Kimbunga
Platinum Member
- Oct 4, 2007
- 14,941
- 9,947
Mkuu bombu una maana yale ni magari yao binafsi? Hata ikiwa hivyo sawa. Sasa kama wanatumia magari yao binafsi aina ya V8 wakichukua nchi ndio watatumia RAV4 au wataendelea kutumia magari yao binafsi V8?Kimbunga, hapo kwenye bold, ndo tunauita unafiki. Kwa nini tupende kudanganywa? Hivi wewe unapenda watu wafanye mambo kwa kificho? Kama mtu ana gari la kifahari halafu akaliweka nyumbani na kupanda daladala ili aweze kuaminika ni miongoni mwa wapanda daladala, huo ni ulaghai na unafiki. Tunachopinga sisi ni Serikali kutumia fedha za walalahoi kufanya anasa. Endapo wangetumia pesa zao za mifukoni/mishahara yao, tusingegomba.
Mie binafsi sioni hatari mtu kutumia alichokipata kwa uhalali, ni mali yake na atumie atakavyo. Na kwa taarifa yako, Viongozi wa chadema hawapendi unafiki, ni tofauti na wale wa MAGAMBA wanaopanda ndege, huku magari yao ya kifahari yakitangulizwa waendako.
Its a shame tunashindwa kuliona jambo hili kwa upana wake. Hakuna dhambi kwa mtu kutumia alichopata kwa jasho lake, dhambi ni kutumia kichotokana na jasho la wengine kwa manufaa ya mtu binafsi.
Last edited by a moderator: