CCM akili fupi.Sisi tunajua kuwa bunge linarejea Jumatatu maana wiki hii lilikuwa kwenye kamati ya matumizi.Nilimsikia Makinda akisema juzi hili ndilo bunge tulilolijua toka nyuma, wiki hii imekuwa kila kitu ndiyo na mipasho ya kusifia tu.Watazamaji tulikuwa tunakosa uhondo sana
Ana shida kubwa kichwani! Nashindwa kuelewa, hivi wanapo tembelea Mabunge ya nchi za wenzao hapa duniani, huwa wanajifunza nini? Au ni hizo posho za safari ndio muhimu kwao?
Hivi katika ulimwengu huu wa leo, kwa kiongozi kama yeye bado anawaza Bunge la Chama Kimoja? Nina hakika hata kiti anacho kikalia hajui hadhi yake.