Waberoya
Platinum Member
- Aug 3, 2008
- 15,169
- 10,786
ki.
Mwenyekiti wa Chama cha kuwakomboa wananchi, anapotumia magari kama ya watawala, inasema nini kuhusu huu ukombozi? VX8, tena sio moja, Wasaidizi, Dreva, MABENDERA, KUCHELEWA KUFIKA UWANJANI, bado hajashika nchi, je akishika tutegemee nini tofauti, maana haya si ndio ya kawaida kwa watawala? Kwenye kuvaa kombati sawa lakini mengine hayo mbona sawa na watawala?
- NAOMBA KUTOA HOJA, MAANA WAKOMBOZI KINA CASTRO, CHE GUEVARA, MAO, NA SAVIMBI HATUKUWAONA NA MA-VX8, AU WASAIDIZI AU NI UKOMBOZI TOFAUTI?
- KUONGOZA SI NI MFANO ZAIDI? MUNGU AIBARIKI TANZANIA!
William.
..kiungo kati ya mwanasiasa na wananchi/wapiga kura wake ni IMANI/TRUST, pamoja na ujumbe wa matumaini kwa wale anaowaongoza/anaotaka kuwaongoza.
..ukiona Mbowe anatembelea magari hayo na wanachama wake hawalalamiki ujue ni kwasababu wamemuamini kwamba anafanya na kusimamia yale waliyomtuma.
..CCM wanalalamikiwa na wananchi kuhusu matumizi ya magari ya kifahari kwasababu wananchi hawaridhiki na utendaji kazi wa CCM. hata sasa hivi CCM wakiamua kutumia bajaji bado wananchi wanaweza wasiridhike kutokana na rekodi ya miaka 30+ ya utawala mbovu.
..Mwalimu Nyerere alikuwa anaishi msasani kwenye beach house na wakati mwingine akiendeshwa kwenye benzi ya milango mitatu, Sokoine amefariki akiwa amepakiwa kwenye benzi high class ya wakati huo. wananchi hawakulalamikia matumizi ya Mwalimu na Sokoine kwasababu waliwaamini.
..pia siyo lazima kiongozi awe masikini ili aweze "ku-connect" na wananchi/wapiga kura masikini. JF Kennedy alizaliwa kwenye familia ya kitajiri lakini aliweza kukubaliwa na wapiga kura ambao wengi wao alikuwa amewazidi kiukwasi. Wananchi walimpa kura Kennedy kutokana na ujumbe wake wa matumaini kwa wananchi wote wa Marekani.
..labda unajiuliza kwanini CCM wanaumiwa wanapotanua na ma-VX wakati CDM r given a free pass. Jibu ni kwamba CCM wanachongewa na kuwepo kwao madarakani kwa muda mrefu bila kuwa na chochote cha maana cha kuonyesha, pamoja na masuala ya rushwa na ufisadi vilivyotamalaki ndani ya chama hicho.
ki.
Mwenyekiti wa Chama cha kuwakomboa wananchi, anapotumia magari kama ya watawala,
william*! mbona magar na mijumba na mimali mliyojilimbikizia nyie masisihemu mafithaad huthemi, majiz makubwa nyie mnaacha kuwasapot watanzania maskin watoto wakina mama wajawazito hospital hazielewek shule hazielewek miundombinu fake, toen kwanza borit mlilo nalo ndio mlitoe la jiran yenu, vilaza nyie
Heshima kwenu wanajamvi,
Mkuu W J M kauliza swali zuri sana bahati mbaya hapewi majibu ana ambulia kejeli na viroja.Wanajamvi wenzangu tuitendee haki JF kama huna uwezo wa kujibu hoja kaa pembeni magauzi ya kweli yatafanikiwa ikiwa tutakubali kukosolewa na kujisahihisha.
CDM leo ni chama cha upinzani kesho kinaweza kuwa chama tawala mambo yanayotendwa na viongozi wake leo yanatoa mwanga wakipewa dola watatutendea nini !.
Tunapinga kwa nguvu zetu zetu serekali ya CCM iachane na matumizi ya magari ya kifahari bahati mbaya mbadala wa CCM naye anatumia magari ya kifahari ?.
CCM can justify all what they are doing simply kwa sababu society iko kimya, ha-riot.........mbona malawi mkate ulipanda bei wananchi waligoma??
jibu lake ni our 'society is sick'
sick of believing everything, trusting anybodu, hating somebody, etc!
ndio maana akina lowassa , chenge, rostam walipendwa na wanapendwa na watu wao
ndio maana pamoja na tuhuma za mwingira, kakobe na lwakatare bado wana waumini wengi tu!
ndio maana kibwetere aliwachoma wenzake moto, yes wale waumini si walikubali wenyewe!
wabunge wangapi na mwaziri ni wezi na bado wananchi wao wanawapenda??
mikutano mingapi ya ccm unaona watu maelfu, na ukiwaona maisha yao wamechoka sana na source ya matatizo yao ni CCM?? jibu lake ni our society is sick!!
Mkuu
Kama sikosei wanachokipigania CHADEMA ni usimamizi wa rasilimali za nchi vizuri, ikiendana na kuacha kutumia mamilioni ya pesa kwenye magari ya kifahali lakini sio kuwakataza wananchi wenye uwezo binafsi kufanya hivyo, kwa hiyo mpaka hapo nitakaposibitishiwa kwamba Gari la Mwenyekiti limetoka kwenye pesa za chama ndio ntaona kuna hoja ya kujadili.
Ben, swali la kujiuliza ni je nini kimefanyika mara baada ya yeye kuondoka hapo?Mtu kama rais akitembelea sehemu kama hiyo ni lazima ajuwe kama kuna kilichofanyika(endapo kuna maagizo yoyote aliyoyaacha) mara baada ya yeye kuondoka.Hii picha ya father christmas (ofcourse aliyekosea itifaki ya mavazi) inaleta uchochezi......
Hapa juu haoni aibu kuwa hafanani na hao wenyeji wake.Sijui ni lini tabasamu lilishatoa tafsiri ya huzuni tofauti na Furaha ama Kejeli.......