Mentee
Senior Member
- Jul 14, 2010
- 142
- 29
Mji wa Mwanza leo umezizima kwa masaa takribani matano baada ya Wamachinga kuteka mitaa yote ya katikati ya jiji. Uongozi wa Jiji la Mwanza umevunja vibanda vya Wamachinga katika operesheni maalumu na Wamachinga wamejikuta wakilazimishwa kuhamia umbali wa kilomita kama kumi hivi ili kuanza makazi yao mapya ya biashara. Hata hivyo, hali haikuwa kama ilivyotarajiwa kwani uongozi wa Halmashauri ya Jiji hili umejikuta ukipata changamoto kama lile la Tunisia na Misri... ingawa hapa hakuna waliojitoa muhanga na kujichoma moto lakini wamegomea amri ya kuhamia makazi mapya. Leo tangu asubuhi Wamachinga wamekuwa wakipora maduka yaliyo wazi hasa ya Wahindi na kuvunja vioo vya magari yanayopita hususan katika barabara kuu kama ya Kenyatta. Je, Watanzania wamechoka na maisha ya dhiki ya kila siku? Je, viongozi wa ngazi za juu hawasomi alama za nyakati?