Boran Jakutay
Senior Member
- Apr 8, 2023
- 110
- 255
Dar: Karim Shabani mwenyeji wa Chanika jijini Dar es Salaam, anadaiwa kuwaua watoto wake wawili kwa kuwapa sumu aliyoiweka kwenye juisi, baada ya kutuhumu mtoto wa mwisho aliyezaliwa na mkewe sio wake na hafanani naye.
Juma Mohammed ambaye ni msemaji wa familia ya marehemu, amesema Karim aligombana na mkewe kutokana na sababu hiyo ya mtoto wa mwisho na kupelekea kutengana miaka miaka miwili iliyopita na watoto kwenda kuishi kwa bibi yao mzaa baba.
Inaelezwa mtuhumiwa huyo juzi alifika kwa wazazi wake na kuwachukua watoto wake watatu kwa lengo la kwenda kusherehekea nao Sikukuu ya Eid sehemu anayoishi lakini aliamua kuwapa watoto wote juisi yenye sumu, watoto wawili walifariki dunia na mmoja anaendelea kupatiwa matibabu katika Hosptali ya Mloganzila jijini Dar es Salaam.
Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema mtuhumiwa wa tukio hilo tayari anashikiliwa na jeshi la polisi mkoani humo.
Chanzo: GADI TV