprili 29, mwaka huu, jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na gazeti hili jana, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Bw. Wiliam Lukuvi, alisema watu hao watalipwa fidia kulingana na madhara yaliyowapata.

Bw. Lukuvi alisisitiza kuwa Serikali ipo pamoja nao kwamba na itawasaidia kuendesha maisha yao ya kila siku.

Alifafanua kuwa mafao watakayokuwa wakilipwa watu hao , yatajulikana baada ya wataalamu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii kutoa mchanganuo wa kile wanachostahili kuwa wanalipwa kulingana na aina ya ulemavu waliopata.

"Wizara ya Afya ndio inahusika na kufanya hesabu, nimewaagiza watuletee idadi kamili ya watu waliopata ulemavu wa kudumu pamoja na mapendekezo yao," alisema Bw. Lukuvi.

Alisisitiza kuwa taarifa hiyo itaambatana na ile tathmini ya maafa itakayotolewa Juni 13, mwaka huu.

Bw. Lukuvi alisisitiza kuwa yupo makini kwa kuwa anaguswa na maafa yaliyowapata wakazi wa Mbagala.

Kuhusu vurugu zilizotokea wakati wa ugawaji misaada kwa waathirika wa mabomu, Bw. Lukuvi alisema kazi ya kusimamia ugawaji wa misaada hiyo ameachiwa Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Bw. Said Mkumbo.


Source:Waliopata ulemavu Mbagala kulipwa mafao milele

Wawaulize kwanza wahanga wa vita ya Kagera wanapata nini milele? Na hapo ndipo watajua kuwa wamelamba jokeli mchana kweupe?
 
Usanii tu mwingine!!!! Je Tz ina walemavu karibu 10% ya Watz wote kwa data za WHO.. je serikali inawapa nini kwa sasa?

Walemavu ni sehemu ya jamii..05% ya nafasi kazi zote inabidi kutengwa kwa ajili yao..kama China! Usipolipa basi 10% ya faidi yako unatoa kusadia walemavu!

Pia inabidi tuwape pesa za kuishi na kuwalipa say 80,000 Tshs kila mwezi kwa kila familia yenye mlemavu!

Huu ndo uzalendo!
 
Usanii tu mwingine!!!! Je Tz ina walemavu karibu 10% ya Watz wote kwa data za WHO.. je serikali inawapa nini kwa sasa?

Walemavu ni sehemu ya jamii..05% ya nafasi kazi zote inabidi kutengwa kwa ajili yao..kama China! Usipolipa basi 10% ya faidi yako unatoa kusadia walemavu!

Pia inabidi tuwape pesa za kuishi na kuwalipa say 80,000 Tshs kila mwezi kwa kila familia yenye mlemavu!

Huu ndo uzalendo!
Msije kushangaa ikatumika sheria ile ile ya mkoloni...! Mara kila mhanga analipwa shs 20/- kwa wiki kama si kila mwezi.
 
Last edited:
Hivi jamani hii mbagala kwa nini isifanywe mkoa jamani kwa sababu kuna nyomi ya watu mbagala jamani,balaaaaaaaa!Ukitaka kujua mbagala kuna watu wengi pita asubuhi uone watu walivyojaa kituoni kusubiri magari kwenda maofisini kujitafutia rizki...Hao tu ni wale wanaofanya kazi,bado wasiofanya kazi(baba na mama wa nyumbani na watoto)
Ungefanywa mkoa tu huu ujitegemee...!!!
Mnalionaje hili swala?!
 
Last edited:
Kuna vigezo na taratibu maalum ili serikali ilitangaze eneo kama Mkoa.

nafikiri wizara inayohusu mambo haya ya mikoa (TAMISEMI) wanajua mengi sana kuhusu ili.

Mimi ningefikiri labda wafanyiwe majimbo mawili ya uchaguzi yaani wawe na wabunge wawili na labda halmashauri mbili ili kuleta serikali karibu zaidi na wananchi ikiwa pamoja na kutolewa maamuzi haraka ya kiutendaji.

Nasriah
 
Shida kuu ya huko Daslamu ni kwamba huduma zote za Kiserikali zimekaa kule mjini, sijui ndo feri, sijui mimi!

Kwanini maeneo kama Mbagala nako kusiwe na sub`offices zinazotoa huduma zilezile?
Haya bana na daslamu yenu, yetu macho!

Lakini kimsingi namwunga mikono Barubaru, kwamba kuwe na majimbo 2 ya kiutendaji!
 
WAATHIRIKA wa mabomu Mbagala Kuu yaliyopelekea kubomoka kwa nyumba zao kutokana na mabomu yaliyosababishwa na kambi ya Jeshi watoa siku tatu kwa serikali la sivyo wataandamana kushinikiza kutimiziwa madai yao.
Waathirika hao wametoa muda huo kwa serikali kwa kuchoshwa na ahadi hewa kutoka serikali inayowafanya waishi maisha ya kutangatanga kama hawakuwa na makazi.

Hatua hiyo ya kuandamana imekuja baada ya serikali kutotoa kauli iliyo thabiti juu ya wahanga hao na kuwapa ahadi hewa ambazo zimewachosha na kuchukua uamuzi huo ili waweze kutimiziwa mahitaji yao.

Akizungumza kwa jazba Makamu Mwenyekiti wa wahanga hao, Bw. Nicklaus Ngaloma amesema kuwa, wanawapa Serikali siku tatu kuanzia jana ili waweze kutimiza ahadi wanazowapa wakazi hao na kama hawatatimiza wataandamana hadi Ikulu kushinikiza kupatiwa fidia za nyumba zao zilizobomoka kufuatia mabomu hayo.

Amesema serikali imekuwa ikitoa ahadi hewa zinazowafanya kucheleweshwa kwa kupewa fidia na kujengewa nyumba hali inayofanya waendelea kuteseka kwenye mahema ambayo wamelundikana zaidi ya familia zaidi ya tano kwenye hema moja.

Amesema serikali inachelewesha mchakato mzima wa kutoa fidia ama kujenga nyumba hizo hali inayowafanya wachoshwe na hali wanayoendelea kuwa nayo sasa.

Hivyo wameamua kufanya hivyo endapo serikali haitaanza mchakato mzima wa nyumba hizo ili warudi katika hali zao za kuishi kama wengine na si kuteseka kulundikana kwenye mahema hayo.

“ Yaani sisi unavotuaona hatuogopi mabomu endapo watakataza maandamano hayo kama mabomu tulishapigwa nayo sasa ni mabomu gani tutakayoogopa ni lazima tuandamane hayo mabomu ya machozi hayatatutisha” walilalama

Wakazi hao wamekuwa wakiishi kwenye mahema hayo ni zaidi ya miezi minne sasa. http://www.nifahamishe.com/NewsDetails.aspx?NewsID=2751258&&Cat=1
 
1

Mmoja wa wazee Mussa Mgeni akionyesha hundi yake yenye thamani ya shilingi 168,000 alizolipwa kama fidia kutokana na nyumba yake kuathirika na mabomu. Hata hivyo mzee huyo asiyeweza kutembea ana umri wa miaka 76 alilia sana kutokana na kuwa nyumba yake ilikuwa ya gharama zaidi ya hiyo pesa aliyopewa.

Source: Pwani Raha
 
Samahani si kwamba sielewi ila tu nauliza hizo pesa wanazolipwa fidia ni za kujenga nyumba nyingine mpya au kurekebisha mahali palipoharibiwa na mabomu? Mbona 168,000 ni ndogo sana kwa kujenga nyumba mpya?
 
Back
Top Bottom