enzo1988
JF-Expert Member
- May 26, 2018
- 732
- 2,874
Tukio la kusikitisha na la kinyama limetokea katika kijiji cha Lusanga ambacho kinapatikana katika wilaya ya Mvomero tarafa ya Turiani.
Tukio lenyewe:
Katika tukio hilo mwanaume ameamua kuwapa sumu watoto wake watatu ambao wote wamefariki. Muhusika aliamua kujitoa uhai wake lakini hakufanikiwa. Muhusika amelazwa katika hospitali ya Bwagala.
Sababu:
Sababu kuu iliyopelekea unyama huu ni mapenzi kwani muhusika alikuwa akimbembeleza mama watoto wake warudiane kwani aliondoka kutokana na ugomvi. Mama watoto alikataa kwani alitaka waoane ,ndipo baba watoto akachukua uamuzi wa kuwanywesha sumu inayoua na kuteketeza magugu.
Mazishi:
Mazishi yamefanyika usiku huu ( Saa tatu usiku) katika kijiji cha Lusanga tarehe 27-11-2018.
Dah!! Mapenzi yana nguvu lakini siyo kwa unyama na ukatili huu.
Chanzo: Mimi mwenyewe.
Nb: Kwa maadili siwezi kuweka picha zao hapa mtandaoni, kwani ni watoto wadogo. Mmoja ana miezi tisa kuelekea kumi mwingine chekechea na mkubwa darasa la kwanza.
Tukio lenyewe:
Katika tukio hilo mwanaume ameamua kuwapa sumu watoto wake watatu ambao wote wamefariki. Muhusika aliamua kujitoa uhai wake lakini hakufanikiwa. Muhusika amelazwa katika hospitali ya Bwagala.
Sababu:
Sababu kuu iliyopelekea unyama huu ni mapenzi kwani muhusika alikuwa akimbembeleza mama watoto wake warudiane kwani aliondoka kutokana na ugomvi. Mama watoto alikataa kwani alitaka waoane ,ndipo baba watoto akachukua uamuzi wa kuwanywesha sumu inayoua na kuteketeza magugu.
Mazishi:
Mazishi yamefanyika usiku huu ( Saa tatu usiku) katika kijiji cha Lusanga tarehe 27-11-2018.
Dah!! Mapenzi yana nguvu lakini siyo kwa unyama na ukatili huu.
Chanzo: Mimi mwenyewe.
Nb: Kwa maadili siwezi kuweka picha zao hapa mtandaoni, kwani ni watoto wadogo. Mmoja ana miezi tisa kuelekea kumi mwingine chekechea na mkubwa darasa la kwanza.