Katika kile kinachoonekana kutafuta mahali pa kujishika, Mbunge wa Iramba Magharibi Mwigulu Nchemba amemtaka msajili wa Vyama vya siasa nchini John Tendwa kusitisha mara moja operesheni Sangara za chama hicho kwa kile anachodai zinatishia amani ya nchi.
Mwigulu alisema baada ya mazishi ya kada wa chama chake hapo jana yaliyotokea huko Ndago atahakikisha anapambana kwa nguvu zote na CHADEMA ili kukomesha tabia yao.
Source:Habari Leo
My Take:
Wachunguzi wa mambo wanadai kuweweseka huku kwa Mwigulu ni kutokana na kutuhumiwa kama mhusika mkuu wa mauaji yaliyotokea kwa kile wanachodai alikodi vikundi vya vijana na kuwapa hela ili wakavuruge mkutano wa CHADEMA na ndipo wananchi walipozidi nguvu kikundi hicho cha wahuni na kuwatimulia mbali.
Hata hivyo mpaka sasa bado jeshi la polisi halijafanya mahojiano yoyote na Mwigulu ili kuchunguza madai hayo. Mwigulu amekuwa mara nyingi akitoa maneno ya hovyo na matusi dhidi ya CHADEMA hasa awapo bungeni na kwenye mikutano ya hadhara.
Tayari jimbo lake la Iramba Magharibi CHADEMA ina nguvu kubwa na kuna uwezekano mkubwa Mwigulu asirudi tena bungeni baada ya uchaguzi ujao.
Mwigulu alisema baada ya mazishi ya kada wa chama chake hapo jana yaliyotokea huko Ndago atahakikisha anapambana kwa nguvu zote na CHADEMA ili kukomesha tabia yao.
Source:Habari Leo
My Take:
Wachunguzi wa mambo wanadai kuweweseka huku kwa Mwigulu ni kutokana na kutuhumiwa kama mhusika mkuu wa mauaji yaliyotokea kwa kile wanachodai alikodi vikundi vya vijana na kuwapa hela ili wakavuruge mkutano wa CHADEMA na ndipo wananchi walipozidi nguvu kikundi hicho cha wahuni na kuwatimulia mbali.
Hata hivyo mpaka sasa bado jeshi la polisi halijafanya mahojiano yoyote na Mwigulu ili kuchunguza madai hayo. Mwigulu amekuwa mara nyingi akitoa maneno ya hovyo na matusi dhidi ya CHADEMA hasa awapo bungeni na kwenye mikutano ya hadhara.
Tayari jimbo lake la Iramba Magharibi CHADEMA ina nguvu kubwa na kuna uwezekano mkubwa Mwigulu asirudi tena bungeni baada ya uchaguzi ujao.